Bomu liko katika hatua za mwisho lilipuke, Ila Serikali inao uwezo mkubwa wa kulitegua ili lisilipuke

Bomu liko katika hatua za mwisho lilipuke, Ila Serikali inao uwezo mkubwa wa kulitegua ili lisilipuke

Paulsylvester

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2021
Posts
1,464
Reaction score
3,379
Tangu kuondokewa kwa aliyekuwa Amiri Jeshi na Rais wa Tanzania wa awamu ya Tano Mh JPM

Mitandaoni kote hakujawahi kutulia, nilidhani labda kwa kuwa nchi yetu haijawahi kukumbwa na kadhia hiyo ya Rais kufa akiwa madarakani, ndiyo maana kila mtu anajaribu kuongea lakwake, na kifo chake, wengi hawakuamini, kwa sababu ilikuwa ni ghafla mno

Lakini kwa kuwa mwenye kuamua mtu awe hai au hapana ni Mungu na Siri hizo anazo yeye peke yake, Watanzania tulilipokea, ingawa kwa huzuni na majonzi makubwa, na kifo chake na kuagwa kwake, kulionyesha kuwa ni mtu aliyekuwa ameshiba mioyoni mwa watu!

Nilijipa matazamio kwamba, kwa muda angalau wa nusu Mwaka, tungeliweza kusahau na maisha yakaendelea, lakini ninachokiona kuwa itatuchukua muda mrefu mno na hata kutufikisha sehemu si salama ni hii mijadara inayoendelea kila uchwao mitandaoni

Mijadala hii ina pande mbili, kuna wale wanaompondea kwa sana na kumsema kwa ubaya na dhihaka kubwa licha ya kwamba nao pia ni binadamu wale wale waliokwenye mawindo ya aliyewaumba na kwa muda wowote aweza kuwachukua, lakini madai yao ni kwamba waliumizwa mno na utawala wake kiasi kwamba hawataki wanyamaze, hili najiuliza, Je, ipo faida wanapata wakimsema?

Lakini kundi la pili ambalo haliamini hivyo kama wale wa kundi la mashambulizi kudai kwamba waliumizwa, wao wanaona aliyekuwa kipenzi chao kwa nini anasemwa vibaya licha ya kwamba hayuko ktk dunia hii na wanataka wasahau angalau kuangalia maisha mengine, ila kunapotokea mmoja akimsema vibaya JPM, mioyo yao inaumia, na wanaamini kiongozi wao alifanya mengi mno mazuri na aliwagusa maisha yao

Na ukifuatilia mjadara unaoendelea sasa, utagumdua kuwa, kuna waka moto ktk mioyo ya makundi haya!!

Ni ombi langu kwa Serikali, mjadara kumhusu JPM ufungwe rasimi, utazaa mengine mabaya zaidi na nchi yetu itaingia kwenye historia mbaya zaidi,

Mbaya zaidi ni kuwepo watu wanaodai kifo cha JPM ni cha utata, haya mambo yakilelewa lelewa ni hatari,

Tumefika mbali sasa kwa dalili hizi, kwamba mtu Fulani asionekane kanda Fulani??

Chonde chonde, Serikali inaouwezo wa kuzuia Bomu hili lisilipuke

Kwa nini tunagawanyika kwa sababu tuu ya kilichoamliwa na mmiliki wa watu wote..?
 
Mbaya zaidi ni kuwepo watu wanaodai kifo cha JPM ni cha utata, haya mambo yakilelewa lelewa ni hatari, ,Tunaomba kauli ya familia ya JPM iruhusiwe kusema au kutoa kauli ya kilichompata JPM?

Hushangai JPM alikuwa na mke na Watoto saba Hakuna alipewa hi kusikilizwa kuhusu kufa cha mume au baba yao?

Mke wa Magufuli alikuwa na kazi gani kama mke kama hawezi kusema yaliyomsibu mume wake hadi akafa ghafla.?
 
Mbaya zaidi ni kuwepo watu wanaodai kifo cha JPM ni cha utata, haya mambo yakilelewa lelewa ni hatari, ,Tunaomba kauli ya familia ya JPM iruhusiwe kusema au kutoa kauli ya kilichompata JPM...
Ikiruhusiwa hii mkuu, halitaisha tu kwa amani,!

Waliofanya kama ni kweli, Mungu atakutana nao tuu!!

Serikali ilisemee tu ili kusiwepo tena mjadara wowote unaohusu JPM
 
Jpm anasemwa kwasababu ya maisha aliyojiamulia eye mwenyewe akiwa hai. Unakumbuka kile kicheko chake cha hiiiiiiiiiiiiiiii wakati akiumiza wenzake ? Ule ulikuwa ni wakati wake wa kutamba ! Unajua familia za aliowaumiza zinajusikiaje huu sasa ni muda wa wengine kusema hiiiiiiiiiiiiiiii kanuni ni moja tu karma kila kipimo unachopimia wengine nawewe utapimiwa.
 
