Bomu la Lowassa: Tumeligundua, Tunaliteguaje?

Bomu la Lowassa: Tumeligundua, Tunaliteguaje?

Nakubaliana na wazo la kila mkoa kujiwekea asilimia 50% ya mapato kwa raslimali zake na ile nyingine kwenda kwenye serikali kuu kutumika katika kuendeleza ile mikoa ambayo haina raslimali. Kwa mfano, Kahama kuna utajiri mwingi wa machimbo ya dhahabu, kama inaweza kutumia asilimia 50% kwa maendeleo yake, uchumi wa Kahama utapanuka na bila shaka Kahama itakuwa magnet kwa vijana wanaotafuta ajira badala ya kujazana Dar-es- Salaam na Arusha, wataelekea Kahama. Na pia kwa kumjibu eric cartman, tunazo raw materials nyingi tu. Tuna pamba. Tuna kahawa, tuna matunda ambayo naona Bakhressa ameanza kuyasindika ya kuyauza Malaysia. We need more of that. Watanzania si watu wa kuvaa mitumba wakati tuna pamba ya kutosha. Tunayo basis ya industrialization at a smaller scale.

Na je unadhani kunaweza kujitokeza tatizo la ukabila na ukanda na pengine siasa za kujitenga iwapo tuta pursue such a policy? na Chadema wanapozungumzia suala la majimbo, hoja yao ya msingi ni nini, utawala (kusogeza mamlaka kwa wananchi zaidi)?uchumi? au vyote? Samahani nakuuliza kuhusu Chadema just incase una ufahamu juu ya hilo, mimi sina uelewa sana wa hilo na sijapata sehemu ya kulisoma kwa undani, vinginevyo sina maana kwamba wewe ni msemaji wa chadema au kitu karibia na hicho;
 
Na je unadhani kunaweza kujitokeza tatizo la ukabila na ukanda na pengine siasa za kujitenga iwapo tuta pursue such a policy? na Chadema wanapozungumzia suala la majimbo, hoja yao ya msingi ni nini, utawala (kusogeza mamlaka kwa wananchi zaidi)?uchumi? au vyote? Samahani nakuuliza kuhusu Chadema just incase una ufahamu juu ya hilo, mimi sina uelewa sana wa hilo na sijapata sehemu ya kulisoma kwa undani, vinginevyo sina maana kwamba wewe ni msemaji wa chadema au kitu karibia na hicho;
Nadhani wazo la Chadema kuhusu majimbo ni sawa na wazo lako la kila jimbo kufaidi raslimali zake. Pia ni kupunguza serikali kuu (Dar-es-Salaam) kuwa kituo cha kila uamuzi. Nakumbuka kuna wakati Mwalimu Nyerere alianzisha utaratibu wa decentralization na kutoa mamlaka kwa utawala mikoa na maeneo kujiamulia wenyewe. Sijui zoezi hilo lilifanikiwa kwa kiasi gani. Ningependa kuona Lindi na Mtwara zinafaidika na gesi iliyopatikana huko. Vile vile kwenye majimbo ya dhahabu, almasi, uranium, etc. kwa sababu hatimaye haya maeneo yatakuwa magnet kwa vijana wanaotafuta ajira na labda kupunguza uvutiaji wa Dar-es-salaam kama eneo pekee ambako vijana wanaomaliza shule wanavutiwa kuelekea. Kuhusu ukabila na ukanda, ningependa kuamini kwamba misingi ya Utanzania wetu ni imara kuliko ukabila na ukanda kiasi kwamba leo mimi nikihamia Kahama nitaonekana kama Mtanzania mwenzao badala ya kuangaliwa kwa kabila au sehemu nilikozaliwa.
 
