Bunge la bajeti 2011/2012 na yatokanayo

there are systems coming to ensure that the money goes to the right channel...stay tuned!

mkuu hiyo system itakuja nzuri kweli kwenye maandishi na kimpango, kazi itakuwa kwenye utekelezaji hamna kitu chochote.
 
there are systems coming to ensure that the money goes to the right channel...stay tuned!
You may wish to understand that sytems in themselves do not curb corruption. Do you want us to believe that currently there no systems? Should your allegations be true, then Tz is a jungle!! No No.
The other question you could be asking is: how many, for example, daladala drivers wlll pay fifty tzs? The possibility is that they will not afford and because they will not afford they will pay less, and because they will pay less the money will find their way in the pockets of law enforcers or the drivers will end in prison.
Prudence seems to dictate that, fine should be affordable, feel pinch and make the defaulter refrain from similar acts.
Most of us notice what the police
do..,,..
 
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA
SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2011/2012

UTANGULIZI:

1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kujadili na kupitisha makadirio ya mapato na
matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012. Pamoja na hotuba hii, vipo vitabu vinne vinavyoelezea kwa kina takwimu
mbalimbali za Bajeti. Kitabu cha Kwanza kinahusu makisio ya mapato. Kitabu cha Pili kinaelezea makisio ya matumizi ya
kawaida kwa Wizara na Idara zinazojitegemea ambapo cha Tatu kinahusu makisio ya matumizi ya kawaida kwa Mikoa na
Mamlaka za Serikali za Mitaa na cha Nne kinaelezea makadirio ya matumizi ya maendeleo kwa Wizara, Idara zinazojitegemea,
Mikoa pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, upo Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2011 ambao ni sehemu
ya Bajeti hii.
2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya
Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuongoza kwa muhula wa 3 pili wa Serikali ya Awamu ya Nne. Aidha, ninamshukuru sana
Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyonayo kwangu kwa kunichagua kwa mara nyingine tena kuongoza Wizara kubwa na
nyeti, ninamuahidi kuwa sitamuangusha. Pia ninampongeza Dkt. Mohammed Gharib Billal kwa kuchaguliwa kuwa Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vile vile, ninampongeza Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb.) kwa
kuchaguliwa kuwa Mbunge na kuteuliwa tena na hatimaye kupitishwa na Waheshimiwa Wabunge kuwa Waziri Mkuu kwa
muhula wa pili wa Serikali ya Awamu ya Nne.

Hii ndiyo nakala halisi ya Bajeti aliyosoma waziri wa fedha na uchumi Mustapha Mkulo Bungeni Dodoma
 
Mfano ni relevant kabisa. Hauna tofauti na huo ulioutoa wewe. Nimezungumzia posho ya kila siku ya kuhudhuria semina, warsha, mikutano nk. Sijazungumzia gharama za kusafiri kikazi. Hata sheria yenyewe ya kodi inazungumzia actual expenses are allowable deductions lakini posho (merely posho) lazima ikatwe kodi.
 
Yaani kama nawaona police wa salendar pale wanajificha kwenye miti wanasubiri upite na taa nyekundu wakurukie kati kati ya barabara....akikuweka kando anakuandikisha fine ya 50,000 kwa kitabu chake fake!!!!mkulo ulie tu zoote zitaenda bar na nyumba ndogo gap la bajeti utatembeza bakuli si tozo za baloon zetu!!!natamani niwe traffic ghafla!!na ili kupata u traffic ukiwa general duty police dau nalo laongezeka!!!hongereni 'maporisi'kwa kupewa deal la mwaka hili......ongezeni watoto wasio na malengo/mnaoshindwa kuwamudu....bar zote mnatawala ninyi...vimada kila mtaa!!!kisa wachache wavivu kufikiriaa aaahh hapana vyanzo vya mapato vimeisha tanzania!!!
 
Kwa uelewa wangu na toka nilipopata ufahamu wa bunge letu hakuna budget ambayo ilishawahi kupingwa ila ni kuponda kwa sana na mwisho wa siku wanaunga mkono asilimia 100. Hivyo basi japo kidogo hicho kilichopatikana, CHADEMA inabidi kupanga mbinu za kuendesha halmashauri zote zilizo chini yake ili wananchi waweze kuona nani anaweza kupewa nchi na akaipeleka rehemani maana hawa jamaa wemeweka pamba masikioni japo wanasikia kwa mbali ila hawaelewi wafanye nini na hapo ndipo pa kuchukulia ujiko kwa raia.
 
Anataka muda wa kujiandaa kuchakachua majibu ndio maana kashindwa kujibu, swali la nyongeza huja pale muulizaji anapokuwa hajarizika na majibu ya swali husika..
 
Mkuu hata mimi nilikuwa mbishi kama wewe na mwenye mapenzi ya ccm kama wewe ila baada ya kujua mimi wala watoto wangu hawatafaidi matunda ya ccm bali ni machungu, chuki na dhihaka muda sio mrefu utakubali mkuu unless otherwise kama una interest Tehe tehe
Ha ha ha! fananisha mimi kuhama CCM ni sawa na kuhama YAanga....haiji yani.
 
hivi serikali haioni kama rushwa barabarani ni tatizo?, mbona wanaichochea?, makosa yenyewe ni ya kipuuzi half wanakomaa na kuongeza faini! Mi nadhani walitakiwa waangalie mfumo wote kabla ya kupayuka bungeni! Mfano kosa la kuendesha gari bila kufunga mkanda halitakiwi kulingana faini na kosa la kuendesha ukiwa umelewa!

