BOT yamwaga mikopo ya mamilioni kwa wafanyakazi wake-Ndio bailout ya serikali hiyo!!

BOT yamwaga mikopo ya mamilioni kwa wafanyakazi wake-Ndio bailout ya serikali hiyo!!

Tatizo letu wengi bado tuna hangover ya siasa za ujamaa na kujitegemea. Eti binadamu wote ni sawa! Kivipi?

Jamani, ingawa ukweli ni kwamba inauma..kwamba Tanzania umaskini umekithiri lakini hebu tuangalie upande mwingine wa shillingi. Hawa jamaa hawapewi hizo hela bure. Wanakopeshwa. Na watarudisha. Hivi inatofauti gani na mtu anayenunua nyumba kwa mortgage huko ulaya au kwingineko na akatakiwa kulipa kwa kipindi cha miaka 30?

People, lets face it. Umasikini TANZANIA hautaisha kwa Gavana Ndullu kuwanyima mikopo wafanyakazi wake. Rather umasikini utaisha kwa wale wanaokabidhiwa dhamana ya kuongoza haya mashirika kwa kuchapa kazi kwa ufanisi kusudi waweze kutoa incentive kwa wafanyakazi wao. Alichokifanya Ndullu ni halali kabisa. Sema tunaona ni abnormal kwa sababu ya umasikini wetu..... wote macho yetu yako BOT. Infact kama mashirika yote yangekuwa yanaendeshwa kwa ufanisi...hii ingekuwa ni namna ya kumotivate watu wachape kazi...

Msisahau kwamba jamani..human being is inherently selfish. Mtu huwezi kumwambia amalize PhD yake Harvard au kwingineko..then aje umpe mshahara wa nyanya! Na mikopo ya namna hii ni mojawapo ya kutoa incetives za kuwa attract wataalamu makini. Hivi Ndullu na PhD yake ya Northwestern..mnadhani angekosa kazi makini huko World Bank au kwingineko? Lets face it. Ndo ukweli unaouma huo.

I may be wrong, lakini nadhani this is a good strategy, as long as watu wanafanya kazi. Harafu tusitake kumsingizia Ndullu..anayeharibu ni JK na serikali yake kwa kushindwa kupambana na ufisadi..there enough for all of us..but when you allow the few to rip off the whole country..even hard working men and women...wanakuwa victims.... Let every hard working man and woman be rewarded. Huwezi sema kwamba kwa vile we are the poorest nation on earth basi mimi Masanja na PhD yangu (mfano) nisipate kitu kusudi tulingane. Hizo ni zama za ujima!

Kama alivyosema Waberoya, its only hard work which can liberate a person from the equation of poverty. Hata hawa wananchi lazima wafike kipindi..wajue kwamba na wao wana obligation kama raia..siyo kutetewa tuu. Mfano wanapohitajika kupiga kura..let them elect serious and responsible leaders. Leo unapewa tshirt unampigia kura fulani..kesho jamaa akijineemesha na wewe unakufa kwa njaa..utamlaumu nani? Otherwise..poverty is here to stay..whether Ndullu gives out Largesse za BoT kwa wafanyakazi wake or not.

Tuache kusingizia ufisadi kila kitu..I say Ndullu amefanya jambo jema. Cha muhimu kuwe na transprency na accountability.

Masanja,

Ni vizuri na ni maneno ya busara uliyoyaeleza but ukae ukijua haya maneno yako yanaapply katika mazingira tofauti na unavyofikiria wewe. Kwanza ukae ukijua mtazamo wa kila mtu alipwe kwa mafanikio au efforts alizozifanya (i.e. pay to performance) ni mtindo unaufanyika katika organisation ambazo mtazamo wake ni profit maximization sasa BOT lengo ni kusimamia pesa za serikali au kumaximize profits!!!!

Perhaps labda tukufafanulie kazi ya BOT imegawanyika katika makundi makuu tano.

Moja Bankers to Bank au msimamizi wa mabenki mengine

Pili Government Banks ambapo inasimamia accounts za serikali.

Tatu Policy making ambapo BOT inasimamia Monetary Policy, vile vile ikishirikiana na Ministry of Finance Kuset up fiscal policy.

Nne Lender of Last Resort kama banks zikiwa na matatizo zinaweza kuenda kuomba rescue BOT.

Tano Clearing house to facilitate payment systems ndani ya nchi.

Sasa kamanda hebu niambie Profit maximization ipo wapi??? Na hoja ya kwamba mtu na PhD ya Harvard kwenda kufanya kazi BOT nataka nikuulize alienda kufanyia kazi nini BOT kama anajua ni civil job. It is a free world akijijua kama yeye ni competitive kwanini asiende HSBC au Barclays ambapo watu wanakula bonus ya $1 Million anang'ang'ana na BOT . BOT mhimimiliki wake mkuu ni mimi na wewe tunaolipa kodi tofautisha bonus na incentives za Barclays na BOT ni vitu viwili tofauti mzee BOT ni kazi ya serikali kama ungelikuwa unataka pesa angelienda private sector.
 
Sasa kama BOt ikijiinvolve katika function za Commercial Banks wasipolipa hao wakopaji wa BOT. BOT itaenda kukopa kwako mzee Masanja!!!!. Hivi unajua kilichosababisha Credit Crunch au umeshasahau kabisa.

BOT ikishindwa kurudisha mikopo ya wafanyakazi wake mfano watu 30 wakikopa milioni 100 unazungumzia Billioni 3 ambao ni mtaji wa kuanzisha benki Tanzania je masanja utawasaidia kulipa!!!!
 
Mndondoaji,

..BOT lazima iwe na uwezo wa ku-compete for, na ku-attract, the best brains nchini. majukumu ya BOT ni muhimu sana kwa ustawi wa uchumi wa Tanzania.

..hebu tujadili ni jinsi gani watumishi wa BOT wataweza kupata incentives kama mikopo ya nyumba.
 
Mndondoaji,

..BOT lazima iwe na uwezo wa ku-compete for, na ku-attract, the best brains nchini. majukumu ya BOT ni muhimu sana kwa ustawi wa uchumi wa Tanzania.

..hebu tujadili ni jinsi gani watumishi wa BOT wataweza kupata incentives kama mikopo ya nyumba.

Unayozungumza yana natija but ukae ukijua kila mtu anavalue na mipangilio ya maisha yake. BOT inatakiwa iattract best brains but nadhani best brains wengine wanaishia kwenda katika private sector.

Kufanya kazi BOT ni kama kuwa waziri wa afya au kufanya kazi wizara sio kila mtu ana passion hiyo. Lazima tuajiri watu wanaopenda kufanya kazi BOT na sio kuvutiwa kuja BOT. Tukiwa tunacreate a bonus culture Tanzania tutaumia maana usaniii wa hali ya juu utatokea hivyo basi la kwanza BOT lazima wakubali kuwaachia wasiotaka kufanya kazi BOT kwa moyo wakaondoka kama wanavyoondoka watu katika academic institution sio kila mtu anapenda kufanya kazi BOT let us be honest!!!.

Tuje katika staff incentives nadhani BOT wanaappraisal zao na mikopo ya wafanyakazi kutokana na vyeo vyao. Swala ni kwamba ni mikopo ya aina gani na inatolewaje. Mfano mkopo wa nyumba kimtazamo wangu wangelikaa wakaingia ubia na NSSF wapewe au kujengewa nyumba wanaotaka nyumba (na hawana nyumba za kwao). Pili incentives zinaweza kuwa in form of training, cheo na kadhalika. But mikopo inayotolewa na BOT inapitia through commercial banks au building society ambao wanacharge interests, wanalipa tax na hivyo serikali inapata faida na sio kutoa in house loans kama hizi.
 
Mdondoaji said:
Tuje katika staff incentives nadhani BOT wanaappraisal zao na mikopo ya wafanyakazi kutokana na vyeo vyao. Swala ni kwamba ni mikopo ya aina gani na inatolewaje. Mfano mkopo wa nyumba kimtazamo wangu wangelikaa wakaingia ubia na NSSF wapewe au kujengewa nyumba wanaotaka nyumba (na hawana nyumba za kwao). Pili incentives zinaweza kuwa in form of training, cheo na kadhalika. But mikopo inayotolewa na BOT inapitia through commercial banks au building society ambao wanacharge interests, wanalipa tax na hivyo serikali inapata faida na sio kutoa in house loans kama hizi.

