BRELA: Kalynda ilipewa leseni ya kuuza vifaa vya kielektroniki

BRELA: Kalynda ilipewa leseni ya kuuza vifaa vya kielektroniki

Kwahyo wakati ina tangaza mtandaoni kupitia reseni hyo wao hawakuona mpk jamaa wana tembea baada ya kushba pesa za wa2?
mkuu tumia akili nyingine ujue kwamba huu ni mradi wa watu wenye kilo nyingi nyingi
 
Kwa hiyo ni wajibu wa nani kukagua kama Leseni mliyotoa inafanya kazi tofauti na matakwa yenu...Nchi hii kila mtu anaamua afanye nini na wakati wowote..
 
KWANZA kabisa nianze kwa salam.

Kuna hili wimbi la polisi wanachunguza LBL na kukamata baadhi ya wahusika. Inaweza kuwa hatua nzuri na hapa naomba niwakumbushe Kalyinda.
IMG_6430.jpeg


Mwaka 2022 ulikua mwaka wa neema sana kwa matapeli wa mifumo ya Ponzi. Kabla ya kalynda walianza SCATEC wakajipigia zao pesa wakasepa na kijiji September 2024.

September hio hio watu hawajapoa ikafunguliwa KALYINDA na sales pitch yao ikawa ile ile sawa na SCATEC tofauti ikawa majina na rangi ya website. Vibali vilipostiwa mtandaoni, kejeli zikawa nyingi, “kama wewe unaogopa acha wenzako watajirike, hizi nyaraka za serikali tumetoa wapi kama sisi ni matapeli”.
Watu wakaweka hela. Hapa watu wakajiaminishana kwamba, sawa ni utapeli ila wa mwanzo wanapata hela kweli. Binafsi niliweza kuchomoa 100,000 nilioweka na nikaongeza 200,000 tena.
IMG_6433.png


wote tunajua KALYINDA ilizimika kama ndoto za kijana alietamani kuwa padri akishanusishwa bangi. Na tukaja kuambiwa vibali vilikua vya biashara ya umeme.
IMG_6429.jpeg


Wakati watu wanapambania KALYINDA IREJESHE PESA ZAO huko huko kwenye magrup zikaanza link za BEST BEI 🤣.


Hawa wakawa wajanja zaidi. Wakawa wamefungua website watu wanaweza kuwekeza hela ila kuvuna ingeanza tarehe 20/10 (kama sikosei)

Watu tukatabiri hao hio siku wanasema kuvuna ndo siku yao kukimbia, tukaonekana masnitch.

Siku ya siku kweli yakatimia. BEST BEI wakafunga website wakasema wamehakiwa na ndo safari.
IMG_6427.jpeg


HAYA YA LBL SIO MAGENI NA WATU HAWASIKII BADO WATATAKA KUJARIBU BAHATI YAO. KUPIGWA NI CONSTANT

Hata KALYINDA waliripotiwa hivo hivo na milard ayo 🤣.
Watu watalia na hautakua mwisho watakuja wengine tena na tutalia.
 
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imesema leseni ya kampuni iitwayo Kalynda E-Commerce Limited iliyotolewa Juni 21, 2022 ni kwa ajili ya uuzaji wa jumla wa vifaa vya kielektroniki na mawasiliano pamoja na ufanyaji wa biashara ya kiteknolojia ya kimataifa mtandaoni.

BRELA imesema kumekuwa na taarifa zinazoleta taharuki kuhusu kampuni hiyo kufanya biashara ya upatu ya kukusanya fedha kutoka kwa wananchi kwa ahadi ya kupata faida ndani ya muda flani kinyume na bidhaa au huduma iliyoombewa leseni.

Taarifa ya BRELA imesema leseni ya biashara ya Kalynda E-Commerce Limited inamruhusu kufanya biashara ya masoko na mauzo ya bidhaa kwa njia ya mtandao pekee, hivyo ufanyaji wa biashara kinyume na leseni iliyotolewa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 19 cha sheria ya leseni za biashara, Sura Na. 208.

Aidha, Wakala imetoa angalizo kwa umma kuwa kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kibiashara na kampuni yoyote ni vema kupata uthibitisho wa uhalali na uwepo wa kampuni hiyo pamoja na biashara husika kutoka BRELA na mamlaka nyingine za Serikali.

Swahili Times.

--
View attachment 2385491View attachment 2385492
Siyo kwamba hatupendi kuchunguza kabla ya kuwekeza, tunapenda sana ila tunaogopa kuchelewa kupata faida.
 
Back
Top Bottom