BOT kushusha riba za mikopo ni mpaka waagizwe ili hali wao ndio wataalam wa kushauri zishuke?

BOT kushusha riba za mikopo ni mpaka waagizwe ili hali wao ndio wataalam wa kushauri zishuke?

Mwendazake sio ndio aliowaweka wachumi waliokariri vitabu na wenye GPA Kali ile exposure sifuri na si ndio waliotufikisha hapa......eti interest rate ikishuka,iflation itatoke.......yaani michumi hata haijui umuhimu wa lower interest rate in economy......kwani kila mtu atakua tu anakopa kijinga kadri anavojisikia?
Kaishi Zimbabwe!
 
Point ni wachumi muliosoma kwenye makaratasi musijifanye wataalam sana
....eti kumpangia rais sijui ujinga ujinga gani muliokariri shule.......dunia imebadilika,sio dunia ya kukariri vitabu tena hii.....by the way last 10 years hakua na vitu kama DEFI,BLOCKCHAINS,cryptocurrencies etc......hivyo vyote vina implications kwenye economy ya sasa almost........mambo ya interest rates,demand and supply,inflation rates ni mambo ya uchumi wa zama za kale munaokariri huko chuo kikuu.....Wachumi wa B.O.T wameshindwa kuruhusu hata matumizi ya PayPal kupokea pesa kwa vijana wafanya biashara Tanzania,nao wapate riziki,wafungue economy,ku-export skills.....sasa ninyi wachumi munafata nini huko,zaidi tu kukalia ujinga ujinga na matejory muliokariri kwenye books zama za mawe
Ndiyo maana nikakwambia akili zako na za mwendazake hazikuwa na tofauti, yeye alikuwa na utaalamu wa kuiba kura,kupima mapapai corona,kupora watu pesa nk
 
Hapo unampotosha.... Yeye amesema Tanzanina inategemea kuimport kila kitu kiufupi Next exports mara nyingi ni negative. Sasa kama hela yako haina thamani obviously utateseka. Iran ina Exports bidhaa za $107 B huku ina Import $54 B pekee!! Sasa hapo huoni currency devaluation ama inflation ni sustainable sababu wanaingiza pesa nyingi za kigeni?
Nashukuru sana mkuu,akishindwa kukuelewa atakuwa na tatizo kubwa somewhere.
 
Suala la kushusha riba nchi hii linaonekana kufanyika kutokana na maagizo ya wanasiasa (liko kisiasa) na si Benki Kuu kama wataalamu kushauri au kushusha riba kwa mabenki ili nayo yashushe riba kwa wananchi.

Kwa mfano, leo Mama kaagiza Benki Kuu kuhakikisha mabenki yanashusha riba kufika chini ya asilimia 10 (jambo jema na la kupongeza).

Swali langu ni je, Benki Kuu kama wataalamu, huwa hawaoni umuhimu wa kushusha riba mpaka waagizwe na wanasiasa?

Katika hili, si BOT kama wataalamu ndio wa kushauri wanasiasa waridhie BoT kushusha riba kama BoT hawana mamlaka hayo mpaka wapete idhini ya watawala?

Kama tatizo ni sherai na taratibu, je hatuoni sheria na taratibu hizo zinastahili kufanyiwa marekebisho?

Mambo ya ajabu sana haya!
Is professionalism nowadays in the toilet? Interest rates are market driven instruments as inflation rates. They can only be controlled through "proper" monetary policies. "Hizi siyo issue za majukwaani".
 
Matatizo ya Tanzania ni mengi sana, mpaka ufumbuzi wake unakuwa na matatizo.

Kwa mfano, hili la riba.

1. Riba ziko juu sana. BOT walitakiwa kushusha riba na kuanzisha "domino effect" ya benki nyingine kushusha riba. Kwa hiyo habari nzima ya kushusha riba inaweza kuwa na msingi mzuri.

2. Kiuchumi, rais hatakiwi kuipangia BOT ishushe riba. Hili ni jambo hatari. BOT inatakiwa kujiendesha kwa uhuru bila kuingiliwa na wanasiasa, kwa kuangalia "economic indicators".

Napata shida ku support rais kuipangia BOT ishushe riba, hata pale ninapoona kwamba riba zipo juu sana.

Hizi habari za rais kuagiza BOT ndizo zilifanywa na Idi Amin alipoagiza hela za Uganda zichapishwe nyingi ili watu wawe na hela, matokeo yake Shilingi ya Uganda ikashuka thamani, na haijafanya recovery fully mpaka leo.
 
Benki kama NMB ina ukwasi usio na kifani, lkn wapi haitaki kuwakwamua wateja wake, ilipaswa ipunguze riba mpaka kufikia 5%
Kila benki imepewa rukhusa kupunguza riba kwa jinsi inavyotaka ndani ya theshold iliyowekwa na BOT tatizo mabenki yote hakuna lenye ubunifu kupunguza riba ili kuvutia wateja yote utakuta riba zinalingana. Hoja ya Rais kupunguza riba ni muhimu kiuchumi vinginevyo watu hawatakopa na pia watashindwa kurejesha mikopo. Kipindi hiki cha recession ya korona hii ndiyo mikakati mojawapo ya kukwamua uchumi. Rais ni mchumi anajua vizuri hali hii.Iwapo BOT wanashindwa kuchukua hatua Rais anayo haki ya kuwaagiza wataalam wa Benki kuu kuliangalia hilo vinginevyo haiwezekani warudi kwake na kushauri wakiwa na options na madhara yake huku wakizingatia hali halisi ya sekta ya fedha inavyoathirika kwa sasa.
 
