Bungeni: Mjadala wa dharura kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta nchini. Mbunge asema tozo mbili zinaongeza 792 kwenye bei
Ndugu Mayalla halafu hapo baadaye unaenda kumtetea Zitto. Yuko kimya kwenye matatizo makubwa yote ya sasa. Anakulipa kiasi gani? Au sababu ni usalama mwenzako?
Acha kupayuka kama huna uhakika na unachokiandika, simpendi Zitto kwa tabia zake za undumilakuwili lakini kwenye hili Zitto amependekeza serikali iondowe tozo za mafuta kwa kiasi cha shilling 500 ili kuwapunguzia mzigo wananchi.

Pita hata kwenye post za Mirrald Ayo za jana utakuta hiyo post ya mapendekezo ya Zitto.

Paskal amekukosea nini? huo usalama hizo kazi huwa anafanya saa ngapi wakati na yeye anasulubika tu kama sisi?
 
Mama naye amekuwa kama panya road tuu.
Anawakata Raia mapanga makubwa zaidi ya Panya Road kama ya kodi, tozo, mfumuko wa bei wa chakula, ujenzi, usafiri, usalama dhaifu, masoko kuchomwa, ajali kuongezeka, mbolea, pembejeo chakula, Umeme, maji, nidhamu hakuna tena. Mikopo inavyotumika, bandari chali.

Kutembea tu itakuwa shida tunapoelekea, never mind kufanya kazi.
 
Wameongea weeee lakini mwisho wa siku Serikali ndio itakuja na jibu maana hakuna cha azimio la Bunge wala nini ila ni maelekezo ya serikali kukaa na kutafakari..

Ukimsikiliza Simbachawene alitoa msimamo wa serikali Kwa hiyo don't expect too much..

Mwisho mimi natoa ushauri,unapotaka haki kuwe na uwajibikaji.. Serikali ikiondoa hizo tozo lazima wabane watu wanaponunua bidhaa wawe na risiti Ili kufidia pengo vinginevyo itakuwa ni serikali ya Zima moto na Hawa Hawa wanaolalamika leo watakuja tena kulalamika Kuhusu barabara ,maji,afya nk na hawatajua kwamba Serikali ilitoa vyanzo vya mapato yake vya kwenye mafuta.
 
Kuna hatari kubwa ya kuingia kwenye recession kutakuwa na upunguzwaji wa wafanyakazi kwenye private sector ili kupunguza gharama za kujiendesha hili ni janga kubwa sababu level ya watu kukosa ajira ni kubwa tayari. Solution ni nini? Serikali ina budget na kwenye budget mapato ya serikali kwa bahati mbaya waliweka kwenye mafuta bila kujuwa mafuta sio bidhaa yetu wala sisi hatuzalishi kwa maana hatuna control na bei zake hii ni kitu hatari sana. Nchi zenye kuzalisha mafuta waki budget wanaweka dola 60$ kwa barrel sasa bei ikipanda nu surplus na mara nyingi wanaweka base na utabiri wa bei kwa mwaka risk ipo na imeshawahi kutokea bei kushuka mpaka 25$ wakati wa corona na siku za nyuma lakini kwa kuwa wana surplus wanaitumia ile pesa ku cover mapungufu kwa muda mfupi na kupunguza gharama zao za uendeshaji. Sasa kwa sisi hapa hatuzalishi mafuta tuna lima, madini lakini mwisho wa siku hatu control bei korosho bei ikianguka hatuna la kufanya wenzetu ndio maana wana OPEC wakiona wako chini wana kata ku regulate bei. Turudi kwetu, huwezi kupanga budget kwa bidhaa isiyokuwa yako wala huna control nayo budget unapanga na yale unayozalisha wewe ukijuwa una mamlaka kamili ya ku dictate bei na uzalishaji. Ni sawa kama una nyumba yako umeipangisha unaweza kujuwa kwa mwaka nitakusanya kiasi hichi si nyumba yako lakini huwezi kupanga budget yako ya nyumbani kwa kutegemea kaka si kasema atanipa kiasi hichi kwa mwaka je kaka akikata? Tanzania ni lazima tubadilike katika kupanga budget zetu ndio maana serikali hawawezi kufanya lolote kwa sasa maana pesa wanataka kuiachia hawawezi vyanzo vingine hawana. Unaweza kupanga budget kwenye bia, sigara sababu unazalisha wewe lakini sio mafuta. kusanya kwenye mafuta kodi lakini isiwe key ya muongozo wa budget yako kosa kubwa. Budget lazima iende na kila unacho produce wewe sio mwenzako, cha mwenzako fanya kama surplus. Viongozi hawana tena mawazo mbadala ya kutanua wigo wa mapato au shida inakuja labda tunataka kuishi maisha sio ya uhalisia na kipato chetu. Serikali italazimisha kukusanya kwenye mafuta ila wana create bomu nalo ni RECCESION.
Una weza kua na point ila ulivyo pangilia maandishi kidogo haiko sawa.
 
