Bunge la bajeti 2011/2012 na yatokanayo

Bunge la bajeti 2011/2012 na yatokanayo

Familia cyo mbuzi leo ukaifunge kimara ipate malisho. Fanya kaz wewe kijana hii 2 je ambao wataiona 2050, unazan bia utauziwa buku jelo. Face reality.
 
embu ileteni hapa hiyo bajeti tuone kama mishahara imeongezeka, maana hali inazidi kuwa tete huku mtaani! riz sijui bado hajaongea na mshua?
 
Hii imekaaje wadau?

Mbona kama nilimsikia akisema sh 50,000?...na wabunge wakaipigia kelele/zomea! Kwa vyovyote vile kutakuwa na 'ulaji' zaidi kwa 'wazee wa fedha'!

Hata mimi nilisikia 50,000. Au hii siyo final version ya hotuba?
 
Hata mimi nilisikia 50,000. Au hii siyo final version ya hotuba?

Inawezekana walifanya marekebisho nyakati za lala salama! Labda Finance Bill inaweza kuwa clear zaidi.
 
HTML:
[HTML]Mheshimiwa Spika, mapato halisi ya ushuru wa forodha yalikuwa shilingi bilioni 343.2, sawa na asilimia 70 ya lengo la mwaka la kukusanya shilingi bilioni 493.1. Mapato kutokana na ushuru wa bidhaa kutoka nje yalifikia shilingi bilioni 455.0, sawa na asilimia 73 ya bajeti ya shilingi bilioni 622.8, wakati shilingi bilioni 258.7, zilikusanywa kutokana na ushuru wa bidhaa zilizozalishwa nchini, ikilinganishwa na bajeti ya shilingi bilioni 404.2, sawa na asilimia 64. Aidha, mapato kutokana na Kodi ya Ongezeko la Thamani kutoka nje yalifikia shilingi bilioni 664.6, ikilinganishwa na bajeti ya shilingi bilioni 999.3, sawa na asilimia 67, wakati shilingi bilioni 611.2 zilikusanywa kutokana na Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa mauzo ya ndani, ikilinganishwa na bajeti ya shilingi bilioni 992.3 sawa na asilimia 62. Makusanyo halisi yanayotokana na Kodi ya Mapato yalikuwa shilingi bilioni 1,255.8, ikiwa ni asilimia 74 ya bajeti ya shilingi bilioni 1,702.3. Aidha, mapato halisi yatokanayo na vyanzo vingine vya kodi yalikuwa shilingi bilioni 449.7, ikiwa ni asilimia 72 ya bajeti ya shilingi bilioni 620.9
.[/HTML]
Hapa inamaanisha serikali haikuweza kukusanya kabisa malengo ya kodi ile. Hii inamaana walipanga matumizi huku pesa hawana. Safari hii bajeti imeongezeka, wana lipi la kuzungumza kama mwanzoni kiashirio ni kwamba serikali haiwezi kufikia malengo?
 
HTML:
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11, Serikali ilipanga kukopa shilingi bilioni 1,397.6, kutoka vyanzo vya ndani ili kugharamia bajeti yake.  Kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 600.0 ni kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo na shilingi bilioni 797.6 ni kwa ajili ya kulipia hatifungani zitakazoiva. Hadi Machi 2011, kiasi cha shilingi bilioni 1,107.5 kilikopwa kwa ajili hiyo. Kiasi hiki kinajumuisha dhamana za Serikali zenye thamani ya shilingi bilioni 607.6 zilizouzwa katika soko ili kulipia zilizoiva  na shilingi bilioni 499.9 zilitumika kugharamia miradi ya maendeleo.
Kwanini wanakopa na si kubana matumizi. Tutajifunza lini kuishi kwa kile tuliokuwa nacho? Kulikuwa kuna ulazima wa kukopa? Hakuna vitu vilivyokuwa vinaahirishika?
 
HTML:
kuwataka wafanyabiashara wenye namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN), kuzuia asilimia 2 kila wanapofanya malipo kwa wasiokuwa na namba hizo, kutokana na bidhaa au huduma walizopata kutoka kwao, ili kuwahamasisha wasiokuwa na namba kwenda kusajiliwa.
Hii strategy ni very poor. Wanacontrol vipi malipo na collusion kwa wafanyabiashara. Kwanini kazi zao wazipeleke kwa watu wengine. Ufanisi wa hili uko wapi?
 
