BOT yamwaga mikopo ya mamilioni kwa wafanyakazi wake-Ndio bailout ya serikali hiyo!!

BOT yamwaga mikopo ya mamilioni kwa wafanyakazi wake-Ndio bailout ya serikali hiyo!!

Nadhani hatua iliyochukuliwa na viongozi wa BOT kuwakopesha wafanyakazi wao fedha kwa ajili ya kujengea nyumba ni cha kupongezwa na kutolewa mfano na wakuu wengine sehemu za kazi. Hivi ni nani jamani katika mishahara inayotolewa Tanzania hii anaweza kudunduliza hela za kujenga nyumba kwa kutegemea mshahara wake??????. Lazima uwe mwizi na mdanganyifu, mbadhirifu ndio utajenga, vinginevyo utakuwa mpangaji mpaka ufe . Hii ni hatua muhimu katika kufikia lengo la taifa la MAISHA BORA kwa kila mtanzania.
 
Kaka watu hawana wivu na hakuna mtu anafaidika lolote ila la msingi ni je hii mikopo inayotoka karibu na uchaguzi ina faida yeyote kwa uchumi wa Tanzania!!!!

Hatukatai kila Idara na Benki Kuu zina budget zake husika but kinacholalamikiwa hapa ni kitendo cha BOT kuingilia kazi za investment banks na commercial banks na building society.

Umeshawahi kusikia wapi Bank of England ikatoa mortgage financing, Federal Reserve ya US imetoa mortagage. These are toxic assets cause kwanza ni long-term commitment and probability of default ni kubwa na ndio maana banks zinacharge interest kubwa kufidia loss zitakazotokea.

Gavana anasema wanafanya uchunguzi yakinifu kabla ya kutoa mikopo but come on hakuna ambaye anayeweza kutabiri kesho mimi na wewe tutaamkaje. Prof Merton mwenyewe anakwambia probability of default na metrics za kumeausure distance to default cannot full explain default risk exposure. The future is unexplainable sasa BOT inakopesha watu Billion 3 bila ya interest chukulia watu watano kati yao wamefariki baada ya miezi 6 tumepoteza milioni 500 ambazo hizo milioni 500 hata kama tutarecove tunabahati sana kupata 75%. Msitudanganye wazee hatujawa wajinga kiasi hicho.

Kwani wamesema hii ni mortgage? Kwani ni lazima tufanane na Bank of England au FRB?

Mbona kama tunafananisha na FRB au Bank of England kuhusiana na mikopo, hatufananishi na mambo mengine?

Discetion ya wao kutoa soft loan kwa wafanyakazi ipo, inafuata kanuni zao na miongozo. Kama wangefanya kinyemela, hapo linaeleweka, lakini limefanyika kihalali na nina uhakika wa masharti yaliyowekwa ili kuhakikisha kuwa fedha zinarudi.

Labda niwakumbushe kitu kimoja, fedha yote iliyoliwa Tanzania na hasa BOT haikuwa mtajiwa BOT au fedha za Serikali, bali ni fedha zilizokaa benki bila kuwa na mtu au specifics.

Pesa zote zilizohujumiwa si mali ya BOT au URT, bali ni mali ya watu ambao hawajulikani walipo au wamesahau kuwa wanafedha zao na badala ya kuwekewa muda wa kuhakikiwa ili zitumike kwa Serikali kama Unclaimed Property, wajanja wakatafuta mbinu kuzichukua na kujisaidia!

May be mkilielewa hilo mtapata majibu kwa maswali yenu.
 
Ni mawazo mgando vile vile kufikiria kuwa uchumi wa kibepari unaendeshwa kiholela kama baadhi ya watu wanavyotaka kutuaminisha si kweli. Mikopo ya hovyo kama hii kwa wafanya kazi wa BoT ndiyo inayo distort circulation ya pesa na kusababisha spiralling ya inflation.

Mashirika yote zamani yalikuwepo kwenye hii bonanza ya kuwagawia wafanyakazi wake fedha kwa mfumo wa kutoa mikopo isiyokuwa na riba. Matokeo yake mambo haya yalisababisha mashirika mengi kufa. Benki kuu inaweza kufa ikifanya ujinga huo? Haiwezi benki kuu itachota moja kwa moja kutoka hazina.

Kulinda soko ni lazima kuwa na Busara katika ufanyaji wa maamuzi. Haya nayaita ni maamuzi ya kijinga wakati huu ambao tuna sera ya serikali kutojihusisha na Biashara. Taasisi nyingine zote wanachofanya ni kujadiliana na Mabenki ili wafanyakazi wao wapate interrest naffuu. Hata Benki kuu hizi fedha wangezikopesha kwa mabenki kwa masharti nafuu zaidi halafu mabenki ya Biashara ndo yakatoa mikopo hiyo kwa wafanyakazi wa benki kuu, hata kama ni kwa interrest kidogo zaidi kuliko wengine fedha hii ingekuwa na maana zaidi. Fedha ingeingia kwenye circulation kwa kufuata sheria zote za mfumo wa kibepari na hao wafanyakazi wangekuwa makini wakati wa manunuzi ya vifaa vyao. Lakini kitakacho tokea ni mtu kwenda kununua kiwanja akiambiwa ni milioni tano anatoa tu bila hata negotiation kwa sababu fedha yake amechotewa tu!! Hii ndo inflation wajomba!

