TANZIA Buriani Abbas Kleist Sykes

TANZIA Buriani Abbas Kleist Sykes

Sio wewe tu, watu kibao hatuelewi hiki kituko cha tanzia.

Muhammed Said anaangalial kila kitu duniani katika lenzi ya TANU, Nyerere, wazee wa Aggrey na Tandamti, na mfumo uliowanyima vyeo baba zake wadogo wa Gerezani.

Tanzia gani haisemi nani kafa bali maisha ya Muhammed Said ?
Kwameh,
Huwezi kuelewa hii historia mpya.

Wengi hamkujua kuwa kadi no. 1 ya TANU ya Julius Nyerere aliandikiwa na Ally Sykes na kadi no. 2 ni Ally Sykes no. 3 Abdulwahid Sykes na no. 7 Abbas Sykes na kadi hizo zilichapwa na Ally Sykes kutoka mfukoni kwake.

Mnajiuliza mbona watu kibao hatuyajui haya?
 
Sheikh Mohamed Said: Eid Muvarak belates! Kile kitabu chako kizuri cha Abdulwaheed Sykes the Forgotten Struggle mbona huyasemi haya? Kumbe mdogomtu alikuwa Balozi wetu Mexico wakati Pele anashinda World Cup 1970? Akawa balozi kwa Ben Bella na Sahrawi, wewe iwehe unasema ni "forgotten"? Umetumia mada hii adhimu kujinadi CV yako safari za majuu, uk9 tayari kusifia Wamanyema na Waislamu wa Kariakoo zaidi, madobi na wapiga mnada, wengine wote hadi Mexico vipi huwaoni? Nchi imeanza kubadilika sasa: tuna Rais Mzenj, tena Mwanamke, na tena ni Islamu. Hiyo Tanganyika yako ya AMNUT na Abduwaheed haipo tena. Majuzi ulimuona Askofu Mkuu akiongoza Ibada maziko ya Magufuli ule Chati? HighTable mbele ya Altare zaidi ya 90% walikuwa ni Waislamu - Rais na Jaji Mkuu wawiliwawili - na hata Mufti! Badilika Kaka, tunapendana asantenyerere!
LGF,
Nadhani umekusudia, ''belatedly.''
Nakuitikia, ''Minalfaizin.''

Kitabu changu unakikosea jina kila siku unapokitaja.

1621345254428.png
 
Mara ulikuwa hotelini Dubai baadaye ulikuwa tanga, which is which

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Burdizzo,
Pole sana inaelekea mandishi yangu yanawakera watu wengi sana.

Historia ile yote ya 1950s Abbas Sykes anakutana na Nyerere nyumbani kwao, anakuja kujuana na Mama Maria, mipango ya kuunda TANU na mengi hukuyaona ulichoona ni kunikamata uongo nifedheheke kuwa mimi sisemi kweli.

BBC siku ile wananipigia simu nilikuwa Dubai na walitaka kujua sisi kama Watanzania tunachukuliaje maradhi ya Mwalimu.

Mwalimu anafariki mimi nipo Tanga.
Ungesoma bila ghadhabu ungeelewa lakini chuki imeziba fikra zako.

Unataabika kuisoma historia hii ambayo wewe hukupata kuijua na sasa unaijua huipendi.
 
BURIANI BABA, RAFIKI NA MZUNGUMZAJI WANGU BALOZI ABBAS KLEIST SYKES

Mwezi October 1999 nilikuwa Dubai na nikikaa Carlton Hotel.

Siku moja jioni simu yangu ikalia.

Walikuwa BBC London Idhaa ya Kiswahili wanataka kunihoji kuhusu Mwalimu Julius Nyerere ambae wakati ule alikuwa amelazwa St. Thomas Hospital, London.

Ulikuwa mwaka wa pili toka kitabu changu, ‘’The Life and Times of Abdulwaid Sykes (1924- 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Aganst British Colonialism in Tanganyika,’’ kichapwe na kitabu hiki kikawa kimenifanya nifahamike na sababu kubwa ni kuwa kilikuja na historia mpya ya yeye Mwalimu Nyerere mwenyewe, historia ya TANU na historia nzima ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Kitabu kilimweeleza Mwalimu Nyerere kwa namna ambayo hakuna mwandishi alipatapo kufanya hivyo.

Hii nadhani ndiyo ikawa sababu ya BBC kutaka kunisikia nikimzungumza Mwalimu Nyerere.

BBC wakawa wanataka tuzungumze kidogo kuhusu Mwalimu na jinsi Watanzania walivyoathirika na ile hali ya Mwalimu kuwa kwenye matibabu Uingereza.

Katika kipindi kile cha maradhi ya Mwalimu akiwa hospitali kila siku habari ya hali yake ilikuwa inatolewa na kwa kweli sote tukifuatilia kwa karibu sana hadi pale alipofariki tarehe 14 Oktoba 1999.

Kishindo chake kilikuwa kikubwa hakijapatapo kutokea na mazishi ya Mwalimu hayapata kutokea halikadhalika simanzi iliyoonyeshwa na Watanzania haijapatapo kutokea.

Umma mkubwa usio na kifani ulijitokeza kupokea jeneza lake Uwanja wa Ndege na maelfu ya watu walijipanga pembeni ya barabara kutoa heshima zao wakati jeneza lake lilipokuwa linapita kuelekea nyumbani kwake Msasani.

Mimi nilikuwa Tanga nikifuatilia kwenye TV na binafsi fikra nyingi zilipita katika kichwa changu.

Mimi sikupata kujuana na Mwalimu lakini katika utafiti wangu wa maisha ya Abdul Sykes na harakati za uhuru nimemjua kwa karibu Mwalimu Nyerere kushinda wale waliokuja kuwa karibu na yeye baada ya uhuru.

Katika utafiti nimekutana na Mwalimu Nyerere ndani ya Nyaraka za Sykes na ndani ya nyaraka hizi nimesoma barua zake akiwa Rais wa TAA na kisha TANU katika miaka ya mwanzoni ya 1950, nimezungumza na Ally Sykes na Dossa Aziz na Mama Daisy (mke wa Abdul Sykes) watu waliokuwanae toka siku ya kwanza wanaanza mapambano ya kudai uhuru.