HTML:
30.   Mheshimiwa Spika, kufuatia kuanza kutengemaa kwa uchumi wa dunia  baada  msukosuko wa kiuchumi duniani na nia ya Serikali ya kuboresha upatikanaji wa taarifa zilizohakikiwa kuhusu mwenendo mzuri wa Taifa kiuchumi, kisiasa, na utawala bora.  Serikali inaendelea kumtafuta Mshauri Mwelekezi wa Kimataifa kwa ajili ya kusimamia zoezi la kutathmini uwezo wa Nchi  wa kukopa na kulipa madeni (Sovereign Credit Rating). Mambo muhimu yanayozingatiwa katika tathmini hii ni pamoja na; hali ya utulivu wa kisiasa; kasi ya kukua kwa uchumi; udhibiti wa usimamizi wa bajeti ya Serikali; udhibiti wa masoko ya fedha na hali ya mfumuko wa bei; na urari wa malipo ya nje ya nchi. Hatua hii itasaidia kuwavutia wawekezaji na wakopeshaji kutokana na kuwepo kwa taarifa ya hali ya uchumi, siasa na utawala wa nchi na hivyo kurahisisha upatikanaji wa mikopo nafuu kutoka nje ya nchi kwa Serikali na kwa sekta binafsi.
Kukopa ni muhim, lakini tokea tumeanza kukopa tumefaidika vipi na mikopo? Utasikia tuna kopa pesa kwa ajili ya miundombinu, wasimamizi wako wapi au ndio washauri. Maana ukiangalia hata uwezo wa kulipa hatuna. Tungejenga nidhamu kwenye matumizi kwanza kabla ya kuwaza kukopa.
 
HTML:
31. Mheshimiwa Spika, mwaka 2000/01, Deni la Taifa, lilikuwa Dola za Kimarekani bilioni 8.55 ikilinganishwa na Dola bilioni 10.01 mwaka 2005/06 na kupungua mwaka 2006/07 hadi kufikia Dola bilioni 7.53. Kupungua kwa deni hilo kulitokana na misamaha mbalimbali ya madeni kutoka nchi wahisani na mashirika ya fedha ya kimataifa chini ya utaratibu wa (HIPC na MDRI). Aidha, Deni la Taifa liliongezeka hadi kufikia Dola bilioni 10.54 mwaka 2009/10, kutoka Dola bilioni 9.36 mwaka 2008/09. Kati ya Deni la mwaka 2009/10, Dola bilioni 5.99 ni deni la nje na Dola bilioni 4.55 ni deni la ndani, ikijumuisha Dola bilioni 1.63 za dhamana za Serikali kwa miradi ya Wizara, Idara na Taasisi za Serikali.

Hii sentensi ni ya kiujanja ujanja. Hawatoi michanganuo ya ndani kwa mwaka 2005 bali wanakuja kuchanganua vizuri. Kifupi deni la ndani limeongezeka zaidi kutokana na ugumu wa kukopa nje. Unaweza kuangalia ongezeko hilo la deni kwa kipindi kifupi hivyo ni kiasi gani
 
Hivi ni lazima hotuba iwe ndefu hivi na kujirudiarudia kwingi hivyo? hakuna namna bora ya kuandika bajeti? Uandishi huu wameutoa wapi? Maana ni hadithi badala ya issues.
 
HTML:
[FONT=Tahoma]i)        Kilimo na umwagiliaji kimetengewa shilingi bilioni 926.2 ikilinganishwa na shilingi bilioni 903.8 mwaka 2010/11, sawa na ongezeko la asilimia 2.5;[/FONT]
[FONT=Tahoma][/FONT]
Hii ni dhihaka kwenye na ile slogan yao ya kilimo kwanza. In real terms bajeti ya kilimo haijaongezeka hasa ukizingatia kuporomoka kwa Tsh. Mwaka jana wakati kama huu BOT indicative rate ya Tsh against USD ilikuwa 1392 na sasa ni 1517 kwahiyo inamaanisha in USd (The currency is regarded to be strong currency) imepungua kutoka bil 0.64 (yaani milioni 640) tu bil 0.62. Maana siku hizi vitu vinafanywa kwa USD kwa hiyo tukitumia Tsh ni kuwaandaa wananchi. Kama ilivyo miundombinu si 84% bali ni between 60-70%
Vivyo hivyo kwenye elimu na afya;
HTML:
i)        Elimu imetengewa shilingi bilioni 2,283.0 ikilinganishwa na shilingi bilioni 2,045.4 mwaka 2010/11, sawa na ongezeko la asilimia 12; na
 
ii)      Afya imetengewa shilingi bilioni 1,209.1 ikilinganishwa na shilingi bilioni 1,205.9 mwaka 2010/11, sawa na ongezeko la asilimia 0.3.
Hawa jamaa wanasema wataendelea kuajiri. Lakini kwenye bajeti hakuna ongezeko la kuonyesha kuna ajira mpya za watumishi wa afya au elimu. Pia kumbuka kuboresha maabara na madarasa. Kitu gani kilichofanyika bajeti iliyopita kwenye wizara ya elimu na afya hakitafanyika sasa. Kuna kupanda mishahara pia watumishi.

