BURIANI Sultan Jamshid BIN Abdulla BIN Khalifa (1926 - 2024)

BURIANI Sultan Jamshid BIN Abdulla BIN Khalifa (1926 - 2024)

Huyu Mzee kila siku anamdisi Mwalimu Nyerere aliyeongoza harakati za uhuru wetu, ila huyu hapa anamsifia Sultani aliyepinduliwa kwa kuwanyima haki za kisiasa n.k wazanzibar.
Kisa na mkasa; Dini.
Mkuu suala kuu la mwandishi huyu wa hii taazia ni DINI.

As far ni ndugu yake ktk imani hata kama ni magaidi ya Houthi, hezbollah, alshabab, al qaeda n.k atawapamba
 
Huyu Mzee kila siku anamdisi Mwalimu Nyerere aliyeongoza harakati za uhuru wetu, ila huyu hapa anamsifia Sultani aliyepinduliwa kwa kuwanyima haki za kisiasa n.k wazanzibar.
Kisa na mkasa; Dini.
Mkuu suala kuu la mwandishi huyu wa hii taazia ni DINI.

As far ni ndugu yake ktk imani hata kama ni magaidi ya Houthi, hezbollah, alshabab, al qaeda n.k atawapamba
 
Sawa mtanganyika mkatoliki unayeumia zaidi kwa Zanzibar kuliko sisi wazanzibari wenyewe.

Hivi unaweza kuteletea jina la mtu mmoja tu aliyefungwa na kuuliwa na Mfalme ?? mimi nitakuletea listi ya watu waliouliwa na hao wakotiliki wenzako pamoja na Nyerere mwenyewe hapa Zanzibar na mpaka juzi bado wanaendelea kuuliwa na legacy ya kikatoliki
Story za kwenye vijiwe vya kahawa hizo
 
Mzee anataka kutuaminisha kwamba Sultani huyu wa mwisho alikuwa mtu mwema sana, tofauti na Usultani wenyewe kwa maana yake. Kwa tafsiri hii ya Mzee kumfurusha kwa namna ile ilikuwa ni makosa na uonezi sana kiasi cha kukosa nauli na kujibanza nyumba mbili.
Taazia hii inalengo la kumfanya Sultani kuwa mtu mwema na kwamba hakutakiwa kufurushwa kwa namna ile. Hazungumzii kuhusu Usultani na kadhia yake kwa watu ila Sultani huyu na wema wake.
Kuna muda Mzee huyu waga busara zinamzidia sana.
Chivundu,
Imetokea kuwa nimetafiti vya kutosha historia ya mapinduzi nikiwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany kuanzi 2003 hadi 2010.

Nimekuwepo katika mahojiano yake na wahusika wakuu wa mapinduzi Tanga na Dar-es-Salaam.

Mimi ndiye niliyemfikisha Daktari Kipumbwi kulipokuwa na kambi ya Wamakonde waliovushwa kuingia Zanzibar kusaidia mapigano mwaka wa 1964.

Historia yote ipo katika kitabu alichoandika Dr. Ghassany, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru."

Ikiwa utakuwa mstaarabu na kujiepusha na lugha za kejeli za "kufurushwa," tunaweza tukafanya mjadala wa kiungwana utakaowanufaisha wengi hapa jamvini.

Nina ujuzi wa kutosha kiasi nimealikwa Zanzibar mara tatu kufanya pitio za vitabu vya mapinduzi hadharani na nikajaza ukumbi pomoni.

Mbali na makala na mahojiano ninayofanya kwenye televisheni na radio za ndani na nje kuhusu historia ya Zanzibar.

Masultani hawakupata kuua Wazanzibari wala kuweka jela za mateso Zanzibar.

Hawana historia hii katika utawala wao wote.
 