Mdondoaji,

..kwenye suala la incentives na jinsi gani ya kuwapa hiyo mikopo tuko pamoja. naomba urejee posting yangu # 36.
 
Mdondoaji,

..kwenye suala la incentives na jinsi gani ya kuwapa hiyo mikopo tuko pamoja. naomba urejee posting yangu # 36.

Yap nafahamu ulicommet hivyo na nakubaliana nawewe 100% but in house loans no.

Hivi unajua mikopo yao hii mara nyingi almost zero interest kama unavyoenda kukopa kwa dingi kama anazo!!!!
 
Ama kweli tumedumaa katika Ujamaa dumavu!

Kwanza, Benki Kuu haijiendeshi kwa kodi za Wananchi, bali ni kutokana na faida yakufanya biashara na mabenki na Serikali kuu! Ondoeni dhana kuwa pesa za mishahara na matumizi ya kawaida ya Benki Kuu ni sehemu ya kodi. Pesa za kodi ni za TRA, nao wanaweka fedha zao Benki Kuu na kutozwa riba, sawa na Serikali Kuu inavyotozwa riba kutokana na kukopa Benki Kuu.

Ndio ni Benki ya kudhibiti uchumi na masuala yote ya pesa yako mikononi mwake. Lakini wao ni wapitishaji na wasimamizi tuu, pesa za walipa kodi ziko Hazina (Wizara ya Fedha)!

Kitendo cha wao kutoa mikopo ya unafuu kwa wafanyakazi wake si jambo geni au la kustaajabisha! Kwenye nchi tajiri, kila mwajiri hutoa huduma fulani za unafuu, iwe ni discount au riba ya chini midhali mtu anatimiza masharti.

Mfano, kwenye maduka ya kuuza stationary, unaweza kukuta wafanyakazi wanapewa discount ya 35% kwa kila kitu. Kwenye mabenki, sehemu yha motisha ni discounted rates, free products kama vile sheking account with no fee na vingine vingi, ikiwa ni motisha kwa wafanyakazi. Mashirika mengine hutoa motisha wa kuchangia mpaka 6% shilingi kwa shilingi kwa akiba ya mfanyakazi ya kustaafu!

Kwa suala la Wizara Tanzania, mwajiri wao si Benki Kuu, bali ni Serikali ya Tanzania. Sasa kama ni kelel tunadai waalimu hawapewi mikopo, basi tussillaumu Shirika linalojiendesha kuwa eti nalo liingie katika matongotongo ya giza kwa kuwa eti Serikali Kuu imedumaa!

Binafsi nilitarajia mashirikia kama NSSF, PPF, Bima, na mengine ambayo yana faida kubwa na fedha za ziada, zingekuwa na mipango kama hii ya Benki Kuu.

Fedha hizi watakazopoewa hawa ndugu si mikopo na watakatwa katika mishahara yao na sehemu ya mafao yao ya kustaafu? Je tatizo liko wapi?

Kama BOT wameonelea kuwa kutoa mikopo ni njia moja ya kutoa motisha badala ya kuongeza mishahara, je kwa nini tusiwapongeze kwa hilo?

Na mikopo hii ni binafsi kwa wafanyakazi ambao wanataka kujenga nyumba, wasiotaka shauri lao, wanaoendelea kukaa kwenye nyumba za Shirika na kuzembea kupata mkopo shauri lao, wasioona umuhimu na maana ya kujijengea nyumba shauri lao!

Inabidi tubadilishe mawazo na kuwa Wajamaa Waendelevu na kuacha kung'ang'ania nongwa na kuona kila kitu kuwa ni kibaya na kukifanya ni sumu!
 
Ama kweli tumedumaa katika Ujamaa dumavu!

Kwanza, Benki Kuu haijiendeshi kwa kodi za Wananchi, bali ni kutokana na faida yakufanya biashara na mabenki na Serikali kuu! Ondoeni dhana kuwa pesa za mishahara na matumizi ya kawaida ya Benki Kuu ni sehemu ya kodi. Pesa za kodi ni za TRA, nao wanaweka fedha zao Benki Kuu na kutozwa riba, sawa na Serikali Kuu inavyotozwa riba kutokana na kukopa Benki Kuu.

Ndio ni Benki ya kudhibiti uchumi na masuala yote ya pesa yako mikononi mwake. Lakini wao ni wapitishaji na wasimamizi tuu, pesa za walipa kodi ziko Hazina (Wizara ya Fedha)!

Kitendo cha wao kutoa mikopo ya unafuu kwa wafanyakazi wake si jambo geni au la kustaajabisha! Kwenye nchi tajiri, kila mwajiri hutoa huduma fulani za unafuu, iwe ni discount au riba ya chini midhali mtu anatimiza masharti.

Mfano, kwenye maduka ya kuuza stationary, unaweza kukuta wafanyakazi wanapewa discount ya 35% kwa kila kitu. Kwenye mabenki, sehemu yha motisha ni discounted rates, free products kama vile sheking account with no fee na vingine vingi, ikiwa ni motisha kwa wafanyakazi. Mashirika mengine hutoa motisha wa kuchangia mpaka 6% shilingi kwa shilingi kwa akiba ya mfanyakazi ya kustaafu!

Kwa suala la Wizara Tanzania, mwajiri wao si Benki Kuu, bali ni Serikali ya Tanzania. Sasa kama ni kelel tunadai waalimu hawapewi mikopo, basi tussillaumu Shirika linalojiendesha kuwa eti nalo liingie katika matongotongo ya giza kwa kuwa eti Serikali Kuu imedumaa!

Binafsi nilitarajia mashirikia kama NSSF, PPF, Bima, na mengine ambayo yana faida kubwa na fedha za ziada, zingekuwa na mipango kama hii ya Benki Kuu.

Fedha hizi watakazopoewa hawa ndugu si mikopo na watakatwa katika mishahara yao na sehemu ya mafao yao ya kustaafu? Je tatizo liko wapi?

Kama BOT wameonelea kuwa kutoa mikopo ni njia moja ya kutoa motisha badala ya kuongeza mishahara, je kwa nini tusiwapongeze kwa hilo?

Na mikopo hii ni binafsi kwa wafanyakazi ambao wanataka kujenga nyumba, wasiotaka shauri lao, wanaoendelea kukaa kwenye nyumba za Shirika na kuzembea kupata mkopo shauri lao, wasioona umuhimu na maana ya kujijengea nyumba shauri lao!

Inabidi tubadilishe mawazo na kuwa Wajamaa Waendelevu na kuacha kung'ang'ania nongwa na kuona kila kitu kuwa ni kibaya na kukifanya ni sumu!

Hebu tupe mfano wa watu wasio wajamaa wadumavu ambao Benki Kuu zao zinatoa mortgage kwa wafanyakazi wao!!! Kama benki kuu inatoa mikopo kwa wafanyakazi ya aina hii hiyo who will manage their risk. Wale jamaa wa banking supervision wanafanya kazi gani????
 
unayozungumza yana natija but ukae ukijua kila mtu anavalue na mipangilio ya maisha yake. Bot inatakiwa iattract best brains but nadhani best brains wengine wanaishia kwenda katika private sector.

Kufanya kazi bot ni kama kuwa waziri wa afya au kufanya kazi wizara sio kila mtu ana passion hiyo. lazima tuajiri watu wanaopenda kufanya kazi bot na sio kuvutiwa kuja bot. Tukiwa tunacreate a bonus culture tanzania tutaumia maana usaniii wa hali ya juu utatokea hivyo basi la kwanza bot lazima wakubali kuwaachia wasiotaka kufanya kazi bot kwa moyo wakaondoka kama wanavyoondoka watu katika academic institution sio kila mtu anapenda kufanya kazi bot let us be honest!!!.