Tatizo wengi hapa tunajiita mabepari wakati bado hangover ya ujamaa ni kubwa. Hii kutoa fedha kwa mtindo kama huo ni hangover ya ujamaa. Tunaamini kuwa tunafanya ubepari, lakini ni uongo. Ubepari unahakikisha kuwa watu hawagawiwi hovyo hovyo bila kufanyia kazi. Ubepari haugawi vitu bure. Hii si mikopo. Ni kama watu kupewa bure, ni mikopo gani isiyo na riba? Ni kutoa bure. Hata kama ina riba, ni sheria gani inayowaruhusu benki kuu kutoa mikopo kwa individuals? LAZIMA TUUNGALIE UBEPARI KWA KILE AMBACHO NI UBEPARI. Tusiwe tunafanya mambo ya kijamaa halafu tunadai eti tunatekeleza ubepari, ubepari wa wapi wa kugawiana bure? Hapa ni rahisi. Benki kuuu wanachota fedha kwa kucharge interrest kwenye kodi za Wabongo halafu wanajidai eti wanafanya biashara, wanashindana na nani?

Kwa mtindo huo Benki kuu inashindana na Mabenki ya Biashara kutoa mikopo ambalo si jambo la haki kabisa. Inabidi Sheria zetu ziwe makini. Hapa ni watu kujigawia chao mapema halafu tunajificha kwenye kichaka cha eti tunatekeleza Ubepari, huo ni uongo, tena ni uzandiki. Hii inasababisha Mabenki ya Biashara kuendelea kucharge riba kubwa kwa wateja wachache wanaowapata. Cream ya watu ambao wanakopesheka na Mabenki mengine ndo hawa hawa ambao Benki kuu inawapa fedha bila riba. Sasa akienda kukopa Benki Mwalimu ni lazima Benki wamcharge interrest kubwa tu.

Hii ni mbovu na inavuruga uchumi, na huu si ubepari. Ni hangover ya ujamaa hii. Mabepari hawagawi bure hata siku moja. Lazima warudishe hata gharama. Mikopo kama hii bila riba hairudishi hata gharama. Ni kuwagawia bure! Kuhakikisha kuwa gharama inarudi lazima fedha hii ingepitishwa kwenye Mabenki ya biashara kwani ndo yanajua na yana utaalamu wa kukokotoa gharama halisi. Hapa Benki kuu hakuna cha ndullu wala nini, wamezama kwenye hangover ya ujamaa tu, full stop.

Mmeshaangalia Balance Sheet ya BOT as BOT kwa kuwangalia mapato na matumizi yake kama Shirika?

Au mnachanganya mambo kwa kuangalia Balance SHeet ya Serikali inayotolewa ripoti na BOT na hivyo mnaanza kudai ni kuvuruga uchumi?
 
Hivi leo TBL na TCC wakitoa motisha wa namna hii tutalalakmika kwa ni na wa Chibuku au Mataputapu wasipewe?
Huu mfano sio sahihi kabisa TBL na TCC ni kampuni binafsi hauwezi kufananisha na BOT chombo cha serikali.
 
Greenspan watanzania badala ya kufikiria ni jinsi gani atawawezesha watanzania milioni 40 pamoja na wawekezaji sera zake ni za kuwafikiria wafanyakazi 600 wa Bot
Hivi kweli tutafika? hivi toka Greenspan wetu ameingia BOT ametoa sera gani ya kuweza kusaidia kufufua Uchumi wa Tanzania? au kuzui EPa ndio achievement yake na kufanya audit ya ajira ya watoto wa Vigogo?
Au tuseme sera za kuendeleza nchi ni Siri?
Hivi Kishoka unaelewa Role mojawapo ya BOT ni kuzuia muzunguko mbovu wa Peesa, kama Capital Flight inayofanywa na RITES? je Greenspan wetu amelishughulikia vipi suala kama Hilo?
Hivi unajua Role nyingine ni kuishauri serikali na kutoa sera ambazo zitawezesha Commercial Bank kuongeza fungu la mikopo ya Nyumba ikiwa ni pamoja kuwa na specific Deparment iwe ni NSSF, PPF, CRDB nk nk ambazo zipo wazi kwa watu wote kwa ajili ya mikopo ya Nyumba, badala ya sasa hivi kila shirika/kampuni nk wamekuwa ma-expert wa kutoa mikopo.
Je waelewa miongozo hiyo unayo sema ya Soft loan ina limitation, inatolewa in terms ya Salary advance, ambayo to the maximum ni 3 years salary.
sasa ukija mkopo unaozidi hapo inabidi ujiulize una resource za kuhifadhi hati za nyumba za wakopaji, wafanyakazi wa ku-manage hiyo mikopo, na siku hizi mambo ya Software, hivyo una progaramme ya kumanage hiyo mikopo?
Ni consequencies za capital outlay ya kutoa hiyo mikopo kwenye core activities zako ipoje?
Halafu hiyo context ya kusema BOT inafanya Biashara ? biashara gani binadamu anayofanya isiyo na Competition? maana Commercial Bank zote lazima wapitishie mambo ya huko, na kwa serikali lazima wapitishie transaction zao huko, na Treasury Bills lazima zipitie huko.mimi ninachona wanatoa huduma kama ilivyo Muhimbili, na angalau Muhimbili Hospital wana Competition ya Agakhan Hospital, Lugalo, Regency Mikocheni, na waganga wa Kienyeji.
Labda tunaweza walinganisha na JWTZ.


Gavana aikingia kifua mikopo ya watumishi BoT
broken-heart.jpg
Na Ramadhan Semtawa

UONGOZI wa Benki Kuu (BoT), umetetea mikopo ya mamilioni ya watumishi wake kwa ajili ya ujenzi wa nyumba, ukisema mpango huo, unalenga kuwajengea maisha bora watumishi hao.

Kauli hiyo, inakuja kufuatia kuwepo kwa waraka wa baraza la mikopo la nyumba, ambalo limetaja viwango vya mikopo kwa madaraja tofauti katika matawi yake yote ya Mwanza, Dar es Salaam, Zanzibar, Arusha na Mbeya.