Una weza kua na point ila ulivyo pangilia maandishi kidogo haiko sawa.
Fikra inaweza kuboreshwa kuna watu wana vipaji kuweza kufikisha kwa wahusika katia ubora zaidi na unaweza kuchukuwa nilichomaanisha na kukiboresha zaidi. Nimesikiliza kidogo Makamba huko bungeni kuhusu hii issue kwa kweli nadhani amefika mwisho katika upeo wake katika hili sidhani kama ana solution yoyote maana kamaliza hotuba lakini ni kama sijamuelewa kaongea nini.
 
Wanabodi,

Moja ya kazi za Bunge ni Kuisimamia serikali. Bunge la Mhe. Job Ndugai, lilituhumiwa kuwa ni Bunge dhaifu kuwahi kutokea, hivyo Spika Job Ndugai kuhesabika ni Spika dhaifu kabisa kuwahi kutokea, hivyo kupachikwa jina la "Bora Spika" Kwa kuanzia mimi niliisikia sauti hii Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...

Job Ndugai alipojiuzulu tukasema Kujiuzulu kwa Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili tupate Spika Bora. CCM itateua Spika Bora au Bora Spika kama kawa?

Kwa vile Dr. Tulia alikuwa ni Naibu Spika wa Spika dhaifu, alipochaguliwa kuwa Spika, kuna watu walidhani Bunge la Tulia litakuwa ni Bunge Dhaifu kama Bunge la Ndugai.

Nilitoa ushauri huu Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!

Sasa hiki ndio kinatokea Leo,

Bunge la Dr. Tulia, sasa limeanza kuisimamia Serikali kiukweli ukweli!, leo limesimamisha shughuli zake zote kujadili hoja ya dharura ya Mhe. Omari Kigua, kujadili kupanda kwa bei ya mafuta ya petrol na dizeli.​


Hongera Sana Spika Tulia, Bunge sasa linaisimamia serikali

Keep Watching Bunge Live

na Kazi iendelee!

Paskali.


Hawa wabunge wa kiki na kuibiwa kura ni sinema tu hapa hakuna kitu. Watanzania wengi wanajua haya ni maonyesho tu wala hawatashutua serikali
 
Acha kupayuka kama huna uhakika na unachokiandika, simpendi Zitto kwa tabia zake za undumilakuwili lakini kwenye hili Zitto amependekeza serikali iondowe tozo za mafuta kwa kiasi cha shilling 500 ili kuwapunguzia mzigo wananchi.

Pita hata kwenye post za Mirrald Ayo za jana utakuta hiyo post ya mapendekezo ya Zitto.

Paskal amekukosea nini? huo usalama hizo kazi huwa anafanya saa ngapi wakati na yeye anasulubika tu kama sisi?
Halafu wengi wanaomshambulia huyu mkongwe Pascal utakuta ni hawa madogo failures wa form four wasiojua mchango wa Pascal kwa taifa hili
 
Leo May 5, mbunge Kilindi, Omary Kigua ametoa hoja ya kuahirisha shughuli zake za kawaida ili kujadili dharula ya ongezeko la bei ya mafuta.

Kigua amesema kuna changamoto ya kupanda kwa haraka sana kwa mafuta ya taa, dizeli na petroli ambapo hivyo vikipanda ni kimepandishwa kila kitu na Tanzania nzima kelele ni suala la mafuta na Bunge linalo wajibu mkubwa wa kuisimamia Serikali katika jambo husika.

Kigua amesema anaamini Serikali ya Tanzania itafanya jambo kama ambavyo Serikali nyingine duniani zinavyochukua hatua kwasababu wananchi hawawezi kulalamika halafu Serikali isichukue hatua yoyote.