Yani kila ninapotaka kutomgusa mzee wangu EL, nachemsha

Hivi, twaweza kuangalia au kuchambua impact ya ufisadi au greedy katika kudumaza opportunities za maendeleo?? na kama ndio? is there any research inaweza kuwa imefanyika kumuiplicate mtu au watu kwa kuchangia hilo??

i tried to ask this question to my friend (yuko pale REPOA) in 2007, lakini tulishindwa kufikia conclusion yoyote kwani hapakua na any research ya "missed opportunities created by greed individual" and in our case tulijaribu kuangalia viongozi, tukasechi Tiger countries lakini wapi

Hapa najaribu kupima mtu anayetoa angalizo kwa jambo ambalo yeye au wenzake (peer) wamechangia kuliasisi na kulikuza??
No harm intended:A S soccer:

Nadhani hili ni suala gumu, hasa ukizingatia kwamba unahitaji data kadhaa kuja na models zitazosadia kutoa jibu hilo; Vinginevyo moja ya njia za kusaidia kupata angalau mwanga wa mbali juu ya hili ni kutazama kiasi cha fedha kinachopotea kupitia TAX EVASION and CAPITAL FLIGHT kwani humo ndio mafisadi hula zaidi; Kwa mfano, kwa mujibu wa gazeti la eastafrican la mwezi juni, kila mwaka Tanzania inapoteza kiasi cha dollar bilioni moja kupitia capital flight and tax evasion; Sielewi chanzo cha hili gazeti ni nini; Lakini vile vile kwa mujibu wa utafiti wa NORAD (2011), Tanzania ilipoteza kiasi kifuatacho:


  • 2002 = $597 Million Dollars;
  • 2003 = $106 Million Dollars;
  • 2004 = $1,146 Million Dollar;
  • 2005 = $85 Million Dollars;
  • 2006 = hakuna data;
  • 2007 = $277 Million Dollars;
  • 2008 = $334 Million Dollars;

Vile vile takwimu zinaonyesha:


  • Kipindi cha 2000 - 2008 = $2,545 Million Dollars;
  • Kipindi cha 1970 - 2008 = $7,356 Million Dollars;

Nadhani iwapo tunajua tunahitaji kiasi gani kufanikisha maendeleo sekta gani au ya namna gani, tunaweza kupata angalau picha juu ya jinsi gani ufisadi kupitia capital flight na tax evasion umedumaza opportunities za maendeleo fulani fulani;
 
Nadhani wazo la Chadema kuhusu majimbo ni sawa na wazo lako la kila jimbo kufaidi raslimali zake. Pia ni kupunguza serikali kuu (Dar-es-Salaam) kuwa kituo cha kila uamuzi. Nakumbuka kuna wakati Mwalimu Nyerere alianzisha utaratibu wa decentralization na kutoa mamlaka kwa utawala mikoa na maeneo kujiamulia wenyewe. Sijui zoezi hilo lilifanikiwa kwa kiasi gani. Ningependa kuona Lindi na Mtwara zinafaidika na gesi iliyopatikana huko. Vile vile kwenye majimbo ya dhahabu, almasi, uranium, etc. kwa sababu hatimaye haya maeneo yatakuwa magnet kwa vijana wanaotafuta ajira na labda kupunguza uvutiaji wa Dar-es-salaam kama eneo pekee ambako vijana wanaomaliza shule wanavutiwa kuelekea. Kuhusu ukabila na ukanda, ningependa kuamini kwamba misingi ya Utanzania wetu ni imara kuliko ukabila na ukanda kiasi kwamba leo mimi nikihamia Kahama nitaonekana kama Mtanzania mwenzao badala ya kuangaliwa kwa kabila au sehemu nilikozaliwa.

Decentralization ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika maeneo mengi kasoro kwenye decision making juu ya masuala ya fedha; Suala hilo limebadikia kuwa centralized na ndio maana sekta ya afya, elimu, zinazidi kuwa duni kwani fedha/resources, kwanza hazitokani na input ya wahusika wa huko chini wana prioritize nini, na pili, hata hizo budgets zinazopangwa at the top, fedha hazishuki chini ipasavyo;

Kuhusu ukabila na ukanda, ningependa kuamini hivyo, lakini kuna dalili ya wanasiasa kuanza kutumia njia hizo kufanikisha malengo yao ya kisiasa; na wao kufanikisha hili huko vijijini sio kazi kwani tangia ukoloni, wanavijiji wamekuwa na misuguano na civic institutions na walifundshwa hivyo na liberation movements (TAA na TANU), na mpaka leo, wengi vijijini wapo more loyal to local and community institutions za huko maeneo yao - za kimila, utamaduni, dini n.k, kuliko civic institutions under the state;