Katika mikoa ya Tanzania nilikokwenda kwa utafiti nimekutana na kuzungumza na watu waliokuwanae bega kwa bega katika siku hizo za mwanzo wakati Mwalimu Nyerere ndiyo anaanza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika akiwa kijana wa miaka 30.

Wakati naangalia TV usiku mmoja wakionyesha ndege ya Air Tanzania Corporation (ATC) iliyokwenda kuchukua mwili wa Mwalimu Nyerere London camera ikapita kwa Abbas Sykes kwa haraka lakini nilimtambua bila wasiwasi wowote kuwa ndiye yeye.

Wakati ule yeye alikuwa ndiye Mwenyekiti wa ATC nafasi aliyoteuliwa na Rais Benjamin Mkapa.

Nilikuwa na kawaida kila nikija Dar es Salaam kutoka Tanga lazima nipite ofisini kwa Bwana Ally Sykes kumjulia hali kisha niende nyumbani kwa Balozi Abbas Sykes.

Safari hii nilikwenda kwa Balozi Sykes kwa nia khasa ya kutaka kujua safari yake ya London kwenda kuchukua mwili wa Mwalimu Nyerere.

Bwana Abbas tukiwa mimi nimekaa kwenye kiti changu ninachokipenda ndani ya ukumbi wake, kiti ambacho kinanipa mandhari ya mchanga mweupe wa bahari na bahari yenyewe na yeye kama kawaida amekaa kwenye kiti cha baba mwenye nyumba kwani huwa siku zote ndicho kiti chake nilianza mazungumzo kwa kumpa pole kwa msiba wa Mwalimu Nyerere.

Balozi Sykes akaitikia ile pole yangu kisha akasema, ‘’Unajua mimi kama Mwenyekiti wa ATC nilitiwa katika msafara wa kwenda kuuchukua mwili wa Nyerere.

Ingekuwa si hii nafasi yangu ya uenyekiti nisingepata fursa na heshima ile kwani hawa viongozi walioko madarakani hawajui kuwa Nyerere sisi ni ndugu yetu.’’

Nilijua bila ya kuuliza kuwa ile, ‘’sisi,’’ Balozi alikusudia wao Sykes Brothers.

Nilikuwa sijapatapo kumsikia Bwana Abbas akijinasibisha udugu na Nyerere.

Mara zote alipokuwa akieleza harakati za kudai uhuru alikuwa akimweleza Nyerere katika nafasi ya urafiki wake na kaka yake Abdul na kama kiongozi wa TANU, hili la udugu ndiyo siku ile nalisikia kwa mara ya kwanza.

‘’Mimi nimejaaliwa kumuona Nyerere siku ya kwanza kaja kwetu pale Mtaa wa Aggrey na Sikukuu kaja kumuona Bwana Abdul akiwa kaongozana na Joseph Kasella Bantu na kuanzia hapo tukawa kama ndugu mama yake Bi. Mugaya akafahamiana na mama yetu na akawa anamtembelea mama nyumbani kwake pamoja na Sophia dada yake Nyerere.

Nikajuana na Joseph mdogo wake na Mama Maria Nyerere ambae alikuja kuwa shoga mkubwa wa Mama Daisy.’’

Bwana Abbas alipomaliza utangulizi huu na hapa alinistua kwani ingawa vifo siku zote vinatokea lakini huwa hatupendi kusikia vile vitu vya karibu vinavyomgusa maiti kama jeneza sanda na kadhalika.

Bwana Abbas akanieleza hali ilivyokuwa ndani ya ndege, ‘’Mohamed Nyerere nimejuananae kuanzia mwaka wa 1952 mimi kijana wa miaka 23 mdogo sana hata Bwana Abdul alikuwa mdogo kwa Nyerere.

Ndani ya ndege tuliweka sanduku lililokuwa na mwili wake mbele kabisa tumelifunika na bendera ya Tanzania.

Ilikuwa tabu sana kwangu kukwepa kulitazama sanduku lile lenye mwili wa Nyerere.

Kila mara fikra zinakwenda mbele na kurudi nyuma zinakwenda mbele zinarudi nyuma namkumbuka Nyerere kijana na Bwana Abdul kijana wote vijana wako pale nyumbani kipindi kile ameacha kazi na siku za mwanzo za TANU.

Endapo mtu angelinambia kwa wakati ule kuwa Nyerere atakuja kuwa kiongozi mkubwa barani Afrika ingekuwa tabu kwangu kuamini kuwa mambo yale waliyokuwa wanayanzungumza wakipanga na kuoangua yatakuja kuwa makubwa kwa kiasi kile kilichofikia.

Nimekuwa na Nyerere kwingi Ulaya katika mikutano na nimeshuhudia kwa macho yangu viongozi wenzake na watu maarufu duniani wanavyokuwa wakiwa mbele yake.

Kwangu mimi ile ilikuwa historia inafunguka mbele ya macho yangu ya mtu niliyemuona akitembea kwa miguu mitaa ya Gerezani akiwa na mimi au na Bwana Abdul wakienda kumuona huyu au yule.

Mtu yeyote angeangaia mikutano ile ya TANU mingine ikifanyika kwa Mzee Clement Mtamila aliyekuwa Mwenyekiti wa TANU pale Mtaa wa Kipata na Sikukuu wajumbe wakiwa akina Bi. Tatu bint Mzee na Bi. Titi Mohamed, Iddi Faizi Mafungo, Nyerere akiwepo na Dossa na Mzee Rupia haikuwa rahisi kuwaza kuwa Muingereza tutamtoa na Tanganyika itajitawala.

Nimekaa ndani ya ndege namwagalia Mama Maria. Mama Maria amezeeka kawa mtu mzima sana kichwa chote cheupe.

Mama Maria alikuwa kazeeka hata kumpita Mama Daisy nikawa najisemea moyoni huenda labda kwa ajili ya kumuuguza mumewe.