Tuje katika staff incentives nadhani bot wanaappraisal zao na mikopo ya wafanyakazi kutokana na vyeo vyao. Swala ni kwamba ni mikopo ya aina gani na inatolewaje. mfano mkopo wa nyumba kimtazamo wangu wangelikaa wakaingia ubia na nssf wapewe au kujengewa nyumba wanaotaka nyumba (na hawana nyumba za kwao). pili incentives zinaweza kuwa in form of training, cheo na kadhalika. But mikopo inayotolewa na bot inapitia through commercial banks au building society ambao wanacharge interests, wanalipa tax na hivyo serikali inapata faida na sio kutoa in house loans kama hizi.

pay ni kitu ambacho kinaatract best brains, bot sio football club eti unashangilia kwa ajili ya mapenzi. Moja ya vitu ambavyo mtu anapenda kufanya kazi sehemu ni pay.

Mfano wako wa nssf ni mbaya kupita kiasi. Kama bot wanaweza kuwapa wafanyakazi wao direct mikopo ya nyumba na kuavoid middle man (nssf) kwa nini wasifanye hivyo?
Hela itoke iende nssf, alafu nssf wawajenge nyumba mbaya kwa bei mbaya, alafu wafanyakazi wa bot walipe interest nssf

je nssf wakitaka kuwapa wafanyakazi wao mikopo ya nyumba waingie ubia na nani????
mimi naona hayo majengo marefu ya nssf yamekuchanganya akili
hii ni part ya nssf, home ownership ni kitu muhimu kwa wafanyakazi wa tz
 
Ama kweli tumedumaa katika Ujamaa dumavu!

Kwanza, Benki Kuu haijiendeshi kwa kodi za Wananchi, bali ni kutokana na faida yakufanya biashara na mabenki na Serikali kuu! Ondoeni dhana kuwa pesa za mishahara na matumizi ya kawaida ya Benki Kuu ni sehemu ya kodi. Pesa za kodi ni za TRA, nao wanaweka fedha zao Benki Kuu na kutozwa riba, sawa na Serikali Kuu inavyotozwa riba kutokana na kukopa Benki Kuu.

Ndio ni Benki ya kudhibiti uchumi na masuala yote ya pesa yako mikononi mwake. Lakini wao ni wapitishaji na wasimamizi tuu, pesa za walipa kodi ziko Hazina (Wizara ya Fedha)!

Kitendo cha wao kutoa mikopo ya unafuu kwa wafanyakazi wake si jambo geni au la kustaajabisha! Kwenye nchi tajiri, kila mwajiri hutoa huduma fulani za unafuu, iwe ni discount au riba ya chini midhali mtu anatimiza masharti.

Mfano, kwenye maduka ya kuuza stationary, unaweza kukuta wafanyakazi wanapewa discount ya 35% kwa kila kitu. Kwenye mabenki, sehemu yha motisha ni discounted rates, free products kama vile sheking account with no fee na vingine vingi, ikiwa ni motisha kwa wafanyakazi. Mashirika mengine hutoa motisha wa kuchangia mpaka 6% shilingi kwa shilingi kwa akiba ya mfanyakazi ya kustaafu!

Kwa suala la Wizara Tanzania, mwajiri wao si Benki Kuu, bali ni Serikali ya Tanzania. Sasa kama ni kelel tunadai waalimu hawapewi mikopo, basi tussillaumu Shirika linalojiendesha kuwa eti nalo liingie katika matongotongo ya giza kwa kuwa eti Serikali Kuu imedumaa!

Binafsi nilitarajia mashirikia kama NSSF, PPF, Bima, na mengine ambayo yana faida kubwa na fedha za ziada, zingekuwa na mipango kama hii ya Benki Kuu.

Fedha hizi watakazopoewa hawa ndugu si mikopo na watakatwa katika mishahara yao na sehemu ya mafao yao ya kustaafu? Je tatizo liko wapi?

Kama BOT wameonelea kuwa kutoa mikopo ni njia moja ya kutoa motisha badala ya kuongeza mishahara, je kwa nini tusiwapongeze kwa hilo?

Na mikopo hii ni binafsi kwa wafanyakazi ambao wanataka kujenga nyumba, wasiotaka shauri lao, wanaoendelea kukaa kwenye nyumba za Shirika na kuzembea kupata mkopo shauri lao, wasioona umuhimu na maana ya kujijengea nyumba shauri lao!

Inabidi tubadilishe mawazo na kuwa Wajamaa Waendelevu na kuacha kung'ang'ania nongwa na kuona kila kitu kuwa ni kibaya na kukifanya ni sumu!


Asante sana mchungaji.

Tatizo kubwa kwa sisi wa tanzania ni siasa za mzee wetu..aliyetuaminisha kwamba binadamu wote ni sawa. Na mtu anakuja hapa bila aibu anaweka argument ya mwalimu na policy director wa BOT! Jamani huo usawa haupo sehemu yoyote duniani. Sorry to be brutal. But if you are a teacher you will get what teachers get! Otherwise..kutakuwa hakuna umuhimu wa kusoma.

Tunachotakiwa kupigania kama wananchi..ni level playing field. Mazingira yamuwezeshe kila mtu kuhangaika na kufanikiwa. In otherwise kama TANESCO, ATCL, TRA nk wangekuwa wanafanya hivi..wengi wangeinuka..ila ndo hao hao..wanaua hayo mashirika. Kama wewe ni mwajiriwa wa serikali..kosa siyo la Ndullu..ni la central government. Hivi jiulizeni..hela zinazopotea kila siku serikali kuu..kwa rushwa na safari....zingeboresha vipi maslahi ya wafanyakazi wake?

Jamani mpaka hapa sijaona kosa la Ndullu...kuwapa watu wake opportunity ya kupewa mkopo! Tena wamekuwa wawazi! Hivi huyu anayesema eti aliye na PhD ya Harvard..aende HCBC au Barclays..ana nia njema na taifa letu kweli? kwa hiyo wewe unahalalisha kwamba serikali ndo sehemu ya mediocres (sorry for the word). Jamani kila sehemu tunahitaji wataalam!

Mfano UN...scale ya mshahara wake...unabase kwenye nchi mwanachama ambaye analipa mshahara wa juu. Ambayo mpaka leo ni serikali ya Marekani! Wanafanya hivi kuweza kuattract anyody from anywhere. Unafikiri kwa nini hawakuweka kigezo cha private sector au kwingineko? precisely because mishahara ya private ni mikubwa sana. Hapa assumption ni kwamba kama UN itahitaji kuajiri muamerica..basi haina budi kumlipa kama ambavyo angelipwa nyumbani kwao! Simple! Hapo ndo akina chokambaya toka dunia ya nne..wanapoponea..maana...they get salaries at the scale..which they can never dream of in their own countries. Yet, mtu wa US...hata akiondoka sehemu kama UN..still he can go in his country and get relatively the same amount. Upo hapo?


Anyway, kama anavyosema mchungaji. Hii issue ya Ndullu, tuichukulie kama changamoto. Kila shirika la umma liwajali wafanya kazi wake. Sasa leo TANESCO, ATCL....wananunuliana magari wenyewe..wakati wanafukuza wafanyakazi...na kesho tunamlaumu Ndullu! Lets be creative to create wealth. Hii kwamba Masanja afanye kazi harafu tugawane....nadhani in real world..it doesnt exist anymore. We should ALL be responsible!

Masanja,
 
Ama kweli tumedumaa katika Ujamaa dumavu!

Kwanza, Benki Kuu haijiendeshi kwa kodi za Wananchi, bali ni kutokana na faida yakufanya biashara na mabenki na Serikali kuu! Ondoeni dhana kuwa pesa za mishahara na matumizi ya kawaida ya Benki Kuu ni sehemu ya kodi. Pesa za kodi ni za TRA, nao wanaweka fedha zao Benki Kuu na kutozwa riba, sawa na Serikali Kuu inavyotozwa riba kutokana na kukopa Benki Kuu.

Ndio ni Benki ya kudhibiti uchumi na masuala yote ya pesa yako mikononi mwake. Lakini wao ni wapitishaji na wasimamizi tuu, pesa za walipa kodi ziko Hazina (Wizara ya Fedha)!

Kitendo cha wao kutoa mikopo ya unafuu kwa wafanyakazi wake si jambo geni au la kustaajabisha! Kwenye nchi tajiri, kila mwajiri hutoa huduma fulani za unafuu, iwe ni discount au riba ya chini midhali mtu anatimiza masharti.