Waraka huo, unaonyesha kila mfanyakazi ataweza kukopa kati ya Sh 100milioni ikiwa ni kiwango cha juu na Sh 30 milioni kiwango cha chini kulingana na wadhifa wa mtumishi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba.

Akizungumzia waraka huo, Gavana wa BoT Profesa Benno Ndulu, alisema ni utaratibu ambao benki imejiwekea ili kuwawezesha wafanyakazi wake kimaisha.

Profesa Ndulu, alisema BoT, ilijiwekea utaratibu huo baada ya kuangalia mahitaji ya msingi ya makazi kwa watumishi wake.

"Ni utaratibu ambao upo kwa karibu miaka 20 sasa, lakini sasa tumeuboresha kwa kuangalia mahitaji ya mikopo kwa umakini," alifafanua Gavana Ndulu.

Profesa Ndulu ambaye amekuwa katika mchakato wa kuisafisha taasisi hiyo ya fedha, aliweka bayana kwamba mikopo hiyo, imekuwa ikitolewa kwa umakini ili kuhakikisha inarejeshwa.

Alisisitiza kabla benki hiyo, haijatoa mikopo, inatafuta taarifa za wahusika ili kubaini kama wana madeni ndani na nje ya benki hiyo.

"Hatukopeshi tu bila kufuata utaratibu, vipo vigezo vya mtu kukopa mbali ya madaraja, tunaangalia madeni ya mtu ili tujue uwezo wake wa kurejesha," alisisitiza Ndulu.

Alisema kiutaratibu benki hiyo, inaangalia madeni ili kila mfanyakazi abaki angalau na theluthi moja ya mshahara baada ya kukatwa madeni anayodaiwa.
"Na wao ni binadamu kwa hiyo lazima tuhakikishe angalau, wanabakiwa japo na theluthi moja ya mshahara, baada ya makato," aliongeza gavana huyo.
Tuma maoni kwa Mhariri
facebookimage.jpg
Facebook
 
Kwani wamesema hii ni mortgage? Kwani ni lazima tufanane na Bank of England au FRB?

Mbona kama tunafananisha na FRB au Bank of England kuhusiana na mikopo, hatufananishi na mambo mengine?

Discetion ya wao kutoa soft loan kwa wafanyakazi ipo, inafuata kanuni zao na miongozo. Kama wangefanya kinyemela, hapo linaeleweka, lakini limefanyika kihalali na nina uhakika wa masharti yaliyowekwa ili kuhakikisha kuwa fedha zinarudi.

Labda niwakumbushe kitu kimoja, fedha yote iliyoliwa Tanzania na hasa BOT haikuwa mtajiwa BOT au fedha za Serikali, bali ni fedha zilizokaa benki bila kuwa na mtu au specifics.

Pesa zote zilizohujumiwa si mali ya BOT au URT, bali ni mali ya watu ambao hawajulikani walipo au wamesahau kuwa wanafedha zao na badala ya kuwekewa muda wa kuhakikiwa ili zitumike kwa Serikali kama Unclaimed Property, wajanja wakatafuta mbinu kuzichukua na kujisaidia!

May be mkilielewa hilo mtapata majibu kwa maswali yenu.
Hapo Kishiko umeniacha hoi! nafikiri ndio maana unatetea BOT kutoa Mikopo kwa staff bila kuelewa Role ya BOT na Majukumu ya GOvernor katika ku-shape uchumi wa nchi na nguvu za Governor katika ku-control Uchumi.
Sasa ningependa kukuuliza nini tofauti ya role ya BoE, FRB, na BOT, na hata ukiachana na hizo angalia labda China, Russia, India, na hata kwa majirani zetu Kenya, Uganda etc.
Halafu unasema bado tumelala kwenye Ujamaa, sasa tukihama huko na kulinganisha na Hao BoE , FRB, unasema kwanini tufananea, sasa sijui msimamo wako upo wapi? Kwenye Ujamaa au Kutoka kwenye Mfumo huo ?
Halafu wapi tumesema vitu vingine hatuvilinganishi na wengine au Basically hao BoE, FRB nk nk.
Huoni tunavyo pigania Demokrasia zaidi tunapigania kuelekea huko?
Tunapo sema uwepo uwazi katika ushindani huoni tunaelekea huko?
Tunapo pinga Ufisadi huoni tunaelekea Huko, maana wenzetu mambo ya Money Laundering wanayatazama kwa Jicho pana zaidi , lakini kwetu njoo na hela zako za Terrorism , au madawa ya kulevya tutakuona Shujaa.
na Hata tunaposema sasa kwamba Hizo instutution ziwe na vitengo maalum kwa ajili ya mortgage tunaelekea huko, maana kwa wenzetu huwezi kukuta Bank specifically kwa ajili ya Mikopo, bali inaweza kuwa part of the Products provided to it's customers na ni open kwa watu wote.
Hiyo Discretion ya kutoa Soft Loan ninavyo elewa Mimi ina limit, moja Interest rate yake inatakiwa at minimal iwe ni rate wanayolipwa Depositors na hiyo ikiwa ni case za instutution kama NMB, NBC, CRDB Stanbic, Standard nk nk ukitaka waulize hao Staff.
Ukija aina nyingine ya Soft Loan ni Salary Advance ambayo pia in limiti 3 month, 6 month at most 3 years.
Infact kutokana Fedha za EPa kupitia katika Certain Banks Leo hii Bank kuu isingepitisha au ingesitisha wakurugenzi wa baadhi ya Bank na wakurugenzi wa makampuni husika kuwekwa katika Probation kama sio kuzuiwa kuwa wakurugenzi wa mashirika husika.
 