Pamoja na ukweli kwamba TANU ilifanikiwa sana katika harakati zake kutokana na kutumia hizi local and traditional institutions, baadae Mwalimu alijaribu sana kugeuza hili, ingawa ni yeye ndiye aliwafanya wanavijiji wazikatae civic institutions za mkoloni wakati wa harakati ya uhuru; TANU iliporithi madaraka, ikaanza mradi mkubwa wa kugeuza mentality ya wanavijiji sasa waanze kuona hizi civic institutions ni muhimu kuliko local and traditional based institutions; hatukufanikiwa sana kwa hilo vijijini, ndio maana ni rahisi sana kwa mtu wa kabila lolote kupita ubunge kwenye maeneo mengi ya miji lakini vijijini kama wewe sio wa kabila la pale, utabakia na utaheshimiwa kwa citizenship yako kama mtanzania but on POLITICAL CITIZENSHIP, you will be denied;

Hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba - napenda kuamini na pia kufuata your position, ila lets not be on denial kuhusu suala hili;
 
As long as tumebinafsisha viwanda vyetu na kutochukua hatua za kuhakikisha kuwa wale waliokabidhiwa viwanda hivyo wanaendeleza shughuli za viwanda badala ya kuvibadilisha kuwa go-down tutaendelea kuwa na tatizo la ajira. Hebu niulize hivi serikali ina sera gani kuhusu viwanda na inachukua hatua gani kuhakikisha viwanda vilivyobinafsishwa vinafufuliwa? Kwa nini mpaka leo hatujajiuliza ilikuwaje Mwalimu Nyerere aanzishe viwanda karibu katika mikoa yote ya Tanzania, na licha ya kwamba vilikufa kutokana na uzembe wetu, sijamsikia mwanasiasa yeyote anayezungumzia sababu zilizopelekea kufa kwa viwanda hivyo na tunachopaswa kufanya. Hatuwezi kutegemea wawekezaji ndio wawe vyanzo vya ajira kwa vijana wetu. Serikali lazima iweke mkakati na msisitizo katika ufufuaji wa viwanda ama sivyo tutaendelea kulitizama hili bomu la ajira kwa vijana likituripukia.
Mkuu Jasusi, point muhimu sana hizi. Niongezee senti thumuni.

Tatizo la ajira tunaliona sasa na tunasahau kuwa huko nyuma lilikuwa kubwa pia.
Hatua za kutawanya viwanda(kwa maana ya viwanda vya nchi zetu) ilifanyika makusudi kabisa, kwanza kuzuia massive urbanization na pili kutoa opportunity kwa watu na wazalishaji wa sehemu husika, na mwisho kuinua maisha ya watu wa eneo husika

Karibia kila kanda ilikuwa na kitu cha kusaidia. Ninakumbuka chuma, mbolea, sabuni kule nyumbani Tanga, Mwanza na viwanda vya nguo na uchambuaji wa pamba ikiwa ni pamoja na mafuta, Morogoro, Arusha, Korosho Mtwara n.k.

Viwanda hivi vilitoa ajira kwa wananchi wote bila kuchagua mfanyakazi au mkulima kwasababu yote yanategemeana.
Soko la ndani lilikuwepo na bado lipo. Tanganyika packers walitumia Ng'ombe wa Shinyanga n.k. Je, ng'ombe hakuna kiasi cha kusema kiwanda kimekosa malighafi. Je, walaji hakuna kiasi cha sisi kuagiza nyama kutoka Brazili.
Kwanini basi Tanganyika packers ilikufa, au kiwanda cha maturubai n.k.

Endapo soko hakuna kwanini leo tuuziwe betri feki za kutumia siku moja, kwanini leo tuagize mitumba, kwanini leo tuagize vineriti kutoka Afganistan na Pakistani. Kwanini mafuta ya kulia yatoke Malaysia na kwanini sisi ni soko kubwa la EAC.

Tulikuwa na soko zuri la nje, tatizo letu tunadhani soko ni lazima liwe la Ulaya. Tuli export nguo kwa majirani zetu, General tyre ilikuwa ni kipusa, betri za Matsushita zilikuwa hot cake Kenya kwa uchache sana wa kutaja mifano.

