Boeing imepata hasara kubwa, yaamua kupunguza wafanyakazi 17,000 na kusimamisha uzalishaji wa baadhi ya matoleo ya ndege zake

Boeing imepata hasara kubwa, yaamua kupunguza wafanyakazi 17,000 na kusimamisha uzalishaji wa baadhi ya matoleo ya ndege zake

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Oct, 11, 2024
"Tunalazimika kupunguza idadi ya wafanyakazi wetu ili kuendana na uhalisi wa hali yetu ya kifedha."
—Kelly Ortberg (Boeing CEO)
Wafanyakazi watakaopunguzwa ni 17,000 ambayo ni sawa na 10% ya wafanyakazi wote. Na hii itaathiri wafanyakazi katika ngazi zote kuanzia executives, managers na wafanyakazi wengine.

KUSIMAMISHA UTENGENEZAJI NA UCHELEWASHAJI WA BAADHI YA MATOLEO YA BOEING
Akizungumzia matoleo ambayo wana mpango wa kusimamisha utengenezaji wake, Ortberg alisema Boeing 767 freighter itaachwa kuzalishwa kufikia mwaka 2026 baada ya kumaliza order ya ndege 29 za mteja wa mwisho.

Kumekuwa na kusuasua kwa uzalishaji tangu Sept 13 kufuatia mgomo wa wafanyakazi 33,000 wa kampuni hiyo wakidai ongezeko la mishahara, wakipinga vigezo vipya vya mikataba ya kazi na wengine wakidai retirement benefits. Yote hayo yameifanya Boeing iwe na weak financial position.

Mgomo huo pia umechangia kucheleweshwa uzalishaji wa ndege za 737 Max na 777x iliyopelekea kuchelewesha kufanya delivery kwa wateja wao kwa wakati.

HASARA NA DENI
KITENGO CHA COMMERCIAL JETS
  • Kwa sasa Boeing ina deni la $60 billion na kufikia nusu ya mwaka huu imepata hasara ya zaidi ya $7 billion.​


KITENGO CHA DEFENSE, SPACE & SECURITY
  • Kitengo hiki kimeripoti hasara ya $2 billion. Ikumbukwe hiki ndio kitengo ambacho kilipewa kandarasi na NASA ya kutengeneza Starliner capsule na kuwapeleka wanaanga wawili wa NASA kwenye Kituo cha Anga cha Kimataifa (ISS) na kushindwa kuwarudisha mpaka leo. Boeing inatarajia hasara kubwa zaidi katika kitengo chake cha defense kutokana na mgomo unaoendelea.​

UBORA NA USALAMA WA NDEGE ZA BOEING
Bwana Ortbrerg amekiri kuwa kuna shida upande wa ubora na usalama wa ndege zao, na watalifanyia kazi hilo.

"Boeing inaendelea kuzingatia usalama na ubora kwa wateja."
—Kelly Ortberg (Boeing CEO)​

FIDIA NA FAINI
Wakati hayo yakiendelea mahakama jijini Texas imeitaka Boeing pia kuzilipa fidia familia 346 za wahanga wa ndege zao za 737 MAX zilizopata ajali mwaka 2018 na 2019 kwa sababu ya hitilafu. Boeing wamesema wako tayari kulipa kiasi cha $487 million kwa familia hizo.

Boeing imekubali pia kutumia $455 million kuboresha usalama huku ikisimamiwa na mahakama na waangalizi huru.


MIPANGO YA BOEING YA KUONGEZA MAPATO
Boeing inapaswa kukusanya kitita cha $10 billion kupitia uuzaji wa hisa na dhamana. Je, itawezekana kupata kiasi hicho? Bad news baada ya tangazo la CEO hisa za Boeing zimeshuka katika soko la hisa.


Baada ya U.S automobile industry kupoteza global hegemony kama vile Ford na GM kupoteana kwenye global market,

sasa inaonekana U.S aerospace industry inaenda kuporomoka. Boeing is in turmoil!
 
Mkuu Mad Max naona habari mbaya za USA zinakufurahisha sana,
Kumbuka bila technology ya USA, china asingetengeneza drones.

Haya mambo sio ya kuombeana mabaya
Biashara ni ushindani, Boeing wamejifelisha wenyewe kwenye safety, ubora na innovation hata CEO amekiri

Hawajafanyiwa figisu kama Marekani wanavyoifanyia China

Ni wakati wa COMAC ya China kuchukua nafasi ya Boeing ishindane na Airbus
 
Hao wafanyakazi watakaopunguzwa, wataenda kufanya kazi wapi?
Wanarudi nyumbani

Ona CEO alichowaambia:


"Tunajua maamuzi haya yatasababisha ugumu kwenu, familia zenu , na ninatamani kwa dhati tungeepuka kuyachukua, hata hivyo, ili tuokoe biashara yetu kwa siku zijazo tunahitaji kuchukua hatua kali."
 