Ilikuwa miaka mingi hatujaonana.

Namkumbuka Mama Maria siku zile msichana mwembamba mrefu, picha inanijia yuko na Mama Daisy wakati mwingine uani jikoni wanapika.

Nakumbuka Mama Daisy akimwambia Maria kuwa wakitoka nje kwenda mahali lazima wajitande kufunika vichwa vyao.

Wengi tuliokuwa pamoja miaka ile wametangulia mbele ya haki.

Nalitazama sanduku lililobeba mwili wa Nyerere namkumbuka Yusuf Bakis kijana wa Bantu Group aliingia hadi Halmashauri Kuu ya TANU lakini alikuwa matata Nyerere akamtoa.

Zuberi Mtemvu na yeye alikuwa katika Halmashauri Kuu na akawa anakwaruzana na Nyerere. Nyerere akataka atolewe Halmashauri Kuu lakini Mzee Rupia akamtetea, siku zile Mzee Rupia Makamu wa Rais wa TANU.

Mzee Rupia tukimuheshimu sana na kama hataki jambo alikuwa hapingwi. Kwetu sisi Mzee Rupia, Rajab Diwani walikuwa kama baba zetu kwa kuwa walikuwa wakifahamiana na baba yetu na akifika dukani kwake na kuhudhuria ile barza ya wazee maarufu kama Aziz Ali.

Uzee katika chama siku zile ulikuwa na nguvu sana achilia mbali mbali Baraza la Wazee wa TANU chini ya mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir.

African Association sisi ilikuwa kama chama chetu baba yetu alikuwa na ushawishi mkubwa katika chama kile na alipotoka katika uongozi chama kikawa chini ya uongozi wa Mwalimu Thomas Saudtz Plantan kama Rais na Clement Mtamila akiwa Katibu.

Bwana Abdul na Hamza Mwapachu walivyokuja kufanya mapinduzi na kumtoa madarakani Thomas Plantan ambae kwetu sisi alikuwa ni baba ikawa kama vile watoto wa Kleist wamewapindua ndugu zao watoto wa Plantan.

Kuwa sisi ni watoto wa Kleist hili lilitupa sisi nguvu kubwa sana katika TAA hadi kufikia TANU.

Hakuna ambacho sisi hakuwa tunakijua katika TAA.

Hawa akina Plantan na sisi ni ndugu kabisa babu zetu ndiyo walioingia Tanganyika kama askari mamluki chini ya Kamanda Mjerumani, Herman von Wissman kuja kuwasaidia Wajerumani kwenye vita yao na Bushiri na Mkwawa.

Baba zetu ni kizazi cha kwanza cha Wazulu waliozaliwa Tanganyika.

Baada ya vita hivi kumalizika na Wajerumani sasa wanatawala Tanganyika hili jeshi la Wazulu likawa kambini likijulikana kama Germany Constabulary na mkuu wa jeshi hili akiwa Affande Plantan baba yao Thomas Saudtz Plantan, Schneider Abdillah Plantan na Ramadhani Mashado Plantan.

Ukweli utabaki kuwa kama Nyerere asingepokelewa na sisi Dar es Salaam na sisi tukamkubali asingeweza kupata uongozi wa TAA wala TANU na historia ya Nyerere na Tanganyika kama nchi ingekuwa nyingine kabisa.

Nyerere aliitoa mbali sana TANU na kuipitisha kwingi na alikuwa na watu waliojitolea kwake na kwa Tanganyika kwa dhati ya nafsi zao – Mzee Rupia, Dossa, Bwana Abdul na Bwana Ally.

Safari ya kurudi Dar es Salaam kutoka London tukiwa na mwili wa Nyerere ilikuwa ndefu sana kwangu.

Nikisinzia na kuamka na nikiamka kumbukumbu nyingi zikinija za furaha na za masikitiko.

Inanijia picha ya Bi. Titi Mohamed kafungwa maisha kisha namuona Bi. Titi Mohamed tuko Mnazi Mmoja miaka ya mwanzo ya TANU.

Uwanja umefurika na wananchi wanamsubiri Nyerere apande jukwaani ahutubie.

Tuko chini ya jukwaa Nyerere anatuambia kuwa leo hana la kusema. Anamwangalia Bi. Titi kisha anasema, ‘’Titi hebu panda wewe uzungumze leo sijisikii vizuri.’’

Bi. Titi anapanda kwenye jukwa, msichana mdogo wa kipwani siku zile za mwanzo akivaa baibui jukwaani.

Bi. Titi alikuwa mzungumzaji anashindana na Nyerere kwa kusema.

Uwanja unawaka moto kwa vimondo anavyorusha Bi. Titi.

Waingereza wanasimangwa kuwa hawana kwao wanang’ang’nia nchi za wenzao.

Nyerere kwa hotuba ya Bi. Titi anachukua ‘’cue’’ kutoka kwake anapanda jukwaani na anapita mle mle alimopita Bi. Titi lakini kwa staili yake.

Mimi nilikuwa kijana mdogo sana mwaka wa 1952 nilipomjua Nyerere ni bwana mdogo wa kutumwa na kaka zangu pamoja na Nyerere kuwafanyie mengi, ‘’Abbas lete kile nenda kwa fulani,’’ nk.

Kiasi kuwa Nyerere alipoacha kazi na kuja kukaa kwetu mimi ndiye niliyehamishwa kwenye chumba changu kumpisha nami nikenda kwenye nyumba yetu nyingine.

Pale jirani tulikuwa na nyumba mbile nyingine Kirk Street na New Street pale lilipo Jumba la Ushirika.

Hii nyumba ya Bwana Abdul kwa viwango vya nyakati zile ilikuwa nyumba ya kusifika.

Ilikuwa na mlango mkubwa ukiangalia Mtaa wa Aggrey ambao ndiyo wa kuingilia nyumba kubwa kisha kulikuwa na mlango mwingine ukiangalia Sikukuu Street, huu ulikuwa ndiyo mlango wa kuingia kwangu kwenye nyumba ndogo yenye chumba na varanda yake.

