Boniface Jacob (Boni Yai): Salamu kutoka Segerea (Ujambazini)

Boniface Jacob (Boni Yai): Salamu kutoka Segerea (Ujambazini)

Hayo ni magereza yaliyo miji mikubwa! Ukienda ya mikoani Kuna ufirauni sana! Kuna dogo wangu alienda mahabusu ya mkuu Rombo unaambiwa waamrishwa wavue nguo zote wapange mstari wafanyiane usodoma mchana kweupe! Hii dhambi ya askari magereza shetani anasubiri sana!
Duuuh, Really? Hii sidhani kama inatokea, ipo kinyume na Sheria za Nchi, Sheria ya Haki za Binadamu, Sheria za Mungu na Sheria ya Ustawi wa jamii

Ndio nalisikia hivi sasa, labda kama ndio inaanza na haijulikani katika uongozi wa eneo husika kwsbb huyo Mkuu wa Gereza angeshashughulikiwa.
 
SALAMU KUTOKA UJAMBAZINI..

Najua ukisikia neno “ujambazini” lazima utashtuka kidogo. Nikutoe hofu neno kabisa. Neno ‘ujambazini’ ni jina la eneo kama ilivyo Posta, Masaki au Manzese.

Nikupeleke sasa Ujambazini huko. Ujambazini ni Magharibi mwa Jiji la Dar es salaam, na kusini mwa Wilaya ya Ilala, kuna sehemu maarufu inaitwa Segerea.

Segerea ni kata katika halmashauri ya Manispaa ya Ilala yenye mitaa ya Ugombolwa, Mfaume, Mgombani na Segerea yenye wakazi 83,000 na KM za mraba 9.6,

Segerea imezungukwa na Kata za Kimanga, Kinyerezi, Tabata na Kipawa. Mtaa wa Segerea kuna Gereza Kuu la Mahabusu Mkoa wa Dar es salaam linaitwa SEGEREA.

Segerea ni gereza maarufu Mkoa wa Dar es salaam. Ni Gereza Kongwe lenye mazingira ya kutisha na kuogopesha. Limezungukwa na mapori na vilima.

Mapori hayo ya kutisha na vilima hivyo vingi vilivyozunguma gereza la Segerea husababisha utulivu mkubwa sana ndani ya gereza la Segerea.

Sasa nikuchukue nikupeleke ndani ya Gereza bila amri ya mahakama, bila kesi na bila pingu mkononi. Yaani, kimawazo tu ujihisi na wewe upo Gerezani.

Ndani ya gereza Kuu la Mahabusu Dar es Salaam - Segerea kuna sehemu kubwa na maarufu kama tano;

Sehemu ya kwanza; nje ya gereza, wageni hufika na kusubiri utaratibu wa kuingia ndani kuona ndugu zao. Kuna Canteen, Duka na eneo la kukaa wageni.

Sehemu ya pili; Jengo la Utawala ambalo ndiyo ofisi ya Mkuu wa Gereza maarufu “Bwana Jela” na askari wake wanasimamia wafungwa na mahabusu ndani ya gereza.

Sehemu ya tatu; “ujambazini”, huko kuna vyumba vya Jela 10 na kila Kimoja kina idadi maalum ya watu, mfano namba 10 inachukua watu zaidi ya 200 na zaidi.

Sehemu ya nne; Upande maalum (Special Wing) wanaishi mahabusu au wafungwa ambao ni watoto chini ya miaka 18, mahabusu, wafungwa wachache

Sehemu ya tano; “PC - Private Cell”. Huko hupelekwa watu watukutu au wanaotenda makosa wakiwa ndani ya gereza nje na makosa wanayopelekwa nayo gerezani.

Huko katika private cell (PC) - kuna vyumba maalum ambavyo mtu hutengwa pekee yake na kupata mlo mmoja kwa siku. Ni kama sehemu ya kutoa adhabu.

UJAMBAZINI

Rudi nyuma siku ya alhamisi 19 September 2024 majira ya saa 4 usiku. Muda nilishushwa na msafara wa Polisi wakiwa na gari mali ya Jeshi la Polisi na Polisi kibao.

Baada ya kupokelewa na kujazwa katika Kitabu, natupa Jicho la udadisi ubaoni getini,hesabu zinasoma jumla mahabusu na wafungwa 1,011 wanaume na wanawake.

Sasa rasmu hadi hapo nipo chini ya ulinzi wa askari Magereza - Segerea. Mamwela wamenimwaga halafu wao wakasepa kwa mbwembwe kama walivyokuja.

