Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KITABU CHA BIUBWA: KARUME, BIUBWA NA BARUA YA ENGEN
Kitabu "Mwanamke Mwanamapinduzi," kinachohadithia maisha ya Biubwa Amour Zahor ni, "thriller," katika viwango vya James Bond.
Zuhura Yunus mwandishi wa kitabu hiki kaifanyia hisani kubwa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.
Mwisho wa kitabu Zuhura Yunus anakipasua kichwa chake na katika kufanya hivyo anatupasua hata na sisi wasomaji wake pale anapopitia maisha ya Biubwa toka udogoni katika usichana hadi kufikia sasa ni mwanamke na ana akili zake kamili.
Hapa ni baada ya mapinduzi na Biubwa kampoteza baba yake kwa kuuliwa akiwa kifungoni.
Kifo hiki ni kilele cha hadithi ya kusikitisha katika maisha ya Biubwa.
Zuhura Yunus sasa ni kama vile anatuambia wasomaji wake tukisome kitabu cha maisha ya Biubwa huku tukitafakari kila neno aliloandika katika mstari kupata kile ambacho huenda labda kimejificha.
Kwa hakika ikiwa msomaji hatofanya hivyo atakuwa kajipunja mwenyewe.
Kukifaidi kitabu hiki msomaji lazima aingie na atembee tena kwa utulivu, atembee kwa miguu yake mwenyewe katikati ya kila mstari anaosoma ndani ya kitabu hiki.
Hakuna njia ya pili.
Angalia mkasa huu wa Mzee Karume na Engen.
Okello, Engen na wenzake walikamilisha kazi yao na Mzee Karume akawaahidi kuwapa ujira wao kwa maandishi.
Hapa ndipo Engen alipopokea barua yake kutoka kwa Mzee Karume.
Sijui kwa nini Zuhura Yumus hakuita hii barua kuwa ni mkataba kati ya Karume na Engen.
Barua hii kwa vyovyote vile itakavyokuwa kwa Engen kwanza ilikuwa mfano wa yeye kupewa mgodi wa dhahabu.
Pili barua ile ilikuwa ushahidi tosha kwa yote yaliyopitika Zanzibar kufanikisha mapinduzi Engen akiwa muhusika mkuu.
Lakini kubwa na sijui kama Engen alilitambua ni kuwa barua ile ilikuwa mkataba wa yeye na wenzake mfano wa yeye kuua watu kwa ajili ya fedha.
Akiwa amekikalia kiti barabara Karume hakuwa na nia ya kutimiza ahadi yake si kwa Engen, John Okello au yeyote yule.
Karume aliitaka barua yake irejeshwe kwake kwa njia yeyote ile.
Nani shujaa anaemwamini anaeweza kufanya kazi hii?
Hapa ndipo Waingereza wana msemo.
Msomaji wa kitabu hiki, "will have to burn the midnight oil."
Karume hakumwamini hata Mussa Makungu Mkuu wa Usalama wa Baraza la Mapinduzi wala hakuiamini ile, "Kamati ya Watu 14," ya Seif Bakari.
Karume aliomba msaada wa Biubwa amrejeshee barua yake.
Huu ni mfano wa, "The Tamarind Seed," na lile "Blue File," la Warusi lililotakiwa na Waingereza.
Hapa ndipo Zuhura Yunus mwandishi aliyetuandikia hiki kitabu alipotokwa jasho yeye na kwa "roho yake mbaya," akaona asife peke yake atuchukue na sisi katika safari yake hii ya mwisho.
Zuhura alipokuwa sasa hayuko tena na Biubwa bali yuko peke yake anamtafakari Biubwa Mwanamapinduzi anataka ayajue yale ambayo bila shaka Biubwa hakumweleza.
Biubwa si mwanamke mwananapinduzi wa kawaida.
Wanafunzi wa historia ya Zanzibar wamepewa zawadi kubwa katika kitabu hiki.
Kitabu "Mwanamke Mwanamapinduzi," kinachohadithia maisha ya Biubwa Amour Zahor ni, "thriller," katika viwango vya James Bond.
Zuhura Yunus mwandishi wa kitabu hiki kaifanyia hisani kubwa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.
Mwisho wa kitabu Zuhura Yunus anakipasua kichwa chake na katika kufanya hivyo anatupasua hata na sisi wasomaji wake pale anapopitia maisha ya Biubwa toka udogoni katika usichana hadi kufikia sasa ni mwanamke na ana akili zake kamili.
Hapa ni baada ya mapinduzi na Biubwa kampoteza baba yake kwa kuuliwa akiwa kifungoni.
Kifo hiki ni kilele cha hadithi ya kusikitisha katika maisha ya Biubwa.
Zuhura Yunus sasa ni kama vile anatuambia wasomaji wake tukisome kitabu cha maisha ya Biubwa huku tukitafakari kila neno aliloandika katika mstari kupata kile ambacho huenda labda kimejificha.
Kwa hakika ikiwa msomaji hatofanya hivyo atakuwa kajipunja mwenyewe.
Kukifaidi kitabu hiki msomaji lazima aingie na atembee tena kwa utulivu, atembee kwa miguu yake mwenyewe katikati ya kila mstari anaosoma ndani ya kitabu hiki.
Hakuna njia ya pili.
Angalia mkasa huu wa Mzee Karume na Engen.
Okello, Engen na wenzake walikamilisha kazi yao na Mzee Karume akawaahidi kuwapa ujira wao kwa maandishi.
Hapa ndipo Engen alipopokea barua yake kutoka kwa Mzee Karume.
Sijui kwa nini Zuhura Yumus hakuita hii barua kuwa ni mkataba kati ya Karume na Engen.
Barua hii kwa vyovyote vile itakavyokuwa kwa Engen kwanza ilikuwa mfano wa yeye kupewa mgodi wa dhahabu.
Pili barua ile ilikuwa ushahidi tosha kwa yote yaliyopitika Zanzibar kufanikisha mapinduzi Engen akiwa muhusika mkuu.
Lakini kubwa na sijui kama Engen alilitambua ni kuwa barua ile ilikuwa mkataba wa yeye na wenzake mfano wa yeye kuua watu kwa ajili ya fedha.
Akiwa amekikalia kiti barabara Karume hakuwa na nia ya kutimiza ahadi yake si kwa Engen, John Okello au yeyote yule.
Karume aliitaka barua yake irejeshwe kwake kwa njia yeyote ile.
Nani shujaa anaemwamini anaeweza kufanya kazi hii?
Hapa ndipo Waingereza wana msemo.
Msomaji wa kitabu hiki, "will have to burn the midnight oil."
Karume hakumwamini hata Mussa Makungu Mkuu wa Usalama wa Baraza la Mapinduzi wala hakuiamini ile, "Kamati ya Watu 14," ya Seif Bakari.
Karume aliomba msaada wa Biubwa amrejeshee barua yake.
Huu ni mfano wa, "The Tamarind Seed," na lile "Blue File," la Warusi lililotakiwa na Waingereza.
Hapa ndipo Zuhura Yunus mwandishi aliyetuandikia hiki kitabu alipotokwa jasho yeye na kwa "roho yake mbaya," akaona asife peke yake atuchukue na sisi katika safari yake hii ya mwisho.
Zuhura alipokuwa sasa hayuko tena na Biubwa bali yuko peke yake anamtafakari Biubwa Mwanamapinduzi anataka ayajue yale ambayo bila shaka Biubwa hakumweleza.
Biubwa si mwanamke mwananapinduzi wa kawaida.
Wanafunzi wa historia ya Zanzibar wamepewa zawadi kubwa katika kitabu hiki.