Brother K wa Futuhi

Mzee wa kamata makofi.. Bonge la komediani...!!
 
Watu mna maneno!
Eti ana shati kama la Le mbebez super bolionea.
 
Aisee jamaa namkubali vibaya sana,mimi natamani ile tengua kauli irudi nilikua napenda wanavyopigana japo hii ya mjini mipango sio mbaya...
Ayayayaaaaa amecharua mashetani hahahaaaa na lile hirizi lake saaaasa.....
 
Hakuna kipind kibaya cha vichekesho kama hcho cha FUTUHI kamwe sipotez mda kukiangalia
 
Mi nikiona kipind cha Futuna nabadilisha channel hebu ngoja next week nipoteze muda ni jaribu kuwaangalia.
Kuna clip moja hivi niliiona WhatsAAp kama ndio huyo comedian anaomba mzigo kwa Mkewe nikacheka sana basi anajua.
 
Mi niliipenda ile waliyoigiza kama walimu wa shule ya msingi ambao wanafumwa baa na wakaguzi wa elimu, yani braza K ndo mwalimu mkuu yuko na mchepuko wake ambao ni mwanafunzi.... braza K upo juu
 
sana huyu jamaa ni shidah..wa kukurupuka ahahahaa.
 
Huyu jamaa anaibeba futuhi kwa sasa
 
Yani muonekano wake tu mie hoi.Sasa akianza kuongea yani huwa ananichekesha sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…