Bunda: Kitimtimu cha Oparesheni 255 kimewaka, Lissu apokelewa kishujaa, Maelfu Wajitokeza

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hakuna namna nzuri ninayoweza kueleza mapokezi ya Tundu Lissu Mjini Bunda , itoshe tu kusema haya ni mapokezi ya kifalme , watu ni wengi kuliko maneno yangu .

Hakika kwa Chadema ni dhahiri sasa kwamba gari limewaka ! Si rahisi tena kuzuia Chadema kwa hali ilivyo , Uchawi na Fitna zote vimechemsha .

Kingine ni hiki , Habari za Mkataba mbovu wa Bandari zimewakasirisha mno wakazi wa Bunda , ambao Wamesisitiza ulazima wa Katiba mpya sasa hivi

Hali ndio kama mnavyoona


 
Duh chadema inataka kuua watu kwa presha
Toka CHADEMA wameanza mikutano ya hadhara na kupata halaiki ya watu, chama cha ACT kimepoa kabisa. Waliamini wao ni mbadala wa CDM, kumbe kiuhalisia ACT iko pemba zaidi.

CHADEMA wasije kulogwa kwa kukubali ule ujinga wa kuunganisha vyama vya upinzani eti kuitoa CCM. Hivyo vyama vingine viko kimya, kisha ikifika wakati wa uchaguzi wanataka waungane na CDM!
 
cdm ina watu makini, manake hata sisi mashabiki tu tupo makini
 
Kinawaka huko
 
Safi sana Mkuu lkn,wasiwasi wangu ni kwamba ccm hawategemei kura zetu sisi wananchi.Tegemeo la ccm ni mahakama,jeshi la polisi na tume ya Taifa ya uchaguzi.
Umewahi kujiuliza swali hili:
Kama CCM wanaweza kuwategemea mahakama, jeshi la polisi na tume ya Taifa ya Uchaguzi", kwa nini CHADEMA na wao wasifanye kila linalowezekana kuwategemea hao hao wakati wa uchaguzi?

Usikurupuke kujibu, wala usibeze kwa kushindwa tu kwako kuelewa maana ya swali hilo muhimu sana.

Kwani CCM wao wanawafanyia nini wote hao hadi kila mara wawe upande wao?

Huu ni mwelekeo mpya wa mawazo ninaouanzisha, ili CHADEMA waanze mara moja kazi kushughulikia upande huo.

CCM haina hati miliki na kitu chochote ndani ya nchi hii.

Mkuu 'monde arabe' nikushukuru kwa kunipa fursa ya kuweka mbele wazo hili, ili CHADEMA walishughulikie haraka.
 
Chadema itazunguka kata zote za Kyela , usiondoke Jf subiri upewe ratiba kamili , Kuanzia Mundamba mpaka Mwitete
SAWA.
Hii vita siyo ya mbinu moja.
Nakukaribisha kwenye mbinu nyingine hapo juu #13; iendane sambamba na mengine yote yanayoendelea wakati huu ndani ya chama.
Usisahau: mtaji mkubwa iliobaki nao CCM ni ukwasi wa pesa. CHADEMA na wanachama na mashabiki n a wapenzi na wengineo haipungui kuwa na milioni zaidi ya 15. Hawa hawawezi kushindwa kupata Tsh 1,000/ kwa mwaka kuichangia CHADEMA ifanye kazi ya kuwandolea uchafu waTanzania.

Kushindwa kwenu safari hii, itakuwa ni kwa ujuha tu, na siyo vinginevyo.
 
Zitto kafungwa mnyororo na Pemba, na Samia kamziba mdomo moja kwa moja.
 
Pweinti!
 
Ni kama ile Join the Chain , eneo hilo tuko makini mno
 
Long live Tundu LissuπŸ‘ŠπŸΎπŸ‘ŠπŸΎπŸ‘ŠπŸΎπŸ‘ŠπŸΎ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…