Greenspan watanzania badala ya kufikiria ni jinsi gani atawawezesha watanzania milioni 40 pamoja na wawekezaji sera zake ni za kuwafikiria wafanyakazi 600 wa Bot
Hivi kweli tutafika? hivi toka Greenspan wetu ameingia BOT ametoa sera gani ya kuweza kusaidia kufufua Uchumi wa Tanzania? au kuzui EPa ndio achievement yake na kufanya audit ya ajira ya watoto wa Vigogo?
Au tuseme sera za kuendeleza nchi ni Siri?
Hivi Kishoka unaelewa Role mojawapo ya BOT ni kuzuia muzunguko mbovu wa Peesa, kama Capital Flight inayofanywa na RITES? je Greenspan wetu amelishughulikia vipi suala kama Hilo?
Hivi unajua Role nyingine ni kuishauri serikali na kutoa sera ambazo zitawezesha Commercial Bank kuongeza fungu la mikopo ya Nyumba ikiwa ni pamoja kuwa na specific Deparment iwe ni NSSF, PPF, CRDB nk nk ambazo zipo wazi kwa watu wote kwa ajili ya mikopo ya Nyumba, badala ya sasa hivi kila shirika/kampuni nk wamekuwa ma-expert wa kutoa mikopo.
Je waelewa miongozo hiyo unayo sema ya Soft loan ina limitation, inatolewa in terms ya Salary advance, ambayo to the maximum ni 3 years salary.
sasa ukija mkopo unaozidi hapo inabidi ujiulize una resource za kuhifadhi hati za nyumba za wakopaji, wafanyakazi wa ku-manage hiyo mikopo, na siku hizi mambo ya Software, hivyo una progaramme ya kumanage hiyo mikopo?
Ni consequencies za capital outlay ya kutoa hiyo mikopo kwenye core activities zako ipoje?
Halafu hiyo context ya kusema BOT inafanya Biashara ? biashara gani binadamu anayofanya isiyo na Competition? maana Commercial Bank zote lazima wapitishie mambo ya huko, na kwa serikali lazima wapitishie transaction zao huko, na Treasury Bills lazima zipitie huko.mimi ninachona wanatoa huduma kama ilivyo Muhimbili, na angalau Muhimbili Hospital wana Competition ya Agakhan Hospital, Lugalo, Regency Mikocheni, na waganga wa Kienyeji.
Labda tunaweza walinganisha na JWTZ.


Gavana aikingia kifua mikopo ya watumishi BoT
broken-heart.jpg
Na Ramadhan Semtawa

UONGOZI wa Benki Kuu (BoT), umetetea mikopo ya mamilioni ya watumishi wake kwa ajili ya ujenzi wa nyumba, ukisema mpango huo, unalenga kuwajengea maisha bora watumishi hao.

Kauli hiyo, inakuja kufuatia kuwepo kwa waraka wa baraza la mikopo la nyumba, ambalo limetaja viwango vya mikopo kwa madaraja tofauti katika matawi yake yote ya Mwanza, Dar es Salaam, Zanzibar, Arusha na Mbeya.

Waraka huo, unaonyesha kila mfanyakazi ataweza kukopa kati ya Sh 100milioni ikiwa ni kiwango cha juu na Sh 30 milioni kiwango cha chini kulingana na wadhifa wa mtumishi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba.

Akizungumzia waraka huo, Gavana wa BoT Profesa Benno Ndulu, alisema ni utaratibu ambao benki imejiwekea ili kuwawezesha wafanyakazi wake kimaisha.

Profesa Ndulu, alisema BoT, ilijiwekea utaratibu huo baada ya kuangalia mahitaji ya msingi ya makazi kwa watumishi wake.

"Ni utaratibu ambao upo kwa karibu miaka 20 sasa, lakini sasa tumeuboresha kwa kuangalia mahitaji ya mikopo kwa umakini," alifafanua Gavana Ndulu.

Profesa Ndulu ambaye amekuwa katika mchakato wa kuisafisha taasisi hiyo ya fedha, aliweka bayana kwamba mikopo hiyo, imekuwa ikitolewa kwa umakini ili kuhakikisha inarejeshwa.

Alisisitiza kabla benki hiyo, haijatoa mikopo, inatafuta taarifa za wahusika ili kubaini kama wana madeni ndani na nje ya benki hiyo.

"Hatukopeshi tu bila kufuata utaratibu, vipo vigezo vya mtu kukopa mbali ya madaraja, tunaangalia madeni ya mtu ili tujue uwezo wake wa kurejesha," alisisitiza Ndulu.

Alisema kiutaratibu benki hiyo, inaangalia madeni ili kila mfanyakazi abaki angalau na theluthi moja ya mshahara baada ya kukatwa madeni anayodaiwa.
"Na wao ni binadamu kwa hiyo lazima tuhakikishe angalau, wanabakiwa japo na theluthi moja ya mshahara, baada ya makato," aliongeza gavana huyo.
Tuma maoni kwa Mhariri
facebookimage.jpg
Facebook

Unajua kaka mie saa zengine sielewi sijui Rev.Kishoka na wenzio mtusaidie majibu ya maswali yafuatayo Kwanza BOT inafanya biashara???? Pili nini kazi ya BOT kama sio kufanya biashara. Tatu kwani wafanyakazi wa BOT hawawezi kwenda kukopa katika Commercial Banks BOT ikawaguarantee mikopo yao kwanini wang'ang'anie mikopo BOT??? Nne je Ndulu ameshindwa mawazo kama BOT inareserve kubwa ya cash kwanini asitoe mikopo kwa mabenki kwa riba ya chini ili mabenki nayo yatoe mikopo ya bei nafuu kwa wakulima??? Tano je hii mikopo tunahakika gani watanzania wengine watafaidika au ndio mwenye nacho ataongezewa na asiye nacho ndio kinachokuliwa ili wapate figure za kuwaonyesha World Bank kwamba nyumba za makaazi zimejengwa wapate kuongezewa pesa kumbe ni nyumba za watu wenye uwezo wa kujenga ndio wamepewa walengwa kalaghabao???? Mkinijibu maswali haya mie nitafahamu kwanini BOT inatoa mikopo but for now it does not make any sense to me.

