Buriani rafiki na ndugu yangu Salum ''Slim'' Shamte (1951 - 2020)

Kwa nini aliitwa Slim, na ilimaanisha nini?
 
Kwa nini aliitwa Slim, na ilimaanisha nini?
Jidu...
Tulipokuwa watoto tuko shule kila mtu alikuwa na ''nickname'' yake.''

Majina tu wala hayakuwa na maana yoyote.

Kulikuwa na Mazola, Kirk Douglas, Marlon Brando, Yongo, Livingstone Madegwa,
Kitonsa na mengine mengi majina ya wacheza mpira Ulaya na waigizaji wakubwa kutoka Hollywood.
 
Asante kwa jibu lako ingawaje linakwepa my follow up question.
Mimi vile vile najua hayo yote maana ni mtoto wa DSM.
Marijani Shaaban tutulisoma wote Tambaza.
Nakujua ndugu yangu MSA, wewe ni mtetezi wa wazee wako wa mwambao ambao ni waislamu.
Sasa huyu "Slim" kujitukuza kwa jina, nickname ya kiingereza, hapo naina unapiga ngima kwenye maji.
 
Jidu...
Huyu ndugu yangu ni marehemu.

Sote sisi tulikuwa na majina ya kupanga na wala hayakuwa na uhusiano wowote na dini au kujitukuza kwa aina yoyote ile.

Majina niliyotaja hapa wengi tukiitana hivyo pale Saigon Club miaka ya 1967 wengi wako shule za msingi ni watoto wadogo.

Tukienda senema Empire kuangalia ''Westerns'' tukimuona muigizaji umempenda unachukua jina lake.

Hayakuwa mambo wanayofanya watu wazima.

Wengi wenu ambao pengine hamkutujua sisi makuzi yetu nimeona mnababaishwa na mengi.

Wasichana wa wakati wetu walikuwa wakijipa majina ya wacheza senama wa kike kama Ann Magret, Ursulla Andress, Nancy Sinatra.

Hizo zilikuwa nyakati nyingine kabisa Waingereza waliziita ''The Roaring 60s.''

Katika safari zangu nje nimewashangaza wengi wanaponialika majumbani kwao nakuta ala za muziki kama piano, guitar nk.

Basi hupiga piano ingawa niko ''rusty,'' kwa kukosa kupiga kwa muda mrefu na hushangaa wakaniuliza wapi nilijifunza.

Hizi ni ''taste'' mtu anazipata kutokana na makuzi.

Nina ufahamu mkubwa sana wa jazz.

Hapo chini niko nyumbani kwa rafiki yangu Dr. Harith Ghassany Muscat nilikuwa nampigia nyimbo tena ni hymn, ''Crying in the Chapel.''

Hii nyimbo ya kanisani iipata umaarufu baada ya kupigwa na Elvis Presley ambae alikuwa ''idol'' wangu katika ''teens.''

Yeye na mkewe walishtuka sana wakaniuliza wapi nimejifunza.
Ikiwa umesoma na Marijani basi wewe ni mdogo sana kwangu.

Namfahamu Marijani toka utoto Gerezani yeye na Yusuf Kaungu wote ni marehemu Allah awalaze pema peponi.

Wote walikuwa wachezaji mpira hodari sana.

Marijani alikuwa mlinda mlango wa Kahe Republic na Kaungu alicheza Simba.

Sikwepi swali wakati mwingine nakaa kimya kwa kuwa panakuwa hapana haja ya kufanya ubishani.

Mimi hupenda kueleza yake ambayo watu hawayajui.

Hii ina tija zaidi.

Mimi sijatetea wazee wangu bali nimeiandika historia ya wazee wangu vipi walipambana na ukoloni wa Muingereza kwa kuasisi vyama vilivyokuja kuwaunganisha watu wakawa wamoja wakapigania uhuru wakiwa wameshikana kama taifa.


Waliunda African Association 1929, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933 na TANU 1954.

Hii ni historia iliyokuwa katika hatari kubwa ya kupotea.

Huku si kutetea.




Humburg nyumbani kwa Abdilatif Abdalla.
 
Brother Moh vijana mfano wa mrangi na rodrick alexander wakikuona hapo kwenye picture wanastaajabu kwamba upande wako wa pili kumbe wewe ni mpiga piano? Hahaha wewe ni GOT kwenye Tasnia hii kongole kaka, unahistorisha, unafunza na kuburudisha
 
Brother Moh vijana mfano wa mrangi na rodrick alexander wakikuona hapo kwenye picture wanastaajabu kwamba upande wako wa pili kumbe wewe ni mpiga piano? Hahaha wewe ni GOT kwenye Tasnia hii kongole kaka, unahistorisha, unafunza na kuburudisha
Makala...
GOT ni nini?

Utoto una mambo mengi.
Iikuwa ukiingia chumbani kwangu utakuta guitar Hoffner electrick.

Nikipigs guitar nikijaribu sana kukopi style ya Hank B. Marvin huyu alikuwa lead guitarist wa The Shadows hawa ndiyo wakmpigia Cliff Richard.

Utakuta viatu vya Addidas kwa ajili ya mpira.

Na blacbord ukutani kwa ajili ya masomo ya shule.

Ulikuwa wakati wake.
 

WHAT DOES G.O.A.T. MEAN?​

Not many people can claim to be the G.O.A.T., but those who can are the Greatest Of All Time in their field. Most often, the acronym G.O.A.T. praises exceptional athletes but also musicians and other public figures.
On social media, it’s common to see the goat 🐐 emoji in punning relation to the acronym
 
Ahsante sana lakini sidhani kama nina sifa hiyo.
 
Pole sana ndugu lakini huyu mjomba wako hii haki miliki alisajiri...kama alisajiri huo ndio ushahidi wa haki yake vinginevyo ni ngumu kuamini!

Hilo la hati miliki ni jambo Moja, lakini kuhusu matibabu na stahiki zake Je?

Nirudie tu Kwa Mara nyingine kumpongeza Mzee wetu Mohamed Said Kwa uandishi murua na weledi lakini pia kuwa na subiria ya kufuatilia jambo bila kujiingiza kwenye kutetea kitu bila kupata taarifa zaidi. Mfano hapa ameomba apatiwe link ya Uzi asome taarifa kamili lakini pia amekiri Kuna kesi mahakamani akatahadharisha tusiongee mambo bila kuwa na ushahidi nayo.

Pole Kwa msiba wa Rafiki Yako Mzee wetu. Safari yetu sote.
 
Pole sana ndugu lakini huyu mjomba wako hii haki miliki alisajiri...kama alisajiri huo ndio ushahidi wa haki yake vinginevyo ni ngumu kuamini!
Brother Mohamed Said hawa jamaa wameleta tuhuma za "dhulma" kwa jamaa zako marhum "Shamte na kwikima", ila imenishangaza kuona mmoja analalamika kwamba mjomba wake alidhulumiwa haki miliki ya ugunduzi wa pombe huyu mwingine rodrick alexander yeye kaficha tuhuma zake, inasikitisha sana kaona kwenye Tanzia ya Shamte (Mola Amrahamu) ndipo pakubumbia tuhuma zake
 
Nikuambie tuhuma zake kama nani,, hata nikizitangaza keshatangulia mbele za haki hakuna kitakachobadilika.
Nimeshasema huyu mtu ana ndugu na familia yake si vizuri ukaanza kuongea hayo mambo wakati Kuna ndugu zake unachotafuta wewe ni umbeya tu wa kutaka kujua habari za marehemu.
 
If you wear a mask for too long, there will come a time when you can not remove it without removing your face.
Matshona Dhliwayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…