Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

Mpina ni jasiri ana heshima yake mbele ya jamii ya watanganyika. Kamati inasema tu ilijiridhisha na GN bila kutuwekea hicho kithibitisho ili nasi tuone, wajinga sana.

Hiyo adhabu anayopewa na wajinga haina maana kwa watanganyika kwasabau wanajielewa, wao sio wajinga.

Haiwezekani wale waliompiga vita Mpina wakiongozwa na Spika Tulia, wakishirikiana na mama Abdul leo wamtendee haki, hiyo mahakama ni batili haina fairness.

• Hii kamati inataka kutudanganya watanganyika kwamba, wakati wa dharura, serikali inaweza kuagiza sukari hata kwa kutumia kampuni zisizo na ujuzi kwenye hiyo issue ilimradi sheria iwaruhusu? na isiyo na mtaji wa kutosha kama ile stationery ya mtaji wa 1 million kuagiza sukari ya bilion 6.6?!

Kamati ya wapuuzi wanajibu hoja za Mpina kama watoto.

Spika Tulia na hiyo kamati yake wasitufanye wajinga, wao wote hawana mamlaka ya kumhoji Mpina kwa kitendo chake cha kuongea na wapiga kura wake nje ya bunge, wasitake kulifanya bunge liwe juu ya mamlaka na uhuru wa watanganyika kutoa maoni yao kikatiba.

Bunge ni lile jengo tu pale Dodoma ambapo wakiwa ndani yake ndio hutakiwa kusema chochote wasishtakiwe, lakini wakitoka nje ya lile jengo wao ni wabunge wa kawaida na raia kama tulivyo wengine, wasijikuze.

Simply Mpina ameonewa, hastahili kuadhibiwa kwani hajavunja sheria yoyote ya nchi, standing orders za bunge haziwezi kuwa juu ya katiba yetu, mafisadi walaaniwe, shame on them.

Hoja za Mpina zijibiwe, mmeshindwa kuzijibu kutuonesha nyie ni mafisadi wa vitendo na ushahidi upo, adhabu yoyote kwa Mpina haitafuta dhambi ya ufisadi wenu, aibu iwe kwenu.
Dawa yao ipo jikoni Wataonesha tu panapowasha
 
tangu wakati ule wa DPW ulivyoamua kukaa kimya nilikuondoa kwenye faili langu la wapinzani walio na uchungu wa kupigania rasilimali za hili taifa.
Tatizo hauna exposure, sisi chadema sera yetu ni mrengo wa kati kulia means kuwapa wawekezaji major means of production ni sera yetu. Hata ilani ya 2020 tuliongelea barabara ya Dar-Moro kujengwa na mtu binafsi watu tulipie tolls. Kama upo chadema na haujui sera yetu kuu ni Market Economy basi inaonyesha how hutambui chama unachojinasibisha nacho. Mimi ni supporter wa Market Economy hata Africa kusini nawa support DA sababu wana sera za PPP ili kuleta ufanisi na ushindani kwenye public goods. Na niamini South Africa itapanda kiuchumi kwenye serikali hii ya GNU.

Haya mlisema bandari imeuzwq cha ajabu TICTS na ADANI wamepewa berth kadhaa. Sasa zimetoka wapi Kama DP World alipewa kila kitu? Hata dp world tukiwakataa ni bora tutafute mwekezaji mwingine sio kuwarudishia hayo mafisadi ya TPA
 
Una chembe chembe za udini, ufisadi, na mihemko ya kitoto, unashangilia Mpina kutorudi bungeni unadhani wakati anajilipua hakujua kama hilo linaweza kumpata?!
Nashangilia sababu Mpina ni sehemu ya utawala uliokua unakiuka sheria hakuwahi upinga sasa leo kakosa uwaziri ndio eti anapigania sheria?

Mfano Chadema iliwahi taka mikataba ipelekwe bungeni ila Mpina alikaa kimya. Cha ajabu leo hii kakosa uwaziri ndio anataka uwazi kwenye vibali? Kama alishabikia usiri wa JPM basi aendelee kushabikia usiri wa Samia otherwise ni mnafiki tu.

CAG mara ngapi alisema kuna ufisadi serikali ya JPM nakumbuka bunge liliwahi mpinga na kusema naye akaguliwe. Cha ajabu leo hii Mpina kakosa uwaziri eti ndio anaamini ripoti za CAG ni za kweli?

Huu unafiki wa Mpina ndio naupinga, na mimi naomba usiku na mchana apewe uwaziri na Mama samia ili wote muone unafiki wake atakavyolamba matapishi yote kama Dr Gwajima.
 
Unasema tumeumbuka?! Tumeumbuliwa na hiyo kamati ya Spika Tulia iliyookoteza majibu ili kujibu tuhuma za Mpina? Kumbe hauna akili kabisa.
Na ndio hoja yangu sasa ya unafiki wa Mpina. Kipindi tunasema uchaguzi wa 2020 ulivurugwa bunge litatekwa aliona ni sawa tu kisa naye ameshinda kwa wizi. Leo hii bunge hilo hilo la mchongo likimnyoosha ndoo mnaona kaonewa ila walipobariki kina Mdee kuwepo alikaa kimya? Hatutaki wanafiki hapa, kama aliona bunge la wizi lina uhalali basi hata hukumu yake ina uhalali.
 
Nashangilia sababu Mpina ni sehemu ya utawala uliokua unakiuka sheria hakuwahi upinga sasa leo kakosa uwaziri ndio eti anapigania sheria?

Mfano Chadema iliwahi taka mikataba ipelekwe bungeni ila Mpina alikaa kimya. Cha ajabu leo hii kakosa uwaziri ndio anataka uwazi kwenye vibali? Kama alishabikia usiri wa JPM basi aendelee kushabikia usiri wa Samia otherwise ni mnafiki tu.

CAG mara ngapi alisema kuna ufisadi serikali ya JPM nakumbuka bunge liliwahi mpinga na kusema naye akaguliwe. Cha ajabu leo hii Mpina kakosa uwaziri eti ndio anaamini ripoti za CAG ni za kweli?

Huu unafiki wa Mpina ndio naupinga, na mimi naomba usiku na mchana apewe uwaziri na Mama samia ili wote muone unafiki wake atakavyolamba matapishi yote kama Dr Gwajima.
Kama Mpina anautaka uwaziri kwanini asiwe chawa wa mama yenu? hauoni akiwa chawa ndio ataupata huo "uwaziri" unaodhani ana shida nao kwa urahisi?

Thinking yako siielewi, yani mtu aamue kwenda against mapenzi ya boss ili amfurahishe boss wake ampe zawadi ya uwaziri?!

Think again, hujui unachosimamia.
 
Na ndio hoja yangu sasa ya unafiki wa Mpina. Kipindi tunasema uchaguzi wa 2020 ulivurugwa bunge litatekwa aliona ni sawa tu kisa naye ameshinda kwa wizi. Leo hii bunge hilo hilo la mchongo likimnyoosha ndoo mnaona kaonewa ila walipobariki kina Mdee kuwepo alikaa kimya? Hatutaki wanafiki hapa, kama aliona bunge la wizi lina uhalali basi hata hukumu yake ina uhalali.
Ndio Mpina anaonewa, wale wabunge wote mule ndani hata kama ni wa mchongo, mbona wengine wapo kimya kuangalia ufisadi wa Bashe na mama Abdul?

Wanamuadhibu Mpina kwa kukiuka sheria halafu unaona sawa tu?!

Kwa hiyo unataka Mpina anyamaze ili Bashe na kundi lake waendelee kutuibia kila siku kwa uhuru, wala asiwepo yeyote wa kuwanyooshea kidole?

Unasubiri mpaka Lissu na Mbowe ndio waseme uwaelewe hata kama hawapo bungeni!.

- Lissu binafsi yupo upande wa Mpina {msikilize akiwa anahutubia wananchi kwenye mikutano yake kule Singida}, kwasababu anajua Mpina anapigania maslahi ya taifa, only you na wenzako wenye akili za kufanana ndio mnamuona Mpina mjinga!.

Narudia tena, thinking yako inanishangaza sana!.
 
Sheria iliyotumika ndio ikawafanya watumie kampuni isiyo na ujuzi wa kuagiza sukari? hapo usalama wa mlaji ulizingatiwa? mtaji wa 1 million wa stationery unaweza kuagiza sukari ya bilion 6.6? hiyo kama sio rushwa ni kitu gani kingine kwa akili yako mbovu!
Wewe ndio huna akili hizo kampuni za stationary ni zipi? Taja moja tu hapa ili tukakague kama ina mtaji wa milioni moja kweli au nyie ndio mnadhani sababu Masumin ni stationery basi ni kampuni ya rejareja? Watu wanasafirisha hadi mafuta unasemaje wana mtaji wa million 1? Anyway kwa Mfano Bakwata ina kibali cha kuagiza sukari tokea miaka ya 90 je ina kiwanda cha kutengeneza sukari?

Mfano Google inadeal na mitandao ila inatengeneza magari ya Waymo. Same to Mitsubishi inauza magari ila pia inauza maharage ya kopo je wametoa wapi kibali? Tatizo kubwa la waTanzania ni exposure kitu ambacho hakijulikani tunaona kama ni utapeli.
Kama Mpina anautaka uwaziri kwanini asiwe chawa wa mama yenu? hauoni akiwa chawa ndio ataupata huo "uwaziri" unaodhani ana shida nao kwa urahisi?

Thinking yako siielewi, yani mtu aamue kwenda against mapenzi ya boss ili amfurahishe boss wake ampe zawadi ya uwaziri?!

Think again, hujui unachosimamia.
Duu kumbe hujui ukiwa mkaidi ndio unakua na leverage kubwa? Ni rahisi kwa Tundu Lissu kuahidiwa uwaziri sababu ni threat kwa mama kuliko chawa kama Lucas Mwashambwa mfano Bashe alikua anaikosoa serikali kiasi ikabidi apewe uwaziri na tokea hapo akawa chawa. Same to Gwajima alikua critical sana ila alipopewa ubunge amegeuka chawa. Ni hivi ukiwa tishio una leverage kubwa kisiasa kuliko chawa maana huhitaji kumpa cheo mtu aliye tayari mtumwa wako ila mtu ambaye hakuelewi ndio inapaswa umvute karibu.
 
Back
Top Bottom