Hapa ndipo alipokaa Nyerere mwaka wa 1955 hadi alipotafutiwa nyumba Magomeni Majumba Sita.

Nyumba hii imeacha historia kubwa sana kwani hakuna mtu mashuhuri wa nyakati zile ambae alikuwa hajakaribishwa katika nyumba ile hadi Wazungu maofisa wa kikoloni.

Bahati mbaya sana historia hii le haitakiwi.

Hamza Mwapachu kafariki mapema sana mwaka mmoja baada ya uhuru mwaka wa 1962 na halikadhalika Bwana Abdul akafariki mwaka wa 1968.

Hawa ndiyo wangeliweza kuieleza historia ya TANU kwa uhakika wake.

Bahati mbaya sana inaelekea kama vile Nyerere hakuipenda sana historia hii.

Ni katika maajabu mengi na qudra ya Allah kuwa katika ndege nzima ile na naamimi Tanzania nzima ni mimi peke yangu niliyekuwa hai ambae nilimuona Nyerere toka siku ya kwanza anakuja kwetu kuonana na Bwana Abdul nikawa na yeye kwa takriban kwa miaka 40 hadi siku ile nakwenda London kuchukua maiti yake kurudi nayo Dar es Salaam kwa mazishi.

Kuwa leo nakuhadithia historia hii yote haya ni mipango ya Allah.’’

Miaka inakimbia ishafika miaka 20 toka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere afariki dunia na sasa ninavyoandika mazungumzo yangu na Balozi Abbas Sykes yeye ameshatimiza miaka 90.

Mkuu nina ujumbe wako upo PM
 
Mkuu,

Wazee wako walifutwa na wewe unawafuta zaidi.
Leo siku ya Sykes, lakini badala ya kuandika tazia ya Sykes, umeandika kitu kimejaa Nyerere kuliko Sykes!

Yani huwezi kumuelezea Sykes ila kama akiwa kivuli cha Nyerere.

Ndiyo maana hujaelezea maisha yake, umeelezea maisha yake kwa uhusiano na Nyerere. Habari inaanza na msiba wa Nyerere. Mwisho wa habari za Sykes ulizoandika ni kwenye msiba wa Nyerere. Kama vile Sykes alikuwa mmoja wa vijakazi wa Firauni ambao Firauni akifariki huzikwa naye. Umeandika kama vile maisha ya Sykes yaliisha kwenye kifo cha Nyerere. Kumbe mtu aliendelea na utumishi wa maana sana hata baada ya Nyerere kufariki.

Yani na wewe umeingia katika mtego ule ule wa kumfanya Nyerere ndiye nguzo ya kila kitu. Kitu ambacho mara nyingi umekikataa kwa kusema kuna historia ndefu na pana haijaandikwa vizuri.

Kwa kujua au kutojua, umempunja balozi Sykes kwenye siku yake muhimu hii.
Kiranga,
Husemi kweli.

Umeghadhibishwa na ukweli uliopo katika taazia ya marehemu.

Nyerere nimemtaja kwa mnasaba wake halisi katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika akiwa na Sykes brothers wote watatu.

Nyerere hakupata kueleza haya na alipata kutoa kwa mpigo medali 3979 tarehe 27 April 1985 katika viwanja vya Ikulu wakati anaacha urais.

Wazalendo wote unaowasoma katika makala za historia ninazoandika hata mmoja hakuwamo katika orodha ile.

Leo unasoma yale alionieleza marehemu kuhusu mchango wa kaka zake Abdul na Ally kwa Nyerere binafsi kwa TAA na TANU.

Hujapendezewa sasa unajibaraguza ati nimemfanya Nyerere nguzo ya kila kitu.

Nashangaa hujajiuliza ikiwa historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ni hii vipi Abdul Sykes na nduguze walifutwa katika historia ya TANU?

Hujapendezewa kusoma kuwa Nyerere alipata kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes na mikakati yote ya kwenda UNO na kuwahamasisha wananchi ilikuwa ikifanyika nyumbani kwa Abdul.

Ukweli huu umekuchoma sana.

Unataabika kujua leo kuwa hawa ndugu watatu hawakumchukua Nyerere kama kiongozi mwenzao bali walimuunga kama ndugu yao.

Iweje katika utunuku wa medali karibu 4000 Nyerere hakuwakumbuka?

Hili jambo linahangaisha nafsi yako kwani unatambua maana halisi ya khiyana hii unaamua kutoa ghadhabu zako kwangu.

Unatamani kumchinja mshenga.

Najua mengi sana katika historia ya TANU.

Huyo hapo kulia ni marehemu Kleist Abdul Sykes.

Tumeishi pamoja maisha yetu toka tu wadogo hadi utu uzima.

Kleist ndiye aliyenieleza urafiki uliokuwapo kati ya baba yake na Earle Seaton Mwanasheria kutoka Bermuda aliyekuwa akiisaidia TAA katika mambo ya sheria na jinsi ya kuwazunguka Waingereza na kuwafikisha UNO.

Hii ilikuwa 1950.

Seaton ndiyo aliyemshauri Abdul Sykes TANU iundwe kwa kutumia katiba ya Convention Peoples Party (CPP) ya Kwame Nkrumah wa Ghana ili Waingereza wasipate sababu ya kuwakwamisha.

Kleist kanionyesha hadi "private dairies," za baba yake.

Abbas Sykes kushoto mengi mengi mengi sana kanisomesha kuhusu harakati za kupigania uhuru.

Kaka usifanye maskhara.
Historia ya TANU naijua.

Tuendelee kuzungumza.

1621373257636.png
 
Kiranga,
Husemi kweli.

Umeghadhibishwa na ukweli uliopo katika taazia ya marehemu.

Nyerere nimemtaja kwa mnasaba wake halisi katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika akiwa na Sykes brothers wote watatu.

Nyerere hakupata kueleza haya na alipata kutoa kwa mpigo medali 3979 tarehe 27 April 1985 katika viwanja vya Ikulu wakati anaacha urais.

Wazalendo wote unaowasoma katika makala za historia ninazoandika hata mmoja hakuwamo katika orodha ile.

