DOKEZO Bosi wa kiwanda cha A to Z Arusha anawadhalilisha na kuwakandamiza Watanzania

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Merchandising executive kwa jina la Perumal aliyepo kiwanda cha A to Z katika kampuni ya Red Earth amekuwa na tabia endelevu ya kuwatukana, kuwabagua, kuwadhalilisha na kuwaonea watanzania wanaofanya kazi katika ofisi ya merchandising kiwandani hapo.

Malalamiko hayo yalipelekwa kwa uongozi wa kiwanda lakini hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi yake badala yake wale walio peleka taarifa kwa uongozi wakafukuzwa kazi, Perumal amekuwa ni Tatizo sugu kiwandani hapo na alifikia hatua ya kusema serikali ya Tanzania ni dhaifu hawezi kufanywa chochote.

Tunaomba uongozi wa Mkoa wa Arusha na ofisi za kazi mkoa wa Arusha wafike kiwandani hapo kuwahoji wafanyakazi juu ya tabia za mtu huyo lakini pia wawatafuta wale waliokuwa wanafanya kazi ofisini hapo waliofukuzwa baada ya kupeleka barua ya malalamiko kwa uongozi wa kiwanda kwa ajili ya kuwahoji na watawasaidia maelezo na email walizowatumia uongozi.

Tusaidiane kupaza sauti kukemea uonevu maeneo ya kazi na kuifanya Tanzania salama.
 
Mamlaka zimshughulikie
 
amewadhalilishaje, hebu fafanua. kawavua nguo, anawatongoza, anawatukana, anafanya nini?
 
Nilifanyaga kibarua hapo 2006-2007. Yani hata jihanam afadhali. Unafanya kila siku masaa 12 na mshahara elfu 60 hadi 70 kwa mwezi.

Wakati ule George Bush alikuja bongo nilikuwepo alipopatembelea hicho kiwanda. Halafu bado nilikuwa under 18. Child labor

Na bado maskini wasichana wanahonga papuch kwa masupervisor wapate kibarua..

Umaskin unatisha.

INASIKITISHA SANA
 
Wanaoumia ni watanzania wenzako vipi mtu aseme serikali haiwezi kumgusa.
 
Napowaambia msiende kuajiriwa kiwandani muwe mnaelewa,ukiacha kutumikishwa na ujira mdogo ila mazingira ya kazi ni mabaya na yenye manyanyaso.
 
Yaonesha we naye ulihonga maana si kwa hasira hizi
 

Ana wadhalilishaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…