Bunge linalokuja mwezi Februari lijadili kwa hati ya dharura Mkopo wa tril 1.3. kwa maslahi ya Taifa. Namna ulivyopatikana na matumizi yake

Bunge linalokuja mwezi Februari lijadili kwa hati ya dharura Mkopo wa tril 1.3. kwa maslahi ya Taifa. Namna ulivyopatikana na matumizi yake

MIAKA yote toka magu anajenga viwanja vya ndege ,mpira ,hostpital na kutaka kubadili chato kuwa mkoa ulikuwa wapi kimaaa wewe ....mpaka unampanda kichwani mama yetu kwa mkopo wa 1.3T....
 
Zanzibar ni nchi huru, mchongameno aliungana na zanzibar kwa hiyari yake chochote kinachopatikana ni nusu kwa nusu na sio izo bil200 asilimia 4 sijui., mama ana kazi bado ya kupeleka hizi fedha zanzibar miaka mingi tanganyika wanazitumia hizi hela peke yao, wamejenga madaraja sijui wamenunua ndege, flyover na ma sgr kule zanzibar hakuna kitu., lakini on top of that zanzibar wanalipa kodi zinaenda tanganyika kupitia TRA., ni unyama mkubwa hawa wanyamawezi wanaowafanyia wazanzibari
Umesahau kuwa Zanzibar Wana ZRA ambayo ni mbadala wa TRA ya bara? Hizo fedha za ZRA haziingii TRA.
 
Kila kitu kiwekwe sawa na ukweli ujulikane. Hata kama ni mkopo wa WB kupitia janga la Uviko lakini kuna giza nene.

Bunge linalofuata mwezi Februari liisimamie serikali iweke wazi namna pesa zilivyotumika na kugawanywa kati ya Zanzibar na Bara.

Bara ni sh ngapi kwa ajili ya nini? Na Zenj sh ngapi kwa ajili ya nini? Matumizi yawekwe wazi kuna siri kubwa.
VIPI KUHUSU 29 trillion ZILIZOKOPWA 5 YEARS AGO! Na yale ma trilion ya makusanyo ya TRA tuliyokuwa tunatangaziwa kila mwisho wa mwezi kwa miaka mitano iliyopita ni trilions ngapi!! Na zimefanya nini nje ya hizo 29 trillion za mkopo!!
 
Umesahau kuwa Zanzibar Wana ZRA ambayo ni mbadala wa TRA ya bara? Hizo fedha za ZRA haziingii TRA.
Hata wawe na kitu gani madam ni kodi zao waache wenyewe., kinachouma ni kukusanyiwa kodi na TRA jasho lako halafu likaenda kumnufaisha mtu mwengine kule nchi ya tanganyika
 
Tatizo una chuki binafsi na mama. Nadhani wangeaza na trillion 20 zilizokopwa kipindi Cha jiwe ndio waje kujadili za mama. Halafu, jiwe alipokuwa anapeleka miradi chato mlishangilia Sana. Mama akipeleka pesa Zanzibar mnalalamika.
Ushuzi kama huu ni mwingi!!??
 
Unajua ukweli mchungu ni kwamba, Mwalimu ndie ""aliiuza Tanganyika kwa ZNZ...

Mwalimu alikubali ku-sacrifice mambo mengi sana ya Tanganyika for the sake of Muungano...

Tena nikisema "alikubali ku-sucrifice" itakuwa ni kama nakosea kwa sababu, I'm certain ni yeye mwenyewe na timu yake ndie waliweka mezani ita-sacrifice ni na nini, na ZNZ atapata nini ili aweze kumshawishi Karume!!!

Moja ya sacrifice ndo kama hizi za huku haruhusiwi kumiliki ardhi kule lakini wa kule anaruhusiwa kumiliki ardhi huku...

Hata kwenye mgawanyo wa ajira mambo ndo yapo hivyo hivyo..

So, my friend, usishangae siku ukija kuambiwa kwamba hata huo mgawanyo umezingatia Sheria ya Mgawanyo wa Pesa za Mkopo!!!

Unajua hili tunaloona ni balaa la SSH kuipendelea ZNZ chimbuko lake ni Serikali ya JK ambayo ilimteua SSH kama Waziri anayeshughulikia Kero za Muungano!!

