Ndugu Mayalla halafu hapo baadaye unaenda kumtetea Zitto. Yuko kimya kwenye matatizo makubwa yote ya sasa. Anakulipa kiasi gani? Au sababu ni usalama mwenzako?
Acha kupayuka kama huna uhakika na unachokiandika, simpendi Zitto kwa tabia zake za undumilakuwili lakini kwenye hili Zitto amependekeza serikali iondowe tozo za mafuta kwa kiasi cha shilling 500 ili kuwapunguzia mzigo wananchi.

Pita hata kwenye post za Mirrald Ayo za jana utakuta hiyo post ya mapendekezo ya Zitto.

Paskal amekukosea nini? huo usalama hizo kazi huwa anafanya saa ngapi wakati na yeye anasulubika tu kama sisi?
 
Mama naye amekuwa kama panya road tuu.
Anawakata Raia mapanga makubwa zaidi ya Panya Road kama ya kodi, tozo, mfumuko wa bei wa chakula, ujenzi, usafiri, usalama dhaifu, masoko kuchomwa, ajali kuongezeka, mbolea, pembejeo chakula, Umeme, maji, nidhamu hakuna tena. Mikopo inavyotumika, bandari chali.

Kutembea tu itakuwa shida tunapoelekea, never mind kufanya kazi.
 
Wameongea weeee lakini mwisho wa siku Serikali ndio itakuja na jibu maana hakuna cha azimio la Bunge wala nini ila ni maelekezo ya serikali kukaa na kutafakari..

Ukimsikiliza Simbachawene alitoa msimamo wa serikali Kwa hiyo don't expect too much..

Mwisho mimi natoa ushauri,unapotaka haki kuwe na uwajibikaji.. Serikali ikiondoa hizo tozo lazima wabane watu wanaponunua bidhaa wawe na risiti Ili kufidia pengo vinginevyo itakuwa ni serikali ya Zima moto na Hawa Hawa wanaolalamika leo watakuja tena kulalamika Kuhusu barabara ,maji,afya nk na hawatajua kwamba Serikali ilitoa vyanzo vya mapato yake vya kwenye mafuta.
 
Una weza kua na point ila ulivyo pangilia maandishi kidogo haiko sawa.
 
Una weza kua na point ila ulivyo pangilia maandishi kidogo haiko sawa.
Fikra inaweza kuboreshwa kuna watu wana vipaji kuweza kufikisha kwa wahusika katia ubora zaidi na unaweza kuchukuwa nilichomaanisha na kukiboresha zaidi. Nimesikiliza kidogo Makamba huko bungeni kuhusu hii issue kwa kweli nadhani amefika mwisho katika upeo wake katika hili sidhani kama ana solution yoyote maana kamaliza hotuba lakini ni kama sijamuelewa kaongea nini.
 


Hawa wabunge wa kiki na kuibiwa kura ni sinema tu hapa hakuna kitu. Watanzania wengi wanajua haya ni maonyesho tu wala hawatashutua serikali
 
Halafu wengi wanaomshambulia huyu mkongwe Pascal utakuta ni hawa madogo failures wa form four wasiojua mchango wa Pascal kwa taifa hili
 
Ushauri wangu, wapunguze siku wanazokaa kwa ajili ya bajeti na fedha itakayopatikana ifidie mafuta. Allowances zipunguzwe, wote wanaokirimiwa na serikali waondolewe mafao yote kwani na wao ni wafanyakazi wanunue mahitaji yao kama wengine. Mishahara yao inajitosheleza tusiwabebe kuwalipia kodi za pango simu nk
 
Panya wakiwa hata.100 Akija Nyau mmoja woote watachimba!
 
Ndugu Mayalla halafu hapo baadaye unaenda kumtetea Zitto. Anakulipa kiasi gani? Au sababu ni usalama mwenzako?
Niache kuitetea Idara yenyewe
inayonilipa, kula, kunywa na kulala, ndio nimtetee usalama mwenzagu Zitto kama utetezi huu

P
 
Kwa gharama hizi hivi kweli wabunge wale walichaguliwa na wananchi au ilikuwaje?
 
Yaani juzi hapa tulipigiwa mahesabu meengi ya hasara iliyotokea baada ya January Makamba kuondoa tozo. Maneno meeeengi.

Leo tunarudi pale pale kwa January.....kuondoa tozo, kama taifa, tuwe na msimamo
 
Mkuu kuna siku nilikuwa mahali fulani halafu TBC walikuwa wanarusha makala nafikiri ilikuwa inahusu sabasaba, wewe ndio ulikuwa unaoongoza mahojiano, kuna mzee mmoja na heshima zake alituambia kuwa wewe ni afisa
usalama...wahenga walinena, lisemwalo lipo🐒
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…