Leo unasoma yale alionieleza marehemu kuhusu mchango wa kaka zake Abdul na Ally kwa Nyerere binafsi kwa TAA na TANU.

Hujapendezewa sasa unajibaraguza ati nimemfanya Nyerere nguzo ya kila kitu.

Nashangaa hujajiuliza ikiwa historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ni hii vipi Abdul Sykes na nduguze walifutwa katika historia ya TANU?

Hujapendezewa kusoma kuwa Nyerere alipata kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes na mikakati yote ya kwenda UNO na kuwahamasisha wananchi ilikuwa ikifanyika nyumbani kwa Abdul.

Ukweli huu umekuchoma sana.

Unataabika kujua leo kuwa hawa ndugu watatu hawakumchukua Nyerere kama kiongozi mwenzao bali walimuunga kama ndugu yao.

Iweje katika utunuku wa medali karibu 4000 Nyerere hakuwakumbuka?

Hili jambo linahangaisha nafsi yako kwani unatambua maana halisi ya khiyana hii unaamua kutoa ghadhabu zako kwangu.

Najua mengi sana katika historia ya TANU.
Huyo hapo kulia ni marehemu Kleist Abdul Sykes.

Kleist ndiye aliyenieleza urafiki uliokuwapo kati ya baba yake na Earle Seaton Mwanasheria sheria kutoka Bermuda aliyekuwa akiisaidia TAA katika mambo ya sheria na jinsi ya kuwazunguka Waingereza UNO.

Hii ilikuwa 1950.

Seaton ndiyo aliyemshauri Abdul Sykes TANU iundwe kwa kutumia katiba ya Convention Peoples Party (CPP) ya Kwame Nkrumah wa Ghana ili Waingereza wasipate sababu ya kuwakwamisha.

Kleist kanionyesha hadi private dairies za baba yake.
Abbas Sykes kushoto mengi mengi mengi sana kanisomesha kuhusu harakati za kupigania uhuru.

Kaka usifanye maskhara.
Historia ya TANU naijua.

Tuendelee kuzungumza.

View attachment 1790207
Kwa makusudi ama kughafilika, umemdhalilisha Balozi Abbas Sykes kwamba hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

Umeniambia sisemi ukweli, hebu twende kimahesabu. Namba hazidanganyi.

Bandiko lako la kwanza limemtaja "Nyerere" au "Mwalimu" mara takribani 43.

Bandiko hilo hilo limemtaja Balozi Abbas Sykes mara takribani 16.

Umemtaja Nyerere zaidi ya mara mbili ya ulivyomtaja Balozi Sykes, katika bandiko la kuenzi maisha ya Balozi Sykes.

Yani umefunika historia ya Balozi Sykes kwa kutupa sana habari za Nyerere, huku ukilalamika wazee wako wanafunikwa hawaandikwi historia yao.

Na wewe umerudia lile lile unalolipinga.

Kisha hujatueleza baada ya Nyerere kufariki Balozi Sykes alifanya kazi gani, imekuwa kama kafa na Nyerere kazikwa naye kama kijakazi wa Farao!

Hujitambui, unafanya kilekile unachokipinga kwa wengine.

Yani hata kama mimi napinga Nyerere kuhodhi ushujaa katika historia ya Tanzania, nikisoma bandiko lako la kwanza naona unaturudisha huko huko kwenye habari za kumfanya Nyerere ndiye subject kubwa hata kwenye tazia ya Balozi Sykes, kama Balozi Sykes hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

You are a walking contradiction.
 
Kwa makusudi ama kughafilika, umemdhalilisha Balozi Abbas Sykes kwamba hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

Umeniambia sisemi ukweli, hebu twende kimahesabu. Namba hazidanganyi.

Bandiko lako la kwanza limemtaja "Nyerere" au "Mwalimu" mara takribani 43.

Bandiko hilo hilo limemtaja Balozi Abbas Sykes mara takribani 16.

Umemtaja Nyerere zaidi ya mara mbili ya ulivyomtaja Balozi Sykes, katika bandiko la kuenzi maisha ya Balozi Sykes.

Yani umefunika historia ya Balozi Sykes kwa kutupa sana habari za Nyerere, huku ukilalamika wazee wako wanafunikwa hawaandikwi historia yao.

Na wewe umerudia lile lile unalolipinga.

Kisha hujatueleza baada ya Nyerere kufariki Balozi Sykes alifanya kazi gani, imekuwa kama kafa na Nyerere kazikwa naye kama kijakazi wa Farao!

Hujitambui, unafanya kilekile unachokipinga kwa wengine.

Yani hata kama mimi napinga Nyerere kuhodhi ushujaa katika historia ya Tanzania, nikisoma bandiko lako la kwanza naona unaturudisha huko huko kwenye habari za kumfanya Nyerere ndiye subject kubwa hata kwenye tazia ya Balozi Sykes, kama Balozi Sykes hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

You are a walking contradiction.
Kiranga,
Umechelewa sana.

Kitabu cha Abdul Sykes kipo leo matoleo manne katika miaka 23.

Nyerere ni sehemu ya historia ya wazee wangu.

Nimemweleza na kumfungamanishanao kama inavyostahili.

Historia sasa imekaa vizuri.

Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika si ile ya mtu mmoja.

Najua mnaumia hili hamkulitegemea.

Hamkutegemea kama iko siku mtamsoma Mufti Sheikh Hassan bin Ameir katika historia ya TANU.
 
Kwa makusudi ama kughafilika, umemdhalilisha Balozi Abbas Sykes kwamba hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

Umeniambia sisemi ukweli, hebu twende kimahesabu. Namba hazidanganyi.

Bandiko lako la kwanza limemtaja "Nyerere" au "Mwalimu" mara takribani 43.

Bandiko hilo hilo limemtaja Balozi Abbas Sykes mara takribani 16.

Umemtaja Nyerere zaidi ya mara mbili ya ulivyomtaja Balozi Sykes, katika bandiko la kuenzi maisha ya Balozi Sykes.