Mfano, kwenye maduka ya kuuza stationary, unaweza kukuta wafanyakazi wanapewa discount ya 35% kwa kila kitu. Kwenye mabenki, sehemu yha motisha ni discounted rates, free products kama vile sheking account with no fee na vingine vingi, ikiwa ni motisha kwa wafanyakazi. Mashirika mengine hutoa motisha wa kuchangia mpaka 6% shilingi kwa shilingi kwa akiba ya mfanyakazi ya kustaafu!

Kwa suala la Wizara Tanzania, mwajiri wao si Benki Kuu, bali ni Serikali ya Tanzania. Sasa kama ni kelel tunadai waalimu hawapewi mikopo, basi tussillaumu Shirika linalojiendesha kuwa eti nalo liingie katika matongotongo ya giza kwa kuwa eti Serikali Kuu imedumaa!

Binafsi nilitarajia mashirikia kama NSSF, PPF, Bima, na mengine ambayo yana faida kubwa na fedha za ziada, zingekuwa na mipango kama hii ya Benki Kuu.

Fedha hizi watakazopoewa hawa ndugu si mikopo na watakatwa katika mishahara yao na sehemu ya mafao yao ya kustaafu? Je tatizo liko wapi?

Kama BOT wameonelea kuwa kutoa mikopo ni njia moja ya kutoa motisha badala ya kuongeza mishahara, je kwa nini tusiwapongeze kwa hilo?

Na mikopo hii ni binafsi kwa wafanyakazi ambao wanataka kujenga nyumba, wasiotaka shauri lao, wanaoendelea kukaa kwenye nyumba za Shirika na kuzembea kupata mkopo shauri lao, wasioona umuhimu na maana ya kujijengea nyumba shauri lao!

Inabidi tubadilishe mawazo na kuwa Wajamaa Waendelevu na kuacha kung'ang'ania nongwa na kuona kila kitu kuwa ni kibaya na kukifanya ni sumu!

umeseme yote. ndio tanzania hiyo. ufisadi umekuwa ndio wimbo wa taifa. hakuna mengine ya kufanya
 
Ama kweli tumedumaa katika Ujamaa dumavu!

Kwanza, Benki Kuu haijiendeshi kwa kodi za Wananchi, bali ni kutokana na faida yakufanya biashara na mabenki na Serikali kuu! Ondoeni dhana kuwa pesa za mishahara na matumizi ya kawaida ya Benki Kuu ni sehemu ya kodi. Pesa za kodi ni za TRA, nao wanaweka fedha zao Benki Kuu na kutozwa riba, sawa na Serikali Kuu inavyotozwa riba kutokana na kukopa Benki Kuu.

Ndio ni Benki ya kudhibiti uchumi na masuala yote ya pesa yako mikononi mwake. Lakini wao ni wapitishaji na wasimamizi tuu, pesa za walipa kodi ziko Hazina (Wizara ya Fedha)!

Kitendo cha wao kutoa mikopo ya unafuu kwa wafanyakazi wake si jambo geni au la kustaajabisha! Kwenye nchi tajiri, kila mwajiri hutoa huduma fulani za unafuu, iwe ni discount au riba ya chini midhali mtu anatimiza masharti.

Mfano, kwenye maduka ya kuuza stationary, unaweza kukuta wafanyakazi wanapewa discount ya 35% kwa kila kitu. Kwenye mabenki, sehemu yha motisha ni discounted rates, free products kama vile sheking account with no fee na vingine vingi, ikiwa ni motisha kwa wafanyakazi. Mashirika mengine hutoa motisha wa kuchangia mpaka 6% shilingi kwa shilingi kwa akiba ya mfanyakazi ya kustaafu!

Kwa suala la Wizara Tanzania, mwajiri wao si Benki Kuu, bali ni Serikali ya Tanzania. Sasa kama ni kelel tunadai waalimu hawapewi mikopo, basi tussillaumu Shirika linalojiendesha kuwa eti nalo liingie katika matongotongo ya giza kwa kuwa eti Serikali Kuu imedumaa!

Binafsi nilitarajia mashirikia kama NSSF, PPF, Bima, na mengine ambayo yana faida kubwa na fedha za ziada, zingekuwa na mipango kama hii ya Benki Kuu.

Fedha hizi watakazopoewa hawa ndugu si mikopo na watakatwa katika mishahara yao na sehemu ya mafao yao ya kustaafu? Je tatizo liko wapi?

Kama BOT wameonelea kuwa kutoa mikopo ni njia moja ya kutoa motisha badala ya kuongeza mishahara, je kwa nini tusiwapongeze kwa hilo?

Na mikopo hii ni binafsi kwa wafanyakazi ambao wanataka kujenga nyumba, wasiotaka shauri lao, wanaoendelea kukaa kwenye nyumba za Shirika na kuzembea kupata mkopo shauri lao, wasioona umuhimu na maana ya kujijengea nyumba shauri lao!

Inabidi tubadilishe mawazo na kuwa Wajamaa Waendelevu na kuacha kung'ang'ania nongwa na kuona kila kitu kuwa ni kibaya na kukifanya ni sumu!
Hivi Mtaji wa Benki Kuu umetokana na kufanya Biashara na Serikali na Hayo Mabenki?
Na Leo hii huo Mtaji umebadilika kuwa wa watu wengine zaidi ya Serikali ya JMT.
Je tutajenga uchumi wa Tanzania Hii au hizo Nyumba kwa kuangalia wafanyakazi wa Benki Kuu tu? ambao wapo DSM, Arusha, Mza na Mbeya?
Je S'wanga itajengeka Vipi, Tabora, Mpanda, Iringa nk
Je Greespan wetu (Ndullu) uwezo wake wa kufikiri ndio umeishia kwenye kutoa incentive kwa wafanya kazi wa Benki Kuu ambao wanaweza kuwa 600 au chini ya Hapo.
Je kwa stlye hio tunataka kumwambia Nini mfanyakazi asiye fanya Benki Kuu, mfano Polisi ambao Bajeti yao ni ya mwaka kwa mwaka wakati mkopo wa nyumba unabidi uende mpaka Miaka 5 na kuendelea? Je na Polisi au Asakari Magereza ajiuzie "stationery" zinazopatikana Ofisini kwake kwa Discount?
Je Nurse, Doctor na wahudumu wa Afya tunawasaidia Vipi? na Wafanyakazi wa Mahakama, Kilimo nk nk?
Je Best Brains zinatakiwa BOT tu?
Vyuo Vyetu havihitaji hizo Best Brains. Au uchumi wa Tanzania Utajengwa na Benki Kuu kuwa na Best Brains?
Hapo nyuma kuliwahi kuwa na malalamiko kuhusu Mikopo inayotolewa kwa Sumaye na Idrisa toka NSSF na kadhalika basada ya hapo wakaanza kwa wakurugenzi na Mameneja, sasa hivi kwa Staff wote, lakini ujeu kwamba kunakuwa na urasimu kwa sababu ni lazima wabalance kinachoingia na kinachotoka, Sasa kutokana na Hizo changa moto ni wazi sio njia iliyo sahihi kututoa katika tatizo la kukosekana kwa mortgage na pia sio njia sahihi ya kukuza Pension Funds zetu, interest free loans kwa Staff or at a reduce rate? wakati mchangiaji au mwanachama hazioni hizo Pesa mpaka afike 65. Au akipewa Mkopo at Higher interest.
Je leo hii BOT wanakitengo maalum cha kumanage Mikopo kama Hii, maana haipo katika Role ya BOT hivyo kulinganisha na Stationery store ambayo itampunguzia staff wake Bei ya Bidhaa zake, ikiwa Barclays Bank au NMB, au NMC etc kwa sababu wana department ya mikopo , hivyo kuhandle kitu kama hiki ni rahisi, kwani ni moja katika majukumu yao, saana sana watakacho fanya ni kumpa hiyo interest rate ya chini, ambayo haitakiwa kuwa below interest rate wanayo toa kwa ajili ya Depositor ili angalau wa-break even na in most cases itakuwa juu zaidi kwa 2% lakini haitofikia wanayotoza wateja wao ili kukidhi gharama zingine kame za management ya huo mkopo na kufidia ile dhamani ya pesa.
na kwa kumalizia ningependa kukuliza Je BOT inaupinzani katika Shughuli zake ili uweze sema kwanini wasipate Faida? Au hiyo faida inatokana na utumishi uliotukuka?
 