Spika Tulia amesema pamoja na kwamba Waziri Mkuu ameshachukua kutua, hoja hiyo ambayo imeungwa mkono na wabunge wengi itajadiliwa na wabunge kama kazi yao ya kuishauri Serikali ifanye nini kwenye jambo husika.

MUSUKUMA;- Mafuta yaliyopanda juzi yamenunuliwa mwezi wa pili
Mbunge Joseph Kasheku amemshukuru Spika kwa kukubali kuwasikiliza na amesema kwa wao wanaotoka majimbo ya vijijini na kununua mafuta kwenye vidumu wananunua 5,000 kwa lita.

Musukuma ameiomba Serikali ieleze ukweli kwani mafuta yaliyopanda juzi yamenunuliwa mwezi wa pili. Musukuma amesema wafanyabiashara yeye akiwa mmojawapo wanacheza na namba.

Musukuma amesema iliwahi kushuka bei ya korosho na Serikali ilipeleka Jeshi ku-rescue suala la korosho na mpaka leo hakuna mtu anachezea bei ya korosho kwasababu wanajua Serikali inaweza kuingia kuchukua biashara.

Musukuma amesema kuna kuna kodi ziliwekwa kodi za mafuta, iangaliwe namna ya kuziondoa kwa dharula ya miezi mitatu ili mafuta yarudi kuwa chini.

Musukuma amemaliza kwa kusema nchi inakubalika kukopa kimataifa na inakopa hivyo wakope kufidia gharama ili mafuta yaweze kushuka, hakuna mtanzania atamudu na kudai hata wabunge linawapiga kwasababu wanalipwa mileage za kwenda vijijini na ya kwake inaishia Shinyanga.

Musukuma: Mheshimiwa spika mimi pia ni msafirishaji, yaani kwasababu watanzania tuna nidhamu ya kuiheshimu Serikali na kuwapa muda, hebu jiulize msafirishaji aliyekuwa anapeleka abiria kwa shilingi 30,000 Mwanza, leo mafuta yamefika 3,400 nauli bado 30,000 Hili haliwezekani, tukubaliane tuishauri Serikali na ije na kauli nzuri.

SONGE;- Serikali itafute fedha kupeleka ruzuku kwenye mafuta
Simon Songe: Naishauri Serikali mambo mawili, kwanza kutafuta fedha kwaajili ya kupeleka ruzuku kwenye mafuta walau kupunguza gharama za mafuta na kupunguza gharama za vitu vingine ambazo vinaenda kupanda bei.

Tuna tozo nyingi tumeweka kwenye mafuta kwaajili ya nchi na kwaajili ya bajeti tuliyoipitisha, sisi ndio wabunge na sisi ndio tulioipitisha, kuna haja ya kuangalia baadhi ya tozo tuweze kuziondoa kwa dharula kwa miezi miwili.

MHAGAMA;- Mafuta yamepanda kwa 92%
Joseph Mhagama: Kati ya mwezi January 2021 mpaka Mei 2022 mafuta ya petroli yamepanda kwa asilimia 92 kutoka Tshs 1,695 mpaka elfu tatu mia mbili na kitu.

Tozo mbili za fuel levy na exercise duty kwa pamoja zinachangia Tshs 792, waziri au Serikali waangalie ni namna gani tutatoka, tunajua umuhimu wa tozo za ujenzi wa mabarabara na maji hizo zibaki lakini nyingine tunaweza kupunguza matumizi ya Serikali tukaenda kuboresha maslahi ya watanzania.

KAKUNDA;- Kwanini Serikali isikope kupunguza maumivu
Joseph Kakunda: Nilikuwa Kenya na nilikutana na waziri wa fedha, nikamuuliza mmepata wapi fedha kwenye bajeti yenu za kutoa ruzuku karibu Tshs bilioni 900, akasema wamezikopa IMF. Kwanini sisi Serikali yetu isikope kwaajili ya kupunguza maumivu kama hayo.

Ningependa kuishauri Serikali yangu, wananchi wanahitaji kupata matokeo ya haraka. Kama kuna mbinu mbadala za kuagiza mafuta ambazo zitashusha bei ya mafuta kwa haraka basi zitumike badala ya mbinu ambayo sasahivi imesababisha ongezeko la bei ya mafuta.