Tulipoua viwanda tukamwathiri mkulima moja kwa moja. Pamba sasa inauzwa ''raw' kwa thamani ndogo, viwanda vya uchambuzi vimekufa, mazao yatokanayo kama mafuta ya pamba hakuna tena.
Matokeo ya yote hayo ni sub standard zilizojaa kutoka China tena zikitengenezewa uani.

Nadiriki kusema tulifika mahali ambapo tulitakiwa tuwekeze katika technology ili tuwe competetive katika world stage hata kama ni third world.

Privitization haikuweza kuepeukika kwasababu ilikuwa ni new world order chini ya IMF, WTO, WB n.k
Wala sioni tatizo na privitization. Tatizo ninaloliona ni kukosekana kwa leadership na political will.
Hili ndilo lilitengeneza loophole ya greedy and covetous leaders kugeuza mali za taifa kuwa maghala kama kule Mang'ula.
Sasa Wapogoro wa Zignal na Kidodi wanahamia mijini kutafuta mkate.

Kibaya zaidi haya yakitendeka hao wanaotabiri ukubwa wa bomu in order to score political point walikuwa ndio waandaji wa sera za kugeuza mali zetu kuwa maghala!

Elimu, hili nalo tutalijadili.
 
Nadhani hili ni suala gumu, hasa ukizingatia kwamba unahitaji data kadhaa kuja na models zitazosadia kutoa jibu hilo; Vinginevyo moja ya njia za kusaidia kupata angalau mwanga wa mbali juu ya hili ni kutazama kiasi cha fedha kinachopotea kupitia TAX EVASION and CAPITAL FLIGHT kwani humo ndio mafisadi hula zaidi; Kwa mfano, kwa mujibu wa gazeti la eastafrican la mwezi juni, kila mwaka Tanzania inapoteza kiasi cha dollar bilioni moja kupitia capital flight and tax evasion; Sielewi chanzo cha hili gazeti ni nini; Lakini vile vile kwa mujibu wa utafiti wa NORAD (2011), Tanzania ilipoteza kiasi kifuatacho:


  • 2002 = $597 Million Dollars;
  • 2003 = $106 Million Dollars;
  • 2004 = $1,146 Million Dollar;
  • 2005 = $85 Million Dollars;
  • 2006 = hakuna data;
  • 2007 = $277 Million Dollars;
  • 2008 = $334 Million Dollars;

Vile vile takwimu zinaonyesha:


  • Kipindi cha 2000 - 2008 = $2,545 Million Dollars;
  • Kipindi cha 1970 - 2008 = $7,356 Million Dollars;

Nadhani iwapo tunajua tunahitaji kiasi gani kufanikisha maendeleo sekta gani au ya namna gani, tunaweza kupata angalau picha juu ya jinsi gani ufisadi kupitia capital flight na tax evasion umedumaza opportunities za maendeleo fulani fulani;

Shkamoo mdogo wangu

You are the greatest JF contributor, sasa ntapenda tu-dwell kidogo hapo halafu tuweke simple logic.... hiyo ya kwenye red itarudi in 2009 na pia 2013-14 na itakua mbaya zaidi (maana hawana uhakika wa previous 2 election periods)

sadly trend ya 1970-2000 na sio fair tungepata ya miaka 10-10 au 5-5 ningeshukuru, but these stats are sexy, i am falling in love with them... naenda kujichimbia aisee

Now if we want to address EL bomb, basi tuna sehemu kubwa nne za kuanzia, na hiyo data ni ya pili kwa priority!!!!!

If i complain about watoto wangu hawafanyi homework, hawana madaftari na hawaendi twisheni kwani hawana ada, halafu nanyatia mfuko wa mama kupata pesa ya bia na gesti, basi I am a worse devil kwani i know that I am depriving my children their rights

I will look at private banks, mobile companies, real estate companies, and bogeymen contract in power, energy, minerals, agriculture and construction where El may have 20% plus chunk in the business and 45-55% influence at least between 2002-2010
 
Hizi ni baadhi ya changamoto muhimu ambazo serikali ya CCM au Chadema, zote zitakumbana nazo Ikulu, na ni suala ambalo lipo katika nchi zote za "dunia ya tatu"; ni muhimu katika mjadala wetu juu ya ufumbuzi wa tatizo la ajira kwa vijana tukawa na ufahamu juu ya changamoto hizi, hasa kuhusu Nini serikali inaweza kufanya, na Nini Serikali haiwezi kufanya, bila ya kujalisha ni chama gani cha siasa au mtu gani anaingia Ikulu 2015;

Hapo kwenye red umenifurahisha sana!
 