Elf 20 yenyewe ilikua kubwa sana kwa baadhi ya makosa kama vile kukutwa gari haliwaki baadhi ya taa!

Hawajui ajali nyingi ni matokeo ya mambo mengi sana ambayo swala la faini ndogo halimo kabisa? Ajali ni matokeo ya rushwa katika utoaji wa leseni, ujenzi wa barabara na kwa askari barabarani!

tuombe Mungu atuepushe na upuuzi huu wa kukamuana badala ya kuneemeshana!
 
Hahahaha jamaa matumbo yatazidi kuwa makubwa tuu. Nilikwenda ubalozi wa Nigeria jtatu iliyopita nilikuwa na wife saa tunarudi tukasimamishwa na trafiki pale colloseum, trafiki janja yao ndogo tuu tukaweka gari pembeni trafiki na tumbo lake kuuubwa akaja mlangoni eti mkuu wewe ndo mlengwa hebu nipe leseni yako si akazunguka upande wa wa pili akakutana na wife bwana wife akamsalimia kama anamjua akatia salama lkn? unanikumbuka? trafiki akasita wapi mama tulionana wife akatia mwenge TRA umeshau ulikuja na mwenzio, trafiki aaargh nakujaga mara nyingi tu pale, wife akatia nipo pale upande wa branch manager trafiki kijasho kikamtoka akatia sawa mama unajua nakutana na watu wengi sana ntakuwa nimesahau akasema wife akasema karibu sana ofisini pale basi endelea na kazi yako trafiki akaona duh huu msala mtu ananijua mimi simjui ishakuwa nuksi akasema kaka basi nendeni nawashukuru kuwafahamu tutazidi kuonana haooooooo tukaondoka sina mbavuuuuuu tehetehe. ukipigwa mkono na trafiki kuwa na confidence tu wala hafanyi lolote
 
Ndio maana nasema chana kadi ya magamba man umeonae..?? mi ntakuuliza tuu habari za ulikotoka ha ha ha ha
Hee!..siyo mbongo?
Huu sasa ni uhuni,wanadisrespect mayanki wa kibongo wenye shule zao.
 
Hii ni dhihaka kubwa sana kwa taifa la wengi wasio watumishi, nanunua uraia kama ccm watakuwa madarakani mpaka 2014 maana wakifika ntaamini hata 2015 yatakuwa yale yale
Wakubwa wanakubali kuwa gharama za maisha zimekuwa juu na hivyo wamebuni mbinu ya kupunguza makali hayo kwa wao wenyewe, kwa hiyo wategeuza malipo yao mengi yawe kwenye category ya posho na hiyo kukwepa makato. Wananchi watabaki kuwa 'cash cow'.
 
Wadau

Nimerudia mara mbili budget yetu kwa mwaka 2011/12. nimejiuliza sana mbona haijaonyesha kama serikali inategemea ongezeko la mapato kwenye madini ambayo kila mara raia wasio na hatia wamekuwa wanauwawa?

Hivi ndo MAISHA BORA kurudisha malipo ya leseni kwa wafanyabiashara wadogo ambayo yanawaongezea watanzania mizigo huku tukiwaacha wawekezaji wakiNEEEEEMEKA?????????

Kwa hili BUDGET hii siyo ya kumpunguzia makali ya maisha MTANZANIA.
 
Yaani kama nawaona police wa salendar pale wanajificha kwenye miti wanasubiri upite na taa nyekundu wakurukie kati kati ya barabara....!!!

mi yamewahi kunikuta!, ila sikutoa rushwa nililipa faini na nikakomaa wanipe lisiti ya serikali walitaka wachakachue!
 
nina miaka 40 ccp watanikubali kweli?
maana nimejaribu kuufikiria ubunge nikaona ni maji marefu.
mwenye namba ya mwema anitumie sasa hivi nijaribu kete ya mwisho kwani umri ndio unaenda hivyo.
kazi tz zipo mbili tu ubunge na sasa trafic
Umesahau TRA!?
 
Mkuu achana nae huyo hajitambui, hakuna mwenye akili timamu then aipende ccm inayotumiza kila cku
 
Haha ukiangalia hizi picha na hiyo budget yao basi hutokubali kama unaakili timamu,hahahhaha,dah,yaani mtu una nyumba ya udogo kijijini,hakuna hata hospital huko wala ambulance ikisha bado unaweka picha ya kikwete,ccm oyeeeee hahahhaha
 
Kodi hii inypendekezwa kusamehewa ni katika posho ambazo hulipwa kwa watumishi wa kadi za juu tu, hivyo mananchi wa kawaida hatanufaika na chochote. Ni heri wanekubali mapendekezo ya TUCTA kupunguza inacome tax ambayo inamgusu kail mtumishi.

Mkuu sheria ya kodi ilikuwa inataka hizo posho zikatwe kodi lakini hakuna kodi yoyote ilikuwa ikikatwa kwenye hizo posho. Kayika hili hakuna jipya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…