Bondia afariki baada ya kupigwa KO katika shindano la ndondi

Bondia afariki baada ya kupigwa KO katika shindano la ndondi

nimeona video ya pambano lake yan ukiangalia unaona kabisa jamaa alishakata moto kocha wake ata hajarusha taulo pia mpinzan wake alikuwa anatwanga hata hakupunguza kas ndo kwanza alizidisha michezo n upendo unaona mwenzako ameflot unazidisha makonde
 
nimeona video ya pambano lake yan ukiangalia unaona kabisa jamaa alishakata moto kocha wake ata hajarusha taulo pia mpinzan wake alikuwa anatwanga hata hakupunguza kas ndo kwanza alizidisha michezo n upendo unaona mwenzako ameflot unazidisha makonde
Duh!!!mkuu tunaweza kuipata na sisi pia tuone hapa jukwani?
 
Refa ndo tatzo jamaa kapgwa ngumi kama tisa bila majibu,refa kau-mute tu,mwsho ngumi tano unatakiwa umalize pambano
 
Jamaa alikuwa anarusha ngumi kama mawe mwenzake anaonekana amekata network ila bado anamkandamiza za kutosha [emoji205]
Mada Maugo alikuwa mbishi sana kwa Fransis Cheka, ila pambano lao la mwisho Mada Maugo alinyosha mikono, alisema ni Cheka alienda kwa mganga, aliongeza kuwa ni aheri kupigwa mawe ila siyo hizo ngumi alizokutana nazo hiyo siku.
 
Nilishawahi kupitia kidogo mafunzo ya boxing na kucheza tu boxing wakati wa mazoezi aisee ukimpata wa kumuonea ukianza kumtupia makonde kuna raha fulani unaipata bila muamuzi makini ni rahisi sana kuua au kumletea mwenzako madhara makubwa
Yeah kuna mzuka fulani hivi unakupanda na kutamani kuvunjavunja kabisa
 
Huu mchezo upigwe marufuku
Kwa mwaka huu tu nimesikia watu watatu wamekufa
Mchezo gani wakuumizana?
 
Kuna makonde yamebeba kifo ndani yake.. Ndondi ni mojawapo ya michezo hatari ya kishetani.. Imagine watu wanachonganishwa wapigane
Mm huu mchezo sijawa kuukubali hata kidogo, wala sipendi kuangalia
 
Yaaani michezo yote wamekosa wanaenda kucheza mchezo huo?? Michezo ya kitwana hii kwakweli hapana [emoji119]
 
Refa kafeli pakubwa alipaswa avunje pambano baada ya ngumi kadhaa bila majibu. Ila tatizo mashabiki wa Kiswahili refa akivunja pambano wanashuku ni dili ama refa anampa mtu ushindi wa chee. Usalama wa wanamichezo hatuzingatii.
Sasa reda angevunja pambano huyo dogo angekufaje?.Kila kifo lazima kiwe na sababu na hiyo ndio sababu ya kifo cha huyo bondia.kikifika kimefika.40 za huyo jamaa zilishafika ndo maana mambo yakaenda jinsi yalivyoenda.
 
Sasa reda angevunja pambano huyo dogo angekufaje?.Kila kifo lazima kiwe na sababu na hiyo ndio sababu ya kifo cha huyo bondia.kikifika kimefika.40 za huyo jamaa zilishafika ndo maana mambo yakaenda jinsi yalivyoenda.
Interesting theory
 
Maswali yanaulizwa kuhusu taratibu za usalama katika ndondi ya Zimbabwe kufuatia kifo cha Taurai Zimunya baada ya kupigwa katika pambano mjini Harare.

Zimunya, 24, wa uzito wa Super bantam, alifariki siku ya Jumatatu, baada ya kuzimia wakati wa pambano lisilo la ubingwa siku ya Jumamosi.

Ni mara ya kwanza kwa bondia kufariki nchini Zimbabwe kutokana na majeraha aliyoyapata ulingoni.

Lawrence Zimbudzana, katibu mkuu wa Bodi ya Kitaifa ya Kudhibiti Ndondi na Mieleka ya Zimbabwe (ZNBWCB), anasema kuwa mipango ya uchunguzi bado haijashughulikiwa.

"Kwa sasa tutaangazia mazishi, na kisha tuketi na kuangalia masuala," Zimbudzana aliambia BBC Sport Africa katika mazishi ya Zimunya Jumatano.

Taarifa iliyotolewa na ZNBWCB ilisema kuwa "taratibu zote muhimu za matibabu zilifuatwa na msaada wa dharura wa matibabu ulitolewa mahali hapo kabla ya kupelekwa hospitali".

Zimunya alipigwa makonde kadhaa kichwani kabla ya kubanduliwa nje katika raundi ya tatu ya pambano la raundi sita.

Aliyekuwa mkufunzi wake Tatenda Gada alihuzunika, akihisi nyota huyo alikuwa na uwezo mkubwa.

"Tumeopokonywa mojawapo ya matarajio yetu mazuri," Gada alisema. "Nilifanya kazi na Taurai kwa zaidi ya miaka minne - nilimtazama akistawi na alikuwa mmoja wa nyota wajao katika fani hii."

Babake Zimunya, Samson, alikuwa bondia mahiri asiye wa kulipwa na alitarajia mwanawe angebeba jina la ukoo na kuwa bingwa.

Ndondi ilikuwa imerejea tu Zimbabwe baada ya vizuizi vya kupambana na janga la corona kulegezwa.
View attachment 1998033
Sir God alisema wanaume tutakula kwa jasho. Apunzike kwa amani mwamba
 
Back
Top Bottom