Mzee anataka kutuaminisha kwamba Sultani huyu wa mwisho alikuwa mtu mwema sana, tofauti na Usultani wenyewe kwa maana yake. Kwa tafsiri hii ya Mzee kumfurusha kwa namna ile ilikuwa ni makosa na uonezi sana kiasi cha kukosa nauli na kujibanza nyumba mbili.
Taazia hii inalengo la kumfanya Sultani kuwa mtu mwema na kwamba hakutakiwa kufurushwa kwa namna ile. Hazungumzii kuhusu Usultani na kadhia yake kwa watu ila Sultani huyu na wema wake.
Kuna muda Mzee huyu waga busara zinamzidia sana.

Sawa mwema alikuwa baba yako Nyerere aliyeuwa watu kwa maelfu pamoja na kuweka legacy ya mauwaji yanayofanywa na CCM mpaka leo
 
Mkuu suala kuu la mwandishi huyu wa hii taazia ni DINI.

As far ni ndugu yake ktk imani hata kama ni magaidi ya Houthi, hezbollah, alshabab, al qaeda n.k atawapamba

Kwani unafikiri lengo la mavamizi ya Zanzibar nalo lilikuwa nini si hiyohiyo dini
 
Kwani unafikiri lengo la mavamizi ya Zanzibar nalo lilikuwa nini si hiyohiyo dini
Lengo lilikuwa nikumrushia sultan na uarabu wake kwao .
Wabaki waafrica weusi halisi
 
Katika kitabu hiki kuna makala ya Jamshid akiwa na watu wapatao 500 wananchi wa kawaida wanaingia porini kuwinda nguruwe.

Sultan Jamshid anaingia porini kwenye msitu mzito bila ulinzi wowote kuwinda pamoja na wawindawenzake wamemzunguka wamebeba mikuki.
 
Hichi kitu cha Sultan na wazanzibar kuwinda nguruwe wa kitoweo kimenishtua sana.
Kumbe Sultani na wazanzibar kiasili walikuwa ni walaji wazuri mnoo wa kitimoto.
Mzee saidi mbona hizi siri hukutupa tangu kitambo?

Wazanzibar sasa tuache unafiki, kitimoto ipatikane wazi na popote Zanzibar. Ni urithi wetu huo.
 
View attachment 3189131
(1929 - 2024)​

Hiyo taazia hapo chini niliandika majuma machache yaliyopita nilipopokea taarifa kuwa Sultan Jamshid kafariki.

Haukupita muda nikapokea taarifa kuwa si kweli yu hai.
Nilijisikia vibaya sana.

Ninachokumbuka ni kupokea ujumbe kutoka kwa rafiki yangu akiniambia nilifanya haraka kuandika.

Sikuwa na la kusema.
Nilibakia kimya.

Niliandika taazia wakati Sultan Jamshid yu hai.
Taazia niliyoiandika ni hiyo hapo chini:

Jana usiku ndugu yangu kaniletea ujumbe mfupi kuwa Sultan Seyyid Jamshid, Sultani wa mwisho wa Zanzibar kafariki.

Asubuhi ndugu yangu huyu akanipigia simu tukazungumza mawili matatu akanifahamisha kuwa yeye hakupata kuonana na Jamshid ila alizungumzanae mara moja kwa simu Jamshid alipokuwa anaishi Portsmouth.

Sasa nikawa najiuliza nini naweza kuandika kuhusu Sultan Jamshid.

Jamshid kaandikwa sana kiasi nimekumbuka maneno ya marehemu Bibi Titi Mohamed aliponiambia, "Bwana Mohamed kipi utakachoandika wewe kuhusu mimi ambacho bado hakijaandikwa?"

Kipi ninachoweza mimi hii leo kuandika kuhusu Sultan Jamshid ambacho bado hakijaandikwa?

Kipo cha kuandika kuhusu Sultan Jamshid bin Abdulla bin Khalifa ambacho bado hakijaandikwa.

Jamshid kaondoka Zanzibar baada ya mapinduzi nafsi yake ikiwa imesalimika.
Jamshid anakwenda kwa Mola wake vidole vyake vikiwa safi havichuruziki damu.

Hakuna Mzanzibari anaeweza kusimama akasema Sultani ameniulia ndugu yangu au Sultani kanidhulumu haki yangu hii au ile.