Chikawe kawaambia tuko katika Ubepari, so get rid of emotions!

We can never run a country with too much emotions na kudai eti kwa nini polisi wanakaa mbavu za mbwa!

Je salary scale ya Polisi inaendana na mtu ambaye ni mganga wa meno au karani?

Kila kitu kina merits zake, so far kwa BOT kutoa mikopo kwa wafanyakazi wake kitu ambacho wana uezo ndani ya bajeti yao tusikionee wivu!

Kwanza hebu jiulizeni, ilikuwaje tukaua viwanda kwa kutumia corporate welfare ambapo kila kitu kilikuwa ni bure? nyumba, gari uniform, matibabu na hata chakula cha mchana?

We are in transition and may the best and strong win.

Kama mnataka kutoa sympahty kwa watu kwa hili la uwiano, mnabidi muwakamate koo wabunge na Serikali.

Hivi leo TBL na TCC wakitoa motisha wa namna hii tutalalakmika kwa ni na wa Chibuku au Mataputapu wasipewe?

Katika mfumo chanya wa uchumi, motisha kama huu unaweza kupokelewa kama shukrani kutoka kwa mwajiri kutokana na wafanyakazi kumwezesha mwajiri wao kutimiza malengo kadhaa. Ndio maana nikauliza, je leo hii wakiamua kuwa waongeze mishahara kwa kuwa tunawaonea gere la mikopo tutasemaje?

Au kama BOT wangetoa dhamana kwa wafsnyakazi wao waende TIB au NSSF kukopa, bado tungeendelea kutoa lawama?

Ndio maana nasema ni udumavu wa sera mufilisi za ujima na wala si ujamaa wa kiafrika!

Ndiyo yale yale ya zamani ya kuchukia mtu mwenye gari au redio, na kumfanya adui!
 
Hivi Mtaji wa Benki Kuu umetokana na kufanya Biashara na Serikali na Hayo Mabenki?
Na Leo hii huo Mtaji umebadilika kuwa wa watu wengine zaidi ya Serikali ya JMT.
Je tutajenga uchumi wa Tanzania Hii au hizo Nyumba kwa kuangalia wafanyakazi wa Benki Kuu tu? ambao wapo DSM, Arusha, Mza na Mbeya?
Je S'wanga itajengeka Vipi, Tabora, Mpanda, Iringa nk
Je Greespan wetu (Ndullu) uwezo wake wa kufikiri ndio umeishia kwenye kutoa incentive kwa wafanya kazi wa Benki Kuu ambao wanaweza kuwa 600 au chini ya Hapo.
Je kwa stlye hio tunataka kumwambia Nini mfanyakazi asiye fanya Benki Kuu, mfano Polisi ambao Bajeti yao ni ya mwaka kwa mwaka wakati mkopo wa nyumba unabidi uende mpaka Miaka 5 na kuendelea? Je na Polisi au Asakari Magereza ajiuzie "stationery" zinazopatikana Ofisini kwake kwa Discount?
Je Nurse, Doctor na wahudumu wa Afya tunawasaidia Vipi? na Wafanyakazi wa Mahakama, Kilimo nk nk?
Je Best Brains zinatakiwa BOT tu?
Vyuo Vyetu havihitaji hizo Best Brains. Au uchumi wa Tanzania Utajengwa na Benki Kuu kuwa na Best Brains?
Hapo nyuma kuliwahi kuwa na malalamiko kuhusu Mikopo inayotolewa kwa Sumaye na Idrisa toka NSSF na kadhalika basada ya hapo wakaanza kwa wakurugenzi na Mameneja, sasa hivi kwa Staff wote, lakini ujeu kwamba kunakuwa na urasimu kwa sababu ni lazima wabalance kinachoingia na kinachotoka, Sasa kutokana na Hizo changa moto ni wazi sio njia iliyo sahihi kututoa katika tatizo la kukosekana kwa mortgage na pia sio njia sahihi ya kukuza Pension Funds zetu, interest free loans kwa Staff or at a reduce rate? wakati mchangiaji au mwanachama hazioni hizo Pesa mpaka afike 65. Au akipewa Mkopo at Higher interest.
Je leo hii BOT wanakitengo maalum cha kumanage Mikopo kama Hii, maana haipo katika Role ya BOT hivyo kulinganisha na Stationery store ambayo itampunguzia staff wake Bei ya Bidhaa zake, ikiwa Barclays Bank au NMB, au NMC etc kwa sababu wana department ya mikopo , hivyo kuhandle kitu kama hiki ni rahisi, kwani ni moja katika majukumu yao, saana sana watakacho fanya ni kumpa hiyo interest rate ya chini, ambayo haitakiwa kuwa below interest rate wanayo toa kwa ajili ya Depositor ili angalau wa-break even na in most cases itakuwa juu zaidi kwa 2% lakini haitofikia wanayotoza wateja wao ili kukidhi gharama zingine kame za management ya huo mkopo na kufidia ile dhamani ya pesa.
na kwa kumalizia ningependa kukuliza Je BOT inaupinzani katika Shughuli zake ili uweze sema kwanini wasipate Faida? Au hiyo faida inatokana na utumishi uliotukuka?

Ama huelewi jinsi gani BOT inafanya kazi au ni ugumu usioeleweka.

Pesa ya mapato kwa BOT kama BOT si pesa ya Serikali ya TZ ambayo iko chini ya Hazina!

Mapato ya TRA, kuuza Pareto na upupu mwingine hizo ni pesa za Serikali ambazo BOT kazi yake ni kuziangalia na kuzilinda na wanalipwa fedha kwa kufanya kazi hiyo.

Malipo yao ndio wanayoyatumia kwa mishahara, majengo na mengine.

Msianze kuchanganyikiwa kudhani mishahara ya BOT inatokana na kodi za mwananchi.

Leo hii wao BOT tunawalipa tunaona kikorosho, lakini tukiletewa Mzungu au MChina tutamlipa bila tatizo?

Wao kuishauri Serikali ni wajibu wao na wanalipwa kwa kazi hiyo, Serikali ikivurunda ni juu ya Serikali na si BOT na ndio maana hutakaa hata siku moja maishani mwako usikie Benki Kuu yeyote Duniani inatangaza bajeti ya nchi!

Kwa wale ambao hawajaajiriwa BOT, waambie wamshikie bango mwajiri wao au wafanye bidii nao waajiriwe BOT, IMF, Voda au Ubalozi wa Marekani!
 
Ni mawazo mgando vile vile kufikiria kuwa uchumi wa kibepari unaendeshwa kiholela kama baadhi ya watu wanavyotaka kutuaminisha si kweli. Mikopo ya hovyo kama hii kwa wafanya kazi wa BoT ndiyo inayo distort circulation ya pesa na kusababisha spiralling ya inflation.

Mashirika yote zamani yalikuwepo kwenye hii bonanza ya kuwagawia wafanyakazi wake fedha kwa mfumo wa kutoa mikopo isiyokuwa na riba. Matokeo yake mambo haya yalisababisha mashirika mengi kufa. Benki kuu inaweza kufa ikifanya ujinga huo? Haiwezi benki kuu itachota moja kwa moja kutoka hazina.

Kulinda soko ni lazima kuwa na Busara katika ufanyaji wa maamuzi. Haya nayaita ni maamuzi ya kijinga wakati huu ambao tuna sera ya serikali kutojihusisha na Biashara. Taasisi nyingine zote wanachofanya ni kujadiliana na Mabenki ili wafanyakazi wao wapate interrest naffuu. Hata Benki kuu hizi fedha wangezikopesha kwa mabenki kwa masharti nafuu zaidi halafu mabenki ya Biashara ndo yakatoa mikopo hiyo kwa wafanyakazi wa benki kuu, hata kama ni kwa interrest kidogo zaidi kuliko wengine fedha hii ingekuwa na maana zaidi. Fedha ingeingia kwenye circulation kwa kufuata sheria zote za mfumo wa kibepari na hao wafanyakazi wangekuwa makini wakati wa manunuzi ya vifaa vyao. Lakini kitakacho tokea ni mtu kwenda kununua kiwanja akiambiwa ni milioni tano anatoa tu bila hata negotiation kwa sababu fedha yake amechotewa tu!! Hii ndo inflation wajomba!