Sasa SSH akiwa waziri alifanikiwa kuyaona "madudu yetu yoooooote" ya kujipendekeza ili tuwe na muungano! Kule ndiko akajua ZNZ anapata nini na nini ambayo wala haikuzingatia population proportionality!!

Itoshe tu kusema kwamba WE SACRFICED A LOT FOR THE UNION!!
Umeongea vyema, na Bado wazanzibar awaoni faida ya Muungano wengi wanaitaji kujitoa kwa kisingizio Cha kutokua na tija kwao
 
Kila kitu kiwekwe sawa na ukweli ujulikane. Hata kama ni mkopo wa WB kupitia janga la Uviko lakini kuna giza nene.

Bunge linalofuata mwezi Februari liisimamie serikali iweke wazi namna pesa zilivyotumika na kugawanywa kati ya Zanzibar na Bara.

Bara ni sh ngapi kwa ajili ya nini? Na Zenj sh ngapi kwa ajili ya nini? Matumizi yawekwe wazi kuna siri kubwa.
Jpm alikuwa ni Chato sasa ni zamu ya zenj kutesa
 
Sasa kama mwalimu ndiye alie scrifice tanganyika kwa Zanzibar, mbona wazanzibari walipotaka kuvunja muungano Lukuvi alisema hatuwezi kuicha Zanzibar lazima tutaishikilia?
Hivi unaamini Viongozi wa CCM Zanzibar na wenyewe wanataka muungano uvunjike kirahisi rahisi tu?! Hivi hushangai hata zile Kura za Maoni (for Katiba Mpya), ni Pemba ndiko walipendekeza zaidi Suala la Serikali 3 ukilinganisha na Unguja?!

WHY? Pemba ilikuwa ni ngome ya CUF wakati Unguja ni ngome ya CCM!! Kwahiyo hao akina Lukuvi wanasimamia kiapo chao cha "imma fahima, lazima muungano uendelee"
Lakini pia fahamu kwamba Zanzibar ni visiwa sio kama huko ubarani eneo lake la ardhi hata hawo wazanzibari wenyewe haliwatoshi
Ni sawa na kusema Msukuma asinunue ardhi Dar es salaam kwa sababu Usukumani ardhi ni kubwa ukilinganisha na Dar es salaam!!
kumiliki ardhi lakini utashangaa bado kuna wanyamwezi kibao kutoka bara kule wako wamepewa mashamba wanalima viazi vitamu,
Unaweza kukuta hao Wanyamwezi wameingia mapema zaidi Zanzibar hata kabla ya babu wa babu zako hawajaingia... kwahiyo acha ubaguzi!!
wanafanya biashara mbali mbali., Nyerere kama aliyoona Zanzibar ni ndogo kwanini alilazimisha kuungana hivyo hivyo?
Jiulize wewe kwanini Karume akakukbali kulazimishwa?!
Zanzibar ndio nchi pekee duniani ambayo wananchi wake wanalipa kodi mara mbili - wanalipa kupitia ZRB kwa maslahi ya Zanzibar wenyewe lakini TRA kwa maslahi ya tanganyika tu,
Kiroja hiki!! Hivi unafahamu kwamba mfumo unaotumika hivi sasa ni kwamba, SMZ wanakusanya kodi zao kupitia ZRB na JMT inakusanya kodi kupitia TRA? Lakini linapokuja suala la matumizi, pesa za ZRB ni Zanzibar peke yake lakini zinazokusanywa na TRA zinatumika pande zote mbili!!
kodi ndizo zinazowapa mdomo tanganyika na kulipana mishahara yao na maposho yao wanayolipana na chakula chao.
Na nyie chanzo chenu cha mapato kinachowawezesha kulipana mishahara ni nini?! Hivi kwa akili yako unadhani Wazanzibar wenzako wote waliopo ZNZ wanalipwa kwa pesa za ZRB?
BOT asili yake Zanzibar ndio walitoa fedha nyingi zaidi za kigeni kuanzishwa kwake lakini leo BOT inaonekana ni zao la Tanganyika pekee,
Wacha we! ZNZ ilitoa trilion ngapi?
Mabalozi walioko nje huko ambao wanaiwakilisha tanzania karibu wote ni wanyamwezi kutoka bara, hakuna mzanzibari hata mmoja
We jamaa ni mbaguzi hadi unakera!! Wewe ancestors wako wanatoka wapi?! Hivi unaweza kueleza hapa MZANZIBAR HANA SIFA ZIPI?
na Zanzibar mpaka leo ikijaribu kutaka mashirikiano na nchi nyengine kibali lazima kitoke tanganyika hivi ndivyo namna
Mashirikianao ya aina ipi?
huyo nyerere wako alivyotaka kuimeza zanzibar mpaka leo., Tanganyika inafaidika kupitia mgongo wa Zanzibar ndio mana hamtaki kuachia.,
Yaani Tanganyika ifaidike kupitia mgongo wa Zanzibar?! Ikiwa kodi yote inayokusanya na ZRB inatumika Zanzibar, sasa hiyo Tanganyika inanufaika nini kutoka Zanzibar?! Tanganyika ina-import nini kutoka Zanzibar?
Sasaivi Mama amekuwa rais kwa mujibu katiba kwa kile kilichotokea basi kina Ndugai kelele kibao na ni miezi 9 tu sasa., wakati nyinyi mumekuwa mnaongoza serikali ya muungano peke yenu mwaka wa 60 sasa njaa tupu.,
Kwani wakati wa JPM hapakuwa na kelele?! Wakati wa JK hapakuwa na kelele?! Au na wenyewe ni Wazanzibari?
 