In addition, someni makala ya raia mwema ya leo jamaa wanaanza kulalamikiana wao kwa wao wafanyakazi wa chini wanadai mikopo ya makarani ni midogo kuliko wanene BOT unajiuliza kumbe hii mikopo ni dili ehhh!!!!
 
Unajua kaka mie saa zengine sielewi sijui Rev.Kishoka na wenzio mtusaidie majibu ya maswali yafuatayo Kwanza BOT inafanya biashara???? Pili nini kazi ya BOT kama sio kufanya biashara. Tatu kwani wafanyakazi wa BOT hawawezi kwenda kukopa katika Commercial Banks BOT ikawaguarantee mikopo yao kwanini wang'ang'anie mikopo BOT??? Nne je Ndulu ameshindwa mawazo kama BOT inareserve kubwa ya cash kwanini asitoe mikopo kwa mabenki kwa riba ya chini ili mabenki nayo yatoe mikopo ya bei nafuu kwa wakulima??? Tano je hii mikopo tunahakika gani watanzania wengine watafaidika au ndio mwenye nacho ataongezewa na asiye nacho ndio kinachokuliwa ili wapate figure za kuwaonyesha World Bank kwamba nyumba za makaazi zimejengwa wapate kuongezewa pesa kumbe ni nyumba za watu wenye uwezo wa kujenga ndio wamepewa walengwa kalaghabao???? Mkinijibu maswali haya mie nitafahamu kwanini BOT inatoa mikopo but for now it does not make any sense to me.

In addition, someni makala ya raia mwema ya leo jamaa wanaanza kulalamikiana wao kwa wao wafanyakazi wa chini wanadai mikopo ya makarani ni midogo kuliko wanene BOT unajiuliza kumbe hii mikopo ni dili ehhh!!!!
Tatizo nililoliona ni ama watu wengine hawaelewi Role ya BOT au kwa makusudi mazima mtu anataka kupotosha ukweli au mtu mwingine anashindwa kutofautisha Benki Kuu na Benki zingine hivyo kushindwa kuelewa taratibu au Principles of Engagement and operations ambazo kwa BoT hazijalishi kama wewe ni mjama au simjaa, kwamba jukumu la benki kuu ni kuzisimamias Benki ili kuwe na level playing field kwa watoa huduma yaani Benki na kwa walaji ambao ndio sisi wakopaji, tuinaowekeza nk.
Na zaidi ya hapo ku-control mambo yanayo husiana na mzungulko wa Pesa iwe za nje au za ndani, ndio hapo Bot inapotakiwa kuishauri/kutoa angalizo na kuzuia transaction fulani ambazo hazina maslahi kwa taifa. kama hiyo ya ukodishaji wa mabehewa ya Rites na Management fees nk nk.
 
Naona sasa wameamua KU-fisadi "kihalali"..!!!

BOT wameshindwa kazi...Roles zao hawajui...Hadi sasa hawajafanya la maana kumake sure alau shilingi ya TZ inakuwa sawa na Shiling ya Kenya. then tuende ktk Dola.!!!
"Wataacha kufanyakazi zao, sasa maana wanajiingiza kufuatilia mikopo ya wafanyakazi wao"

Wananchi Hali zao ni DUNI mfumuko wa Bei umekuwa Mkubwa. Leo hii Ukiwa dola elf20,000 huwezi jenga TZ, lkn the same amount ya pesa India waweza jenga.

Bank ya Nyumba ipo wapi? Lipo wapi shirika la Nyumba la Taifa? next utasikia Bunge nalo wanakopeshana.

Itafikia Kipindi tutacharazana "BAKORA" na "MAWE" ili kupunguza ufisadi
 
Tatizo nililoliona ni ama watu wengine hawaelewi Role ya BOT au kwa makusudi mazima mtu anataka kupotosha ukweli au mtu mwingine anashindwa kutofautisha Benki Kuu na Benki zingine hivyo kushindwa kuelewa taratibu au Principles of Engagement and operations ambazo kwa BoT hazijalishi kama wewe ni mjama au simjaa, kwamba jukumu la benki kuu ni kuzisimamias Benki ili kuwe na level playing field kwa watoa huduma yaani Benki na kwa walaji ambao ndio sisi wakopaji, tuinaowekeza nk.
Na zaidi ya hapo ku-control mambo yanayo husiana na mzungulko wa Pesa iwe za nje au za ndani, ndio hapo Bot inapotakiwa kuishauri/kutoa angalizo na kuzuia transaction fulani ambazo hazina maslahi kwa taifa. kama hiyo ya ukodishaji wa mabehewa ya Rites na Management fees nk nk.


Unajua kamanda katika behaviour finance kuna kitu kinaitwa behavioral bias (kupendelea au mtazamo wa aina moja) na moja ya vitu vinavyosababisha balaa hilo ni overconfidence and greedy (optimism). Mara nyingi wanaadamu wanakuwa ni selfish and too much optimism can led severe consequences.

Nasubiria majibu wataalamu wa BOT
 
Ni obvious kama nilivyosema haya ni masalia ya Ujamaa. Angalia wanavyoitetea, wanasema ni utaratibu uliokuwepo kuwa miaka ishirini sasa wana uboresha.

Ninachosema ni kuwa mashirika mengi ya umma, kwa kipindi hicho wanachosema watu wa Benki kuu kuwa utaratibu huo ulikuwepo, walikuwa vile vile na taratibu kama hizi. Lakini mageuzi ya kiuchumi yalivyokuja ukaonekana huo ni utaratibu usiofaa.