Mimi naona kitu hapa katika hoja zako hapo juu:
(1) Uwezo wa Viongozi- Hii hasa ni baada ya kushindwa katika ule mfumo wa ujamaa na tukiwa na viwanda vyetu. Baada ya huu mfumo mpya wa mixed Economy hatujapata uongozi imara unaoendana na mfumo huo. ZAidi sana wauza nchi.
(2) Mikataba ya kinyonyaji- Baada ya kushindwa katika viwanda na ujamaa wa wakati huo, kitu pekee tulichokuwa tumebaki nacho na ambacho awamu mbili za mwanzo hawakudhubutu kugusa ni madini rasilimali asili za nchi. Kama mikataba ingefungwa kwa nia njema ya uzalendo wa kiutu leo hii tusingekuwa tumeumia sana na hata hivyo viwanda vingefufuliwa kwa mtazamo mpya na siyo kuviuza kwa matapeli. Mfano. Mkataba wa Richmond.
(3) Rushwa- Ni tatizo kubwa maana limeathiri hata katika mikataba mikubwa ambayo ingelinufaisha taifa( wananchi) na kupunguza matatizo ya uchumi. Rushwa hii imejikita kwa kuanzia na kununua uongozi na katika taasisi zote za kiserikali. Inawezekana kabisa kuna wawekezaji ambao wangekuja kuwekeza katika sekta ya viwanda hapa nchini na wameshindwa kufanya hivyo kwa sababu ya rushwa ambayo imejenga urasimu mkubwa. Kiongozi anayeingia kwenye uongozi kwa rushwa awezaondoa tatizo hili?? KAma mimi mwekezaji nilianza biashara yangu kwa rushwa je, naweza pia kulipa kodi??
(4) Power - Tanzania imekuwa na tatizo la umeme kwa muda mrefu na kikubwa na maslahi binafsi katika shirika hili la Tanesco. badala ya kujenga uwezo wa kuwa na umeme wa uhakika, kikubwa kinachofanyika ni mshiko kwanza yaaani 10%. Je, mwekezaji gani anaweza kuja kuwekeza katika mazingira ambayo hakuna umeme wa uhakika??!!.
(5) Mgongano wa kimaslahi - Leo hii tumeshuhudia wafanyabiashara wakubwa katika nchi hii ni viongozi wa serikali. Je, wanaweza kufanya kazi zao zilizorasmi bila kuwa na mgongano wa kimaslahi.
(6) n.k.
 
katika unafiki wa kisiasa huu ni mmoja wapo ( ungekuwa wazi tu kuwa uko hapa kumsafisha fisadi lowasa)
 
Nadhani hili ni suala gumu, hasa ukizingatia kwamba unahitaji data kadhaa kuja na models zitazosadia kutoa jibu hilo; Vinginevyo moja ya njia za kusaidia kupata angalau mwanga wa mbali juu ya hili ni kutazama kiasi cha fedha kinachopotea kupitia TAX EVASION and CAPITAL FLIGHT kwani humo ndio mafisadi hula zaidi; Kwa mfano, kwa mujibu wa gazeti la eastafrican la mwezi juni, kila mwaka Tanzania inapoteza kiasi cha dollar bilioni moja kupitia capital flight and tax evasion; Sielewi chanzo cha hili gazeti ni nini; Lakini vile vile kwa mujibu wa utafiti wa NORAD (2011), Tanzania ilipoteza kiasi kifuatacho:


  • 2002 = $597 Million Dollars;
  • 2003 = $106 Million Dollars;
  • 2004 = $1,146 Million Dollar;
  • 2005 = $85 Million Dollars;
  • 2006 = hakuna data;
  • 2007 = $277 Million Dollars;
  • 2008 = $334 Million Dollars;

Vile vile takwimu zinaonyesha:


  • Kipindi cha 2000 - 2008 = $2,545 Million Dollars;
  • Kipindi cha 1970 - 2008 = $7,356 Million Dollars;

Nadhani iwapo tunajua tunahitaji kiasi gani kufanikisha maendeleo sekta gani au ya namna gani, tunaweza kupata angalau picha juu ya jinsi gani ufisadi kupitia capital flight na tax evasion umedumaza opportunities za maendeleo fulani fulani;

Kaka huu mwaka 2006 sijui ulikuwa na laana gani...........kwangu ulikuwa mgumu sana kimaisha
 
Mkuu Jasusi vipi ukahamia Unguja bado utaonekana mtanzania hasa baada ya tetesi upo uwezekano wa mafuta huko ?.Je hudhani hii sera ya majimbo [CDM] inaweza kupelekea mikoa ya Lindi na Mtwara kutamani kujitenga ?.

. Ningependa kuona Lindi na Mtwara zinafaidika na gesi iliyopatikana huko. Vile vile kwenye majimbo ya dhahabu, almasi, uranium, etc. kwa sababu hatimaye haya maeneo yatakuwa magnet kwa vijana wanaotafuta ajira na labda kupunguza uvutiaji wa Dar-es-salaam kama eneo pekee ambako vijana wanaomaliza shule wanavutiwa kuelekea. Kuhusu ukabila na ukanda, ningependa kuamini kwamba misingi ya Utanzania wetu ni imara kuliko ukabila na ukanda kiasi kwamba leo mimi nikihamia Kahama nitaonekana kama Mtanzania mwenzao badala ya kuangaliwa kwa kabila au sehemu nilikozaliwa.[/QUOTE]
 
Last edited by a moderator:
katika unafiki wa kisiasa huu ni mmoja wapo ( ungekuwa wazi tu kuwa uko hapa kumsafisha fisadi lowasa)

Nimsafishe Lowassa kwa lipi; I am investing in the future, not the past, pamoja na pilika pilika zao za sasa, hawa wanasiasa wote baada ya miaka 10-15 watakuwa chali kama wastaafu wakila pensheni zao, na vijana wanaojipendekeza sasa hivi wakija kuwafuata miaka hiyo watapewa jibu rahisi sana: "Mimi Mstaafu Bwana, Siwezi kukusaidia kwa hilo"; Nimewekeza katika maisha yangu throughout ili baadae nije kujisaidia mwenyewe, sio kusaidiwa na mtu, na nina amini mwenyezi mungu amenijalia na mengi, uzalendo kwa nchi yangu ikiwa ni moja ya hayo; Otherwise, for me, investing in the future begins with choosing the right side of history today;
 
Mtambuzi hoja yako imekaa vizuri ila tumpongeze lowasa kwa lipi ndugu yangu, Rushwa, kuchezea uchumi wa nchi(richmönd) au kujilimbikizia mihela isiyosaidia wtz ?...Tanzania ina kila kitu maji,madini,mafuta/gesi,ardhi,mifugo...tunae adui wa taifa mpya UBINAFSI ambaye anaturudisha kulekule ktk ujinga, maradhi na umaskini...tukiacha ubinafsi ajira zinaweza kutengenezwa/kujitengeneza eg,wtz wanaanzisha machimbo then Wabinafsi wanapeleka ffu kuwatimua na kuwapa wageni kwa kodi za kipumbafu.. Mtambuzi ubinafsi umetufikisha pahala tunadhani hatuwezi kufanya kitu..vijana wa tz wamejaa hamasa na wako tayari kwa fursa itakayojitokeza, nani wa kuonyesha njia,hapa tatizo siyo maamuzi magumu bali MAONO..imeandikwa MBINAFSI HANA MAONO kila anapoangalia ni palipo na tumbo lake tuu.. Wapo wtz wanye uwezo wa kututoa hapa..je wataruka kiunzi cha adui Ubinafsi?
 
katika unafiki wa kisiasa huu ni mmoja wapo ( ungekuwa wazi tu kuwa uko hapa kumsafisha fisadi lowasa)

Mkuu, nimesoma hii post ya jamaa ina mlengo wa limsafisha lowasa, lakini kwa context ya habari yenyewe na data zake, na jinsi watu wanavyochangia ki ukweli wamebase sana kwenye mada, kwa hiyo mleta mada hapa ameshindwa kumsafisha EL.
 
