Bodaboda ni kero kubwa na chanzo cha ajali kwenye Zebra ya Msimbazi Kariakoo ambazo zimefutika

Bodaboda ni kero kubwa na chanzo cha ajali kwenye Zebra ya Msimbazi Kariakoo ambazo zimefutika

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
photo_2024-06-17_08-57-02.jpg
Mamlaka za Jiji kwa kushirikiana na Kitengo cha Usalama Barabarani (Polisi) waangalie kwa jicho la tatu namna Bodaboda wanavyotumia vibaya kipande cha Mwendokasi eneo la Msimbazi la Kariakoo, Dar es Salaam.

Bodaboda wamekuwa kero kubwa na kusababisha ajali za mara kwa mara kwenye njia hiyo kutokana na kuwa na uharaka ambao hauzingatii Usalama wa Raia.

Kibaya zaidi alama maarufu kama 'Zebra' kwenye kipande hicho zimefutika jambo ambalo limeongeza kero zaidi na kufanya Bodaboda wengi washindwe kusimama au kupunguza mwendo kasi, huku abiria wakiwa wanakatiza eneo lolote.
photo_2024-06-17_08-57-00.jpg

photo_2024-06-17_08-57-03.jpg
Kulingana na njia hiyo ilivyo licha ya mabasi ya mwendokasi kusimama kupisha abiria kukatiza lakini kwa bodaboda wengi wamekuwa wakiitumia njia hiyo vibaya mithiri ya kujimilikisha, pia wamekuwa wakiwapa wakati magumu madereva wa mwendokasi kuepusha ajali huku na wao wenyewe kujiweka katika mazingira hatari.

Ni vyema mamlaka za Jiji zikaiona kero hiyo na kushirikiana na Askari wa Barabarani 'Traffic' kuweka utaratibu rafiki ambao utaondoa kero hiyo hususani kuweka vibao vya msisitizo kwa bodaboda kuzingatia usalama wa raia pamoja na usalama wao binafsi inapotokea wametumia njia hiyo kwa dharura.

Pia alama za zebra kwenye eneo hilo ni vyema zikakolezwa zaidi ili ziweze kuonekana kwa uharaka jambo ambalo litasaidia wananchi kutokatiza ovyo ovyo kwenye kipande hicho chenye harakati nyingi pande zote mbili.

Bila kuwajibika kuchukua hatua tutaendelea kuwa tunaweka hatarini maisha ya raia wengi na inweza kuja kutokea janga kubwa zaidi ambalo kimsimgi kutowajibika kwetu kwa wakati inaweza kuwa kisababishi.
 
Back
Top Bottom