Bribery and corruption: Athreat to an early Bagamoyo Port

Bribery and corruption: Athreat to an early Bagamoyo Port

Pile F

Senior Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
121
Reaction score
170
Habari gani Wakuu ninaamini mpo vyema kabisa. Naomba Moja kwa moja niende kwenye mada

Tanzania ni Taifa lenye bahati kubwa. Wazo la bandari ya Bagamoyo ni la kipekee na Mataifa Mengi yangeona yapo nyuma mno kama nchi ya Tanzania ingekuwa na hii bandari leo.

Mradi huu umeachwa na kuchelewa kwa sababu kuu ya hofu ya Utitiri wa Viongozi wapenda rushwa, wenye uadilifu mdogo na siasa za kusifiana, kuficha taaluma zao, maovu na kutii makubaliano legevu katika Taifa letu.

Bandari hii ingekuwepo katika Taifa letu tusingekuwa tunapambana na mambo Madogo na ya kionevu kama kuwaondoa Machinga Mtaani maana wangekuwa wameajiriwa au kujiajiri katika njia au maeneo mengine Mengi. Na inawezekana kuwa wasingekuwepo vilevile katikati ya miji ambako ndipo Wateja wao wengi na wakubwa walipo.

Kwa mfano;
Biashara zinazolazimika kufanyika Bandari ya LOBITO kule Angola kutoka katikati na kusini mwa Afrika-Congo DRC, Congo Brazzaville, CAR, Zambia, Zimbabwe, Botswana, Malawi na kwingine zingemwacha Mtanzania akizalisha pesa za kigeni kupitia kuuza huduma na bidhaa kwa pesa nzuri na kupunguza makali ya Umaskini.

Kukua kwa sekta ya Utalii, Usafirishaji, Biashara za Supermarket na Hoteli kwa hadhi ya kimataifa. Pia kupitia uwepo wa Jamii ya kimataifa kutachangia sana kukua kwa Teknolojia na Uwekezaji katika Elimu, Viwanda, Kilimo na Masoko, Mawasiliano, Miundombinu na Mengi mazuri.

Wazawa watafanya Biashara za kisasa na Umaskini utapungua kwa kasi kupitia Ulimwengu unaotaka mazingira ya kufanyia biashara kwa gharama ya Dola nyingi na wakati mwingine kwa gharama ya pesa ya kiwango chochote.

Taifa litajitangaza bila nguvu kubwa kama ilivyo kwa UAE na mji wao maarufu wa Dubai pia Brazil zinazopata pesa nyingi kupitia Wageni wa kibiashara nchini.

Hili linawezekana kwa kuwa tuna mwambao mrefu wa bahari na wenye hazina kubwa ya Mali bahari pia visiwa salama kwa mazingira ya uzalishaji wa kisasa.

Tanzania itachapuka haraka na kuanza kuimarisha zaidi ulinzi pekee pamoja na Matumizi Bora ya Mazingira huku raia wake wote wakipata nafuu kubwa ya maisha kupitia kukua kwa Miji, AJIRA nyingi na Uchumi Imara wa Nchi.

NIONAVYO MIMI;
Ni fikra duni kuona kuwa TUTAIBIWA kama bandari ITAJENGWA.

Ni vipi uonavyo wewe kuhusu hii Bandari katika Pwani ya Tanzania kule Bagamoyo?
 

Attachments

Tatizo sio kujenga Bandari; tatizo ni huo utitiri wa masharti unaoambatana na ujenzi wa hiyo Bandari. Ndio maana watu walitaka hayo masharti yawekwe wazi kwenye vyombo vya habari; ili wananchi waweze kuyapitia na kuyajadili kwa uwazi.

Ili tuone kama kuna maslahi mapana kwa Taifa. Sasa inaonekana bado mambo yanafichwafichwa; na mtu mmoja mmoja ndio anaongea kutokana na kile alichopewa huko U-CHINA.

Isije ikawa kama yale mambo aliyofanya Professor Mkweli (Muongo); wa kusaini mikataba ya Madini, na kisha kuificha; hata kamati ya Bunge ilivyokwenda kutaka kuiona, yeye akakataa. Baadae ikagundulika tuliingizwa Kingi kama nchi. Sasa hatutaki hayo yatokee.
 
Tatizo sio kujenga Bandari; tatizo ni huo utitiri wa masharti unaoambatana na ujenzi wa hiyo Bandari. Ndio maana watu walitaka hayo masharti yawekwe wazi kwenye vyombo vya habari; ili wananchi waweze kuyapitia na kuyajadili kwa uwazi. Ili tuone kama kuna maslahi mapana kwa Taifa. Sasa inaonekana bado mambo yanafichwafichwa; na mtu mmoja mmoja ndio anaongea kutokana na kile alichopewa huko U-CHINA. Isije ikawa kama yale mambo aliyofanya Professor Mkweli (Muongo); wa kusaini mikataba ya Madini, na kisha kuificha; hata kamati ya Bunge ilivyokwenda kutaka kuiona, yeye akakataa. Baadae ikagundulika tuliingizwa Kingi kama nchi. Sasa hatutaki hayo yatokee.
Tutapona kweli? Huyu Muongo kama bado yupo hai sio ajabu tukashangaa siku akaapishwa kuwa Waziri. Watu hawatosheki na wanakula walewale wasioweza kutupana

Masharti! Kwani lazima wajenge Wachina?
 