Tatizo wengi hapa tunajiita mabepari wakati bado hangover ya ujamaa ni kubwa. Hii kutoa fedha kwa mtindo kama huo ni hangover ya ujamaa. Tunaamini kuwa tunafanya ubepari, lakini ni uongo. Ubepari unahakikisha kuwa watu hawagawiwi hovyo hovyo bila kufanyia kazi. Ubepari haugawi vitu bure. Hii si mikopo. Ni kama watu kupewa bure, ni mikopo gani isiyo na riba? Ni kutoa bure. Hata kama ina riba, ni sheria gani inayowaruhusu benki kuu kutoa mikopo kwa individuals? LAZIMA TUUNGALIE UBEPARI KWA KILE AMBACHO NI UBEPARI. Tusiwe tunafanya mambo ya kijamaa halafu tunadai eti tunatekeleza ubepari, ubepari wa wapi wa kugawiana bure? Hapa ni rahisi. Benki kuuu wanachota fedha kwa kucharge interrest kwenye kodi za Wabongo halafu wanajidai eti wanafanya biashara, wanashindana na nani?

Kwa mtindo huo Benki kuu inashindana na Mabenki ya Biashara kutoa mikopo ambalo si jambo la haki kabisa. Inabidi Sheria zetu ziwe makini. Hapa ni watu kujigawia chao mapema halafu tunajificha kwenye kichaka cha eti tunatekeleza Ubepari, huo ni uongo, tena ni uzandiki. Hii inasababisha Mabenki ya Biashara kuendelea kucharge riba kubwa kwa wateja wachache wanaowapata. Cream ya watu ambao wanakopesheka na Mabenki mengine ndo hawa hawa ambao Benki kuu inawapa fedha bila riba. Sasa akienda kukopa Benki Mwalimu ni lazima Benki wamcharge interrest kubwa tu.

Hii ni mbovu na inavuruga uchumi, na huu si ubepari. Ni hangover ya ujamaa hii. Mabepari hawagawi bure hata siku moja. Lazima warudishe hata gharama. Mikopo kama hii bila riba hairudishi hata gharama. Ni kuwagawia bure! Kuhakikisha kuwa gharama inarudi lazima fedha hii ingepitishwa kwenye Mabenki ya biashara kwani ndo yanajua na yana utaalamu wa kukokotoa gharama halisi. Hapa Benki kuu hakuna cha ndullu wala nini, wamezama kwenye hangover ya ujamaa tu, full stop.
 
Kwa mtindo huo Benki kuu inashindana na Mabenki ya Biashara kutoa mikopo ambalo si jambo la haki kabisa. Inabidi Sheria zetu ziwe makini. Hapa ni watu kujigawia chao mapema halafu tunajificha kwenye kichaka cha eti tunatekeleza Ubepari, huo ni uongo, tena ni uzandiki. Hii inasababisha Mabenki ya Biashara kuendelea kucharge riba kubwa kwa wateja wachache wanaowapata. Cream ya watu ambao wanakopesheka na Mabenki mengine ndo hawa hawa ambao Benki kuu inawapa fedha bila riba. Sasa akienda kukopa Benki Mwalimu ni lazima Benki wamcharge interrest kubwa tu.

Ninakubaliana na wewe kwa mawazo yako hapo juu mia/mia.

Tatizo la nchi yetu ni mfumo kama alivyosema Salim Ahmed Salim.

Ukichunguza kwa umakini si mikopo tu ya BOT, hata ngazi za mishahara n.k. Tokea serikali waanze kuchagua BOT, TRA kuwa wao ndo wapate mishahara ya kipekee, wakatofautisha na wafanyakazi wa Serikalini, Polisi, Walimu n.k hapo ndo huo Upepari anaoanza kuuzungumza Chikawe na sisi humu tunapinga kuwa hii nchi haiendeshwi hivyo kumbe ndivyo.

Tunahitaji Kiongozi Madhubuti wa kufumua kila mahala ila ndo hivyo tena sisi wenyewe (Wanachi) bado hatujitambui. Ukiitishwa uchaguzi kesho Polisi, Walimu, mwanachi wa kima cha chini hao hao ndo wanaoongoza kwenda kumsimika kiongozi ambaye na yeye hajitambui.

Pia kuna vyombo vinavyosimamia hawa wafanyakazi wote kwa ujumla TUKTA, RAAWU n.k kila kukicha ni migogoro, na wenyewe bado hawajitambui, juzi nilisikia wanataka kuandamana kumpongeza JK kwa uongozi wake!! Hawa ndo wakuwasemea kwenye issue kama hii ya mikopo, mishahara n.k.

Safari bado ni ndefu sana.
 
pay ni kitu ambacho kinaatract best brains, bot sio football club eti unashangilia kwa ajili ya mapenzi. Moja ya vitu ambavyo mtu anapenda kufanya kazi sehemu ni pay.

Mfano wako wa nssf ni mbaya kupita kiasi. Kama bot wanaweza kuwapa wafanyakazi wao direct mikopo ya nyumba na kuavoid middle man (nssf) kwa nini wasifanye hivyo?
Hela itoke iende nssf, alafu nssf wawajenge nyumba mbaya kwa bei mbaya, alafu wafanyakazi wa bot walipe interest nssf

je nssf wakitaka kuwapa wafanyakazi wao mikopo ya nyumba waingie ubia na nani????
mimi naona hayo majengo marefu ya nssf yamekuchanganya akili
hii ni part ya nssf, home ownership ni kitu muhimu kwa wafanyakazi wa tz

Hivi wewe unafahamu kufanya kazi kama civil servant na kufanya kazi private institution ni vitu viwili tofauti. Kwanza kaa ukijiuliza BOT dhumuni ya wenye BOT ambao ni serikali ni kutengeneza faida au kusimamia pesa usizungumze vitu usivyovijua kamanda.

NSSF si mfano mbaya hivi unafahamu wakopaji wengi Tanzania ni waongo. Mie nimefanya kazi bank na nimewahi kusupervise mikopo mtu unakuta anadai anakopa kujenga nyumba kumbe anakopa kwa ajili ampeleke bibi kufanya shoping. Sasa sie tunasema BOT wawape Nssf kazi hiyo kwasababu BOT sio commercial bank na wala building society. NSSF wanafanya vitu hivyo ijapokuwa sio commercial bank but wao ni mmoja ya financial institution za tanzania kwajina lengine ni kama Thrift institution. sasa Kuweka mazingira mazuri itasaidia kucrack down wafanyakazi waongo wanaotaka mikopo wakaendeleze biashara zao vichochoroni.

Vilevile BOT wakiinject pesa kwa NSSF kunakuwa na mzunguko sasa imagine unakopesha watu Bilioni 3 (i.e. 30 X 100 million) halafu hawa wote hawalipi interest yeyote yaani bureeeeee!!! unadhani ni Busara hiyo!!! Gavana Ndulu najua ana nia nzuri but nadhani wenzie huku US, UK na Ujerumani (Nchi zilizokuwa na ubepari uliotukuka) hawafanyi hivyo kamwe kwasababu wanajua haina faida kwa uchumi hata chembe. Sasa ni natija ya mikopo kama hii ni kuwanyamazisha midomo vijana pale BOT wasitoe siri za wakubwa basi
 
Chikawe kawaambia tuko katika Ubepari, so get rid of emotions!

We can never run a country with too much emotions na kudai eti kwa nini polisi wanakaa mbavu za mbwa!

Je salary scale ya Polisi inaendana na mtu ambaye ni mganga wa meno au karani?

Kila kitu kina merits zake, so far kwa BOT kutoa mikopo kwa wafanyakazi wake kitu ambacho wana uezo ndani ya bajeti yao tusikionee wivu!

Kwanza hebu jiulizeni, ilikuwaje tukaua viwanda kwa kutumia corporate welfare ambapo kila kitu kilikuwa ni bure? nyumba, gari uniform, matibabu na hata chakula cha mchana?

We are in transition and may the best and strong win.