Jpm anasemwa kwasababu ya maisha aliyojiamulia eye mwenyewe akiwa hai. Unakumbuka kile kicheko chake cha hiiiiiiiiiiiiiiii wakati akiumiza wenzake ? Ule ulikuwa ni wakati wake wa kutamba ! Unajua familia za aliowaumiza zinajusikiaje huu sasa ni muda wa wengine kusema hiiiiiiiiiiiiiiii kanuni ni moja tu karma kila kipimo unachopimia wengine nawewe utapimiwa.
JPM aliumiza wachache Ili kuponywa mamilion ya watu.
 
FUBRbXaXoAUFxwl.jpeg
 
Tangu kuondokewa kwa aliyekuwa Amiri Jeshi na Rais wa Tanzania wa awamu ya Tano Mh JPM

Mitandaoni kote hakujawahi kutulia, nilidhani labda kwa kuwa nchi yetu haijawahi kukumbwa na kadhia hiyo ya Rais kufa akiwa madarakani...
Ifungwe kwa nini mbona yeye jpm alikuwa anawasema watangulizi wake kwa miaka mitano kama syo sita.
Mfuate aliko mfyuuu
 
Mbaya zaidi ni kuwepo watu wanaodai kifo cha JPM ni cha utata, haya mambo yakilelewa lelewa ni hatari, ,Tunaomba kauli ya familia ya JPM iruhusiwe kusema au kutoa kauli ya kilichompata JPM...
Mke wa Ben saa nane na azory gwanda nawengine wengi wanataka kujua ilipo miili ya ndugu zao au unadhani Ben na wenzake waliopotea walikuwa wanatumia gesi mwilini na sio damu? JPM kabla hajampiga risasi lissu aliongea kwa dharau sana eti this is government khaaaaaa mzee yule au mnadhani damu ya lissu ni ya mercury.
 
Anasemwa sana mwalimu Nyerere tena mpaka kuwekewa na makongamano, je mbona kwa miaka yote hii nchi haijalipuka? Kwa nn anaposema jpm tu ndio nchi ilipuke?

Hii maana yake ni moja tu, huyu ndio alikuwa tatizo na ameacha tatizo na bila shaka tatizo mojawapo ni wewe mwenyewe mleta mada.

Tatizo lako ni ujinga. Jamaa aliwajaza ujinga kiasi kwamba mnahisi ninyi ndio mlikuwa bora na mlifanya bora kuliko wengine wote.

Kumbe mliofanya yote nayo ni ujinga tu. Wanapotokea watu kuondoa ujinga wenu kwenye mnakuja na vithread hapa vya kutishia nyau [emoji23]
Tangu kuondokewa kwa aliyekuwa Amiri Jeshi na Rais wa Tanzania wa awamu ya Tano Mh JPM

Mitandaoni kote hakujawahi kutulia, nilidhani labda kwa kuwa nchi yetu haijawahi kukumbwa na kadhia hiyo ya Rais kufa akiwa madarakani, ndiyo maana kila mtu anajaribu kuongea lakwake...
 
Tangu kuondokewa kwa aliyekuwa Amiri Jeshi na Rais wa Tanzania wa awamu ya Tano Mh JPM

Mitandaoni kote hakujawahi kutulia, nilidhani labda kwa kuwa nchi yetu haijawahi kukumbwa na kadhia hiyo ya Rais kufa akiwa madarakani, ndiyo maana kila mtu anajaribu kuongea lakwake...
Umeongea la maana sana japo wapo wengine watakuponda sioni mantiki ya kuendelea na mjadala huu lakini kwanza waonywe viongozi wakuu wao kila siku lazima wamponde JPM ili wasikike kumbe ndio wanajiharibia hata 2025 itakuwa heka heka
 
Ikiruhusiwa hii mkuu, halitaisha tu kwa amani,!

Waliofanya kama ni kweli, Mungu atakutana nao tuu!!


Serikali ilisemee tuu ili kusiwepo tena mjadara wowote unaohusu JPM

Hakuna mjadala wowote utafungwa, na hata ikifungwa hapa kuna majukwaa kibao ya kujadili utawala ule wa kidhalimu. Wakati alipokuwa akiumiza watu, kuteka, kuwaua na kunajisi chaguzi za nchi hii mliona ni sawa. Sasa tunaendelea kutoa mrejesho wa utawala ule wa kidhalimu, mnakimbia majibu! Hiyo familia yake waruhusiwe kusema lolote watakalo lakini ukweli mtu wao alikuwa katili na mlevi wa madaraka.

Na huko kanda ya ziwa mnakotaka kujifanya alikuwa na haki miliki watu wataenda, na watapata kura za kishindo kwani kura hupangwa na vyombo vya dola na sio wananchi, na yeye ni muasisi wa uhayawani ule. Sasa vuneni alichopanda, na hili litakuwa fundisho kwa viongozi wengine kutawala kwa mabavu.
 
Back
Top Bottom