Mikopo inatakiwa itolewe na commercial banks au financial institution ambazo zimeruhusiwa kutoa mikopo. Mashirika ya umma au serikali yenyewe inatakiwa itumie service za mabenki ya biashara ili kuwakopesha wafanyakazi wao. Mashirika mengi ya umma yaliyobaki yanafuata utaratibu huo, si kwa sababu hawana fedha za kutoa kwa wafanyakazi wao, bali ni kufuata sheria na taratibu za flow ya fedha kwenye mfumo mpya wa uchumi.

Benki kuu hawatoi mikopo kwa mtu mmoja mmoja na hawana infrastructure na capacity ya kushughulika na utoaji wa mikopo. Kwa hiyo wao ilitakiwa wawasaidie wafanyakazi wao kwa kuwapa guarantee na kuwasaidia kupata interrest rates kidogo. Lakini Benki kuu kutoa mikopo moja kwa moja kwa wafanya kazi wake kunatoa message gani kwa taasisi nyingine za serikali ambazo zinawaelekeza wafanyakazi wao kwenda kwenye Mabenki ya biashara?

Nimesema huu si ubepari ni masalia ya ujamaa. Tabia za ujamaa ni Tabaka la wanaoongoza kuamini kuwa wao taasisi za umma wanazoziongoza ni kama mali yao. Na hivyo kuzitumia kwa manufaa yao, jambo ambalo si kweli.

Benki kuu inatakiwa wawe mfano. Waka 'negotiate interrest rates' nzuri kwa ajili ya wafanyakazi wao kwenye Mabenki ya biashara. Wao waendelee na kazi zao za msingi. Hizi taratibu zilizokuwepo kwa miaka ishirini na zaidi iliyopita ndo taratibu zilizotufikisha hapa tulipo. Ndullu na wenzake haikutakiwa wajitetee kwa kusema eti huu utaratibu ulikuwepo, wamekuja basi kufanya nini? Kurekebisha yaliyokuwepo ambayo hata yameshathibitika kuwa ni uozo?
 
Naona kelele zetu zimemstua mwenye Nyumba/karani wa mwenye nyumba

Matumizi ya BoT yaishtua Serikali

Habari mbalimbali
pix.gif
Habari zaidi zinasema BoT imesitisha nyongeza ya mikopo ya nyumba ya asilimia 50 iliyoidhinisha kwa wafanyakazi wake, hatua ambayo imekuja siku chache baada ya kuidhinishwa na menejimenti ya taasisi hiyo kubwa ya fedha.

Taarifa za matumizi hayo makubwa ya fedha hizo za walipakodi katika kujenga makazi ya gavana ziliripotiwa na Mwananchi Ijumaa iliyopita katika habari iliyoeleza jinsi nyumba ya kigogo huyo wa BoT ilivyogharimu Sh1.4 bilioni kuikarabati, kabla ya Ndulu kutoa ufafanuzi kuwa nyumba hiyo ilijengwa upya na si kwamba ilikarabatiwa.

Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano juzi, Mkulo alisema pamoja na kushtushwa na taarifa hizo, jambo hilo ni kubwa na linahitaji umuhimu wa kipekee kuchunguzwa ili walipakodi wajue ukweli wa matumizi ya fedha wanazoilipa serikali.
"Lazima tuchunguze ukweli wa taarifa hizo, maana hili ni jambo kubwa na linamhusu mtu mkubwa," alisema Mkulo katika mahojiano na gazeti hili.

Mkulo alisema kuwa alikuwa safarini nje ya nchi na kwamba baada ya kurejea nchini juzi, ofisi yake itatumia wiki hii kufanyia uchunguzi suala hilo na wiki ijayo atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuweka mambo yote hadharani.
Akitoa ufafanuzi wa tuhuma hizo wiki iliyopita, licha ya kukiri matumizi hayo ya fedha, Profesa Ndulu alisema kuwa nyumba anayoishi ilianza kujengwa kutoka chini na kwenye kiwanja ambacho ni cha BoT.

"Nyumba haijakarabatiwa, imejengwa from the ground (kutoka chini)... ni tofauti kukarabati na kujenga nyumba mpya... huu ni upotoshaji wa wazi na kujaribu kuchafua mema," alilalamika gavana huyo.
Aliongeza: "Napenda taarifa sahihi ambazo hazipotoshi ukweli kwa maana taarifa kama hizo zinaharibu kila kitu, kizuri na kujenga taswira mbaya kwa wananchi, kitu ambacho si sahihi."

Mwananchi toleo la Desemba 23, mwaka huu iliripoti kuwa nyumba anayoishi sasa gavana huyo ilikarabatiwa kwa takriban Sh1.4 bilioni na kwamba ilikuwa kwenye mradi wa kukarabati nyumba za vigogo wanne wa BoT; ya Ndulu na manaibu wake watatu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, nyumba nyingine ni pamoja na aliyokuwa akiishi gavana wa zamani, marehemu Daudi Balali ambayo Prof Ndulu alidaiwa kuikataa kwa kuwa haina bwawa la kuogolea.
Licha ya tuhuma hizo, BoT inalalamikiwa kwa kujiidhinishia mamilioni ya fedha za mikopo yenye tofauti kubwa ya viwango baina ya wafanyakazi wa chini na vigogo.

Katika hatua nyingine, BoT imesimamisha nyongeza ya mikopo ya nyumba kwa asilimia 50, ambayo menejimenti hiyo iliridhia nyongeza yake ambayo watumishi wa kada ya chini wangejipatia mkopo wa hadi Sh30milioni na vigogo hadi Sh100milioni.
Habari zilizolifikia Mwananchi na kuthibitishwa na Gavana wa BoT, Profesa Ndulu zimethibitisha kusimamishwa kwa mikopo hiyo.
Kabla ya kusimamishwa kwa mikopo hiyo baadhi ya watumishi wa taasisi hiyo walikaririwa na vyombo vya habari (siyo Mwananchi), wakilalamika kuwa nyongeza hiyo ililenga kuwanufaisha zaidi vigogo.

