Bungeni Leo: Sera ya "elimu bure" kufutwa? CCM kama kawaida yao wanatanguliza mbunge Kasheku Msukuma kupima upepo. Wewe unasemaje?

Bungeni Leo: Sera ya "elimu bure" kufutwa? CCM kama kawaida yao wanatanguliza mbunge Kasheku Msukuma kupima upepo. Wewe unasemaje?

Yes. Something like that...

Inashangaza kuwa, sera ya "elimu bure", mafanikio yake yanapimwa kwa kigezo cha NUMBER/QUANTITY of "pupils/students enrollment" in schools badala ya kigezo cha QUALITY EDUCATION...!

Ndiyo maana kuna watu humu arguments za ni; Unajua idadi ya wanafunzi walioenda (kuhudhuria) shule kwa sababu ya elimu bure?

Badala yake swali linapaswa ku - base hapa:

Ni wanafunzi wangapi wanamaliza shule ktk ngazi zote na wana uwezo wa kutumia maarifa waliyoyapata shuleni/vyuoni kuboresha maisha yao..?
Je wewe unaweza kutupa iyo idadi ya wanafunzi waliokuwa na maarifa ya dunia kipindi cha ada tofauti na sasa usomi chawa ni janga kwa nchi sasa
 

CCM kama kawaida yao wanatanguliza mbunge Kasheku Msukuma kupima upepo. Wewe unasemaje???? hIKI ULICHOANDIKA SIYO NDOTO??? NANI ALIKUAMBIA KUWA WAMEMUTANGULIZA??? EBU CHUKUA JEMBE KALIME USILAL E MCHANA NA KUTUPA NDOTO HIZI​

Hata hivyo elimu bwelele haitekelezeki
 
Hii sera ifutwe, ni sera ya kipumbavu inayolea taifa la wavivu na kudumaza ubora wa elimu yetu
Serikali kazi yake ni kujenga miundombinu ya elimu na kuajiri walimu, kusomesha ibaki jukumu la mzazi

Kama kuna masikini wasioweza kulipa basi uchambuzi ufanywe wakipiwe. Lakini nina uhakika zaidi ya 80% ya watanzania wanaweza kulipa ada ya laki moja kwa mwaka
 
Sera ya elimu bure ni mojawapo ya maeneo nilipotofautiana na Magufuli.
Nilliona elimu bure kama kufuga na kukaribisha umaskini endelevu tu. Katika dunia hii na zama hizi vitu vyote bora ni aghali,
na kwa hali ilivyo elimu ya msingi inayotolewa bure kwa ni duni sana kwa sababu ya ubure bure.
 
Kasheku Msukuma(MB) - Geita Vijijini leo bungeni akichangia kwenye bajeti ya Wizara ya Elimu na Ufundi, amesema yawezekana walikosea kuja na sera ya "elimu bure" ama sometime hutumia kiswahili cha "elimu bila malipo" mwaka 2015..

Kuna kila dalili kuwa Msukuma ametangulizwa na CCM kulichokoza hili lakini ukweli ukiwa mpango umekwisha kuiva kurejesha ada mashuleni...

Ukiniuliza mimi, nitajibu kwa herufi kubwa kabisa, kuwa YES huu ulikuwa uamuzi wa kimakosa. Wazazi na walezi ni Sharti wachangie gharama za kusomesha watoto wao ktk ngazi zote za elimu..!

Mtazame na msikilize hapa.

View attachment 2219306
Kama wewe hautaki mwanao asome bure si umpeleke katika shule za kulipia
 
Msukuma hajatoa maelezo ya kutosha zaidi ya kuonyesha uwepo wa upungufu wa walimu, ambao ufumbuzi wake ni kuajiri walimu wa kutosha. Walimu wapo mitaani hawana kazi.

Labda nikuulize, kwanini wewe umekubaliana na huyo Musukuma?? Tuanzie hapo
Serikali haiwezi kuajiri walimu, kujenga madarasa na kulipia wanafunzi ada, lazima itachemsha tu, ndio maaana hakuna walimu na madarasa tunajenga kwa mikopo ya Covid

Serikali ijitue huu mzigo usiokuwa wa lazima wa kulipia watu ada..ni ujinga
 
Yaani Serikali ikiruhusu hili suala la Elimu na michango lirudi Tena, aisee wananchi maskini wapigwa Sana na hao wanaojiita walimu uchwara, nielewe Mimi mkuu! Kipindi Elimu na michango inafanya kazi ktk hizo Shule za kata kulikuwa na michango ya kipumbavu Sana, yaani unakuta Mzazi anaambiwa achangie Feza kwa ajiri ya maktaba na maktaba yenyewe unakuta Haina vitabu vya kutosha