WAITARA;- Zambia dizeli 2,470
Mwita Waitara: Nchi kama Zambia, dizeli ni 2,470 lakini tunajua mizigo yao wanapitisha hapa, dizeli Tanzania imetangazwa bei ya EWURA zaidi ya Tshs 3000, wamezungumza bei ya mafuta Zanzibar na wanajaribu pia kutugawa.

Ni jambo ambalo Serikali lazima ichukue hatua za dharula.

KASALALI;- Kuondoa tozo hakuepukiki
Mageni Kasalali: Naiomba Serikali katika hatua ambazo imeanza kuchukua, jambo la kuondoa tozo za Serikali kwenye mafuta ni jambo ambalo haliepukiki. Umefika wakati ni lazima sasa tuache kugeuza mafuta kuwa sehemu pekee ya kutafuta pesa, ni lazima tufikire njia nyingine kwa huu muda.

TAARIFA;- Saasisha ataka Serikali iuze madini yaliyokamatwa kusaidia uchumi
Sasisha: Pamoja na tozo hizi za kitaasisi, kuna fedha ambazo zipo kwenye madini, yale madini ambayo yamekuwa yakikamatwa kama faini sasahivi ni wakati sahihi Serikali iuze iweze kuingiza huku kama sehemu ya kusaidia uchumi wetu ikiwa ni pamoja na dhamana zinazowekwa mahakamani, ziletwe ziingie huku.

SHANGAZI: Tozo zilikuwepo miaka sita iliyopita na hazijawahi kuwa tatizo
Rashid Shangazi: Matumizi yetu kwa mwezi ni kama lita milioni 300, tungekuja na mpango wa 'stabilization fund'. Serikali ije iombe kibali kwa Bunge, wakakope japo bilioni 300, kila lita moja tuiwekee ruzuku ya Tshs 1,000 kila lita.

Hii itatusaidia kwamba hatutakwenda kugusa tozo pamoja na kodi n
Leo May 5, mbunge Kilindi, Omary Kigua ametoa hoja ya kuahirisha shughuli zake za kawaida ili kujadili dharula ya ongezeko la bei ya mafuta.

Kigua amesema kuna changamoto ya kupanda kwa haraka sana kwa mafuta ya taa, dizeli na petroli ambapo hivyo vikipanda ni kimepandishwa kila kitu na Tanzania nzima kelele ni suala la mafuta na Bunge linalo wajibu mkubwa wa kuisimamia Serikali katika jambo husika.

Kigua amesema anaamini Serikali ya Tanzania itafanya jambo kama ambavyo Serikali nyingine duniani zinavyochukua hatua kwasababu wananchi hawawezi kulalamika halafu Serikali isichukue hatua yoyote.

Spika Tulia amesema pamoja na kwamba Waziri Mkuu ameshachukua kutua, hoja hiyo ambayo imeungwa mkono na wabunge wengi itajadiliwa na wabunge kama kazi yao ya kuishauri Serikali ifanye nini kwenye jambo husika.

MUSUKUMA;- Mafuta yaliyopanda juzi yamenunuliwa mwezi wa pili
Mbunge Joseph Kasheku amemshukuru Spika kwa kukubali kuwasikiliza na amesema kwa wao wanaotoka majimbo ya vijijini na kununua mafuta kwenye vidumu wananunua 5,000 kwa lita.

Musukuma ameiomba Serikali ieleze ukweli kwani mafuta yaliyopanda juzi yamenunuliwa mwezi wa pili. Musukuma amesema wafanyabiashara yeye akiwa mmojawapo wanacheza na namba.

Musukuma amesema iliwahi kushuka bei ya korosho na Serikali ilipeleka Jeshi ku-rescue suala la korosho na mpaka leo hakuna mtu anachezea bei ya korosho kwasababu wanajua Serikali inaweza kuingia kuchukua biashara.

Musukuma amesema kuna kuna kodi ziliwekwa kodi za mafuta, iangaliwe namna ya kuziondoa kwa dharula ya miezi mitatu ili mafuta yarudi kuwa chini.