Kama mnataka kutoa sympahty kwa watu kwa hili la uwiano, mnabidi muwakamate koo wabunge na Serikali.

Hivi leo TBL na TCC wakitoa motisha wa namna hii tutalalakmika kwa ni na wa Chibuku au Mataputapu wasipewe?

Katika mfumo chanya wa uchumi, motisha kama huu unaweza kupokelewa kama shukrani kutoka kwa mwajiri kutokana na wafanyakazi kumwezesha mwajiri wao kutimiza malengo kadhaa. Ndio maana nikauliza, je leo hii wakiamua kuwa waongeze mishahara kwa kuwa tunawaonea gere la mikopo tutasemaje?

Au kama BOT wangetoa dhamana kwa wafsnyakazi wao waende TIB au NSSF kukopa, bado tungeendelea kutoa lawama?

Ndio maana nasema ni udumavu wa sera mufilisi za ujima na wala si ujamaa wa kiafrika!

Ndiyo yale yale ya zamani ya kuchukia mtu mwenye gari au redio, na kumfanya adui!

Kaka watu hawana wivu na hakuna mtu anafaidika lolote ila la msingi ni je hii mikopo inayotoka karibu na uchaguzi ina faida yeyote kwa uchumi wa Tanzania!!!!

Hatukatai kila Idara na Benki Kuu zina budget zake husika but kinacholalamikiwa hapa ni kitendo cha BOT kuingilia kazi za investment banks na commercial banks na building society.

Umeshawahi kusikia wapi Bank of England ikatoa mortgage financing, Federal Reserve ya US imetoa mortagage. These are toxic assets cause kwanza ni long-term commitment and probability of default ni kubwa na ndio maana banks zinacharge interest kubwa kufidia loss zitakazotokea.

Gavana anasema wanafanya uchunguzi yakinifu kabla ya kutoa mikopo but come on hakuna ambaye anayeweza kutabiri kesho mimi na wewe tutaamkaje. Prof Merton mwenyewe anakwambia probability of default na metrics za kumeausure distance to default cannot full explain default risk exposure. The future is unexplainable sasa BOT inakopesha watu Billion 3 bila ya interest chukulia watu watano kati yao wamefariki baada ya miezi 6 tumepoteza milioni 500 ambazo hizo milioni 500 hata kama tutarecove tunabahati sana kupata 75%. Msitudanganye wazee hatujawa wajinga kiasi hicho.
 
MILANGO ya neema imefunguka kwa wafanyakazi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Kila mfanyakazi ataweza kukopa kati ya Sh 100milioni na Sh 30milioni kulingana na wadhifa wake kwa ajili ya ujenzi wa nyumba.

Habari ambazo Mwananchi imezipata zinasema kwamba mikopo hiyo itatolewa katika madaraja manane. Viwango hivyo vya mikopo ni vipya ambavyo vimetokana na maombi ya wafanyakazi hao ya kuongezewa kiasi cha mikopo hiyo kutoka katika kiwango cha awali walichokuwa wakipewa.

Wafanyakazi wa daraja la chini kabisa, watakuwa wanakopeshwa Sh30milioni, wakati wafanyakazi wa ngazi ya juu kabisa watapata mkopo wa Sh100milioni.

Wafanyakazi wa daraja la kwanza ambalo ni la juu kabisa na ambao watakuwa wanapata mkopo huo wa Sh100milioni ni pamoja na wakurugenzi, wakurugenzi washiriki na wataalamu washauri waandamizi.

Daraja la pili ni la wafanyakazi wenye vyeo vya mameneja na wataalamu washauri ambao watapata mkopo wa Sh90milioni, wakati daraja la tatu linawahusisha mameneja wasaidizi na maafisa wakuu waandamizi (professional I) ambao wao watapata mkopo wa Sh70milioni.

Daraja la nne linawahusisha wafanyakazi wenye vyeo vya maafisa wakuu (professional I) na maafisa wakuu waandamizi (professional II), ambao wao watajipatia mkopo wa Sh 60milioni, huku wafanyakazi katika daraja la tano ni wale wenye vyeo vya maafisa waandamizi (professional I) na maafisa wakuu (professional II) ambao watajipatia mkopo wa Sh 55milioni.

Katika daraja la sita kuna wafanyakazi wenye vyeo vya maafisa ngazi ya III-I (professional I), maafisa waandamizi (professinal II) na maafisa- makarani wakuu (cleric officers) ambao watajipatia mkopo wa Sh45milioni.

Daraja la saba ni la wafanyakazi wenye vyeo vya maafisa-makarani kuanzia ngazi ya III hadi ngazi ya maafisa-makarani waandamizi (cleric officers), makarani waandamizi na makarani wakuu (clerks) ambao wao watajipatia mkopo wa Sh40milioni.

Daraja la nane ambalo ni la chini kabisa linawahusisha wafanyakazi wa taasisi hiyo ambao ni walinzi, wapishi, madereva, wahudumu wa ofisi na wa zahanati na makarani ngazi ya daraja la III-I ambao watapata mkopo wa Sh30milioni.

Habari hizo zinasema kwamba viwango vya awali kwa wafanyakazi wa daraja la kwanza na la pili kama ilivyoainishwa hapo juu vilikuwa ni Sh50milioni, daraja la tatu vilikuwa Sh35milioni, daraja la nne na la tano Sh30milioni.

Katika daraja la sita viwango vya awali vilikuwa ni Sh25milioni, daraja la saba walikuwa wakipata mkopo wa Sh20milioni wakati daraja la nane ambalo ni la chini walikuwa wakipata mkopo wa Sh15milioni.

Kwa mujibu wa waraka uliosainiwa na Naibu Mwenyekiti wa Mfuko wa Mikopo ya Nyumba, Len Kisarika kwenda kwa wafanyakazi wote wa makao makuu na katika matawi ya Mwanza, Arusha, Mbeya, Zanzibar na Chuo cha Benki Mwanza kuwafahamisha kuridhia nyongeza hiyo, menejimenti hiyo imeridhia nyongeza hiyo ya mikopo ili kukidhi ongezeko la gharama za ujenzi.

Katika waraka huo wa Desemba 2, mwaka huu ambao nakala yake imepelekwa kwa Gavana wa BoT, Profesa Beno Ndullu na kwa Manaibu Gavana, menejimenti hiyo pia imeidhinisha ongezeko la kiwango cha mkopo kwa ajili ya matengenezo ya nyumba kutoka asilimia 15 hadi 20 ya mkopo uliotolewa.

Waraka huo pia unabainisha kuwa kufuatana na hali ya Mfuko wa Mikopo ya Nyumba na ili kuhakikisha kuwa mikopo inayotolewa inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa, utoaji wake umefanyiwa marekebisho kutegemea vipaumbele na masharti mbalimbali.

Kwa mujibu wa waraka huo, kipaumbele cha kwanza ni kwa waombaji wapya, cha pili ni maombi ya nyongeza ya mikopo kwa ajili ya nyumba ambazo bado hazijakamilika na kipaumbele cha tatu ni maombi ya nyongeza ya mikopo kwa ajili ya uboreshaji wa nyumba.

Masharti yaliyotajwa katika waraka huo kwa kipaumbele cha kwanza ni pamoja na salio la theluthi moja ya mshahara wa mwombaji baada ya makato, kama ilivyoainishwa kwenye Sheria ndogo za utumishi za (BoT Staff By Laws, 2008), uwezo wa mkopaji kurejesha mkopo na kuwasilisha hati ya kiwanja ambayo haijatolewa kama dhamana na isiyo na kikwazo chochote.

Katika kipaumbele cha pili na cha tatu, mbali na masharti yanayotajwa katika waraka huo pamoja na masharti ya kwenye kipaumbele cha kwanza, kuna nyongeza ambayo ni pamoja na ukaguzi wa nyumba husika itakayofanyiwa uboreshaji kwa kipaumbele cha tatu.

Masharti mengine ya kipaumbele cha pili ni ukaguzi wa nyumba husika ili kuthibitisha hatua iliyofikia katika ujenzi, tathmini ya thamani ya nyumba husika kutoka kwa mthamini wa majengo aliyesajiliwa, tathmini ya kamati ya kuthibitisha kama kiasi cha mkopo kinachoombwa kama kinatosheleza kukamilisha ujenzi wa nyumba husika.