Serikali yangu pendwa chondechonde msirudi Nyuma Wala msiruhusu hili lirudi Tena Kuna baadhi ya walimu walikopa Hadi Magari kwa kutegemea Michango ya wazazi amini Wananchi maskini na ninawajua Tena wengine baada ya kuibuka kwa Elimu Bure waliachana na Kazi ya kufundisha,

Wananchi wamepigwa Sana kipindi Cha Elimu na michango pia niwaombe walimu kuweni wazalendo hii nchi niyetu sote ukimsaidia mtoto wa mwenzio sawa umelisaidia Taifa kwa ujumla acheni ubinafsi na ukilitimba Walimu. Tuna fahamu mnaumuhumu ila msizue kitimtim Hadi wizara ya Elimu.
Hiyo michango holela ndio serikali ilitakiwa kudhibiti, serikali ilitakiwa kuweka kiwango kuwa mwanafunzi anatakiwa kuchangia kiasi fulani cha fedha na hakuna mwalimu wa kuanzisha michango mipya
Mambo ya maabara, maktaba, walinzi n.k yatalipiwa kutoka kwenye hiyo ada na kama kuna upungufu serikali itatoa ruzuku
Ila hii elimu bure ni upumbavu mtupu, ni siasa za kilaghai walizokuwa wakihubiri akina Lowassa na CCM walikuwa desperate wakaingia mkenge
 
Hiyo michango holela ndio serikali ilitakiwa kudhibiti, serikali ilitakiwa kuweka kiwango kuwa mwanafunzi anatakiwa kuchangia kiasi fulani cha fedha na hakuna mwalimu wa kuanzisha michango mipya
Mambo ya maabara, maktaba, walinzi n.k yatalipiwa kutoka kwenye hiyo ada na kama kuna upungufu serikali itatoa ruzuku
Ila hii elimu bure ni upumbavu mtupu, ni siasa za kilaghai walizokuwa wakihubiri akina Lowassa na CCM walikuwa desperate wakaingia mkenge
Unakuta baraza la Elimu limesema Malipo ya mtihani wa Moko, au wilaya au mkoa gharama ni 10000 likini wao wanataja 60000 na ukute Kuna vichwa 300_400 unategemea nini hapo kama siyo upigaji

Yaani mkuu upigaji upo Kila Kona wananchi wamepigwa Sana ktk hayo mashule ya kata sijui Serikali.
 
Unakuta baraza la Elimu limesema Malipo ya mtihani wa Moko, au wilaya au mkoa gharama ni 10000 likini wao wanataja 60000 na ukute Kuna vichwa 300_400 unategemea nini hapo kama siyo upigaji

Yaani mkuu upigaji upo Kila Kona wananchi wamepigwa Sana ktk hayo mashule ya kata sijui Serikali.
Hata sasa unafikiri hakutakuwa na upigaji wa hizo hela zinazotumwa? Upigaji always upo, dawa ni kutafuta njia ya kupambana nao tu
 
Kasheku Msukuma(MB) - Geita Vijijini leo bungeni akichangia kwenye bajeti ya Wizara ya Elimu na Ufundi, amesema yawezekana walikosea kuja na sera ya "elimu bure" ama sometime hutumia kiswahili cha "elimu bila malipo" mwaka 2015..

Kuna kila dalili kuwa Msukuma ametangulizwa na CCM kulichokoza hili lakini ukweli ukiwa mpango umekwisha kuiva kurejesha ada mashuleni...

Ukiniuliza mimi, nitajibu kwa herufi kubwa kabisa, kuwa YES huu ulikuwa uamuzi wa kimakosa. Wazazi na walezi ni Sharti wachangie gharama za kusomesha watoto wao ktk ngazi zote za elimu..!

Mtazame na msikilize hapa.

View attachment 2219306
Hawa Watanzania maskini muwabane kila kona halafu bado serikali hata elimu iwalipishe? Huku bidhaa zimepanda Bei, huku mafuta, tena mnataka kuwatwika mzigo huu wa ada! Siyo haki kabisa ukizingatia hii ni katika ahadi na ilani ya uchaguzi ya CCM. Mkibadilisha hii, hapo mmevuka mipaka! Basi waambieni walipie na hayo madarasa mnayojenga. Kujibu hoja ya Msukuma, ingekuwa vyema hiyo hela ya Uviko ikaelekezwa kwanza kwenye vifaa vya kufundishia na kuzalisha walimu wengi bora badala ya kujenga madarasa.
 