Musukuma amemaliza kwa kusema nchi inakubalika kukopa kimataifa na inakopa hivyo wakope kufidia gharama ili mafuta yaweze kushuka, hakuna mtanzania atamudu na kudai hata wabunge linawapiga kwasababu wanalipwa mileage za kwenda vijijini na ya kwake inaishia Shinyanga.

Musukuma: Mheshimiwa spika mimi pia ni msafirishaji, yaani kwasababu watanzania tuna nidhamu ya kuiheshimu Serikali na kuwapa muda, hebu jiulize msafirishaji aliyekuwa anapeleka abiria kwa shilingi 30,000 Mwanza, leo mafuta yamefika 3,400 nauli bado 30,000 Hili haliwezekani, tukubaliane tuishauri Serikali na ije na kauli nzuri.

SONGE;- Serikali itafute fedha kupeleka ruzuku kwenye mafuta
Simon Songe: Naishauri Serikali mambo mawili, kwanza kutafuta fedha kwaajili ya kupeleka ruzuku kwenye mafuta walau kupunguza gharama za mafuta na kupunguza gharama za vitu vingine ambazo vinaenda kupanda bei.

Tuna tozo nyingi tumeweka kwenye mafuta kwaajili ya nchi na kwaajili ya bajeti tuliyoipitisha, sisi ndio wabunge na sisi ndio tulioipitisha, kuna haja ya kuangalia baadhi ya tozo tuweze kuziondoa kwa dharula kwa miezi miwili.

MHAGAMA;- Mafuta yamepanda kwa 92%
Joseph Mhagama: Kati ya mwezi January 2021 mpaka Mei 2022 mafuta ya petroli yamepanda kwa asilimia 92 kutoka Tshs 1,695 mpaka elfu tatu mia mbili na kitu.

Tozo mbili za fuel levy na exercise duty kwa pamoja zinachangia Tshs 792, waziri au Serikali waangalie ni namna gani tutatoka, tunajua umuhimu wa tozo za ujenzi wa mabarabara na maji hizo zibaki lakini nyingine tunaweza kupunguza matumizi ya Serikali tukaenda kuboresha maslahi ya watanzania.

KAKUNDA;- Kwanini Serikali isikope kupunguza maumivu
Joseph Kakunda: Nilikuwa Kenya na nilikutana na waziri wa fedha, nikamuuliza mmepata wapi fedha kwenye bajeti yenu za kutoa ruzuku karibu Tshs bilioni 900, akasema wamezikopa IMF. Kwanini sisi Serikali yetu isikope kwaajili ya kupunguza maumivu kama hayo.

Ningependa kuishauri Serikali yangu, wananchi wanahitaji kupata matokeo ya haraka. Kama kuna mbinu mbadala za kuagiza mafuta ambazo zitashusha bei ya mafuta kwa haraka basi zitumike badala ya mbinu ambayo sasahivi imesababisha ongezeko la bei ya mafuta.

WAITARA;- Zambia dizeli 2,470
Mwita Waitara: Nchi kama Zambia, dizeli ni 2,470 lakini tunajua mizigo yao wanapitisha hapa, dizeli Tanzania imetangazwa bei ya EWURA zaidi ya Tshs 3000, wamezungumza bei ya mafuta Zanzibar na wanajaribu pia kutugawa.

Ni jambo ambalo Serikali lazima ichukue hatua za dharula.

KASALALI;- Kuondoa tozo hakuepukiki
Mageni Kasalali: Naiomba Serikali katika hatua ambazo imeanza kuchukua, jambo la kuondoa tozo za Serikali kwenye mafuta ni jambo ambalo haliepukiki. Umefika wakati ni lazima sasa tuache kugeuza mafuta kuwa sehemu pekee ya kutafuta pesa, ni lazima tufikire njia nyingine kwa huu muda.

TAARIFA;- Saasisha ataka Serikali iuze madini yaliyokamatwa kusaidia uchumi
Sasisha: Pamoja na tozo hizi za kitaasisi, kuna fedha ambazo zipo kwenye madini, yale madini ambayo yamekuwa yakikamatwa kama faini sasahivi ni wakati sahihi Serikali iuze iweze kuingiza huku kama sehemu ya kusaidia uchumi wetu ikiwa ni pamoja na dhamana zinazowekwa mahakamani, ziletwe ziingie huku.

