BoT fanyeni msako wa kushitukiza, bado ziko taasisi za kifedha zinazokaa na kadi za benki za wateja wao

BoT fanyeni msako wa kushitukiza, bado ziko taasisi za kifedha zinazokaa na kadi za benki za wateja wao

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Katika hili, BOT ni kama wamelala, tena usingizi wa pono, kwani bado ziko taasisi za kifedha zinazokaa na kadi za Benki za wateja wanaoenda kuomba mikopo kama moja la shariti la kupewa mikopo wakiamini kukaa na kadi ya mteja ndio security ya fedha zao.

Ukweli ni kwamba, kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, wakopeshaji kukaa na kadi za wateja wao hakutoi tena security ya fedha wanazokopesha kwani siku hizi mtu unaweza kuhamisha fedha kwa kutumia simu ya mkononi mara tu mshahara unapoingia (unapopata sms).

Kwahiyo,wakopeshaji hawa kukaa na kadi ni swala tu la mazoea kwani kama mteja sio muaminifu, anaweza tu kuhamisha fedha kwa kutumia simu yake na kadi isiwe na msaada wowote na zaidi hawezi kwenda kushitaki popote kwani mwenyewe anavunja sheria kukaa na kadi ya Benki ya mteja.

Kitendo cha taasisi hizi ndogo ndogo za kifedha kukaa na kadi za wateja kinaleta usumbufu kwa wateja wao pale wanapokuwa wamesafiri na mishahara ikatoka wakiwa safarini either kikazi, likizo au kuhudhuria misiba na hata mtu anapohitaji huduma kama bank statement n.k.

Hivyo,tunaishauri Benki Kuu kuweka msisitizo wa katazo hili na zaidi waendeshe msako wa kushitukiza tarehe za mwisho wa mwezi mishahara inapotoka ili kuwabaini wale wanaondelea kukiuka sheria.

Pia, kukaa na kadi kunanufaisha mawakala wa mabenki wanaotumia mashine zao kutoa fedha kutoka kwenye akaunti za wateja na kuumiza wateja(wakopaji) kwani makato kwenye hizi mashine ni makubwa tofauti na makato ya kwenye ATM ambayo ni nafuu. Katika hili, naamini mabenki wana nafasi nzuri ya kugundua mawakala wanaoshirikiana na wakopeshaji kutoa fedha kupitia mashine hizi kwa kuangalia transactions zinazofanyika kwa wingi kila mishahara inapotoka.

BoT fuatilieni hali hii na muikomeshe kwani haipendezi na pia si salama kwa watu kutoa namba zao za siri kwa mtu ambae kadi ya benki sio yake.

Watumishi wa nchi hii wanapita kipindi kigumu sana awamu hii na kulazimika kuishi kwa madeni huku kadi zao za benki zikimilikiwa na wakopeshaji wakati sheria hairuhusu.
 
Hawajakupora
Wengine wanakabidhi hadi bima za afya
Na sasa wanachukua mpaka vyeti, na vitambulisho kama dhamana
Hali tete
Mpaka bima za afya?Duh, hii kali. Sasa ikitokea uko likizo na umeugua huku kadi umeiacha ukikotoka,hapo inakuwaje?

Hii ni sababu nyingine kwanini BOT wanapaswa kufanya ukaguzi wa kushitukiza katika hizi taasisi.
 
Kwa mfano, Kwenye ATM za benki ya NMB Wilayani Sikonge ,Kuna vijaaa wakurya ndiyo mawakala wa kukopesa,huwa wanashinda pale Benki wakiwa na mamia ya Kadi za wadaiwa.

Hivyo kila anayedaiwa akifika ATM wale vijana wanatoa pesa zao Kisha mdaiwa wanampa pesa kiasi silizosalia na wanabaki na Kadi,Tena mbele ya viongozi wa Benki na asikari walinzi.
 