As long as tumebinafsisha viwanda vyetu na kutochukua hatua za kuhakikisha kuwa wale waliokabidhiwa viwanda hivyo wanaendeleza shughuli za viwanda badala ya kuvibadilisha kuwa go-down tutaendelea kuwa na tatizo la ajira. Hebu niulize hivi serikali ina sera gani kuhusu viwanda na inachukua hatua gani kuhakikisha viwanda vilivyobinafsishwa vinafufuliwa? Kwa nini mpaka leo hatujajiuliza ilikuwaje Mwalimu Nyerere aanzishe viwanda karibu katika mikoa yote ya Tanzania, na licha ya kwamba vilikufa kutokana na uzembe wetu, sijamsikia mwanasiasa yeyote anayezungumzia sababu zilizopelekea kufa kwa viwanda hivyo na tunachopaswa kufanya. Hatuwezi kutegemea wawekezaji ndio wawe vyanzo vya ajira kwa vijana wetu. Serikali lazima iweke mkakati na msisitizo katika ufufuaji wa viwanda ama sivyo tutaendelea kulitizama hili bomu la ajira kwa vijana likituripukia.

Mkuu, the late Nyerere alikuwa binadamu mwenye... sijuhi nesemeje labda MAONO, hakuwa binadamu wa kawaida YULE! Cha kushangaza ni kwamba efforts zake za kutaka kuinua waswahili wenzake ziligonga mwamba kutokana na mawaziri na viongozi wengine wa karibu naye walikuwa ni wanafki wakubwa, walikuwa wanaitikia hewala bwana wakisha mpa kisogo wanafanya mambo mengine tofauti kabisa.

Back to the point, mimi nakumbuka viwanda hivi viliajili vijana wengi sana na kusema kweli vijana walikuwa wanachakalika sana na walikuwa na amani na maisha, siyo kwamba walikuwa wanalipwa mshahara mikubwa, cha muhimu kwao ni kupata ajila ya uhakika. Tatizo lililo kuja kukumba viwanda hivi ni poor management na kuweka ndugu kwenye key posts; si hilo tu hata dhana ya kufikili mtu akiwa na cheti cha Chuo Kikuu ndio kila kitu, vijana waliomaliza vyuo vikuu wakapewa taasisi hizi ndio walifanya madudu ya kutisha. Wenzetu katika nchi zilizo endelea hawakurupuki kumkabidhi mtu yeyote aendeshe kiwanda simply ana degree!! hawafanyi hivyo hata kidogo, wanam-groom kwa muda mrefu wakiangalia utendaji kazi, mausianoa wa wenzake nk; sasa sisi hilo utukulizingatia! Wahitimu wengi walikuwa na VIBURI sana na kujisikia, wakageuza viwanda kama mali yao binafsi - hawakuwa na ubunifu wowote, matokeo yake viwanda vikafa kimoja baada ya kingine!!

Sina nia ya kuwasema vibaya wasomi, tatizo ili lipo mpaka dakika hii: Tuchukulie mfano mdogo kuhusu usafiri jijini DSM - Wizara ya uchukuzi ina wasomi wengi mainjinia pale wizarani, kuna vitego chungu mzima na wakurugezi wake actually kazi nyingine zinaingiliana lakini miaka yote hakuna mbunifu yeyote aliye wahi kulivalia njuga swala ya usafiri mpaka alipo kuja Mh. Mwakyembe! Kumbuka Mwakyembe taaluma yake ni Mwanasheria, swali ni: Inakuwaje mwana sheria awe na upeo wa kiufundi na ubunifsi kuliko watu walio somea fani ya Ufundi,mwishoni mwamwezi huu train inaanza kazi licha ya watu wenye akili timamu kumsema vibaya Mh.Mwakyembe - walikuwa hawataki afanikiwe hata kidogo, na ukiangalia kwa umakini asili mia kubwa iliyokuwa inampiga madogo/vijembe Mh.Mwakyembe wanatoka Wizara anayo iongoza? Je, wawekezaji wanapo shinikiza kuja na wataalamu wao wa kiufundi nani anaweza kuwalahumu.

