Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Ninachokiona hapa ni watu kudharau "makande" na si kingine. Yaani ukiuza makande unaonekana kama hujui vile...

Ila makande hayo hayo yanaweza kumtajirisha huyo dada. Just give her time.

Kingine wanaomponda wengi nadhani si wajasiriamali...maana huwezi kuidharau fursa ambayo inaweza kuwa chanzo kikubwa cha fedha. Wewe unapoona kuuza makande kuwa ni upumbavu, yeye anaona pesa.

Lastly, elimu inayosomewa darasani mara nyingi haimuandai msomi kujiajiri...bali humuandaa kama mtumishi sehemu fulani. Ndiyo maana darasa la 7 anaweza kumuajiri mtu mwenye masters.

Kusoma Marekani tu bado hakukupatii fedha, kurudi nyumbani Tz ni uamuzi mzuri maana fursa bado ni nyingi sana compared na US ambako almost kila eneo tayari limeendelezwa. Rudi home jenga uchumi wa nyumbani.
 
Shida ni kwamba mnapondea huku anaingiza pesa. wewe hapo Kesho ukikutana na barua ndo mwisho wa ujanja. yeye hafanyii mwanaume kazi yoyote ile.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu mawazo yako kama yangu,
Napata tabu hata kuchangia kwakua wengi tuna tatizo la mtizamo, ila utawasikia wanataka kufanikiwa sasa unajiuliza atafanikiwaje huyu! na anakuomba ushauli umpe ushauli afanikiwe.
Safari ya mafanikio ni ndefu na siyo wote watafika lazima wengine wawe wafanyakazi wa wengine walio thubutu kufikiri tofauti na ilivyo zoeleka.
 
Unaweza ukaajiriwa ila ukawa unalipwa 25 million kwa mwezi,so be careful

Noma
1.gif


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama umesoma elimu yako haijakukomboa bado, nachelea kusema nawe utakuwa kundi moja mliokosa ajira na kushindea kuitumia elimu mliopata mkaamua kukimbilia kilimo cha matiki tiki, ufugaji wa kuku na upikaji makande

Mfumo wa elimu unakuandaa kuja kuwa/kufanya kazi fulani ndio maana una invest muda na pesa kupata hiyo elimu, kama umeshindwa kuitumia elimu yako wewe ni failure hata hivyo vyeti ukavichome moto.

Usitake kuaminisha wote walioajiriwa ni mafala kuna kada ambazo huwezi kuanza tuu kwa kujiajiri mf. Walimu wote wakimaliza chuo watoke wakafungue shule zao au tuition centre na madaktari hivyo hivyo.

Wakulima wajasiriamali mnafurahisha sana na mindset zenu za kimasikini kama ishu ni kujiajiri kwanini asitumie elimu yake kufanya kitu?Na hata kama ni mjasiriamali kwanini asifanye corporate level entrepreneurship?kwa elimu yake ya masters anazidi kupoteza muda

Ninajua watu waliojiri na walioajiriwa wanafanya hizi biashara kama chanzo kingine cha mapato

Mifano ipo mingi ya wajasiriamali ambao hawajapoteza mda shule kihivyo ma wamefanikiwa hao ndio tunatakiwa kuwapongeza na kuwatumia kawa watu wanao inspire wengine, siyo failure walioshindwa kutumia elimu yao
 
Kazi ya hadhi ni ipi boss?
ni ile ambayo kila mtu angependa kuifanya lakini wanayoifanya ni wachache kutokana na uwezo,education level,experience,personalities,system etc.
swali lako ni sawa ma kuniuliza nyumba nzuri ni ipi wakati unajua kuna watu wanaishi kwenye mbavu za mbwa na wengine wanaishi kwenye kasri
 
Kutu kwenye chuma ndio kuoza kwake.
 