Kwa mfano,
Kwenye ATM za benki ya NMB Wilayani Sikonge ,Kuna vijaaa wakurya ndiyo mawakala wa kukopesa,huwa wanashinda pale Benki wakiwa na mamia ya Kadi za wadaiwa,
Hivyo kila anayedaiwa akifika ATM wale vijana wanatoa pesa zao Kisha mdaiwa wanampa pesa kiasi silizosalia na wanabaki na Kadi,Tena mbele ya viongozi wa Benki na asikari walinzi.
Kipato hakikidhi mahitaji
Mtumwa wa ATM yako mwenyewe
 
Bado ni afadhali kuliko pale ambapo security ni macho au miguu yako ingawa wakopaji wengi wanaelekea huko.
 
KWANI HAO MAWAKALA WAO NDIO WANAOWALAZIMISHA HAO WATUMISHI WAKAKOPE KWAO?? SI WATUMISHI WENYEWE WANAWAPELEKEA HIVYO VITAMBULISHO ATM. WAKUELIMISHWA HAPA NIWATUMISHII.
 
KWANI HAO MAWAKALA WAO NDIO WANAOWALAZIMISHA HAO WATUMISHI WAKAKOPE KWAO?? SI WATUMISHI WENYEWE WANAWAPELEKEA HIVYO VITAMBULISHO ATM. WAKUELIMISHWA HAPA NIWATUMISHII.
Wewe unadhani mshahara wa mwaka 2015 unakidhi mahitaji ya leo?Ni shida tu ila hizo shida zao zisiwe sababu ya wakopeshaji kuvunja sheria..
 
Wewe unadhani mshahara wa mwaka 2015 unakidhi mahitaji ya leo?Ni shida tu ila hizo shida zao zisiwe sababu ya wakopeshaji kuvunja sheria..
Toka lini mshahara ukakidhi mahitaji ya binadamuu?? Kama ni suala la watumishi kukopa kwenye vibanda umiza, hili suala liko kwa mda mrefu saaana mimi nimeanza kulishuhudia toka miaka ya 2000.

Kwahiyo suala la watumishi kukopakopa kwenye hivi vibanda umiza vinavyoitwa microfinance vya wauza chips hili suala nila mdamrefu saaana rafiki yangu salary slip.

Nikushauli tuu kwamba, serikali haiwezi kuliingilia kati kwakuwa mikokopo hiyo huwa nimakubaliano binafisi kati ya mkopaji na anaye kopesha.

Kwahiyo elimu binafsi ipelekwe kwa watumishi wanaojipeleka huko. Wapo wanaokopa kwa malengo lakini wengine wanakopa huko kwa ajili ya tamaa ya kufanya anasaa.
 
Toka lini mshahara ukakidhi mahitaji ya binadamuu?? Kama ni suala la watumishi kukopa kwenye vibanda umiza, hili suala liko kwa mda mrefu saaana mimi nimeanza kulishuhudia toka miaka ya 2000. Kwahiyo suala la watumishi kukopakopa kwenye hivi vibanda umiza vinavyoitwa microfinance vya wauza chips hili suala nila mdamrefu saaana rafiki yangu salary slip. Nikushauli tuu kwamba, serikali haiwezi kuliingilia kati kwakuwa mikokopo hiyo huwa nimakubaliano binafisi kati ya mkopaji na anaye kopesha. Kwahiyo elimu binafsi ipelekwe kwa watumishi wanaojipeleka huko. Wapo wanaokopa kwa malengo lakini wengine wanakopa huko kwa ajili ya tamaa ya kufanya anasaa.
We acha kutetea upuuzi. Mishahara duni ni chanzo kikubwa cha haya yote. Jiulize ni kwanini watumishi wa hali ya chini tu ndio wanaocha kadi na si vibosile au wale wenye marupurupu mengi?

Hii mishahara sio tu haitoshi, bali haikidhi hata maihitaji ya msingi na ndio maana watu wanaacha Utumishi wa umma na kukimbilia kwenye siasa au hata kwenda private.

Mishahara serikalini ni duni tangu siku nyingi ila awamu hii imeifanya iwe duni mara mbili na hivyo kuongeza tatizo ambalo teyari lilikuwepo badala ya kulipunguza.

Msitetee huu unyonyaji kwa kisingizio mishahara huwa haitoshi.
 
Back
Top Bottom