Bunge labaini kusuasua kwa usafiri wa Mwendokasi Dar

Bunge labaini kusuasua kwa usafiri wa Mwendokasi Dar

Bla bla nyingi kila siku Kafulila anatamba kwenye vyombo vya habari juu ya ushirikiano wa serikali na watu binafsi huku akiwaita wafanyabiashara binafsi kama wameona fursa waende wapewe. Wameshindwa nini kumpa baadhi ya njia Bakhresa au mwekezaji mwingine yoyote mzawa? Hivi mradi mdogo kama mwendokasi bado serikali itataka mwekezaji toka nje?

Zaidi ya mwaka sasa mabasi ya mwendokasi yamepungua kwa kiasi kikubwa je hatua gani zimechukuliwa na serikali zaidi ya kuwabadilisha mabosi wa mwendokasi kila kelele zikizidi ili kuwazuga wananchi. Nilitegemea bunge liiwajibishe serikali kwenye hili lakini inaonekana kama bunge nalo linalalamika tu kama raia wa kawaida wa Kimara na Mbezi.
 

BUNGE LABAINI KUSUASUA USAFIRI WA MWENDOKASI (BRT) DAR

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) imetoa taarifa kuhusu uendeshaji wa mradi wa mabasi yaendayo Haraka (BRT) jijini Dar es Salaam na kubaini tija ndogo katika utekelezaji wake licha ya uwekezaji mkubwa wa serikali.

Hayo yamebainishwa bungeni jijini Dodoma, Jumatatu Februari 10, 2025 na Mwenyekiti wa PIC, Augustine Holle ambapo amesema kuwa Serikali imewekeza Sh1.3 trilioni katika awamu mbili za mradi na Dola za Marekani 148.2 milioni kwa awamu ya tatu.

“Hata hivyo, Kamati imegundua kuwa Awamu ya Kwanza (Kimara - Kivukoni) inatumika kwa kiwango kidogo, Awamu ya Pili (Mbagala Rangitatu - Katikati ya Jiji) imekamilika lakini haijapata mwendeshaji kwa zaidi ya mwaka mmoja, na Awamu ya Tatu (Azikiwe - Gongo la Mboto) imekamilika kwa asilimia 55 bila mchakato wa kumpata mwendeshaji,” amesema Holle.

Kamati imeitaka DART kuharakisha upatikanaji wa watoa huduma kwa awamu zote ili kuhakikisha mradi huu unatumika kikamilifu na kuleta tija kwa wananchi na taifa.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2025-02-13 at 13.42.42.mp4
    2.8 MB
Sema kikao cha chama!!
Kweli kimechelewa kujua ilo mwananchi w kawaida anateseka TU tangu wameanza mpk leo.
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Katika miradi iliyofeli vibaya ni huu wa Mwendokasi...wamejazana maofisini na kulipana Posho ila Ufanisi ni zero.
Saivi Gari zinazofanya kazi Gerezan to Mbezi hazizidi 5.
Gari nyingi zimepaki tu kisa ni mbovu
 
tatizo wajinga wajinga ndio wanapewa vyeo kwenye nyanja muhimu kama hizi wanakosa ubunifu zaid ya kukaa ofsini na kujambajmba tu
.
ukienda ubungo pale kuna bas za mwendokas golden dragon zaid ya 50 zote mbovu madereva wa hizo gar wapo wanadhurura mataani mwisho wa mwez mshahara kama kawaida
Hela za serikali zinaliwa sana.
Unakuta mtumishi anasimamishwa kazi miaka minne huku anakula mshahara mwisho wa mwezi kusubiria uchunguzi mfano wa upotevu wa simu.
Anaendelea na mishe zake mtaani au biashara au anapiga kazi sekta biashara baada ya uchunguzi hakuna ushahidi anarejeshwa kazini hali miaka minne hajatumika ni sawa hao madereva
 
Kutoka 2019 leo ndo wanagundua kwa sababu uchaguzi umefika?😥
 
Katika miradi iliyofeli vibaya ni huu wa Mwendokasi...wamejazana maofisini na kulipana Posho ila Ufanisi ni zero.
Saivi Gari zinazofanya kazi Gerezan to Mbezi hazizidi 5.
Gari nyingi zimepaki tu kisa ni mbovu
Daa. Moyo umeniuma sana😥😢. Tuwafanye nini hawa wazembe?
 
Back
Top Bottom