Tetesi: Boom: Wajumbe wote wa Bodi ya Simba upande wa Mo Dewji wajiuzulu

Hivi wajumbe wa bodi ya Simba ndio tatizo la msingi la Simba kufanya vibaya? Je Yeye mwekezaji alikuwa anatimiza majukumu yake ipasavyo? Kama wajumbe 3 wamekataa kujiuzulu Ina maana Kuna mengi chini ya kapeti wanayajua juu ya mwekezaji wanaona anataka kuwatoa mbuzi wa kafara wakati yeye mwenyewe ndio chanzo Cha tatizo, zile bilioni 20 aliziweka benki Gani?
 
Ndio maana Ngungus Boy hataki kujiuzulu sababu anajua tatizo kuu la 5imba ni Mwamedi
 
Mwekezaji wa klabu ya Simba, Mfanyabiashara Mohamed Dewji ameripotiwa kutoa shinikizo la kujiuzulu nafasi zao kwa wajumbe wote aliowateua yeye ambapo mpaka sasa wajumbe watatu wamejiuzuli huku wengine watatu wakigoma.

Wajumbe waliogoma kutii amri ya tajiri mpaka sasa ni pamoja na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Salim Abdallah Muhene 'Tryagain', Rashid Shangazi ambaye pia ni Mbunge wa Mlalo na Hamza JOHARI ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mamlaka za viwanja vya ndege Tanzania.

#KitengeSports
 
🚨 BREAKING.

wajumbe wote wa bodi ya klabu ya Simba SC kutokea upande wa muwekezaji, Mohamed Dewji wamejiuzulu

Mohamed Dewji aliwapigia Simu wajumbe wote wanaotokana na upande wake ambao aliwateua yeye na kuwataka wajiuzulu.

Mbali na Amri iyo ya Mohamed Mjumbe pekee aliegoma kujiuzulu mpaka Sasa ni Salim Abdalha Tray Again.

 
Tuwapongeze wamewajibika Kwa kujiuzulu na kuruhusu nguvu mpya iingie madarakani
 
Hata wakiondoka wote pamoja na Mo mwenyewe, kama kikosi hakitaboreshwa taabu iko pale pale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…