Halafu kwa nini awe yeye? Mkuu Sio China walewale waliomuokota na Illegalities nchini mwao?
Hawa jamaa huwa wanatuona kama akili haziko sawa. Walianza na makaribisho ya Spika na kumpigia wimbo wa Tanzania, akarudi akisifia ukarimu. Nadhani watakuwa wamegundua ubwege wa yeyote mwenye maamuzi ya Bagamoyo na uhusiano wake na huyo Riziwani. Sioni sababu nyingine maana hata Bungeni hana kamati anayoiongoza.
 
Habari gani Wakuu ninaamini mpo vyema kabisa. Naomba Moja kwa moja niende kwenye mada

Tanzania ni Taifa lenye bahati kubwa. Wazo la bandari ya Bagamoyo ni la kipekee na Mataifa Mengi yangeona yapo nyuma mno kama nchi ya Tanzania ingekuwa na hii bandari leo.

Mradi huu umeachwa na kuchelewa kwa sababu kuu ya hofu ya Utitiri wa Viongozi wapenda rushwa, wenye uadilifu mdogo na siasa za kusifiana, kuficha taaluma zao, maovu na kutii makubaliano legevu katika Taifa letu.

Bandari hii ingekuwepo katika Taifa letu tusingekuwa tunapambana na mambo Madogo na ya kionevu kama kuwaondoa Machinga Mtaani maana wangekuwa wameajiriwa au kujiajiri katika njia au maeneo mengine Mengi. Na inawezekana kuwa wasingekuwepo vilevile katikati ya miji ambako ndipo Wateja wao wengi na wakubwa walipo.

Kwa mfano;
Biashara zinazolazimika kufanyika Bandari ya LOBITO kule Angola kutoka katikati na kusini mwa Afrika-Congo DRC, Congo Brazzaville, CAR, Zambia, Zimbabwe, Botswana, Malawi na kwingine zingemwacha Mtanzania akizalisha pesa za kigeni kupitia kuuza huduma na bidhaa kwa pesa nzuri na kupunguza makali ya Umaskini.

Kukua kwa sekta ya Utalii, Usafirishaji, Biashara za Supermarket na Hoteli kwa hadhi ya kimataifa. Pia kupitia uwepo wa Jamii ya kimataifa kutachangia sana kukua kwa Teknolojia na Uwekezaji katika Elimu, Viwanda, Kilimo na Masoko, Mawasiliano, Miundombinu na Mengi mazuri.

Wazawa watafanya Biashara za kisasa na Umaskini utapungua kwa kasi kupitia Ulimwengu unaotaka mazingira ya kufanyia biashara kwa gharama ya Dola nyingi na wakati mwingine kwa gharama ya pesa ya kiwango chochote.

Taifa litajitangaza bila nguvu kubwa kama ilivyo kwa UAE na mji wao maarufu wa Dubai pia Brazil zinazopata pesa nyingi kupitia Wageni wa kibiashara nchini.

Hili linawezekana kwa kuwa tuna mwambao mrefu wa bahari na wenye hazina kubwa ya Mali bahari pia visiwa salama kwa mazingira ya uzalishaji wa kisasa.

Tanzania itachapuka haraka na kuanza kuimarisha zaidi ulinzi pekee pamoja na Matumizi Bora ya Mazingira huku raia wake wote wakipata nafuu kubwa ya maisha kupitia kukua kwa Miji, AJIRA nyingi na Uchumi Imara wa Nchi.

NIONAVYO MIMI;
Ni fikra duni kuona kuwa TUTAIBIWA kama bandari ITAJENGWA.

Ni vipi uonavyo wewe kuhusu hii Bandari katika Pwani ya Tanzania kule Bagamoyo?
Tatizo si kujenga ila ni ufisadi uliopo katika mradi mzima. Bila ufisadi ni mradi mzuri.
 
Hakuna mtanzania hata wale wa la saba anayekataa umuhimu wa bandari na ungetusaidia sana badala ya kuja na faida ukaweka hayo yanaitwa mashart ili tuyaone wazi. Tusaidie hayo masharti 20 ya wachina tuyaone.
 
Tatizo si kujenga ila ni ufisadi uliopo katika mradi mzima. Bila ufisadi ni mradi mzuri.
Kuna mahakama ya Ufisadi nchini Tanzania.

Hawa wafanyabiashara wa Kichina na Oman kama wana mpango kujenga na kuiibia Tanzania Ina kitu gani?

Lengo lao nahisi ni kurahisisha masuala yao ya kuifikia Afrika kirahisi na kufanya Biashara kwa wingi zaidi.

Sasa Hawa wezi kwa nini kama wanajulikana wasikamatwe mapema kabla hawajachota Mamilioni
 
Hakuna mtanzania hata wale wa la saba anayekataa umuhimu wa bandari na ungetusaidia sana badala ya kuja na faida ukaweka hayo yanaitwa mashart ili tuyaone wazi. Tusaidie hayo masharti 20 ya wachina tuyaone.
 
Bandari ya Dar inamchango wa % ngapi kwenye pato la Taifa.? Miradi mingi ndani ya nchii hii watawala wa naweka maslahi yao mbele kwanza.
 
Dogo kichwa chake kiko tupu! Hata lugha yetu ya biashara iligoma siku nyingi sana!
Mishipa ya AIBU kule Msoga ilishakatika

Wananchi wa Chalinze hawakuwa na Jinsi maana pesa zao wenyewe ndizo zilizomuweka huyo Mb anaejali Biashara za familia kwanza
 
Mheshimiwa Rais safi sana, Mungu akupe afya njema tunakupenda. Ambae inamkera Bagamoyo port atulie au akajinyonge.
 
Back
Top Bottom