Mwamba mbona yupo fresh tu kwa viashiria vya picha maana kwa muonekano ana afya njema, ngozi ina nuru nzuri labda kama tuseme umri umesogea na amebadilisha mfumo wa maisha tofauti na awali. (au mleta uzi ana vigezo gani kuonyesha jamaa amechoka zaidi ya hiyo picha)
Vinginevyo tunaingia kwenye record yetu ya muda mrefu ya "Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani zinazompima mtu kuchoka iwe kimwili au kiuchumi kutokana na mwonekano wake".Na ndio maana utapeli haumaliziki mjini, lijitu linapiga suti kali na ntambi yake linamtepeli mtu akishituka mtu ameshapotea