Wakati nchi ina njaa!!! maskini wanaongezeka watu wananeemeka wasikimbie tu tutakapowakomalia kutwambia wanachaji interest kiasi gani hao wanaokopa??? Waliolipa wangapi??? na vigezo vinavyotumika kufatilia mikopo ikishindikana!!!! Hawa jamaa baada ya kupata pesa ya World Bank kwa ajili ya kujenga nyumba za gharama ya bei nafuu kwa wananchi wameenza kuzitafuna haya baba!!! tutabanana tu Tanzania Hivi nyie subirini maskini akizidi kuwa maskini hubadilika na kuwa mnyama (Martin Luther King and Malcom X)!!!


Mnashangaa leo ya BOT, mbona EWURA iliripotiwa hivyo kwamba wakubwa wanakopeshana mpaka milioni 60? Nasikia kashfa hiyo ilisababisha mwandishi mmoja akafukuzwa kazi.
 
Uvujaji nyaraka za serikali wampasua kichwa Mkulo
Na Thobias Mwanakatwe
17th December 2009
B-pepe
Chapa
Maoni
Awapa somo wafanyakazi Hazina
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.

Baada kushamiri kwa wimbi la uvujishaji wa nyaraka nyeti za Serikali ambazo zimeianika vibaya kama kwenye kashfa ya Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na zile za vitambulisho vya taifa, sasa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, anasaka mbinu za kufunika kombe ili mwanaharamu apite.

Waziri Mkulo akifungua Baraza la Wafanyakazi wa wizara yake jana jijini hapa, alitumia fursa hiyo kuwapiga marufuku watumishi hao kuvujisha nyaraka za serikali kwa masuala ya kisiasa hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Mkulo anatoa kauli hiyo ukiwa ni takribani miaka miwili tangu tukio la kwanza la kuvuja kwa nyaraka za EPA ambazo ziliibua mjadala mkubwa nchini hadi kusababisha kufanyika kwa uchunguzi ambao ulianika ufisadi wa kutisha uliofanywa na makampuni fisadi ndani ya BoT.

Katika sakata la EPA ambalo limekuwa donda ndugu katika safu za serikali, kiasi cha Sh. bilioni 133 zilibainika kuchotwa kifisadi BoT baada ya ukaguzi uliofanywa na kampuni ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young.

Katika ripoti ya Ernst & Young kuhusu EPA ilibainisha makampuni 22 yaliyoendesha ufisadi na Rais Jakaya Kikwete kuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Takukuru na Mkurugenzi wa Mashitaka kufungua kesi kwa wahusika, baadhi ya makampuni hadi leo wahusika hawajafikishwa mahakamani.

Miongoni mwa makampuni hayo ni Kagoda Agriculture Limited ambayo ilibainika kujichotea Sh. bilioni 40 za EPA.

Mbali na EPA, sakata la kuvuja kwa nyaraka kuhusu mchakato wa vitambulisho vya taifa nalo lilimweka pabaya Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha Februari mwaka huu.

Katika sakata hilo nyaraka zilizovuja zilionyesha kwamba Waziri Masha alikuwa ameingilia mchakato wa zabuni ya vitambulisho mradi utakaogharimu Sh. bilioni 200 utakapoanza.

Akizungumza na wafanyakazi hao, Mkulo aliwapiga marufuku kuvujisha siri za serikali.

Katika mkutano huo wa siku mbili unawashirikisha pia wajumbe wa mikoa ya Tanzania Bara, Waziri huyo alisisitiza kuwa ingawa kanuni za utumishi wa umma zinaheshimu haki na uhuru wa mtumishi wa umma kuwa mwanachama na kukipigia kura chama chochote cha siasa anachokipenda, lakini ni marufuku kutumia nyaraka au taarifa za ofisi ya umma kwa masuala la kisiasa.

"Mwakani tunaelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge nawakumbusha watumishi wa umma kutotumia nyaraka au taarifa za ofisi ya umma kwa masuala ya kisiasa kwani kufanya hivyo ni uvunjaji wa taratibu za utumishi wa umma," alisema katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Leonidas Gama.

Alisema pamoja na kwamba mtumishi wa umma anaruhusiwa kushiriki katika shughuli za kisiasa, hata hivyo kusiwepo na upendeleo kwa upande wowote katika kutekeleza majukumu yake kwa wananchi.

Alisema ili wizara hiyo iweze kutekeleza malengo iliyojiwekea, kila mtumishi adhamirie kufikia kiwango cha juu cha uadilifu na uwajibikaji kwa lengo la kujenga imani kwa wadau na wananchi.

Alisema watumishi wa umma wanatakiwa kutekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, kutumia utaalam kwa uaminifu, kutoa huduma bora na kutokuwa na upendeleo wakati wa kuhudumia wananchi na kutumia ipasavyo taarifa wanazozipata na kutoziacha ovyo hatimaye kuwafikia watu wasiohusika.

Akizungumzia Mpango wa Kilimo Kwanza, alisema katika bajeti ya 2009/2010, Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo wa Kimataifa (IFAD) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), wameisaidia Tanzania Dola za Marekani milioni 24 kwa ajili ya kutekeleza mpango wa ASDP na pia Benki ya Dunia wanasaidia mradi huo kwa dola za Marekani milioni 160 ili kuhakikisha chakula cha kutosha kinapatikana nchini.

Kuhusu kuporomoka kwa uchumi duniani, alisema serikali katika kukabiliana na tatizo hilo imetenga kiasi cha Sh. trilioni 1.7 katika bajeti yake ya mwaka 2009/2010 kwa ajili ya kuchangamsha uchumi.

Alisema serikali pia imetoa Sh. bilioni 20 kwa Bodi ya Pamba ili kufidia upungufu wa bei ya zao hilo katika msimu wa mwaka huu, na Sh. bilioni 20 kuboresha na kupanua mifuko ya kudhamini mikopo ijulikanayo kama Export Credit Guarantee Scheme (ECGS) na Small and Medium Enterprises Scheme (SMES).

Aliongeza kuwa kiasi cha Sh.bilioni 141 kimetengwa kuboresha na kuongeza uzalishaji wa chakula kwa ajili ya Ghala la Taifa la Chakula na kuhakikisha upatikanaji wa zana za kilimo.

Kwa upande wa mkakati wa kukusanya mapato ya ndani kuendeleza uchumi, alisema wizara hiyo imepewa jukumu la kukusanya mapato na kusimamia matumizi ya serikali na kuimarisha uchumi tulivu, hivyo itaandaa sera za mapato zenye kupanua wigo na kukuza uchumi kwa njia ya kuongeza pato la taifa.

Alisema katika mwaka 2009/2010, Serikali imeweka lengo la kukusanya mapato ya ndani yanayokadiria kuwa Sh. trilioni tano ili kufikia malengo hayo wizara imejipanga kupanua wigo wa kodi, kufanya marekebisho katika baadhi ya kodi zinazotozwa kwenye sekta ya madini, kupunguza misamaha ya kodi na kuendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato yasiyo na kodi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wiraza ya Fedha na Uchumi, Ramadhani Khijjah, alitoa wito kwa watumishi wa serikali kutonunua vitu bila kuzingatia sheria ya manunuzi hali inayosababisha kununuliwa kwa vitu visivyokuwa na ubora na hivyo kuiingizia hasara serikali.

Khijjah alisema pia utaratibu wa kuwapata wazabuni wa kununua vitu vinavyohitajika kwa matumizi ya serikali, kanuni na sheria zilizopo zizingatiwe ili visinunuliwe vitu vibovu kwani ofisi za serikali ni za umma ambao unalipa kodi kuiwezesha serikali yao.

CHANZO: NIPASHE

Niliwahi kuwaambieni katika post za mwanzo ni strategy za kuwanyamazisha watu midomo particularly vijana wadogo katika ofisi hizi wasitoe siri za wanene maofisini. Sitoshangaa tukasikia na wizara ya fedha wanagawana pesa kama BOT!!! We are simply finished!!! Mkulo anadhania bila ya hawa whistleblowers wangelikamatwa akina Mgonja waliojiona ni waungu watu pale wizara ya fedha, Au Yona!!!
 
Back
Top Bottom