Bodi ya mikopo ni kero kubwa kwa wanafunzi nayo imejigeuza mhimili

Bodi ya mikopo ni kero kubwa kwa wanafunzi nayo imejigeuza mhimili

Tulimumu

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2013
Posts
14,409
Reaction score
13,262
Ukweli ni kuwa hii tasisi ni kero kubwa kwa wanafunzi kutokana na usumbufu wanaopata wanafunzi na wazazi. Wanafunzi walishajaza maombi lakini Bodi sasa imeanza kuleta masharti kama mganga wa kienyeji mara wanafunzi wanaambiwa walege nyaraka zile zile ambazo washaziwasilisha kwaajili ya mikopo kwa kile wanachokiita kukata rufaa.

Rais alisha tamka hakuna mwanafunzi atakaye kosa mikopo lakini hali ilivyo sivyo hata wale wanafunzi waliowekewa vipaumbele kwa maana ya wasichana wanaosoma sayansi sasa nao wananyimwa mikopo. Mwanafunzi anapoambiwa akate rufaa wakati yupo nje ya chuo na wakati huo huo wenzake wanaendelea na masomo ni dhambi kubwa na kumpotezea muda. Rufaa yenyewe inatakiwa ithibitishwe na chuo na wakati huo huo chuo wanakataa kuthibisha kwakuwa mwanafunzi ili asajiliwe lazima alipe nusu ya ada. Mimi naona sehemu ambapo rais anapaswa sasa kuingia na kuwafutilia mbali viongozi ni hapo bodi ya mikopo.

Kusema wanafunzi wakate rufaa maana yake pesa ipo isipokuwa nao wanataka kujimwambafai kwa kuongeza urasimu. Watu washaomba mikopo halafu wanaambiwa wakate rufaa kana kwamba walikuwa na kesi wakashindwa. Mimi namuomba rais hebu aende pale loan board kwa ghafla na kuwatimua wote pale waende waka kae na wake zao nyumbani wanasumbua sana wanafunzi. Haiwezekani rais anasema pesa zipo na nchi hii ni tajiri halafu wanatokea wa kumkwamisha ili aonekane ni mwongo. Loan board kwakweli ni shida sana kwa wanafunzi.
 
Ukweli ni kuwa hii tasisi ni kero kubwa kwa wanafunzi kutokana na usumbufu wanaopata wanafunzi na wazazi. Wanafunzi walishajaza maombi lakini Bodi sasa imeanza kuleta masharti kama mganga wa kienyeji mara wanafunzi wanaambiwa walege nyaraka zile zile ambazo washaziwasilisha kwaajili ya mikopo kwa kile wanachokiita kukata rufaa.

Rais alisha tamka hakuna mwanafunzi atakaye kosa mikopo lakini hali ilivyo sivyo hata wale wanafunzi waliowekewa vipaumbele kwa maana ya wasichana wanaosoma sayansi sasa nao wananyimwa mikopo. Mwanafunzi anapoambiwa akate rufaa wakati yupo nje ya chuo na wakati huo huo wenzake wanaendelea na masomo ni dhambi kubwa na kumpotezea muda. Rufaa yenyewe inatakiwa ithibitishwe na chuo na wakati huo huo chuo wanakataa kuthibisha kwakuwa mwanafunzi ili asajiliwe lazima alipe nusu ya ada. Mimi naona sehemu ambapo rais anapaswa sasa kuingia na kuwafutilia mbali viongozi ni hapo bodi ya mikopo.

Kusema wanafunzi wakate rufaa maana yake pesa ipo isipokuwa nao wanataka kujimwambafai kwa kuongeza urasimu. Watu washaomba mikopo halafu wanaambiwa wakate rufaa kana kwamba walikuwa na kesi wakashindwa. Mimi namuomba rais hebu aende pale loan board kwa ghafla na kuwatimua wote pale waende waka kae na wake zao nyumbani wanasumbua sana wanafunzi. Haiwezekani rais anasema pesa zipo na nchi hii ni tajiri halafu wanatokea wa kumkwamisha ili aonekane ni mwongo. Loan board kwakweli ni shida sana kwa wanafunzi.
Nimeishia hapa... "rais katamka.. "

Mkuu tumia akili acha mihemko. Huyo unayesema katamka ndiye tatizo lenyewe.

Poleni sana kwa kusoma awamu ya wanyonge. Enzi za jk ilikua mkopo ni uhakika.
 
Naskia watoto wengi hawajaenda shule sababu ya mkopo

Inasikitisha sana..!!
 
Ivi kumbe.kuna watu uwa wana yaamini maneno ya yule bwana akiwa jukwaani [emoji28][emoji28]
 
Ivi kumbe.kuna watu uwa wana yaamini maneno ya yule bwana akiwa jukwaani [emoji28][emoji28]
Ndio maana nikamshauri mleta mada asiwe mpumbavu kwa kutumia mihemko kumsikiza mzee meko akiwa jukwaani, maana vingi anavyoongea ni fix!
 
Wakuu me mwenyewe mhanga wa hili.Hadi sasa sijasajiliwa chuoni halafu bado bodi kukata rufaa wanahitaji ile fomu ya rufaa isainiwe na dean of studies wa chuo husika.Mwaka Jana sikwenda chuo sababu ya mkopo na na mwaka huu naelekea kubaki kwa kukosa mkopo na wazazi hawana uwezo wa kunisomesha chuo.Yani everything is a mess sielewi naelekea wapi na mustakabali wangu wa elimu hata siuelewi.
 
Write your reply...sisi wengine tulikosa mwaka jana tukajimwambafai tukauza viwanja sasa cha mtema kuni nimekiona najuta nimetia umaskini familia sasa nimewaacha chooni kwani na mwaka uhu nshakosa uo mkopo na sheria ya kuairisha mwaka poa nayo lazima ulipe nusu ada ndo ufanye hivo na sina ata mia so nadisco kisheria sababu usajir unakarbia fungwa na sijasajir wala kuairisha mwaka nadsco kwa sheria inauma nimepoteza mwaka na kuzidisha umaskini kwa familia eli ningefeligi darasa la 4 mapema
 
Write your reply...sisi wengine tulikosa mwaka jana tukajimwambafai tukauza viwanja sasa cha mtema kuni nimekiona najuta nimetia umaskini familia sasa nimewaacha chooni kwani na mwaka uhu nshakosa uo mkopo na sheria ya kuairisha mwaka poa nayo lazima ulipe nusu ada ndo ufanye hivo na sina ata mia so nadisco kisheria sababu usajir unakarbia fungwa na sijasajir wala kuairisha mwaka nadsco kwa sheria inauma nimepoteza mwaka na kuzidisha umaskini kwa familia eli ningefeligi darasa la 4 mapema
Pole sana ndio maisha ..........dont give up
 
Back
Top Bottom