Bodaboda zinachangia kumomonyoka kwa maadili

Bodaboda zinachangia kumomonyoka kwa maadili

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Wakuu,

Biashara ya bodaboda imekuwa mkombozi kwa kurahisisha usafiri katika maeneo mengi nchi hii, mijini na hata nje ya miji.

Lakini pia imekuja na mambo mengi maovu, kama vile kutumika katika ujambazi na unyang'anyi ukiachilia mbali ajali nyingi zinazosababisha ulemavu wa kudumu hata vifo kwa madereva na abiria.

Hata hivyo, mada yangu inaangalia zaidi mmomonyoko wa maadili unaotokana na jinsi dereva na abiria wanavyokaribiana viungo vyao wakati wa safari. Hapa sitazingatia jinsia za abiria au dereva maana nadhani athari zake ni zile zile.

Mfano mimi ni mwanaume 😎😎, leo asubuhi nimepanda bodaboda, alipofika nikagundua amevaa boxer tu bila suruali au nguo nyingine juu yake. Kwa kuwa siko huko na sijaumbwa kumuwazia mwanaume mwenzangu, nikawaza tu, je uvaaji wa namna ile una maana gani? Je, hauwezi kuwaathiri wengine, abiria au hata dereva mwenyewe?

Na ni vipi wanaume watatu au wakati mwingine wanne wanapobanana katika style ya mishkaki! Hili nalo halina athari kweli za muda mrefu kwa watu hawa kimaadili?
 
Wakuu,

Biashara ya bodaboda imekuwa mkombozi kwa kurahisisha usafiri katika maeneo mengi nchi hii, mijini na hata nje ya miji.

Lakini pia imekuja na mambo mengi maovu, kama vile kutumika katika ujambazi na unyang'anyi ukiachilia mbali ajali nyingi zinazosababisha ulemavu wa kudumu hata vifo kwa madereva na abiria.

Hata hivyo, mada yangu inaangalia zaidi mmomonyoko wa maadili unaotokana na jinsi dereva na abiria wanavyokaribiana viungo vyao wakati wa safari. Hapa sitazingatia jinsia za abiria au dereva maana nadhani athari zake ni zile zile.

Mfano mimi ni mwanaume 😎😎, leo asubuhi nimepanda bodaboda, alipofika nikagundua amevaa boxer tu bila suruali au nguo nyingine juu yake. Kwa kuwa siko huko na sijaumbwa kumuwazia mwanaume mwenzangu, nikawaza tu, je uvaaji wa namna ile una maana gani? Je, hauwezi kuwaathiri wengine, abiria au hata dereva mwenyewe?

Na ni vipi wanaume watatu au wakati mwingine wanne wanapobanana katika style ya mishkaki! Hili nalo halina athari kweli za muda mrefu kwa watu hawa kimaadili?
Mhhh!! Hivi inawezekana kweli mtu avae boxer tu bila suruali au nguo nyingine juu yake!!! Ulitakiwa utafute boda boda nyingine bila shaka, kwa usalama wako.
 
Mhhh!! Hivi inawezekana kweli mtu avae boxer tu bila suruali au nguo nyingine juu yake!!! Ulitakiwa utafute boda boda nyingine bila shaka, kwa usalama wako.
Ndiyo aisee! Ila ninapoishi huku hawa bodaboda sijui wanatuchukuliaje?

Juzi juzi asubuhi asubuhi hivi, mwingine amefika kabla sijapanda, namcheki usoni naona ana michirizi ya udenda kwenye mashavu. Yaani hata kunawa uso, hamna kitu!
 
Shida sio bodaboda, shida ni baadhi ya watumiaji wa bodaboda zina faida nyingi sana ukizitumia vizuri.

Hata smart phone pia zinasababisha sana mmomonyoka wa maadili zikitumika vijana lakini zikitumika vizuri huwa zinasaidia sana na zinafaida nyingi.
 
Uko sawa sawa kichwani? Au unataka kututangazia biashara yako?
 
Mmh! Sijui sijakuelewa vizuri? Yaani bodaboda anaendesha huku akiwa kavaa boxer tu mchana kweupe, ni mzima wa akili kweli huyo? na wewe ukapanda kabisa bila wasiwasi duh!
 
Mawazo yako ndo maisha yako katika hilo sikuungi mkono, unaweza karibiana kabisa ila kama hujawaza kuhusu ngono hauathiriki chochote, ni kweli bodaboda imechangia mmomonyoko wa maadili ila sio kwa mtazamo uliozungumza wewe
 
Umekubali vipi kupanda bodaboda ya mtu ana boxer tu!?
Nalog off
 
Back
Top Bottom