Yani umefunika historia ya Balozi Sykes kwa kutupa sana habari za Nyerere, huku ukilalamika wazee wako wanafunikwa hawaandikwi historia yao.

Na wewe umerudia lile lile unalolipinga.

Kisha hujatueleza baada ya Nyerere kufariki Balozi Sykes alifanya kazi gani, imekuwa kama kafa na Nyerere kazikwa naye kama kijakazi wa Farao!

Hujitambui, unafanya kilekile unachokipinga kwa wengine.

Yani hata kama mimi napinga Nyerere kuhodhi ushujaa katika historia ya Tanzania, nikisoma bandiko lako la kwanza naona unaturudisha huko huko kwenye habari za kumfanya Nyerere ndiye subject kubwa hata kwenye tazia ya Balozi Sykes, kama Balozi Sykes hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

You are a walking contradiction.

Na wewe hujapenda kutajwa Nyerere au hujapenda kuwa Nyerere aliishi nyumbani kwa Abdu Sykes?


Naona hata maana ya "contradiction" huifahamu, pata darsa kuhusu "contradiction" kutoka kwenye Bible...

2 Samuel 24:1​

“And again the anger of the LORD was kindled against Israel, and he moved David against them to say, Go, number Israel and Judah.”

1 Chronicles 21:1​




“And Satan stood up against Israel, and provoked David to number Israel.”



Kitabu hicho hicho, Muandishi huyo huyo "Mungu", baada ya kusoma hapo tuambie aliyetoa amri alikuwa "Mungu" au "shetani"


Kijana hiyo ndio "contradiction".

Kama darsa halijakuingia nikuongeze "Bible" ikufundishe maana ya "contradiction".
 
Na wewe hujapenda kutajwa Nyerere au hujapenda kuwa Nyerere aliishi nyumbani kwa Abdu Sykes?


Naona hata maana ya "contradiction" huifahamu, pata darsa kuhusu "contradiction" kutoka kwenye Bible...

2 Samuel 24:1​

“And again the anger of the LORD was kindled against Israel, and he moved David against them to say, Go, number Israel and Judah.”

1 Chronicles 21:1​




“And Satan stood up against Israel, and provoked David to number Israel.”



Kitabu hicho hicho, Muandishi huyo huyo "Mungu", baada ya kusoma hapo tuambie aliyetoa amri alikuwa "Mungu" au "shetani"


Kijana hiyo ndio "contradiction".

Kama darsa halijakuingia nikuongeze "Bible" ikufundishe maana ya "contradiction".
Ngoja tuongezee mifano mujarab kutoka kwenye Quran.


A contradiction occurs when one statement on a subject excludes the possibility of another. The first one here is a good example. In Surah 19:67, it states that man was created out of nothing. In 15:26, man is created from clay. Since clay is something, we have a contradiction since “nothing” excludes the possibility of “clay.”
 
Bagamoyo,
Mchango wa Abdul Sykes katika historia ya TANU upo uthibitisho kuwa haukutakiwa ujulikane.

Hili nimelieleza katika kitabu cha maisha yake kwa ushahidi wa mmoja wa wanajopo wa Chuo Cha CCM Kivukoni.
Alihoji kwa nini mwenyekiti anakataa kupokea ''notes'' zake kuhusu Abdul Sykes katika kuunda TANU.

Jibu alilopewa ni kuwa historia ya TANU inayoandikwa haina uhusiano wowote na Abdul Sykes.

Huyu aliyehoji jina lake ni Hassan Upeka kijana wa Kidar es Salaam aliyekuwa katika Idara ya Usalama ya TANU toka mwaka wa 1956 baada ya kumaliza masomo Tabora School.

Alipokufa Abdul Sykes mwaka wa 1968 magazeti ya TANU, The Nationalist na Uhuru hawakuandika chochote kuhusu Abdul Sykes isipokuwa mistari michache kueleza kuwa Mwalimu Julius Nyerere kahudhuria mazishi yake.

Mhariri wa Tanganyika Standard Brendon Grimshaw ndiye aliyeandika taazia ya kueleza Abdul Sykes ni nani.
Nakuweka cutting la toleo hilo:

View attachment 1788864

kuna comment hapo juu naona umeiruka kuhusu Martin Kayamba na uhusiano wake katika kuanzisha African Association iliyoizaa TAA na baadae TANU

unaweza kutoa historia japo kiduchu kuhusu huyu mtu maana inaonekana historia ya mapambano ya kuleta uhuru unaijua kiundani zaidi
 
Ngoja tuongezee mifano mujarab kutoka kwenye Quran.


A contradiction occurs when one statement on a subject excludes the possibility of another. The first one here is a good example. In Surah 19:67, it states that man was created out of nothing. In 15:26, man is created from clay. Since clay is something, we have a contradiction since “nothing” excludes the possibility of “clay.”
Safi sana.

Siioni contradiction hapo bali naona "ignorance" kwako kama kwa yule niliekuwa nampa darsa la "contradiction".


Wewe kabla ya kuumbwa ulikuwepo?

Be honest, boy.
 
Ndugu yangu Mohamed Said,umeweka simulizi nzuri lakini mara zote kama kawaida moyo wako haukubali kama Nyerere alikuwa Rais wa kwanza wa TANU, Tanganyika,Tanzania na CCM.Unaamini kuwa kuna watu wako walistahili,ulitamani leo Hamza (RIP) na Abdul (RIP) ndio wawe wenye kuelezea historia ya nchi hii,unaamini Julius hajui historia ya nchi hii.Ni dhahiri moyo wako unatoa machozi kwani historia haiko kama unavyotaka.Uongozi ni riziki itokayo kwa Mola!
Riziki zipo za aina mbili, kuna riziki ya halali na kuna riziki ya haramu.
 
Kwa makusudi ama kughafilika, umemdhalilisha Balozi Abbas Sykes kwamba hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

Umeniambia sisemi ukweli, hebu twende kimahesabu. Namba hazidanganyi.

Bandiko lako la kwanza limemtaja "Nyerere" au "Mwalimu" mara takribani 43.