 
HTML:
MASUALA YANAYOHUSU SERIKALI ZA MITAA:
70.   Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha utendaji na uwajibikaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia Programu ya Maboresho ya Serikali za Mitaa (LGRP II) ili kuwawezesha Wakurugenzi kusimamia majukumu yao kikamilifu. Serikali pia itawajengea uwezo Waheshimiwa Madiwani ili wasimamie utendaji wa Halmashauri zao na kuhakikisha nidhamu ya kazi inaimarishwa kulingana na sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma. Aidha, kamati za kupambana na rushwa pamoja na kamati za maadili za Halmashauri zitaimarishwa ili kusimamia nidhamu ya watumishi wa kada zote na kuhakikisha utendaji wao unazingatia maslahi ya taifa.
Hizi kamati za kupambana na rushwa na kamati za maadili. Why zinakuwa tofauti? kwani maadili na rushwa kuna tofauti gani? Hivi vikamati ndio mzigo unless wanasiasa wetu waseme ni miradi kwao
 
HTML:
i)     Kuanzisha utaratibu wa marejesho ya Kodi kwenye mauzo ya rejareja kwa bidhaa za ndani zinazouzwa kwa abiria ambao sio raia wa Tanzania wanaosafiri nje ya nchi. Utaratibu huu utaanza kutekelezwa kwa kuanzia na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kwa mauzo ya thamani ya shilingi 400,000 na zaidi. Utekelezaji wa utaratibu huu mpya utaanza  rasmi tarehe 1 Januari 2012.
Hili linastahili pongezi maana wenzao wameanza kufanya siku nyingi. Lakini gharama yake ni kupunguza mapato kwa serikali licha ya kwamba mauzo na profit kwa wafanyabiashara yanaweza kuongeza kinadharia. Hivi wamefanya tathmini na kuona kwa hatua hii, serikali imejipanga kiasi gani kulisimamia? Maana linahitaji utaalamu na vifaa vya hali ya juu. Tanzania watu wanaforge saana maana wafanyabiashara watatokea hapo. halitakuwa kero kwa raia wa kigeni. deficit ya hiyo kodi wanahakika italipikika kupitia ongezeko la mauzo kwa wafanyabiashara that means profit?
 
HTML:
i)     Kuondoa unafuu wa Kodi ya Ongezeko la Thamani uliokuwa unatolewa kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (Non Governmental Organizations). Hatua hii haitazihusu Taasisi za Kidini (Religious Organizations); na
ii)  Kutoa unafuu wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa Mashirika yasiyo ya kiserikali (Non Governmental Organizations) kwa vifaa vya matumizi binafsi ya kawaida (household consumables) kama vile vyakula, mavazi, na vifaa kama sabuni ambavyo vinatolewa msaada kwenye vituo mahsusi vya kulelea watoto yatima na shule.
Ubunifu huu wa vyanzo vya mapati ni kuwatapata. Yaani hivi navyo wanaviona vyanzo? Kuna tatizo kwenye NGO's kweli wengi tunafaham ni kijiwe cha watu kukwepea kodi. lakini tunashindwa kutengeneza misingi ya kuzuia hali hiyo? hatuoni manufaa ya NGO's? Zipo NGO's zimefanya vizuri saana kwa haki za wanawake na watoto kazi ambayo ilitakiwa ifanywe na Idara ya Ustawi wa jamii. Idara ile imechoka saana na haijiwezi ipo taabani. leo hii tukianza kuwabana hawa, serikali imejipanga vipi kusaidia hilo gap litakalotokea hapo.
Hivi serikali inatambua pesa za NGO's zinavyopatikana. Watu wanaweka effort kubwa saaana kuzikusanya ughaibuni. Yaani ni voluntary contribution kwa ajili ya program fulani kwa nchi zinazoendelea. leo hii kupiga tax ni uungwana. labda wangeweka ukomo wa exemption kwa kila NGO's atleast au la ni kuweka mechanisms za kuzuia wizi through tax exemptions
 
Back
Top Bottom