Ccm kwa maksudi kabisa ukiiangalia kwa jinsi wanavyoigawana keki ya taifa kwa manufaa yao, na kwa jinsi wasivyo na uchungu kwa wananchi kwa utawala huu,

Na kwa jinsi Rais asivyoshaurika kuhusu mawaziri mizigo na hataki kabisa kuwaondoa, licha ya kwamba wanamchafua sana, na yeye kukubaliana na hali ya kuchafuliwa na anaona ni sawa tuu

Mambo mengi magumu nchi inapitia na hakuna hatua za maksudi ya kuitoa nchi kwenye mkwamo huo, ukijumlisha na hili la kuondoa elimu bule, ni dhahiri kabisa kuna mpango mahususi kutoka humohumo CCM kwamba, 2025 watakipa ushindi chama B" kipya kinachohangaika kupata usajiri wa kudumu

Kwa sababu ninachokijua, CCM piga ua garagaza, hswawezi kukipa ushindi Chadema ni bora hata itokee vita Ila si chadema kupewa nchi, basi watakipa chama chochote Ila sio Chadema

Kwa maana hiyo nawahakikishieni kuwa, 2025 hata kwa fimbo, hakuna mtu atakaye mpa kura mama Samoa Rais aliyepo

Kwa sababu moja tu, wananchi watakuwa wamechoka vibaya na maisha magumu, watakuwa wamechoka vibaya na huduma mbovu kwenye nchi inayowakamua kila uchwao

Niamini mimi
Mtu anavunja sheria ya Kodi iliyopitishwa na Bunge anaachwa hivi hivi. Sijawahi kuona hii
 
Elimu bure iendelezwe,kwani kutokomeza ujinga ni vita takatifu, kwa kila mwananchi.Nimeona kuna watu maskini huko vijijini, hata kununua uniform ni shida.
Huwezi kukatisha elimu kwa wanafunzi ambao watakaoshindwa kulipa karo,ni unyama.
Hayo majigambo ya uchumi wakati ni fix,sisi na Bangladesh hatuchekani.
Baada ya miaka 10 serikali ipime ni njia ipi twende nao.
Jambo muhimu ni kuboresha elimu yenyewe.
Mwisho turudi kwenye sera ya Baba wa Taifa ya Uzazi wa Mpango.
 
Kasheku Msukuma(MB) - Geita Vijijini leo bungeni akichangia kwenye bajeti ya Wizara ya Elimu na Ufundi, amesema yawezekana walikosea kuja na sera ya "elimu bure" ama sometime hutumia kiswahili cha "elimu bila malipo" mwaka 2015..

Kuna kila dalili kuwa Msukuma ametangulizwa na CCM kulichokoza hili lakini ukweli ukiwa mpango umekwisha kuiva kurejesha ada mashuleni...

Ukiniuliza mimi, nitajibu kwa herufi kubwa kabisa, kuwa YES huu ulikuwa uamuzi wa kimakosa. Wazazi na walezi ni Sharti wachangie gharama za kusomesha watoto wao ktk ngazi zote za elimu..!

Mtazame na msikilize hapa.

View attachment 2219306
Wafute tuu ni hasara Kwa Taifa.
 
Ukiniuliza mimi, nitajibu kwa herufi kubwa kabisa, kuwa YES huu ulikuwa uamuzi wa kimakosa. Wazazi na walezi ni Sharti wachangie gharama za kusomesha watoto wao ktk ngazi zote za elimu..!
Magufuli aliingizwa cha kike na wapinzani. Aliposikia wananadi elimu bure yeye hakushughulisha akili yake kujua hiyo elimu bure ingetolewa kwa mfumo gani na yeye kuingia kichwa kichwa kutekeleza sera zisizokuwa za chama chake.
 
Hiyo sera waliivamia toka CHADEMA. Hawakuwa wamejiandaa nayo.
 
Bomu kivipi?? Wengi hao ni masikini hohehahe, wenye vijisenti bongo watoto wao wanasoma shule za kulipia. Elimu bure ni kwa masikini na watu wa vijijini ambao buku 10 ya ghafla ni mtihani. Watu hawana hela ya kununua uniform tu, halafu wewe unasema wachangie. Kweli?

Mkiondoa elimu bure mjipange kuwa na taifa la mbumbumbu ambao hata basics tu kama kusoma na kuandika hawajui. Kutakuwa na ongezeko la watoto wa mitaani na panya road wataongezeka. Ajira za utotoni kuongezeka na kadhalika. Kitendo cha mtoto kwenda shule Kila siku ni kutoa structure flani, ambayo kama ada na michango itarudi na yenyewe itapotea. Watoto wa masikini mijini na vijijini watakuwa idle siku nzima na kujiingiza katika upuuzi niliotaja hapo juu pamoja, ngono za utotoni na kadhalika.
Mbumbumbu wanatamnufaisha nani? Kumbuka msemo wa wahenga "usimwamshe aliyelala..."
 
Watu baadhi wamekimbilia Heading tu hawajasikiliza wanakimbilia kureply
 
Back
Top Bottom