Bandiko hilo hilo limemtaja Balozi Abbas Sykes mara takribani 16.

Umemtaja Nyerere zaidi ya mara mbili ya ulivyomtaja Balozi Sykes, katika bandiko la kuenzi maisha ya Balozi Sykes.

Yani umefunika historia ya Balozi Sykes kwa kutupa sana habari za Nyerere, huku ukilalamika wazee wako wanafunikwa hawaandikwi historia yao.

Na wewe umerudia lile lile unalolipinga.

Kisha hujatueleza baada ya Nyerere kufariki Balozi Sykes alifanya kazi gani, imekuwa kama kafa na Nyerere kazikwa naye kama kijakazi wa Farao!

Hujitambui, unafanya kilekile unachokipinga kwa wengine.

Yani hata kama mimi napinga Nyerere kuhodhi ushujaa katika historia ya Tanzania, nikisoma bandiko lako la kwanza naona unaturudisha huko huko kwenye habari za kumfanya Nyerere ndiye subject kubwa hata kwenye tazia ya Balozi Sykes, kama Balozi Sykes hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

You are a walking contradiction.
Kiranga,
Hapa tutakesha.

Mimi nina faili zima la marehemu.

Mimi nina hazina ya mazungumzo na marehemu yanarudi nyuma takriban miaka 40.

Kama ulitegemea mimi niandike taazia ya kazaliwa mwaka gani kafa mwaka upi ana watoto na wajukuu wangapi haya kwa wengi hayana maana yeyoye.

Katika hayo ningetaka ningeeleza kuwa Abbas Sykes kasoma King's College Budo, Uganda na alikwenda Kampala kafuatana na baba yake.

Hapo Budo marehemu alisoma darasa moja na Kabaka Freddie Mutesa.

Ningekueleza pia Abbas Sykes akiwa kijana mdogo alichukua fedha kwa mama yake Bi. Mruguru bint Mussa akaenda dukani kununua Citroën mpya.

Ningeweza pia nikakuchomekea nikakufahamisha kuwa kaka yake Abdul yeye tayari alikuwa akiendesha Mercedes Ben 220 SE uhuru bado.

Nadhani umeelewa.

Mimi nataka nieleze yale muhimu yasiyofahamika yaliyokataliwa kupokelewa na Mwenyekiti wa jopo la Chuo Cha CCM Kivukoni walipokuwa wanaandika historia ya TANU mwaka wa 1981.

Hutaki habari za Nyerere zikaunganishwa na hawa wazee wangu.

Nashangaa sana imekuwaje ghafla unatokwa na jasho kuwa taazia ya marehemu haikuandikwa vyema na Mohamed Said.

Ati kalamu yangu inamdhalilisha Abbas Sykes.

Mimi Mohamed Said nimdhalilishe Bwana Abbas.

Hivi waliofunika historia ya TANU (si ya Abbas Sykes) huwajui?

Mbona hujasema lolote kuhusu kukosekana kwao mazikoni?

Hivi unajua kama hilo nimeliandika?
Give me a break.
 
kuna comment hapo juu naona umeiruka kuhusu Martin Kayamba na uhusiano wake katika kuanzisha African Association iliyoizaa TAA na baadae TANU

unaweza kutoa historia japo kiduchu kuhusu huyu mtu maana inaonekana historia ya mapambano ya kuleta uhuru unaijua kiundani zaidi
Eyce,
Martin Kayamba hakuwa muasisi wa African Association.

Ukitaka habari zaidi za Kayamba msome Daisy Sykes Buruku, "Kleist Sykes The Townsman," katika "Modern Tanzanians," John Illife (Ed.) 1973.

Haya aliyoandika Daisy yeye kayatoa kwenye mswada ambao babu yake aliandika kabla hajafariki mwaka wa 1949.

Katika kitabu hicho utasoma ya Martin Kayamba ambayo yeye mwenyewe hakuyasema.

Katika kitabu hicho utasoma nini Daisy kapokea kuhusu Kayamba kutoka kwa babu yake kupitia kalamu ya Erika Fiah na gazeti lake Kwetu.
 
Kiranga,
Hapa tutakesha.

Mimi nina faili zima la marehemu.

Mimi nina hazina ya mazungumzo na marehemu yanarudi nyuma takriban miaka 40.

Kama ulitegemea mimi niandike taazia ya kazaliwa mwaka gani kafa mwaka upi ana watoto na wajukuu wangapi haya kwa wengi hayana maana yeyoye.

Katika hayo ningetaka ningeeleza kuwa Abbas Sykes kasoma King's College Budo, Uganda na alikwenda Kampala kafuatana na baba yake.

Hapo Budo marehemu alisoma darasa moja na Kabaka Freddie Mutesa.

Ningekueleza pia Abbas Sykes akiwa kijana mdogo alichukua fedha kwa mama yake Bi. Mruguru bint Mussa akaenda dukani kununua Citroën mpya.

Ningeweza pia nikakuchomekea nikakufahamisha kuwa kaka yake Abdul yeye tayari alikuwa akiendesha Mercedes Ben 220 SE uhuru bado.

Nadhani umeelewa.

Mimi nataka nieleze yale muhimu yasiyofahamika yaliyokataliwa kupokelewa na Mwenyekiti wa jopo la Chuo Cha CCM Kivukoni walipokuwa wanaandika historia ya TANU mwaka wa 1981.

Hutaki habari za Nyerere zikaunganishwa na hawa wazee wangu.

Nashangaa sana imekuwaje ghafla unatokwa na jasho kuwa taazia ya marehemu haikuandikwa vyema na Mohamed Said.

Ati kalamu yangu inamdhalilisha Abbas Sykes.

Mimi Mohamed Said nimdhalilishe Bwana Abbas.

Hivi waliofunika historia ya TANU (si ya Abbas Sykes) huwajui?

Mbona hujasema lolote kuhusu kukosekana kwao mazikoni?

Hivi unajua kama hilo nimeliandika?
Give me a break.
Ma shaa Allah, wakati huo Marehem Nyerere hata baiskeli hana. Ndio ukweli huo.
 
