Godman
JF-Expert Member
- Jun 23, 2013
- 423
- 650
Mkuu, sasa kama Watu tunaowategemea watuongoze kwenye kudai hiyo Katiba ndiyo hawa wanaopigia magoti Watawala,! Sidhani kama Katiba mpya itapatikana, bado pia sioni nani ataasisi hayo machafuko ya kudai hiyo Katiba mpya.Bora iwepo kisha isiheshimiwe ili tuone. Kinachofanya katiba yetu isiheshimiwe ni hiki kitendo cha rais kuwa na madaraka makubwa kupita inavyotakiwa, kisha kupata kinga ya kikatiba asishitakiwe akiwa madarakani au akiwa ametoka. Hapo ndio matatizo yote yanapoanzia. Mimi huu mjadala wa katiba mpya bila kuwa na machafuko, najua fika itapatikana katiba ambayo haitaheshimiwa. Machafuko tu ndio sahihi ya kupata katiba itakayoheshimiwa na wote.