Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Makala yangu gazeti la Mwananchi.
Wiki iliyopita kwenye safu hii nilimpongeza Spika Dr. Tulia, kwa kazi nzuri aliyoifanya kwenye Mabunge ya Dunia, IPU kwa kuwakoromea maspika wenzake wa nchi za mabeberu, nikasema tunamuomba aliendeshe Bunge letu liisimamie serikali kikamiifu.
Makala ya leo ni swali kuhusu Bunge, Bunge ndicho chombo kikuu cha uwakilishi wa wananchi, Bunge likisema ni wamanchi wamesema, na kazi kuu ya Bunge ni kutunga sheria na kuisimamamia serikali, hakuna ubishi kuwa "Bunge letu ni Bunge Kibri na Jeuri, kwenye kazi yake kuu ya kutunga sheria Bunge letu ni Bunge kweli la kutunga sheria au ni Bunge Ruber Stemp ya Serikali? Kwanini linaogopwa hivi na Mhimili wa Mahakama?.
Bunge letu linatoa wapi hii kibri hiki na jeuri hii sio tuu ya kuidharau mahakama, kwa kutotekeleza amri za mahakama tu, bali hata ukifungua shauri lolote mahakamani, linalohusu Bunge, ujijue ni unajipotezea tuu muda wako bure, mhimili wa Mahakama unaliogopa sana Bunge kuliko hata unavyo muogopa Mungu!.
Msingi wa maswali yangu haya ni kuendelea kuwaelimisha kuhusu katiba, sheria na haki, kwa dhima ya mtunga katiba alidhamiria nini?
Je, sasa ni wakati sisi wapenda haki, kulishinikiza Bunge letu litimize wajibu wake kikamilifu kama Bunge, ikiwemo kuisimamia serikali kikamilifu na Bunge sasa ndio litunge Sheria na sio Bunge kutumika kama rubber stamp ya miswada ya serikali?
Sii mara moja wala mbili Bunge, mnasikia Mahakama imebatilisha sheria fulani kwa kwenda kinyume na Katiba. Hiyo maana yake ni Bunge limetunga sheria batili. Kwa vile kuna kanuni ya mihimili kuheshimiana, Mahakama inabatilisha tuu sheria batili bila kuliuliza Bunge linatungaje sheria batili, huku limeshehenezwa na wanasheria wabobezi na wabebovu?
Sababu Bunge letu kutunga sheria batili, ni moja tuu, Bunge halitungi sheria, bali linatumika tuu kama rubber stempu kuipitisha miswada ya sheria inayotungwa na serikali, hivyo anayetunga miswada batili ni serikali yetu tukufu!. Kutokana na kule kule kuheshimiana kwa mihimili, serikali inatunga muswada wa sheria batili, Bunge linapitisha na kuitunga sheria batili, na rais wetu analetewa sheria batili na kuzisaini kuanza kutumika!
Kubwa kuliko ni sheria ya uchaguzi iliyopita ilikuwa ni sheria batili, kwa kwenda kinyume cha katiba. Mahakama Kuu ikaibatilisha, serikali ikakata rufaa kupinga kubatilishwa huko, ikashindwa, ikapeleke Bungeni, mabadiliko batili ya katiba, na kuichomekea kiubatili kipengele batili, ndani ya katiba yetu, ili kuihalalisha ile sheria batili kuwa ni sheria halali, kwasababu sasa iko ndani ya Katiba!.
Mahakama Kuu ikaigomea serikali kwa kushikilia msimamo kuwa sheria ya uchaguzi ni batili, na mabadiliko ya katiba, yaliyofanywa na Bunge, kuichomekea batili hiyo ndani ya katiba, pia ni batili!. Kitendo cha kuichomekea batili ndani ya katiba yetu, na sawa na kuinajisi katiba!.
Serikali ikakata rufaa Mahakama ya Rufaa, na kesi kusikilizwa na majaji watu, kisheria inaitwa (half bench), ikaunga mkono uamuzi wa mahakama kuu kuwa sheria ya uchaguzi ni batili, na mabadiliko ya katiba yaliyofanywa kuichomekea batili hiyo ndani ya katiba ni batili. Ndipo serikali ikaomba kufanya mapitio, Mahakama ya Rufaa, ikakaa na majaji 7, (Full Bench) chini ya Jaji Mkuu mwenyewe wa wakati huo. Tena Mahakama ya Rufaa, haikukaa peke yake, ikawaita mabingwa watatu wa sheria kuwa marafiki ya mahakama (amicus curiae).
Mahakama ya Rufaa, ikatoa uamuzi wa ajabu kabisa kutolewa na mahakama za Tanzania kwa kusema “The court is not the custodians of the will of the people! But the perliament” kumaanisha mhimili wa Mahakama sio mlinzi wa matakwa ya watu, huo ni wajibu wa Bunge”.
Huku ni kuligwaya Bunge!. Yaani Bunge litunge sheria batili kinyume cha katiba, kisha lifanye mabadiliko batili ya katiba, kisha liuchomekee kipengele batili ndani katiba yetu ili kuihalalisha ile sheria batili kuwa ni sheria halali kwasababu sasa ubatili huo umechomekewa ndani ya katiba yetu!
Badala ya Mahakama ya Rufaa kuangalia ubatili wa katiba na ubatili wa sheria uliofanywa na Bunge, mahakama ikiwa ndio mamlaka pekee ya kutafsiri sheria, yenyewe iliangalia uwezo wa Mahakama Kuu kuliamuru Bunge, likarekebishe katiba kuuondoa huo ubatili na kuibadili sheria ya uchaguzi. Mahakama ya Rufaa, ikalirudisha hili suala Bungeni, nalo Bunge lilivyo jeuri na kiburi, limeidharau Mahakama ya Rufaa, halijafanya kitu mpaka leo.
Kwenye hili nashauri Mahakama zetu zianze kutoa SMART judgments.
Kufuatia Mahakama kuligwaya Bunge, mpaka hapa ninapoandika leo, ule ubatili uliochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu bado upo, sheria mpya ya uchaguzi iliyotungwa mwaka huu, umekitumia kipengele hicho batili, hivyo tumetungiwa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule, ulikwisha batilishwa na Mahakama. Bunge letu linapata wapi kiburi hiki?
Mihimili Mitatu
Tumerithi utaratibu wa uendeshaji wa nchi kupitia mihimili mitatu ya Serikali, Bunge, na Mahakama toka kwa Waingereza. Utaratubu huu una kanuni zake. Sisi tumeiga uendeshaji tuu lakini hatufuati kanuni zake.
Mhimili hii inaongozwa na wakuu wa mihimili, Serikali ikiongozwa na Rais, Bunge likiongozwa na Spika, na Mahakama ikiongozwa na Jaji Mkuu.
Kila mhimili una kazi zake, majukumu yake, mamlaka yake, madaraka yake, na mipaka yake, ambayo haipaswi kuingiliana. Kwa mujibu wa muundo wa mihimili hii kinadharia, mihimili hii inapaswa kuwa sawa, (equal), hakuna mhimili mkubwa wala mhimili mdogo, yote ina haki sawa.
Je, ni kweli mihimili yote mitatu iko sawa au kuna mhimili uliojichimbia chini zaidi? Tukutane wiki ijayo kwa sehemu ya pili ya mada hii.
Paskali
Makala yangu gazeti la Mwananchi.
Wiki iliyopita kwenye safu hii nilimpongeza Spika Dr. Tulia, kwa kazi nzuri aliyoifanya kwenye Mabunge ya Dunia, IPU kwa kuwakoromea maspika wenzake wa nchi za mabeberu, nikasema tunamuomba aliendeshe Bunge letu liisimamie serikali kikamiifu.
Makala ya leo ni swali kuhusu Bunge, Bunge ndicho chombo kikuu cha uwakilishi wa wananchi, Bunge likisema ni wamanchi wamesema, na kazi kuu ya Bunge ni kutunga sheria na kuisimamamia serikali, hakuna ubishi kuwa "Bunge letu ni Bunge Kibri na Jeuri, kwenye kazi yake kuu ya kutunga sheria Bunge letu ni Bunge kweli la kutunga sheria au ni Bunge Ruber Stemp ya Serikali? Kwanini linaogopwa hivi na Mhimili wa Mahakama?.
Bunge letu linatoa wapi hii kibri hiki na jeuri hii sio tuu ya kuidharau mahakama, kwa kutotekeleza amri za mahakama tu, bali hata ukifungua shauri lolote mahakamani, linalohusu Bunge, ujijue ni unajipotezea tuu muda wako bure, mhimili wa Mahakama unaliogopa sana Bunge kuliko hata unavyo muogopa Mungu!.
Msingi wa maswali yangu haya ni kuendelea kuwaelimisha kuhusu katiba, sheria na haki, kwa dhima ya mtunga katiba alidhamiria nini?
Je, sasa ni wakati sisi wapenda haki, kulishinikiza Bunge letu litimize wajibu wake kikamilifu kama Bunge, ikiwemo kuisimamia serikali kikamilifu na Bunge sasa ndio litunge Sheria na sio Bunge kutumika kama rubber stamp ya miswada ya serikali?
Sii mara moja wala mbili Bunge, mnasikia Mahakama imebatilisha sheria fulani kwa kwenda kinyume na Katiba. Hiyo maana yake ni Bunge limetunga sheria batili. Kwa vile kuna kanuni ya mihimili kuheshimiana, Mahakama inabatilisha tuu sheria batili bila kuliuliza Bunge linatungaje sheria batili, huku limeshehenezwa na wanasheria wabobezi na wabebovu?
Sababu Bunge letu kutunga sheria batili, ni moja tuu, Bunge halitungi sheria, bali linatumika tuu kama rubber stempu kuipitisha miswada ya sheria inayotungwa na serikali, hivyo anayetunga miswada batili ni serikali yetu tukufu!. Kutokana na kule kule kuheshimiana kwa mihimili, serikali inatunga muswada wa sheria batili, Bunge linapitisha na kuitunga sheria batili, na rais wetu analetewa sheria batili na kuzisaini kuanza kutumika!
Kubwa kuliko ni sheria ya uchaguzi iliyopita ilikuwa ni sheria batili, kwa kwenda kinyume cha katiba. Mahakama Kuu ikaibatilisha, serikali ikakata rufaa kupinga kubatilishwa huko, ikashindwa, ikapeleke Bungeni, mabadiliko batili ya katiba, na kuichomekea kiubatili kipengele batili, ndani ya katiba yetu, ili kuihalalisha ile sheria batili kuwa ni sheria halali, kwasababu sasa iko ndani ya Katiba!.
Mahakama Kuu ikaigomea serikali kwa kushikilia msimamo kuwa sheria ya uchaguzi ni batili, na mabadiliko ya katiba, yaliyofanywa na Bunge, kuichomekea batili hiyo ndani ya katiba, pia ni batili!. Kitendo cha kuichomekea batili ndani ya katiba yetu, na sawa na kuinajisi katiba!.
Serikali ikakata rufaa Mahakama ya Rufaa, na kesi kusikilizwa na majaji watu, kisheria inaitwa (half bench), ikaunga mkono uamuzi wa mahakama kuu kuwa sheria ya uchaguzi ni batili, na mabadiliko ya katiba yaliyofanywa kuichomekea batili hiyo ndani ya katiba ni batili. Ndipo serikali ikaomba kufanya mapitio, Mahakama ya Rufaa, ikakaa na majaji 7, (Full Bench) chini ya Jaji Mkuu mwenyewe wa wakati huo. Tena Mahakama ya Rufaa, haikukaa peke yake, ikawaita mabingwa watatu wa sheria kuwa marafiki ya mahakama (amicus curiae).
Mahakama ya Rufaa, ikatoa uamuzi wa ajabu kabisa kutolewa na mahakama za Tanzania kwa kusema “The court is not the custodians of the will of the people! But the perliament” kumaanisha mhimili wa Mahakama sio mlinzi wa matakwa ya watu, huo ni wajibu wa Bunge”.
Huku ni kuligwaya Bunge!. Yaani Bunge litunge sheria batili kinyume cha katiba, kisha lifanye mabadiliko batili ya katiba, kisha liuchomekee kipengele batili ndani katiba yetu ili kuihalalisha ile sheria batili kuwa ni sheria halali kwasababu sasa ubatili huo umechomekewa ndani ya katiba yetu!
Badala ya Mahakama ya Rufaa kuangalia ubatili wa katiba na ubatili wa sheria uliofanywa na Bunge, mahakama ikiwa ndio mamlaka pekee ya kutafsiri sheria, yenyewe iliangalia uwezo wa Mahakama Kuu kuliamuru Bunge, likarekebishe katiba kuuondoa huo ubatili na kuibadili sheria ya uchaguzi. Mahakama ya Rufaa, ikalirudisha hili suala Bungeni, nalo Bunge lilivyo jeuri na kiburi, limeidharau Mahakama ya Rufaa, halijafanya kitu mpaka leo.
Kwenye hili nashauri Mahakama zetu zianze kutoa SMART judgments.
Kufuatia Mahakama kuligwaya Bunge, mpaka hapa ninapoandika leo, ule ubatili uliochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu bado upo, sheria mpya ya uchaguzi iliyotungwa mwaka huu, umekitumia kipengele hicho batili, hivyo tumetungiwa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule, ulikwisha batilishwa na Mahakama. Bunge letu linapata wapi kiburi hiki?
Mihimili Mitatu
Tumerithi utaratibu wa uendeshaji wa nchi kupitia mihimili mitatu ya Serikali, Bunge, na Mahakama toka kwa Waingereza. Utaratubu huu una kanuni zake. Sisi tumeiga uendeshaji tuu lakini hatufuati kanuni zake.
Mhimili hii inaongozwa na wakuu wa mihimili, Serikali ikiongozwa na Rais, Bunge likiongozwa na Spika, na Mahakama ikiongozwa na Jaji Mkuu.
Kila mhimili una kazi zake, majukumu yake, mamlaka yake, madaraka yake, na mipaka yake, ambayo haipaswi kuingiliana. Kwa mujibu wa muundo wa mihimili hii kinadharia, mihimili hii inapaswa kuwa sawa, (equal), hakuna mhimili mkubwa wala mhimili mdogo, yote ina haki sawa.
Je, ni kweli mihimili yote mitatu iko sawa au kuna mhimili uliojichimbia chini zaidi? Tukutane wiki ijayo kwa sehemu ya pili ya mada hii.
Paskali