Abbas Sykes nilipokuwa naongea naye alikuwa anapenda sana kusema watu wa Bara hawatuamini Siri watu wa Pwani na ni vigumu Sana kutusaidia wakati tuna shida. Kwa hiyo lazima tuweke watu wetu katika nafasi za uongozi.
Kwa ajili hiyo nadhani yeye ndiye almost single_handedly amewaweka madarakani watu kama Omar Ali Juma au Mohammed Shein.
Najua hii ni kama kumgombanisha marhemu na watu, lakini hayo ndiyo mawazo yangu.
 
Kiranga,
Hapa tutakesha.

Mimi nina faili zima la marehemu.

Mimi nina hazina ya mazungumzo na marehemu yanarudi nyuma takriban miaka 40.

Kama ulitegemea mimi niandike taazia ya kazaliwa mwaka gani kafa mwaka upi ana watoto na wajukuu wangapi haya kwa wengi hayana maana yeyoye.

Katika hayo ningetaka ningeeleza kuwa Abbas Sykes kasoma King's College Budo, Uganda na alikwenda Kampala kafuatana na baba yake.

Hapo Budo marehemu alisoma darasa moja na Kabaka Freddie Mutesa.

Ningekueleza pia Abbas Sykes akiwa kijana mdogo alichukua fedha kwa mama yake Bi. Mruguru bint Mussa akaenda dukani kununua Citroën mpya.

Ningeweza pia nikakuchomekea nikakufahamisha kuwa kaka yake Abdul yeye tayari alikuwa akiendesha Mercedes Ben 220 SE uhuru bado.

Nadhani umeelewa.

Mimi nataka nieleze yale muhimu yasiyofahamika yaliyokataliwa kupokelewa na Mwenyekiti wa jopo la Chuo Cha CCM Kivukoni walipokuwa wanaandika historia ya TANU mwaka wa 1981.

Hutaki habari za Nyerere zikaunganishwa na hawa wazee wangu.

Nashangaa sana imekuwaje ghafla unatokwa na jasho kuwa taazia ya marehemu haikuandikwa vyema na Mohamed Said.

Ati kalamu yangu inamdhalilisha Abbas Sykes.

Mimi Mohamed Said nimdhalilishe Bwana Abbas.

Hivi waliofunika historia ya TANU (si ya Abbas Sykes) huwajui?

Mbona hujasema lolote kuhusu kukosekana kwao mazikoni?

Hivi unajua kama hilo nimeliandika?
Give me a break.
Vitu vya msingi nilivyoandika, kwa ushahidi wa namba, ambavyo hukavikanusha, ni kuwa.

1. Umemuandika Nyerere kuliko Abbas Sykes katika siku ya msiba wa Abbas Sykes. Umemuandika Nyerere takribani mara 43 na Abbas Sykes takribani mara 16.

2. Umeshindwa kueleza maisha ya Abbas Sykes baada ya kufariki kwa Nyerere yaliendeleaje na alifanya nini.

Umemshusha Abbas Sykes na kumfanya kuwa mtu ambaye hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

Halafu hapo hapo unalalamika kwamba Nyerere anaandikwa sana kuliko mashujaa wengine walioanzisha mapambano ya kudai uhuru.

Wewe mwenyewe, kwa kujua au kutojua, ni kati ya watu wamaomuandika sana huyo Nyerere kuliko hao mashujaa wengine waliopigania uhuru.

Umeji contradict.
 
Vitu vya msingi nilivyoandika, kwa ushahidi wa namba, ambavyo hukavikanusha, ni kuwa.

1. Umemuandika Nyerere kuliko Abbas Sykes katika siku ya msiba wa Abbas Sykes. Umemuandika Nyerere takribani mara 43 na Abbas Sykes takribani mara 16.

2. Umeshindwa kueleza maisha ya Abbas Sykes baada ya kufariki kwa Nyerere yaliendeleaje na alifanya nini.

Umemshusha Abbas Sykes na kumfanya kuwa mtu ambaye hakuwa na maisha zaidi ya kuwa kivuli cha Nyerere.

Halafu hapo hapo unalalamika kwamba Nyerere anaandikwa sana kuliko mashujaa wengine walioanzisha mapambano ya kudai uhuru.

Wewe mwenyewe, kwa kujua au kutojua, ni kati ya watu wamaomuandika sana huyo Nyerere kuliko hao mashujaa wengine waliopigania uhuru.

Umeji contradict.
Karanga,
Hivi mimi nikukanushe wewe kwa lipi.

Mimi nalalamika.
Nilalamike ili iwe nini?

Unajua kulalamika hadi uwe mlalamishi.

Mimi ni mwandishi si mlalamishi.

Wewe ndiye mlalamishi unataka niandike historia ya wazee wangu utakavyo wewe.

Ulosema katika yote na hakika umenisuuza ni hilo kuwa namwandika sana Nyerere.

Si kuwa namwandika tu hata kumzungumza namzungumza sana.

Nitafute You Tube.

Nimemweleza Nyerere toka siku ya kwanza mwaka 1952 kaletwa nyumbani kwa Abdul Sykes na Joseph Kasella Bantu hadi 1999 anafariki.

Nimemweleza Nyerere kuanzia 1955 wakati anaimbiwa nyimbo za lelemama na shangazi zangu akina Bi. Hawa bint Maftaha katika mikutano ya mwanzo ya TANU Mnazi Mmoja hadi hadi miaka ya mwisho ya maisha yake; jina lake likitajwa...

Subhanallah...

Nimemzungumza Nyerere na Abdul Sykes Zentrum Moderner Orient, Berlin...

Nimemzungumza Abdul Sykes na Nyerere Northwestern University Evanston, Chicago...

Nimemwandikia Nyerere taazia alipokufa...

Ingia hapo chini:
mohamedsaidsalum.blogspot.com.

Fanya "name search," utajua kuwa ushahidi wako wa namba hauna maana yeyote kwani umeelemewa na huo utaokutananao.

Unadhani mie niko hapa kufanya mzaha na wewe?
 
Back
Top Bottom