Bob Chacha Wangwe naye atema ya moyoni, aungana na Lissu, japo mbowe ndiye rafikiye mkubwa!

Bob Chacha Wangwe naye atema ya moyoni, aungana na Lissu, japo mbowe ndiye rafikiye mkubwa!

Wanaoumia wote ni chawa wa Ccm, vyama gani vingine vinavyopiga debe kwamba Mbowe ni masta? Vile vya mfukoni vinasubiri script toka Lumumba ndo viongee hapo badaye! Kwa ss ni uvccm kila nusu saa kuna uzi mpya hapa
nadhani wale watakao kataliwa na wajumbe wa mkutano mkuu Taifa wa chadema ndio watakao umia zaidi gentleman,

wasio husika hawatababaika na ushirikina wa watu wengine 🐒
 
Mimi naogopa sana kuweka matumsini kwa binadamu.lissu watu wanamwamini sana ila nina wasiwasi atakuja kuwastaajabisha.namwona ni mtu wakuongea zaidi hisia.Siasa zake nizaharakati zaidi badala ya hoja zakijamii zinazohitaji staha kuziendea.Ngoja tuone kwasababu wote wako na haki kulingana na katiba ya chama chao.Uku nje sisi niwachochea kuni tu bila kujua kilichoko ndani ya chungu.
Sasa shida iko wapi?
Akivuruga si anabwagwa miaka mitano ijayo?
Hio ndio faida ya Demokrasia.
 
nadhani wale watakao kataliwa na wajumbe wa mkutano mkuu Taifa wa chadema ndio watakao umia zaidi gentleman,

wasio husika hawatababaika na ushirikina wa watu wengine 🐒
Wanaofanya big deal ni uvccm hao wajumbe wala hawana habare mkuu!
 
Bob Wangwe ameongea fact!

Samia akitaka kubadili katiba kuongeza muda wa utawala, CHADEMA ya Mbowe haitokuwa na moral authority ya kumpinga maana mwenyekiti wao si mfano mwema!
 
Mtoto wa Makamu mwenyekiti wa Chadema aliyekufa ajalini hayati Chacha Wangwe amesema huu ni wakati wa Tundu Lisu

Bob Wangwe amesema Mzee Mbowe sasa apumzike
 
Hivi wanaposema vijana taifa la kesho, wanawajumuisha na vijana wa chadema?
 
Kwa Watanzania na Wanamageuzi wenye mapenzi mema na CHADEMA na Taifa letu. Kwa vijana wanaotamani kufanya siasa za Upinzani kwa miongo kadhaa ijayo. Lissu is the way! Hawezi kuwa mkamilifu kama Binadamu, lakini ana sifa muhimu kwa maslahi ya CHADEMA na Taifa. Kwa kizazi hiki watu wa aina yake ni wachache sana. Lissu kuwa Mwenyekiti wa Chadema, haiwezi kuwa habari njema kwa Watawala. Huyu ndiye mtu sahihi.

Tutakuwa na wakati mgumu sana katika kufanya siasa kama atashinda mtu mwingine zaidi ya Lissu. Mfano, ikitokea Mhe Mbowe ametetea kiti chake, kule Bungeni kesho kutwa kina Kibajaji wakipeleka Muswada wa kuondoa ukomo wa Urais tutakuwa na hoja gani za kutetea ukomo? Zipo hoja nyingi ambazo tutakosa uhalali wa kuzisemea. Tuwaunge mkono tunaowapenda lakini tufikirie pia uendelevu wa chama (sustainability) baada ya Uchaguzi.

Natambua uwezo na mchango mkubwa wa Mhe. Mbowe na nikiri tu tumekuwa na ukaribu kuliko ukaribu wangu na Mhe. Lissu lakini kwa maslahi mapana ya Chama ambacho amekijenga kwa gharama kubwa, naona Lissu anatosha kabisa kumpokea kijiti cha Uenyekiti hasa kwa wakati huu ambao tuko kwenye matatizo makubwa ya Kidemokrasia. Morali za watu wetu iko chini hasa baada ya kuumizwa na mifumo ya Uchaguzi. Kwa mazingira haya, mabadiliko ni muhimu ili kuirejesha.

Lissu akishinda tutakuwa na timu kamili (Mwenyekiti Mbowe atabaki kuwa Mzee wa Chama mjumbe wa kudumu wa Kamati kuu ya Chama). Hivyo, bado atakuwa na nafasi ya kujenga Chama. Waliorudi nyuma kisiasa naamini watarudi kazini na wasioitakia mema CHADEMA wataona aibu sana.
Habari ya kuwa ‘neutral’ ni unafiki! Mimi niko na Lissu! Tufanye kampeni za Kistaarabu wote hawa ni viongozi wetu ili tuendelee kutoa somo kuwa chama chetu ni cha Kidemokrasia.
View attachment 3184410
Hivi ndivyo alivyo andika Wakili Msomi?

Amandla...
 
Back
Top Bottom