Kama umesoma elimu yako haijakukomboa bado, nachelea kusema nawe utakuwa kundi moja mliokosa ajira na kushindea kuitumia elimu mliopata mkaamua kukimbilia kilimo cha matiki tiki, ufugaji wa kuku na upikaji makande

Mfumo wa elimu unakuandaa kuja kuwa/kufanya kazi fulani ndio maana una invest muda na pesa kupata hiyo elimu, kama umeshindwa kuitumia elimu yako wewe ni failure hata hivyo vyeti ukavichome moto.

Usitake kuaminisha wote walioajiriwa ni mafala kuna kada ambazo huwezi kuanza tuu kwa kujiajiri mf. Walimu wote wakimaliza chuo watoke wakafungue shule zao au tuition centre na madaktari hivyo hivyo.

Wakulima wajasiriamali mnafurahisha sana na mindset zenu za kimasikini kama ishu ni kujiajiri kwanini asitumie elimu yake kufanya kitu?Na hata kama ni mjasiriamali kwanini asifanye corporate level entrepreneurship?kwa elimu yake ya masters anazidi kupoteza muda

Ninajua watu waliojiri na walioajiriwa wanafanya hizi biashara kama chanzo kingine cha mapato

Mifano ipo mingi ya wajasiriamali ambao hawajapoteza mda shule kihivyo ma wamefanikiwa hao ndio tunatakiwa kuwapongeza na kuwatumia kawa watu wanao inspire wengine, siyo failure walioshindwa kutumia elimu yao
Kwa kukusoma hapa na kwenye ile thread nyingine, you are being unfair to the girl. Ukimwangalia kama individual, with her own agency, and the ability to make her own determinations usingeongea yote unayosema ukifikiri unamsaidia. Unaweza kuwa na tatizo na yeye kusifiwa au kupata spotlight kwenye media, na unaweza kutumia story yake kumdrive towards bigger things, au kufundisha jamii ya waliobahatika kupata elimu na exposure kuwa na ndoto kubwa zaidi bila kumkatisha tamaa yeye binafsi. Unapomuattack personally who are you helping exactly? You don't know her drive, her plans, her journey. She wakes up everyday to do what she does and seemingly she's content . Unapodimish what she currently lives and does as a waste of a life, unamsaidia? Kwa nini unampa majukumu ya kuwa mfano kwa jamii nzima kwa sababu ya elimu na nafasi alizo wezeshwa na familia yake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tumia akili yako vizuri,hapa duniani hakuna kazi inayodhalilisha ili mradi tu iwe halali,kama ni hvo basi tunaweza kusema kazi unayo ona haidhalilishi mm naweza kuiona ya ovyo na inadhalilisha hvo usiseme kuna kazi zinadhalilisha....

Sent using Jamii Forums mobile app
Shida iko wapi kwani! Mimi natumia akili yangu vizuri sana kuliko nyie manyangau mnaotaka kwenda kufagia choo ulaya. shame on you. Siwezi tengua hii kauli. Kama unaona bora ukatumikishwe huko ungana na huyu fala mwenzio nendeni. Na kama nataka connection nawapeleka scandinavia huko mkafanya wenzenu walienda wakaishia kurudi wanasikitika. Msipende kupalamia mambo msiyoya jua
 
Kwa kukusoma hapa na kwenye ile thread nyingine, you are being unfair to the girl. Ukimwangalia kama individual, with her own agency, and the ability to make her own determinations usingeongea yote unayosema ukifikiri unamsaidia. Unaweza kuwa na tatizo na yeye kusifiwa au kupata spotlight kwenye media, na unaweza kutumia story yake kumdrive towards bigger things, au kufundisha jamii ya waliobahatika kupata elimu na exposure kuwa na ndoto kubwa zaidi bila kumkatisha tamaa yeye binafsi. Unapomuattack personally who are you helping exactly? You don't know her drive, her plans, her journey. She wakes up everyday to do what she does and seemingly she's content . Unapodimish what she currently lives and does as a waste of a life, unamsaidia? Kwa nini unampa majukumu ya kuwa mfano kwa jamii nzima kwa sababu ya elimu na nafasi alizo wezeshwa na familia yake?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sijasema “waste of life” katika maneno yangu na mimi sina tatizo nae as long as anapata mahitaji yake na anayo furaha ni sawa ni maisha yake anaishi siyo kupoteza...now my problem is anafanya kitu cha kawaida sana kuwa mfano kwa vijana na wanawake kama njia ya kujikwamua kiuchumi, kama inavyoonyeshwa na media na wadau huku jf.