Mwisho, labda niseme kwamba TAIFA letu lisipo address VICES zilizo pelekea viwanda vyetu kwenda jehanamu in the first place tutaendelea kubaki nyuma kiviwanda miaka yote. Mimi nasikitika sana ninapo sikia Serikali yetu unawekea mkazo KILIMO kwanza badala ya kufufua VIWANDA na kuviendesha kiufanisi, ili la kusema KILIMO ndio kitatoa ajila kwa wingi kwa vijana - personally sihafiki nalo - chukulia wanavyo chezea pembejeo za kilimo na kuuzia wakulima mbolea fake akili zao ziko kwenye wizi wa ruzuku sio kuendeleza KILIMO, ndio maana wanapigia debe KILIMO kwanza wanajua fika hapo ndio shamba la BIBI, sisemi hili out of the blue-kuna my close relative aliwahi kunieleza kwamba Mtanzania mwenye asili ya nje na mwenye high connection nchini aliwahi kumwambia washirikiane katika mbinu za kujipatia fedha kutokana na ruzuku za KILIMO/Kilimo kwanza!!!!! Kwa hiyo nilipo sikia wabunge wana lalamika sana kuhusu mbolea na pembejeo sikushangaa. Waziri mkuu mtoto wa mkulima ana nia nzuri sana na TAIFA letu, tatizo ni kwamba yuko peke yake - wengine wanatoa lip services kwake lakini hawako nae; mimi namuomba ahachane na mambo ya Kilimo kwanza badala yake akazanie ufufuaji wa viwanda, wale walio binafsiwa viwanda alafu wakavigeuza godown wafungwe bila ya kufikishwa mahakamani.
 
Mkuu mimi nakupongeza sana yote uliyoongea ni ya kweli, lkn cha kujiuliza Mzee Lowasa alikuwepo kwenye serikali hiix2 hata siku moja hatukumsikia akiongela suala la ajira kwa vijana, lkn leo hasa baada ya mitafaruku kibao ndani ya chama chake na yeye ndo anatamka haya, kwanza tunachotakiwa kumuuliza, nafasi aliyokuwa nayo nikubwa sana serikalini, alifanya nini kuhusu hilo tatizo? Au mtu ukishatolewa tu tena kwa kashfa ndo unaanza kuongea yale ambayo yalikushinda, hakika watanzania bado tupo gizani. tunatakiwa kujifakari upya, vinginevyo tutakuwa tunaingiza watu wale wale halafu mambo yatazidi kuwa yalex2 tu.
 
...Inasemekana Lowassa ni mwanasiasa anaejua kuzichanga karata zake vizuri, may be YES! maybe NO!, lakini he is coming back. Alianza kushiriki harambee za makanisa, akaja na hili Bomu la ajira kwa vijana, na sasa anaenda kwa Wanawake kupitia vikundi vyao (VICOBA,UWT etc). Hao wote ni wapiga kura, na ndio mtaji huo....But wait a minute, tatizo letu ni lile lile, Kulalamika. Viongozi wanalalamika, wananchi wanalalamika. Lowassa ni kiongozi na ameona kuna Bomu litalipuka, yeye amefanya nini kusaidia hili mimi sijui, labda kwasababu kwake huu ni mtaji katika safari yake kisiasa..

Mind you tatizo la ajira halipo huku kwetu tu, hata nchi zilizoendelea ni tatizo, leo hii ili Rais Obama ajihahakikishie ushindi ni lazima awaambie wamerekani atatatua vipi suala la ukosefu wa ajira, Romney nae lazima aeleze mikakati yake, huo kwao ni mtaji wa kura...

Badala ya kulalamika, tuweke mjadala wa wazi baina na wanasiasa,Lowassa akiwepo kama mchokoza mada, tusemezane tunateguaje hili Bomu.

Lakini pia kuna hili la Uvivu wa kufanya kazi na Ukosefu wa Uzalendo kwa vijana wa kitanzania wa leo, Je tunao vijana walio tayari kufanya kazi?, Je vijana hao ni wazalendo wa kweli katika hizo kazi wanazopewa? Huo ni mjadala mwingine
 
Back
Top Bottom