Mapokezi katima lango la gereza kwanza wananijua kwa majina yote matatu wengine wanaiita Boniface Jacob, Mstahiki meya na baadhi wakanitambua kama Boniyai,

Wananisalimia halafu wananiacha, wanasogea pembeni wanamuuliza incharge wao, tumpeleke wapi? Jibu linatoka kwa incharge wao mpelekeni UJAMBAZINI!

Rohoni nikaguna. kwanini ujambazini? Mwisho nikakumbuka somo la utayari (The chameleon principal) “ukikutana na wahuni kuwa muhuni mwenzao.”

Kweli. Jamaa wakanipekua kisha wakaanza kuniogoza kuelekea ujambazini. akilini najiandaa kwenda kukutana na majambazi hatari na watu katili sana gerezani.

Nakaribia mlangoni pembeni dirishani naona ndani watu wamelala wanakoroma, muda huo taa zinawaka kwa mwanga mkali sana kama karabai za wavuvi.

Nyapara wa selo namba 10 kijana mmoja mrefu, anaitwa MWITA, anakabidhiwa anipokee anitafutie sehemu ya kulala ndani ya selo ambapo ndiyo kiongozi wake.

Kabla hawajaniacha wakaniuliza, Boniyai umekula? nikakumbuka kauli ya mama “ugenini siku ya kwanza usije ukavunga kuhusu chakula, utaanza vibaya”

Nikajibu sijala tangu asubuhi, nilipelekwa Mahakamani Kisutu saa 10 jioni na usiku wa Saa 3 ndiyo shauri langu lilihairishwa na hadi jumatatu ya 23 September 2024

Tukiwa wote tumesimama mlangoni, jamaa wanaulizana kama Jikoni kuna ugali na maharage, kwa bahati mbaya wanajibiwa hakuna kitu chochote kilichobakia.

Itaendelea…
Kamilisha hii stori yote
 
Wakati unaangakia
Special wing” ni sehemu maalum katika magereza kwa ajili ya wafungwa wenye mahitaji maalum au wale ambao wanahitaji ulinzi wa ziada,, hiki kitu nina experience nacho aisee, Boniyai kanikumbusha nyuma sana 😬
wakati unaangalia muvi za damme
 
Dah mbona mnatuchanganya sasa mara jela kubaya , na wewe unahadithia story ya boni yai akiwa jela kama yalikuwa maisha mazuri.
Any way sidanganyiki na hiyo story ya boni yai ,
Jela ingawaje namshukuru Mungu sijawahi kuishi hata kwa siku moja naendelea kumuomba Mungu aniepushj na kwenda sehemu hiyo.
Pole sana kamanda boni yai kwa kupelekwa huko jela kimizengwezengwe tu na kwa uonevu .
Inshalah Mwenyezi Muungu awalipe kwa ubaya waliokufanyia kadri atakavyoona inafaa
 
Duuuh, Really? Hii sidhani kama inatokea, ipo kinyume na Sheria za Nchi, Sheria ya Haki za Binadamu, Sheria za Mungu na Sheria ya Ustawi wa jamii

Ndio nalisikia hivi sasa, labda kama ndio inaanza na haijulikani katika uongozi wa eneo husika kwsbb huyo Mkuu wa Gereza angeshashughulikiwa.
Naunga mkono hoja hapo mkuu wa gereza na timu yake yote ingekula kwao ,ulawiti ni kosa kubwa sana jela ila wakati mwingine lisemwalo lipo
 
Sasa nimegundua kwanini Ruge alikomaa na kung'ang'ania kubaki mahabusu ni kwasababu alikuwa special wing akila good time. Angekuwa ujambazini angeshakufa.
 
SALAMU KUTOKA UJAMBAZINI..

Najua ukisikia neno “ujambazini” lazima utashtuka kidogo. Nikutoe hofu neno kabisa. Neno ‘ujambazini’ ni jina la eneo kama ilivyo Posta, Masaki au Manzese.

Nikupeleke sasa Ujambazini huko. Ujambazini ni Magharibi mwa Jiji la Dar es salaam, na kusini mwa Wilaya ya Ilala, kuna sehemu maarufu inaitwa Segerea.

Segerea ni kata katika halmashauri ya Manispaa ya Ilala yenye mitaa ya Ugombolwa, Mfaume, Mgombani na Segerea yenye wakazi 83,000 na KM za mraba 9.6,

Segerea imezungukwa na Kata za Kimanga, Kinyerezi, Tabata na Kipawa. Mtaa wa Segerea kuna Gereza Kuu la Mahabusu Mkoa wa Dar es salaam linaitwa SEGEREA.

Segerea ni gereza maarufu Mkoa wa Dar es salaam. Ni Gereza Kongwe lenye mazingira ya kutisha na kuogopesha. Limezungukwa na mapori na vilima.