kwa msomi ambaye angeamua kuitumia elimu yake kujiajiri hapo ningempa heko, tuwe na tabia ya kukubali unapokosolewa, ila ukikosolewa ukachukulia kama ni personal attack hapo utakuwa na shida nyingine, anaweza kupokea criticism na zikamjenga zaidi kwenye biashara yake kwa kutu prove wrong, ila kum peti peti anafanya maajabu hilo siwezi kwa sababu sio kitu ambacho ninategemea kwa msichana mdogo na mrembo kama yeye na ninarudia kusema ni “waste of time”

Hilo la hongera ninawaachia nyie mumpatie, kwangu, bado ninaona kuna GAP na ninampa moyo the hardway
 
Ktk ndugu zako wote hakuna anaeweza kukupa mtaji wa biashara ya kande. Mie nitafute nikupe mahindi ya kuanzia. Lawama zingine hazina misingi. Neno mtaji lisitumike vibaya
 
Aisee nimesoma comments za Uzi huu nimebaki nacheka tu!
Aiseee tuna safari ndefu sana kama vijana Maana Wengi wetu inaonekana Kuna shida mahali sio bure!

Yaani hiyo kuhijiwa na blog kubwa Hapa Tanzania ni fursa kubwa sana kwake ila humu ndani mijitu inasema Eti Kuna wangapi wanafanya hizo shughuli hawajitangazi!
Kwahiyo kutojitangaza ni sifa??[emoji23] [emoji23]
 
Dada wa Kande asubuhi akiamuka anenda ofisini kwake. ni Mwanamke na hafanyi kazi ya mwana mme au mwana mke mwenzake.

Sasa nashangaa Sisi wenye Kufanyia kazi wanaume wenzetu ndo mabingwa wa kuponda ila wale wanao amka asubuhi n kwenda kutekeleza idea zao wenyewe ndo wanao msifia

Mwanaume kama una fanya kazi kwa mwanaume mwenzako then una mponda Mwanamke ambaye yeye anafanya kazi kwake mwenye basi una matatizo makubwa sana.


Yaani Sisi waajiriwa ndo mabingwa wa kukosoa biashara za watu kwamba Oo anajidhalilisha, ana Degree kwa nini auze kande.

Wewe mbona na usomi wako una fanya kazi ya mwanaume mwenzako? ni mara hata 100 wanawake ndo wamponde mwanamke mwenzao ila sio Sisi Wanaume tunao fanya kazi kwa wanaume wenzetu.

NI LITARAJIA WAFANYA BIASHARA AKA WAJASIRIANALI NDO WAMPONDE DADA ILA SASA NI KINYUME CHAKE

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukuru kwa uwezo ulionao, huyo Dada tuu umesema ni mtoto wa kishua. Then haitokaa itokee watu wote kujiajiri, huyo Dada mwenyewe kuna watu kawaajiri , ukiwa na maduka yako 10 utauza yote pekeyako? ni lazima uajiri watu,hivo concept ya kuponda walioajiriwa wakati umeajiri watu ni nonsense, huyo Dada nampongeza kwa kujiajiri na kuajiri wengine,. Ndo dunia ilivogawanyika , ndo maana kuna wabeba mizigo, mainjinia, madaktari, walimu, wanasheria, wote tunategemeana hivo ukiona umefanikiwa usione wengine kwamba hawawezi kutumia fursa, la hasha ni nature ndo ipo hivo, hakuna asiyependa maisha mazuri,, kama una maisha mazuri shukuru kwa ulicho jaliwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom