BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetangaza nafasi za kazi 42 katika taaluma mbalimbali kwa Watanzania wasiozidi umri wa miaka 45 kuanzia leo Ijumaa Aprili 21, 2023 na mwisho wa kutuma maombi ni Mei 4, 2023.
Tangazo hilo la kazi limetolewa leo Ijumaa Aprili 21, 2023 likitoa nafasi kwa madereva sita wa daraja la II, mchumi mmoja daraja la II, mhandisi umeme mmoja daraja la II, ofisa usimamizi wa fedha mmoja daraja la II, waandishi 10 wa taarifa rasmi za Bunge daraja la II.
Nafasi nyingine ni Ofisa Tehama (Network Administrator) mmoja daraja la II, Ofisa Sheria mmoja Daraja la II, Katibu wasaidizi wa Bunge (Sheria) wawili daraja la II, Katibu wasaidizi wa Bunge (Uchumi) wawili daraja la II, Katibu wasaidizi wa Bunge (Afya ya Jamii/Menejimenti ya huduma za afya) wawili daraja la II, Katibu wasaidizi wa Bunge (Usimamizi wa mazingira) mmoja daraja la II.
Katibu Msaidizi wa Bunge (sosholojia) mmoja daraja la II, Makatibu Mahsusi saba daraja la III, Mteknolojia Maabara mmoja daraja la II, Wafiziotherapia wawili daraja la II, Msaidizi wa kumbukumbu mmoja, Ofisa kumbukumbu mmoja daraja la II, Ofisa utafiti mmoja daraja la II.
BUNGE TANZANIA