Maagizo ambayo hayana tija. Watu wafanye kazi halali na kulipa kodi stahiki, inflation na interest rates zitaji-adjust accordingly. Hakuna pesa za bure popote ulimwenguni, wananchi wahimizwe kufanya kazi halali na sio kukimbilia utajiri wa haraka haraka bila kufanya kazi halali na kipato stahiki. The cake is big enough for everybody.
Mimi nataka nikope 800M niingize kwenye biashara zangu. Hizo 800M ni za bure!!??
 
Nadhani hujui kuwa BOT haipunguzi riba za commercial banks kwa kuwaamrisha, bali wanawashauri tu kupunguza riba kwa kuwapa incentives fulani, fulani. Riba za Commercial banks zinajengewa na vitu vingi kuanzia, riba wanazotozwa kuchukua pesa BOT, risk, n.k.

Sasa utauliza kwanini BOT wasishushe riba wanazotoza Commercial banks ili riba ziwe ndogo?

So far BOT imekuwa ikishusha Centra Bank rate (CBR), ili kuwapunguzia gharama banks ila riba bado zimebaki kuwa juu, hii ina maana kuwa kuna factors nyingine nje ya CBR ambazo zinafanya riba zibaki juu, kwa uelewa wangu mdogo hizo factor nyingine ni pamoja na risk za kumkopesha mtanzania.

Imagine bank wamkopeshe mmachinga ambaye kwanza biashara yake haina permanent address, makazi yake rasmi hayajulikani na vitu vingi vinavyoenda na hivyo, so ili kuhedge against hizi risk lazima wakupenalize riba kubwa incase ukishindwa kulipa wawe wamepata hela yao kidogo.
Suala la risk compensation haiwezi kuwa kigezo pekee cha kuongeza riba. Mabenki yenyewe pia yaangalie operational costs zake, weledi katika kutathmini risks na hapo rushwa iondoshwe kwa kuajiri wafanyakazi waaminifu, matumizi ya mifumo ya kisasa kudhibti Non perfomaning Loans na kubadilishana taarifa za wakopaji. Serikali nayo iangalie macro economic policies, monetory and fiscal policies kulegeza riba vinginevyo tusahau kupata wawekezaji
 
Point ni wachumi muliosoma kwenye makaratasi musijifanye wataalam sana
....eti kumpangia rais sijui ujinga ujinga gani muliokariri shule.......dunia imebadilika,sio dunia ya kukariri vitabu tena hii.....by the way last 10 years hakua na vitu kama DEFI,BLOCKCHAINS,cryptocurrencies etc......hivyo vyote vina implications kwenye economy ya sasa almost........mambo ya interest rates,demand and supply,inflation rates ni mambo ya uchumi wa zama za kale munaokariri huko chuo kikuu.....Wachumi wa B.O.T wameshindwa kuruhusu hata matumizi ya PayPal kupokea pesa kwa vijana wafanya biashara Tanzania,nao wapate riziki,wafungue economy,ku-export skills.....sasa ninyi wachumi munafata nini huko,zaidi tu kukalia ujinga ujinga na matejory muliokariri kwenye books zama za mawe
Shida uchumi wetu unapaswa ubadilike kwa kuendana na msukumo wa uchumi wa dunia ie paypal etc. Lakini pia milango ya biashara ifunguliwe kati serikali na sekta binafsi tukwepe kabisa kurudi kwenye state monopoly type of economy itatugharimu.
 
Matatizo ya Tanzania ni mengi sana, mpaka ufumbuzi wake unakuwa na matatizo.

Kwa mfano, hili la riba.

1. Riba ziko juu sana. BOT walitakiwa kushusha riba na kuanzisha "domino effect" ya benki nyingine kushusha riba. Kwa hiyo habari nzima ya kushusha riba inaweza kuwa na msingi mzuri.

2. Kiuchumi, rais hatakiwi kuipangia BOT ishushe riba. Hili ni jambo hatari. BOT inatakiwa kujiendesha kwa uhuru bila kuingiliwa na wanasiasa, kwa kuangalia "economic indicators".

Napata shida ku support rais kuipangia BOT ishushe riba, hata pale ninapoona kwamba riba zipo juu sana.

Hizi habari za rais kuagiza BOT ndizo zilifanywa na Idi Amin alipoagiza hela za Uganda zichapishwe nyingi ili watu wawe na hela, matokeo yake Shilingi ya Uganda ikashuka thamani, na haijafanya recovery fully mpaka leo.
Politics are killing this country.Hakuna kinachotekelezeka
 
Huo uchumi muliokalili chuo umelisaidia nini Taifa ......thus why wanasiasa wanaweza adjust mambo na kisiharibike kitu......maana huko chuo vitabu hata vya uchumi si vya Tanzania......kisha mjinga mmoja anaongea eti usiige uchumi wa nchi fulani.
Mkuu mmefikia wapi kwenye hzo adjustment zenu za riba mpaka sasa 🤣 🤣
 
Mkuu mmefikia wapi kwenye hzo adjustment zenu za riba mpaka sasa [emoji1787] [emoji1787]
Monetary policy committee imebariki na ina-expect quarterly hii mambo yataimalika.....ni muda sasa mkuu wa kupitia policies na economic informations za nchi yako...ingia website ya B.O.T....hakuna faida vizazi vyako viwe masikini kwa kupenda ubishi kuliko kujifunza
 
Monetary policy committee imebariki na ina-expect quarterly hii mambo yataimalika.....ni muda sasa mkuu wa kupitia policies na economic informations za nchi yako...ingia website ya B.O.T....hakuna faida vizazi vyako viwe masikini kwa kupenda ubishi kuliko kujifunza
🤣 🤣 🤣 Muda ni ukuta,anyway-Ngoja tusubirie nyama hope hiyo quarter yenu hata iwe ndefu vp haifiki december 🤣 🤣 🤣
 
Back
Top Bottom