KERO Bodaboda wa Tanzania wameshindikana kwa tabia zao barabarani au wameendekezwa?

KERO Bodaboda wa Tanzania wameshindikana kwa tabia zao barabarani au wameendekezwa?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

mlinzi mlalafofofo

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2008
Posts
725
Reaction score
1,282
_123614664_boda2.jpg.jpg

Sasa hivi jamaa wanaleta vitimbi vyao hadharani na hamna kitu unaweza kuwafanya.

Ni kama wana utawala wao wapo Dunia yao isiyo na Sheria. Wao ndio mabingwa wa kubebana mishikaki na kuchomekea wengine kwa mbele kwa kisingizio cha wana haraka.

===========

Bodaboda sehemu nyingi hawakai kwenye foleni, hata kwenye Taa za Barabarani wao wanachoangalia ni kwamba kuna kikao? Kama hakuna wanaamsha na kupita bila kujali ni zamu ya upande wao au la!

Wanapita sehemu ambazo sio wanazotakiwa kupita, mfano kwenye njia ya Mwendokasi au kwenye service Road tena wakiwa speed.

Ukienda kwenye vituo vya Afya kama vile MOI, unakuta watu wengi wakiwa na majeraha makubwa na wengine wamepoteza maisha wengine wamekuwa na ulemavu wa kudumu kutokana tu na tabia zao ambazo ni chanzo cha ajali nyingi.
 
Bodaboda wengi hawaiheshimu kazi yao, lakini pia wanachukulia mambo ya barabarani kirahisi rahisi sana. Na wanajikuta wana haraka kuliko vyombo vyote vya usafiri hata kama anaenda kupaki tu

Unakuta boda yupo speed 70 high way au mtaani na wkt huohuo hana helmet, hajavaa viatu zaidi ya tusendo ambato katuegeshea tu kwenye miguu, hana jacket zito la kumkinga na upepo mkali, wengine wanakalia kiti kiupande ili mradi tu ajione ni mjanja... Na hawa wa hivi kuchomekea ndiyo zao

Poleni sana bodaboda wote msiojielewa, kifo na ulemavu vinawapenda sana kuliko tunavyowapenda
 
Back
Top Bottom