Mapori hayo ya kutisha na vilima hivyo vingi vilivyozunguma gereza la Segerea husababisha utulivu mkubwa sana ndani ya gereza la Segerea.

Sasa nikuchukue nikupeleke ndani ya Gereza bila amri ya mahakama, bila kesi na bila pingu mkononi. Yaani, kimawazo tu ujihisi na wewe upo Gerezani.

Ndani ya gereza Kuu la Mahabusu Dar es Salaam - Segerea kuna sehemu kubwa na maarufu kama tano;

Sehemu ya kwanza; nje ya gereza, wageni hufika na kusubiri utaratibu wa kuingia ndani kuona ndugu zao. Kuna Canteen, Duka na eneo la kukaa wageni.

Sehemu ya pili; Jengo la Utawala ambalo ndiyo ofisi ya Mkuu wa Gereza maarufu “Bwana Jela” na askari wake wanasimamia wafungwa na mahabusu ndani ya gereza.

Sehemu ya tatu; “ujambazini”, huko kuna vyumba vya Jela 10 na kila Kimoja kina idadi maalum ya watu, mfano namba 10 inachukua watu zaidi ya 200 na zaidi.

Sehemu ya nne; Upande maalum (Special Wing) wanaishi mahabusu au wafungwa ambao ni watoto chini ya miaka 18, mahabusu, wafungwa wachache

Sehemu ya tano; “PC - Private Cell”. Huko hupelekwa watu watukutu au wanaotenda makosa wakiwa ndani ya gereza nje na makosa wanayopelekwa nayo gerezani.

Huko katika private cell (PC) - kuna vyumba maalum ambavyo mtu hutengwa pekee yake na kupata mlo mmoja kwa siku. Ni kama sehemu ya kutoa adhabu.

UJAMBAZINI

Rudi nyuma siku ya alhamisi 19 September 2024 majira ya saa 4 usiku. Muda nilishushwa na msafara wa Polisi wakiwa na gari mali ya Jeshi la Polisi na Polisi kibao.

Baada ya kupokelewa na kujazwa katika Kitabu, natupa Jicho la udadisi ubaoni getini,hesabu zinasoma jumla mahabusu na wafungwa 1,011 wanaume na wanawake.

Sasa rasmu hadi hapo nipo chini ya ulinzi wa askari Magereza - Segerea. Mamwela wamenimwaga halafu wao wakasepa kwa mbwembwe kama walivyokuja.

Mapokezi katima lango la gereza kwanza wananijua kwa majina yote matatu wengine wanaiita Boniface Jacob, Mstahiki meya na baadhi wakanitambua kama Boniyai,

Wananisalimia halafu wananiacha, wanasogea pembeni wanamuuliza incharge wao, tumpeleke wapi? Jibu linatoka kwa incharge wao mpelekeni UJAMBAZINI!

Rohoni nikaguna. kwanini ujambazini? Mwisho nikakumbuka somo la utayari (The chameleon principal) “ukikutana na wahuni kuwa muhuni mwenzao.”

Kweli. Jamaa wakanipekua kisha wakaanza kuniogoza kuelekea ujambazini. akilini najiandaa kwenda kukutana na majambazi hatari na watu katili sana gerezani.

Nakaribia mlangoni pembeni dirishani naona ndani watu wamelala wanakoroma, muda huo taa zinawaka kwa mwanga mkali sana kama karabai za wavuvi.

Nyapara wa selo namba 10 kijana mmoja mrefu, anaitwa MWITA, anakabidhiwa anipokee anitafutie sehemu ya kulala ndani ya selo ambapo ndiyo kiongozi wake.

Kabla hawajaniacha wakaniuliza, Boniyai umekula? nikakumbuka kauli ya mama “ugenini siku ya kwanza usije ukavunga kuhusu chakula, utaanza vibaya”

Nikajibu sijala tangu asubuhi, nilipelekwa Mahakamani Kisutu saa 10 jioni na usiku wa Saa 3 ndiyo shauri langu lilihairishwa na hadi jumatatu ya 23 September 2024

Tukiwa wote tumesimama mlangoni, jamaa wanaulizana kama Jikoni kuna ugali na maharage, kwa bahati mbaya wanajibiwa hakuna kitu chochote kilichobakia.

Itaendelea…
Iendel
 
Jera ni pabaya, sikuwahi kwenda ila sikuwahi kusikia mtu anapasifia kama ilivyo kwa post hii, nilichogundua ni kuwa gerezani kuna madaraja (classes) ya wafungwa hivyo kuna ambao hawanyanyasiki ila wanateswa na kukosekana kwa uhuru. Na kuna akina pangu pakavu ndiyo wanaipata ile suruba tunayoifahamu tulio wengi...
 
Back
Top Bottom