kwa hali hiyo basi hata biashara ya meli, mabasi na ndege itakuwa marufuku!!!
Si zote.
Meli za mizigo hazikatazwi, mabasi ya kusafirisha watu ambayo yanamilikiwa na anaesafiri ( kama timu ya mpira) hayajakatazwa, ndege itategemea, zile za mizigo hazijapigwa marufuku. Kilichokatazwa kina pande mbili, ni lazima awe mtu, na pilu yawe yamefanyika malipo.
Hasafiri bali anasafirishwa bilautashi na hiari yake
Sasa huyo katekwa, kidnapped! Hawaongelei kuteka hapa, wangesema.
Anakuwa binadamu lakini utu wake unaondolewa kabisa na kuvishwa daraja la UTUMWA
Hiyo sasa Slave Trade, biashara ya utumwa! Hawajasema biashara ya utumwa marufuku, ila biashara ya kusafirisha binadamu.
Biashara ya kusafirisha viumbe hai(hapo binadamu hahusishwi, wamo Twiga simba ndege, nyoka,smaki na hata bacteria)
Hiyo ni biashara ya kusafirisha wanyama! Kwa swala la Twiga, ni usafirishaji wa nyara za serikali.
linasisitiza uharamia dhidi ya binadamu.
Uharamia unaongeza wewe. Wangetaka wangesema uharamia, hawajasema wamekataza uharamia dhidi ya binadamu, wamesema tatizo ni biashara ya kusafirisha binadamu!
Biashara ya kusafirisha BINADAMU ni tofauti kabisa na Biashara ya kusafirisha ABIRIA..... Kwa kawaida na katika mazungumzo ya kawaida, usafiri wa daladala ndege au bodaboda unaitwa kusafirisha watu na katika kiswahili fasaha huitwa kusafirisha abiria.
Huwezi kusema "kusafirisha abiria."
Abiria ni mtu anaesafirishwa, kwa hiyo ni kiswahili kibovu kusema "kusafirisha mtu anaesafirishwa"! Ndio maana hawakusema wanapiga marufuku biashara ya kusafirisha abiria, bali binadamu.
Neno abiria ndilo neno mahususi katika biashara halali ya kusafirisha watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Abiria haihusiani na biashara. Unapompa jirani yako hisani ya kumbeba kwenye gari lako mkielekea eneo moja moja huyo ni abiria wako! Daladala halisafirishi abiria, linapandisha abiria, lakini halisafirishi abiria, linasafirisha umma.
Kama rasimu itapita kama ilivyo utakuwa wakati mgumu sana kwa wengi. Wanaotegemea shughuli za biashara hii na pia wananchi tusio na vyombo vyetu vya usafiri tupeleke vilio vyetu kwa watunga katiba.