Kila kitu kiwekwe sawa na ukweli ujulikane. Hata kama ni mkopo wa WB kupitia janga la Uviko lakini kuna giza nene.

Bunge linalofuata mwezi Februari liisimamie serikali iweke wazi namna pesa zilivyotumika na kugawanywa kati ya Zanzibar na Bara.

Bara ni sh ngapi kwa ajili ya nini? Na Zenj sh ngapi kwa ajili ya nini? Matumizi yawekwe wazi kuna siri kubwa.
Usisahau na hela zote zilizokopwa na mzee baba na zenyewe ziwekwe wazi ili tumjue muongo ninan.
 
Kila kitu kiwekwe sawa na ukweli ujulikane. Hata kama ni mkopo wa WB kupitia janga la Uviko lakini kuna giza nene.

Bunge linalofuata mwezi Februari liisimamie serikali iweke wazi namna pesa zilivyotumika na kugawanywa kati ya Zanzibar na Bara.

Bara ni sh ngapi kwa ajili ya nini? Na Zenj sh ngapi kwa ajili ya nini? Matumizi yawekwe wazi kuna siri kubwa.
Katika hiyo pesa yote Zanzibar imepewa tzsh billion 230. Zaidi ya 20% percent yote ya 1.3 trillion mama kapeleka Zanzibar. Vile visiwa ni vyote viwili vina ukubwa Sawa na wilaya moja au ni vidogo zaidi ya wilay moja ya Tanganyika. Zanzibar yote population yake inakadiriwa kuwa 1.5 million people wakati Tanganyika yote inakadiriwa kuwa na 60 million people. Bado pesa yote utalipwa na watanganyika

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Jpm alikuwa ni Chato sasa ni zamu ya zenj kutesa
Zenj watatesaje wakati hawana mchango wowote ule kwenye muungano . Yaani mtanganyika yeyote Yule anaweza kuajiriwa chato airport but mtanganyika haruhusiwi kufanya kaxi Zanzibar au kujenga tuu haruhusiwi kabisa. Kwamaana hiyo tunanyonywa Sana na huu muungano

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Kila kitu kiwekwe sawa na ukweli ujulikane. Hata kama ni mkopo wa WB kupitia janga la Uviko lakini kuna giza nene.

Bunge linalofuata mwezi Februari liisimamie serikali iweke wazi namna pesa zilivyotumika na kugawanywa kati ya Zanzibar na Bara.

Bara ni sh ngapi kwa ajili ya nini? Na Zenj sh ngapi kwa ajili ya nini? Matumizi yawekwe wazi kuna siri kubwa.
Ijadiliwe mara ngapi na kwa faida yako wewe binafsi au?
 
Back
Top Bottom