Serikali kamwe haiwezi ikaiacha kampuni kubwa kama Boeing ifirisike kwani ina mchango mkubwa sana kwa uchumi wa Marekani na dunia kwa ujumla.

Walifanya hivyo kwa GM na FORD kwa kuzipa ruzuku, lakini mpaka leo hizo kampuni hazijajipata kama zilivyokuwa awali
 
Hao wafanyakazi watakaopunguzwa, wataenda kufanya kazi wapi?
20240710_160635.jpg
 
Sept, 11. 2024
"Tunalazimika kupunguza idadi ya wafanyakazi wetu ili kuendana na uhalisi wa hali yetu ya kifedha."
—Kelly Ortberg (Boeing CEO)
Wafanyakazi watakaopunguzwa ni 17,000 ambayo ni sawa na 10% ya wafanyakazi wote. Na hii itaathiri wafanyakazi katika ngazi zote kuanzia executives, managers na wafanyakazi wengine.

KUSIMAMISHA UTENGENEZAJI NA UCHELEWASHAJI WA BAADHI YA MATOLEO YA BOEING
Akizungumzia matoleo ambayo wana mpango wa kusimamisha utengenezaji wake, Ortberg alisema Boeing 767 freighter itaachwa kuzalishwa kufikia mwaka 2026 baada ya kumaliza order ya 29 za mteja wa mwisho.

Kumekuwa na kusuasua kwa uzalishaji tangu Sept 13 kufuatia mgomo wa wafanyakazi 33,000 wa kampuni hiyo wakidai ongezeko la mishahara, wakipinga vigezo vipya vya mikataba ya kazi na wengine wakidai retirement benefits. Yote hayo yameifanya Boeing iwe na weak financial position.

Mgomo huo pia umechangia kucheleweshwa uzalishiaji wa ndege za 737 Max na 777 jets iliyopelekea kwa kampuni hiyo kuchelewesha kufanya delivery kwa wateja wao kwa wakati.

HASARA NA DENI
KITENGO CHA COMMERCIAL JETS
  • Kwa sasa Boeing ina deni la $60 billion na kufikia nusu ya mwaka huu imepata hasara ya zaidi ya $7 billion.​


KITENGO CHA DEFENSE, SPACE & SECURITY
  • Kitengo hiki kimeripoti hasara ya $2 billion. Ikumbukwe hiki ndio kitengo ambacho kilipewa kandarasi na NASA ya kutengeneza Starliner capsule na kuwapekeka wanaanga wawili wa NASA kwenye Kituo cha Anga cha Kimataifa (ISS) na kushindwa kuwarudisha mpaka leo. Boeing inatarajia hasara kubwa zaidi katika kitengo chake cha defense kutokana na mgomo unaoendelea.​

UBORA NA USALAMA WA NDEGE ZA BOEING
Bwana Ortbrerg amekiri kuwa kuna shida upande wa ubora na usalama wa ndege zao, na watalifanyia kazi hilo.

"Boeing inaendelea kuzingatia usalama na ubora kwa wateja."
—Kelly Ortberg (Boeing CEO)​

FIDIA NA FAINI
Wakati hayo yakiendelea mahakama jijini Texas imeitaka Boeing pia kuzilipa fidia familia 346 za wahanga wa ndege zao za 737 MAX zilizopata ajali mwaka 2018 na 2019 kwa sababu ya hitilafu. Boeing wamesema wako tayari kulipa kiasi cha $487 million.

Boeing imekubali pia kutumia $455 million kuboresha usalama huku ikisimamiwa na mahakama na waangalizi huru.


MIPANGO YA BOEING YA KUONGEZA MAPATO
Boeing inapaswa kukusanya karibu dola bilioni 10 kupitia uuzaji wa hisa na dhamana. Je, itawezekana kupata kiasi hicho? Bad news baada ya tangazo la CEO hisa za Boeing zimeshuka katika soko la hiss.


Baada ya U.S automobile industry kupoteza global hegemony kama vile Ford na GM kupoteana kwenye global market.

Sasa inaonekana U.S aerospace industry inaenda kuporomoka. Boeing is in turmoil!
Airbus wanasemaje
 
Kwanini mkuu? Sababu ni ipi?
Kuna sababu kadhaa hata kwenye uzi zimeelezwa mfano

Kuchelewa kwenye kufanya delivery order za wateja. Kuna wateja walitakiwa wafanyiwe delivery za Boeing 777x mwaka 2024 wamesogeza hadi 2026

Kuacha kutengeneza 767 ni kutokana na kukosekana kwa demand yake

Plus madeni, migomo ya wafanyakazi, kupungua kwa wafanyakazi, hasara, suala la safety, jinsi ya kuraise $10 billion n.k

Ukichanganya vyote hivyo ni bomu hilo
 
Back
Top Bottom