SHANGAZI: Tozo zilikuwepo miaka sita iliyopita na hazijawahi kuwa tatizo
Rashid Shangazi: Matumizi yetu kwa mwezi ni kama lita milioni 300, tungekuja na mpango wa 'stabilization fund'. Serikali ije iombe kibali kwa Bunge, wakakope japo bilioni 300, kila lita moja tuiwekee ruzuku ya Tshs 1,000 kila lita.

Hii itatusaidia kwamba hatutakwenda kugusa tozo pamoja na kodi nyingine kwasababu hizi tozo zilikuwepo miaka sita iliyopita na hazijawahi kuwa tatizo. Kwahiyo leo sio kwamba mafuta yamepanda bei tatizo ni hizi tozo, tozo zinatusaidia kwenye mambo mengine kama kupeleka umeme vijijini, barabara, maji nk.

yingine kwasababu hizi tozo zilikuwepo miaka sita iliyopita na hazijawahi kuwa tatizo. Kwahiyo leo sio kwamba mafuta yamepanda bei tatizo ni hizi tozo, tozo zinatusaidia kwenye mambo mengine kama kupeleka umeme vijijini, barabara, maji nk.
Ushauri wangu, wapunguze siku wanazokaa kwa ajili ya bajeti na fedha itakayopatikana ifidie mafuta. Allowances zipunguzwe, wote wanaokirimiwa na serikali waondolewe mafao yote kwani na wao ni wafanyakazi wanunue mahitaji yao kama wengine. Mishahara yao inajitosheleza tusiwabebe kuwalipia kodi za pango simu nk
 
Wanabodi,

Moja ya kazi za Bunge ni Kuisimamia serikali. Bunge la Mhe. Job Ndugai, lilituhumiwa kuwa ni Bunge dhaifu kuwahi kutokea, hivyo Spika Job Ndugai kuhesabika ni Spika dhaifu kabisa kuwahi kutokea, hivyo kupachikwa jina la "Bora Spika" Kwa kuanzia mimi niliisikia sauti hii Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...

Job Ndugai alipojiuzulu tukasema Kujiuzulu kwa Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili tupate Spika Bora. CCM itateua Spika Bora au Bora Spika kama kawa?

Kwa vile Dr. Tulia alikuwa ni Naibu Spika wa Spika dhaifu, alipochaguliwa kuwa Spika, kuna watu walidhani Bunge la Tulia litakuwa ni Bunge Dhaifu kama Bunge la Ndugai.

Nilitoa ushauri huu Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!

Sasa hiki ndio kinatokea Leo,

Bunge la Dr. Tulia, sasa limeanza kuisimamia Serikali kiukweli ukweli!, leo limesimamisha shughuli zake zote kujadili hoja ya dharura ya Mhe. Omari Kigua, kujadili kupanda kwa bei ya mafuta ya petrol na dizeli.​


Hongera Sana Spika Tulia, Bunge sasa linaisimamia serikali

Keep Watching Bunge Live

na Kazi iendelee!

Paskali.
Panya wakiwa hata.100 Akija Nyau mmoja woote watachimba!
 
Ndugu Mayalla halafu hapo baadaye unaenda kumtetea Zitto. Anakulipa kiasi gani? Au sababu ni usalama mwenzako?
Niache kuitetea Idara yenyewe
inayonilipa, kula, kunywa na kulala, ndio nimtetee usalama mwenzagu Zitto kama utetezi huu

P
 
Kwa gharama hizi hivi kweli wabunge wale walichaguliwa na wananchi au ilikuwaje?
 
Yaani juzi hapa tulipigiwa mahesabu meengi ya hasara iliyotokea baada ya January Makamba kuondoa tozo. Maneno meeeengi.

Leo tunarudi pale pale kwa January.....kuondoa tozo, kama taifa, tuwe na msimamo
 
Niache kuitetea Idara yenyewe
inayonilipa, kula, kunywa na kulala, ndio nimtetee usalama mwenzagu Zitto kama utetezi huu

P
Mkuu kuna siku nilikuwa mahali fulani halafu TBC walikuwa wanarusha makala nafikiri ilikuwa inahusu sabasaba, wewe ndio ulikuwa unaoongoza mahojiano, kuna mzee mmoja na heshima zake alituambia kuwa wewe ni afisa
usalama...wahenga walinena, lisemwalo lipo🐒
 
Back
Top Bottom