Uchaguzi 2020 Bunda: Haijawahi kutokea Esther Bulaya avunja rekodi akusanya watu kwa maelfu,Wazee wa mji wasema niyeye tu Bunda Mjini Oct 25

Wanawake wakiamua wanaweza haya zaidi ya wanaume...hongera kwake bulaya...mzee wasira anamsoma vema huyu bibie...alichomfanya 2015..hatokaa aje asahau
 
Mzee umeweka likizo akili yako, hivi kweli huoni jinsi wapinzani wanavyozuiwa, juzi tu hapa Tunduma mbunge kazuiwa kisa taarifa za kiintelijensia

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu huyu sio mzee kiumri bali mzee wa akili sio bure.

Wazee huongozwa na hekima na busara kabla hawajaongea au kufanya jambo lolote.

Hivi kwa hali ya sasa ya nchi kisiasa kuna mtu asiyeona hali ya upinzani ilivyongumu kufanya siasa za ushindani na chama tawala.

Dokt. Bashiru na Polepole kila siku wanafanya mikutano ya kisiasa sehemu yoyote ile wanayoitaka wao ndani ya nchi hii hivi wale jimbo lao ni lipi.

Kwa nini wao wanafanya mikutano bila pingamizi ila wapinzani wao ndio kuna intelijensia ya kutokuwa hali ya usalama kwenye mikutano yao.

Hawa wanaojiita wazee wengine ni wa kuwapuuza tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanakatazwa sana, heche analazimishwa Na polis kufunga mkutano wake Wa kuongea Na wananchi wake.
LIMBOMAMBOMA, ukisema alilazimishwa kufunga mkutano utakuwa unatuambia pia kuwa alikuwa anafanya mkutano, si ndiyo?
 
..angalia jinsi POLISI walivyojizatiti kwa SILAHA.

..unaweza kudhani labda wabunge wa CDM ni magaidi.


Cc Mzee Mwanakijiji
Ningelikuwa waziri Wa mambo ya ndani ningekomesha ujinga huu Wa jeshi LA polis.polis walinde usalama Wa RAIA Na Mali zao, siasa sio kazi yao wawaachie wanasiasa.
 
LIMBOMAMBOMA, ukisema alilazimishwa kufunga mkutano utakuwa unatuambia pia kuwa alikuwa anafanya mkutano, si ndiyo?
Kwani Ni dhambi kwa mbunge kufanya mkutano? Mbunge ana haki ya kuongea Na RAIA wake wakati wowote.wanasiasa wawe huru kama kina bashiru Na polepole wanapepea popote Tanzania kumwaga Sera zao.
 
Kwani Ni dhambi kwa mbunge kufanya mkutano? Mbunge ana haki ya kuongea Na RAIA wake wakati wowote.wanasiasa wawe huru kama kina bashiru Na polepole wanapepea popote Tanzania kumwaga Sera zao.
LIMBOMAMBOMA, sheria inasemaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…