Walidai kuwa matarajio yao yalikuwa wafanyakazi wa kawaida wangepewa kipaumbele zaidi, lakini hali ikawa kinyume.
Kusimamishwa kwa mikopo hiyo pia kumeibua mitazamo tofauti kwa wafanyakazi wa taasisi hiyo, wengi wakionyesha mashaka kwa hatua hiyo wakidai inawaaminisha kuwa nyongeza hiyo ilikuwa na lengo la kuwanufaisha zaidi wakubwa.
"Hii inaleta mashaka kwani kama hapakuwa na tatizo ni kwa nini baada tu ya kuripotiwa kwenye vyombo vya habari ndipo ikasimamishwa?" alihoji mmoja wa wafanyakazi wa benki hiyo.

"Sina hakika sana juu ya sababu zilizofanya mikopo hiyo isimamishwe na hatua au marekebisho yanayokusudiwa kuchukuliwa, lakini hii inaweza kutoa picha kuwa kuna mambo hayakuwa sawa ndio sababu imesimamishwa baada ya vyombo vya habari kuiripoti."
Lakini juzi, Gavana Ndulu alisema lengo la kusitisha mikopo hiyo ni kutoa elimu zaidi kwa wafanyakazi hao kuhusu mikopo hiyo.

Alisema imebainika kuwa wafanyakazi hao hawakuwa na elimu ya kutosha kuhusu vyongeza hiyo ya viwango vya mikopo na kwamba ndio maana walikaririwa na vyombo vya habari wakilalamika.
Ndulu alifafanua kuwa upo umuhimu wa elimu hiyo kwa wafanyakazi ili wasije wakabeba mzigo wasiouweza kwa kuwa mikopo hiyo ina masharti mengi kwa mkopaji.

"Tumeongeza masharti mengi na hatutaki mtu abebe mzigo asiouweza. Tumegundua wafanyakazi wengi hawakuelewa na ndio maana tumeona kuna umuhimu wa kuelimishana kwanza," alisema Prof Ndulu.

"Pengine elimu ilipaswa itangulie kwanza. Mara nyingi hivi vitu ni kuelewana. Ilionekana wengi hawakuelewa ndio sababu wakalalamika kwenye vyombo vya habari. Kwa hali hiyo sasa tumeisimamisha mikopo hiyo kwanza na tayari nimewaagiza maofisa husika kusimamia utaoaji wa elimu hiyo."

Gavana Ndulu alisema mfuko huo wa mikopo kwa nyumba umekuwepo kwa muda mrefu na kwamba kilichofanyika ni kuongeza tu viwango vya mikopo ili kuendana na mabadiliko ya hali ya maisha.
Kuhusu chanzo cha pesa hizo, alisema si za serikalini bali zinatokana na operesheni mbalimbali za benki hiyo ikiwa ni pamoja na riba inayotokana na mikopo mbalimbali wanayoitoa kwa serikali na kwa mabenki mengine nchini.

Kuhusu masharti ya mikopo hiyo alisema inapotokea mtumishi amestaafu kabla ya kumaliza kurejesha mkopo huo, basi sehemu ya mafao yake hutumika kufidia kiasi kilichosalia.
BoT imekuwa ikiangaliwa kwa karibu tangu kuibuka kwa kashfa ya wizi wa zaidi ya Sh133 bilioni kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Taasisi hiyo pia imekumbwa na kashfa nyingine kama za bima ya maghorofa yaliyo jijini Dar es salaam na Zanzibar, kuongeza gharama katika uchapishaji wa noti na matumizi mabaya ya madaraka katika ujenzi wa maghorofa pacha.
Wafanyakazi wa benki hiyo pia wamejikuta kwenye kashfa za kufanikisha njama za wizi, kuajiriwa kwa kutumia vyeti vya kughushi na tuhuma za watoto wa vigogo kupewa ajira za upendeleo.

CHANZO: MWANANCHI
 
Waziri amesema kuna tatizo,wamesimamisha utoaji mikopo.MTAALAMU WETU WA BENKI KUU bwana KISHOKA UKO WAPI?
maana wewe ulisema tunawasingizia,
 
Waziri amesema kuna tatizo,wamesimamisha utoaji mikopo.MTAALAMU WETU WA BENKI KUU bwana KISHOKA UKO WAPI?
maana wewe ulisema tunawasingizia,

Mimi na August tuliwahi kusema mikopo hii ni hatari kwa uchumi wa Tanzania waichunguze Serikali. Sijajua wale waliokuwa wanasupport wanasemaje????
 
Mimi na August tuliwahi kusema mikopo hii ni hatari kwa uchumi wa Tanzania waichunguze Serikali. Sijajua wale waliokuwa wanasupport wanasemaje????

Ndullu kama bosi wake aliyemteua naye kazi imemshinda lakini kutokana na rekodi ya boss wake ya kushindwa kumuachisha kazi yoyote hata kama kwa manufaa ya umma huyu naye ataendelea katika hiyo nafasi yake na hata kama mkataba wake unakaribia kuisha akapewa mwingine. Si tumesikia kule kwenye ugavi wa umeme wanataka kumrudisha tena Idrissa Rashid pamoja na rekodi yake ya kukatisha tamaa.
 
Prof. Benno Ndulu; Wafanyakazi wa BoT:
Mnakumbuka kisa cha “political propaganda” ya “Mimi ni Profesa wa Uchumi” (Mazungumzo Baada ya Habari) - enzi za Azimio la Arusha? Huyu mwana-uchumi Profesa Benno Ndulu ana visa, kama hivyo!

