Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...
 
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...
Acha kupotosha we Mzee, kwa maana hiyo kulikuwa na maana gani ya sisi kutoa maoni yetu?

Akili zikizidi sana zinageuka kuwa hasara.
 
Wakipitisha katiba isiyokidhi viwango basi haitadumu itabadilishwa tena ndani ya miaka kumi.
Mimi hata ije rasimu ingine bora tu iweke mbele maslahi ya nchi na haki ya mtanzania mmojamoja ipatikane.
 
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...

Hatua tuliyofikia ni

1:CCM wapitishe Rasimu yao kinyume na matakwa ya umma

2:Tusiwe na katiba mpya- Hii ni kwa sababu wanajua wakipitisha rasimu yao ni ama ikubaliwe au ikataliwe na hivyo tuendelee na katiba ya sasa


CCM hawataki katiba mpya sasa
 
Kwa hali hiyo tumeuziwa Mbuzi kwenye Gunia kumbe ndo maana walikuwa wanataka tume isiendelee kuwepo kumbe walikuwa na lao Jambo dhalau hii kwa Watanzania kamwe haitavumilika kama ni kweli hakika uvumilivu utaelekea kutushinda kama kuvumilia Watanzania tumevumilia mengi sasa kwenye hili la Katiba Watanzania tuamke Tuwe kitu kimoja.
 
Hatua tuliyofikia ni

1:CCM wapitishe Rasimu yao kinyume na matakwa ya umma

2:Tusiwe na katiba mpya- Hii ni kwa sababu wanajua wakipitisha rasimu yao ni ama ikubaliwe au ikataliwe na hivyo tuendelee na katiba ya sasa


CCM hawataki katiba mpya sasa

Ben, mchakato mzima toka mwanzo ulitengenezwa kuweza ukiangalia matakwa ya CCM. CCM watafanyia mabadiliko makubwa rasimu ya Warioba na watapiga kura na kura zitaamua nani anakubalika. Wakipitisha basi watakuja kwa wananchi ambako threshold ya kupitisha ni ndogo mno kuliko ya huko Bungeni...
 
Mzee Mwanakijiji hoja yako naikubali 100%.

Anayekupinga inabidi ajihoji ni kwa nini kuna fununu za kuwepo Rasimu Mbadala ambayo pia imeshaanza kuombewa jukwaa Bungeni!

Enyi watanzania hasa hasa watanganyika; kumbukeni kauli za akina Mathias Chikawe, Celina Kombani, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, n.k.

Nachelea kusema kuwa KATIBA MPYA iliyo upande wa wananchi ni ndoto ndiyo maana wawakilishi wengi wanataka posho tu kwa sasa!

Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...
 
WEll.. subirini mshangae.. si mlikubali mchakato... ndiyo hivyo... Bunge litafuta vipengele na uzuri ni kuwa watapiga kura na wengi watapewa!!!
Wazo hili ndilo lilikuwepo tangia mwanzo, kuwa mtawala ambaye amekuwa akikumbushwa mara zote kusimamia na kufuata katiba iliyopo huku akipuuza hawezi hata siku moja kuanzisha mfumo wa kuzirekebisha sheria zile zile ili zimbane yeye.
Wanaodhani kuwa hili linawezekana wakumbuke kuwa katiba mpya lilikuwa wazo la wapinzani na watawala walilidandia. Kutokana na nia yao kutokuwa halisi (sincerely) ndio maana limezungukwa na usanii ili 'lionekane limefanyika'.
Kinachoendelea hadi sasa ni ushahidi wa MMK kuwa mawazo feki yalizaa mchakato feki ambao umepelekea sheria feki, bunge feki (kama alivyoliita Mtikila) na mwisho itakuwa product feki.

 
Ben, mchakato mzima toka mwanzo ulitengenezwa kuweza ukiangalia matakwa ya CCM. CCM watafanyia mabadiliko makubwa rasimu ya Warioba na watapiga kura na kura zitaamua nani anakubalika. Wakipitisha basi watakuja kwa wananchi ambako threshold ya kupitisha ni ndogo mno kuliko ya huko Bungeni...

