Bungeni, Dodoma: Spika Ndugai ataka NIDA kuitwa na Kamati. Asema haifanyi vizuri

Uongo umeuona wapi? Kwenye andiko langu kuna uongo? Halafu napata faida gani kwa kuandika uongo hapa?.
Hiyo ID unayo sema expired imetumia miaka mingapi??
Na imetolewa mwaka gani?
 
Ni shida watu wengi wanazo namba tu za kitambulisho cha NIDA, kitambulisho haijulikani kitafika lini. Inaleta usumbufu mkubwa sana
 

Hilo bunge ni genge la majizi ya kura na halina makali yoyote. Huwezi kuingia bungeni kwa wizi wa kura kisha ukawa na ubavu wa kuhoji udhaifu. Sana sana hilo bunge liko kwa ajili ya kutungiwa sheria kandamizi na kusubiri kupitisha kwa sauti ya ndiooo. Kwanza nimeshangaa hata bunge lipo!
 
Ni shida watu wengi wanazo namba tu za kitambulisho cha NIDA, kitambulisho haijulikani kitafika lini. Inaleta usumbufu mkubwa sana

Hivi zile pesa za kitambulisho kwa walio poteza zinatumika ktk shughuri ipi?....
 
Inaelekea huna taarifa sahihi kuhusu hivi vitambulisho,labda inaweza kuwa faida kwako kwa kujifunza kitu: Kitambulisho kilitolewa December 18, 2017 kwa miaka miwili hadi December 19, 2019. Leo ni zaidi ya mwaka mmoja na nusu mhusika anasotea kupewa kitambulisho kipya na ameisha lipia. Naamini umeelewa sasa.
 
Binge lenyewe halifanyi vizuri sijui liitwe nanani? Au tundu lissu
 
Aliitwa aletewe GAG, Gwajima,Slaa kafanya Nini Cha maana?
Kuonyesha tu kuwa yeye ni mtu mkubwa.
Hovyo.
Hujiulizi maspika wenzio mbona walikuwa wastaarabu?
 
Nida wanazingua sana,
Ila kipindi cha usajili wa line za simu walijitahidi sana
 
Labda ku update picha maana baada ya miaka 10 sura haiwezi kua ile ile
Mmmh.
Kuna dogo nilijiandikisha nae 12 mwezi wa 9 mwaka 2020.amepata mwaka huu 2021.
Anasema mwaka 2022 kina expire
 
Mmmh.
Kuna dogo nilijiandikisha nae 12 mwezi wa 9 mwaka 2020.amepata mwaka huu 2021.
Anasema mwaka 2022 kina expire
Mmmh inakuaje viwe tofauti. Changu kina expire baada ya miaka 10 na sio changu tu na vya wengine nlionao karibu.
Labda hiko feki
 
Kwani Bunge linafanya kazi vizuri, ni wale wale tu asitake kushikia chini wenzie wakati ye mwenyewe kimeo!!!
kwa hiyo unataka kumaanisha Bunge nalo liitwe kwenye kamati lihojiwe [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Ndugaye hana ujanja wa kumhoji waziri
Juzi amesikika akisema et miswada wanayopelekewa kujadiri mingine ni mibaya,wabunge wanaikataa lakini mawaziri wanang'ang'ania hivo hivo ipite na wao hawana jinsi inabidi waipitishe hivo hivo,baada ya mwaka ubovu unaonekana wanairudisha tena kujadiriwa
 
Huyo jamaa naona madhara ya yule bundi yameanza kumtafuna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…