Profesa Benno Ndulu aliwahi kulihakikishia taifa, mwanzoni mwa kudorora kwa uchumi wa dunia, kuwa Tanzania haitaathirika kwa sababu ilikuwa imewekeza (au imetunza mapesa yake mapema) kwenye “bonds” maalum zisizoyumbika.

Sijui alikuwa na maana gani!

Na hivi majuzi, katamka kuwa pesa ya Tanzania iko juu, kama mkungu wa ndizi bila wasiwasi (au iko imara)!
Hili pia silielewi. Naomba kufundishwa, kwani nina uwezo wa kufundishika!

Hebu tliangalie la wafanyakazi wake kutaka kujijengea majumba (huku akijua kuwa tayari yeye na ma-Gavana wadogo tayari walikuwa wameishajijengea ya kwao):
Kuna mifano mingi katika Agano Jipya ya Yesu kuwafundisha watu kuelewa ya ufalme wa mbinguni. Mfano wa talanta kwa watumishi upo karibu na visa vya BoT na pesa za umma.

Yesu angekuwepo ki-mwili hapa Tanzania ya leo, angefundisha juu ya kuwajibikia pesa za umma kwa kutoa mfano huu:

"Ni sawa na mtu mmoja tajiri aliyetaka kusafiri ng`ambo. Aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake. Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili; mwingine talanta moja; na mwingine nusu talanta, kisha akasafiri.

"BoT ikapewa nusu talanta. Ikafanya kazi nazo ikapata faida kubwa ya nusu talanta. Sasa Tanzania inataka kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.

“BoT inakuja amechukua zile talanta nusu na faida yake juu. Inaiambia Tanzania, ulinikabidhi talantanusu, hapa pana talanta nusu zaidi kibindoni faida niliyopata. Hizi hapa ni nusu talanta zile ulizotukabidhi. Chukua nusu talanta yako. Nusu talanta faida ni mali yetu sisi watumishi!”

Gavana Benno Ndulu alinukuliwa na gazeti moja akitamka kuwa pesa hizo "si za serikalini bali zinatokana na operesheni mbalimbali za benki hiyo ikiwa ni pamoja na riba inayotokana na mikopo mbalimbali wanayoitoa kwa serikali na kwa mabenki mengine nchini.”

Ndio! Hii ndicho kitovu cha sababu ya Gavana Benno Ndulu kutamka wazi kuhusu chanzo cha pesa hizo za mikopo wafanyakazi wa BoT kujijengea majumba.
Na sio hiyo tu; ni kitovu cha sababu ya viongozi hao wa BoT kujijengea majumba ya fahari yasiyolingana na hali ya mazingira hapo Jijini Dar es Salaam! Sakafu za mawe nje ya majumba hayo (kuongeza joto hapo wakati wa jua kali) badala ya nyasi! Wala hazitumii umeme wa jua au upepo!

Badala ya Tanzania kusema, "Vema, mtumishi mwema na mwaminifu,” hawa BoT, wakiongozwa na Bodi yao, wanadai kuwa SIO PESA ZA SERIKALI!

Profesa benno Ndulu amekuja na Kozi Mpya ya Uchumi 101: Faida Sio Mali ya Mjasiriamali.

Kwani faida hiyo ilitokana na pesa za nani! Profesa Ndulu na BoT WANAIBA faida!

Prof Benno Ndulu na watumishi wa BoT, hamana “compassion” hata kidogo?

Hamtaki kusikia sauti ya ukombozi (a voice of liberty-re-conquered)!

Wananchi wangu hawakuwa na nyumba nzuri, mkanisaidia kuwajengea nyumba bora.

Watoto wangu hawakuwa na shule na madawati, mkanisaidia kuwajengea shule.
Wananchi wangu vijijini hawakuwa na maji safi na y a kutosha, mkanisaidia kuwajengea visima vya maji.

Wananchi wangu walikuwa na njaa, mkanisaidia kuondoa jembe la mkono ili waongeze uzalishaji wa mazao ya chakula.

Wananchi wangu walikuwa uchi, mkanisaidia kuwavika.
Wananchi wangu walikuwa wagonjwa wa HIV/AIDS mkanisaidia kuwapatia dawa.

Wananchi wangu walikuwa wagonjwa wa HIV/AIDS mkanisaidia kuwapatia dawa.

Wakina mama walikuwa hawajui kusoma na kuandika, mkanisaidia kuwaelemisha.

Wananchi wangu walikumbwa na mafuriko na wengine kufunikwa kwa vifusi vya tope poromka, mkanisaidia kuwarejeshea nyumba zao na kuwafariji.

_______

Wa-Tanzania wenzangu, hayo ya Benno Ndulu na mgao wa faida ya umma hayakuanza wakati wa Benno; yaliwahi kutokea miaka ya kuanzia muongo wa 1970s wakati wa Edwin Mtei. Wakati huo, BoT walitaka kugawana sehemu ya faida kwa kujipa marupurupu (gratuities) kila mfanyakazi shilingi 1000 (yaani masai kumi za wakati huo)!

Lakini Mwalimu Julius Nyerere aling’aka na kutamka rasmi:

“Yaani wanataka kugawana faida ya umma badala ya kuiweka ghalani!”

Kwa nini Tanzania isitamke kutoka kwa kwa Rais Jakaya Kikwete, kupitia kwa Waziri wa Fedha:

“Nawaambieni kweli, ninyi watumishi wa BoT, kila mnapokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa walalahoi, mnalisaliti taifa letu…Mmewekwa kwenye mizani na kuonekana mmepunguka…kwa herini; nendeni kuliko na kulia na kusaga meno!

Hawa wa BoT wanafaa kufukuzwa!
 
Back
Top Bottom