Nakubaliana na wewe .Nakumbuka mwezi April mwaka 2012 nilipinga composition ya Bunge la Katiba.Nadhani nilikua nikichangia kwenye mjadala ulioanzisha na tulikua wachache sana tuliopinga huu mchakato tangu Mwanzo.Miaka 2 baadae tuko hapa

Historia ya Kenya ipo njia kujirudia hapa Tanzania

Historia ya alliance ya chama tawala cha MMD na chama cha UPND dhidi ya hoja za Patriotic Front na wanaharakati pamoja na wananchi wa Zambia kwenye katiba inajirudia na chama tawala wakajichimbia shimo kwenye uchaguzi mkuu uliofuata Upinzani ukashinda

Hofu ya chama tawala ilikua kuogopa reforms za tume ya uchaguzi na pendekezo la mshindi wa urais kupata 50%+1 ya kura zote.

Sasa uchaguzi mkuu uliofuata 2011 upinzani ukashinda ingawa hawakufikisha 50% + 1 .Wangekua na katiba mpya wasingetangazwa washindi

Wananchi waliungana na upinzani kwa kuwa walijua chama tawala hakina nia thabiti ya kushiriki mchakato wa katiba mpya kwa maslahi ya wazambia wote.

CCM hapa hawajifunzi.Nasi tuendelee kuwakumbusha wananchi historia na upinzani tujipange kuonyesha misimamo hata kama tumeshafanya makosa

Nilisema hatuwezi kufanya mazungumzo na watu wasio na nia njema.Wengine wakanikemia kuwa katiba mpya eti haipatikani barabarani

Msimamo wangu ni kuwa wasiotaka kukaa mezani kwa nia njema tukutane nao barabarani kisha turudishane mezani tukiwa na maumivu sasa tujadiliane kwa nidhamu.
 
Kwa hali hiyo tumeuziwa Mbuzi kwenye Gunia kumbe ndo maana walikuwa wanataka tume isiendelee kuwepo kumbe walikuwa na lao Jambo dhalau hii kwa Watanzania kamwe haitavumilika kama ni kweli hakika uvumilivu utaelekea kutushinda kama kuvumilia Watanzania tumevumilia mengi sasa kwenye hili la Katiba Watanzania tuamke Tuwe kitu kimoja.
Hapo kwenye red mara nyingi hunitia mashaka kutokana na hulka za Watanzania. Umejipanga kiasi gani 'kushindwa uvumilivu'!?
Jana nilisikiliza interview moja juu ya nchi ya mwisho Ulaya kuuangusha mfumo wa Kikomunisti, Albania. Sikuamini niliposikia kuwa wakati mageuzi yalishafanyika kote Ulaya Mashariki yenyewe ilisalia na siasa za 'gilba' kama zetu huku wananchi wakiwaangalia watawala kwa mazoea kama kawaida.
Walikuwa ni wanafunzi wa chuo kikuu kimoja wasiofikia hata 800 (mia nane) walioanzisha mgomo wa kula chakula ndio ulipelekea serikali kuanguka. Beware of 'talk the talk...'!
 
Hatua tuliyofikia ni

1:CCM wapitishe Rasimu yao kinyume na matakwa ya umma

2:Tusiwe na katiba mpya- Hii ni kwa sababu wanajua wakipitisha rasimu yao ni ama ikubaliwe au ikataliwe na hivyo tuendelee na katiba ya sasa


CCM hawataki katiba mpya sasa

Mkuu sasa ndio anatambua kuwa CCM hawataki katiba mpya?? Tangu mwanzo kwani waliitaka? Hoja ya katiba mpya aliidandia mwenyekiti wao na baadaye umeona mwenyewe alivyogeuka. Tusubiri tu miujiza!!!
 
Msimamo wangu ni kuwa wasiotaka kukaa mezani kwa nia njema tukutane nao barabarani kisha turudishane mezani tukiwa na maumivu sasa tujadiliane kwa nidhamu.

right on; nadhani mwanzoni watu walidandia wazo la "Katiba Mpya" bila kufikiria sana kwani wengi waliamini kile kilichoitwa "nia njema" ya Rais Kikwete. Ikumbukwe kuwa mchakato huu haukuanzishwa na chama chochote cha siasa na hata kwenye CCM haukuanzia katika utaratibu wa vikao vya chama; ni kama Kikwete aliamka tu usiku mmoja na kuamua kuwapatia wananchi Katiba Mpya! Wapinzani ambao ndio walikuwa na hoja hii walikumbatia pendekezo hilo wa furaha wakiamini wameshinda.. sasa miaka mitatu baadaye watu wanaanza kuona machungu.

