The Sunk Cost Fallacy
JF-Expert Member
- Dec 1, 2021
- 19,582
- 14,167
Bora kawachana,unajua Chadomo wanadhani Katiba mpya itawasukumiza Ikulu kama mlevi huku ccm ikihofia kivuli tuu..Wakati hoja ya Katiba Mpya ikitawala mijadala na hotuba za viongozi mbalimbali katika Baraza Kuu la CHADEMA,
mwanasiasa wa upinzani kutoka nchini Uganda ambaye
alikuwa mgeni rasmi kwenye baraza hilo amesema katiba
mpya pekee haiwezi kuwa mwarobaini wa matatizo.
Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine ambaye ni kiongozi wa chama cha National Unity Platform amesema ni wazo zuri kuwa na katiba mpya, lakini isichukuliwe kama ndio itamaliza matatizo yote kwenye nchi husika.
Uganda tuna katiba nzuri sana, naweza kusema moja ya
katiba bora zaidi duniani licha ya kuwa Jenerali [Rais YowerilMuseveni amebadili katiba mara nyingi sana. Katiba yetuhaiheshimiwi, sheria nchini Uganda ni nzuri tu kama ilivyokwenye karatasi ilimoandikwa" ameeleza.
Akitoa mbadala wa hayo amesema kuwa ni lazima kuwajengea uwezo wananchi waweze kuisimamia katiba ambayowanakusudia kuwa nayo.
Ametoa wito kwa CHADEMA kuwashawishi vijana zaidi
kushiriki kwenye shughuli za kisiasa kwani Afrika ni bara
changa, na hivyo hatma ya Afrika ipo mikononi mwao, kwa wao kujua ni wapi wanakusudia kwenda.
************†**********†************†*****************†
Dkt Slaa alituambia tusije tukawaaminishi wananchi kuwa Katiba Mpya ndiyo kila kitu.View attachment 2220695
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa Tzn ukiwaambia wamama kwamba wapinzani wanahatarisha amani,hapo tayari kula zote wanazoa..