Mwisho wa siku nadhani ama wataamua kujitoa when it is too late au watalazimika kushindwa kwa nguvu ya kura na kujikuta kuwa hawana uwezo wa kuleta mabadiliko mengine wao wenyewe. Ni bora tungechelewa ili tuwe na mchakato mzuri na wenye kuzaa Katiba Bora kuliko kuwahi na kujikuta tunaburuzana na kubambikiziana Katiba mpya
 
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...

Basi kama ni hivyo hapakuwa na haja ya kuunda Tume ya Warioba,tungeanza na Bunge la Katiba moja kwa moja ili kuepuka gharama zisizokuwa za msingi. Kwa sababu kama Bunge la Katiba lina uwezoa pia wa kutengeneza rasimu tofauti kabia na ile ya Jaji Warioba, maana yake ni kwamab litakuwa ni Bunge la kutunga Katiba kulingana na linavyoona lenyewe. Rasimu a Warioba ndiyo imebeba mapendekezo ya watanzaina wote, Bunge la Katiba likitengeneza rasimu nyingine tofauti na ile ya Warioba, litakuwa limetengeneza rasimu isiyotana na maoni ya watanzania, sasa je, in case ikitokea hivi kutakuwa kulikuwa na hjaa gani ya kuwa na tume ya Warioba?
 
Na ikiwa itatokea watafanya kubadili maoni ya rasimu ya katiba kutoka kwenye tume ya Warioba ambayo yametokana na wananchi halafu wakaweka madudu yasiyo na chembe ya utaifa bali vyama vyao kwenye kura ya maoni lazima tuiteme, NI HERI KUWA NA PENGO KULIKO KUWA NA JINO BOVU LITAKALOKUSUMBUA USIKU NA MCHANA KWA MAUMIVU
 
Hatua tuliyofikia ni

1:CCM wapitishe Rasimu yao kinyume na matakwa ya umma

2:Tusiwe na katiba mpya- Hii ni kwa sababu wanajua wakipitisha rasimu yao ni ama ikubaliwe au ikataliwe na hivyo tuendelee na katiba ya sasa


CCM hawataki katiba mpya sasa

Hakuna tofauti kubwa ya mfumo uliotumiwa na tume ya walioba na huu wa bunge la sasa kupata maoni.tume ya walioba ilitumia sampling kupata maoni kwa maana haikuweza kuwafikia watanzania wote na baadaye kufanikisha kuwa na document ya kuanzia.

Bunge maalumu la katiba ni wawakilishi wa wananchi,taasisi na asasi zenye malengo yanayofanana,hivyo waliopo bungeni nao ni wawakilishi wa wananchi kupitia kura ama kwa nafasi mbalimbali walizokuwa nazo.Kwa ujumla tunasema ni wawakilishi wanaosimama kwa niaba ya wananchi bila kujali wana itikadi gani za siasa.

Inawezekana kabisa katika maeneo mengine tume ya Jaji Walioba haikuwa sahihi,ama sehemu nyingine kampeni za ushawishi zilikuwa kubwa na watu kuchangia bila utashi wao kwa maana ya kushawishiwa na makundi ya kisiasa,lakini pia inawezekana katika maeneo mengine tume ya jaji walioba ilikuwa sahihi kwa asilimia mia moja.Jaji walioba anastahili kupewa pongezi,kama kuna mapungufu ni ya kibinadamu kama binadamu yeyote yule.Sasa mjadala upo mezani,muda upo wa kutosha na hapo kikubwa ni kutofautisha kati ya hoja ya nguvu na nguvu ya hoja.

Tofauti za mitazamo zinazotengeneza magenge tofauti,lazima tukubali,lakini kikubwa zaidi ni kwa waheshimiwa wetu wabunge kujitaidi kujenga hoja ambazo hata mwenzako hakiwa na kichwa kigumu ama msimamo usiobadilika ambaye ameingia bungeni kwa kuapa kwamba piga huo msimamo wangu huu lazima upite itafikia hatua ataona aibu tu.
 
Back
Top Bottom