Jamshid kaondoka Zanzibar hakuacha jela za mateso.
Jamshid hakuacha jela za mateso kwa kuwa hakurithi jela ya mateso.

Jamshid hakupata kukalia kiti cha enzi kilicholowa damu.
Hakika lipo la kuandika na la kusema kuhusu Jamshid.

Nimeingia Maktaba.
Natalii farahasha ya kitabu cha Harith Ghassany, "Kwaheri Uhuru Kwaheri Ukoloni."

Nataka nijikumbushe.

Najikumbusha kwa kuwa nilikuwa msaidizi wa Dr. Ghassany wakati wa utafiti wa kitabu hiki chake.

Nasoma yaliyomfika Jamshid halikadhalika nayasoma yale waliyopitia Wazanzibari waliokuwa nje ya Zanzibar mapinduzi yalipotokea.

Nayasoma na kuona kama vile ndiyo kwanza hayo nisomayo nayasikia leo.
Sultan Jamshid kapewa hifadhi Dar es Salaam yeye na familia yake na baadhi ya watu.

Wako wamejibanza kwenye nyumba mbili jumla yao watu 43.
Serikali ya Tanganyika inafanya mawasiliano na Waingereza kuhusu Sultan Jamshid.

Jamshid Sultan wa Zanzibar ni mtu masikini kwani hana fedha nje ya Zanzibar hata senti moja.

Sultan hana nauli ya kumfikisha Uingereza.

Nimetosheka.
Navuta kitabu kingine ninachokumbuka kuna habari za Sultan Jamshid.

Hili ni buku la mapicha kutoka matoleo ya gazeti maarufu DRUM lililokuwa likimilikiwa na Jim Bailey kutoka Johannesburg, Afrika Kusini.

Nilisaidia kuhariri na kuchapwa kwa kitabu hiki.

Katika kitabu hiki kuna makala ya Jamshid akiwa na watu wapatao 500 wananchi wa kawaida wanaingia porini kuwinda nguruwe.

Sultan Jamshid anaingia porini kwenye msitu mzito bila ulinzi wowote kuwinda pamoja na wawindaji wenzake wamemzunguka wamebeba mikuki.

Hakika yako mengi ya kusema kuhusu Jamshid.

Sura inayofuatia katika DRUM ni kuhusu mapinduzi chenye kichwa cha habari, "Bloodshed on the Spice Isle."

Nahitimisha safari yangu Maktaba kwa kitabu muhimu sana katika historia ya masultani: "Omani Sultans in Zanzibar," kilichoandikwa na Ahmed Hamoud Al Maamiry.

Mwanzo wa kitabu mwandishi anasikitika kuhusu damu iliyomwagika katika mapinduzi.
Siku zote historia ya mapinduzi itakuacha na majonzi.

Mwenyezi Mungu amfanyie wepesi hisabu yake ndugu yetu Sultan Jamshid bin Abdulla bin Khalifa.

View attachment 3189147

Alikuwa mtu mwema sana.Mzanzibar halisi,muongea kiswahili fasaha.Hakika propaganda zilizopigwa na ccm zilitunyima mambo mengi mazuri.Mungu amazed pema peponi.
 
Sultan alinyang'anya haki za watu Kwa kuwa kwao ni Oman kwanini aje atawale ardhi ya watu wengine?
Sultan aliyetoka Oman siyo Jamshid,Jamshid ni kizazi cha mbali sana cha babu wa mababu zake yeye.Sultan wa Oman na Zanzibar ni Seyyid Said aliyefariki 1856.Hapo ufalme wake uligawanywa pande mbili ,Zanzibar alirithi Sultan Majid na Sultan Thuwein ,Oman. JAMSHID alikuwa mswahili na Mtanzania kama sito Fiona na ghilba za CCM.Jamshid alikuwa Sultan kwa mujibu wa katiba,hakuwa mtendaji wa serikali,serikali ilikuwa chini ya waziri mkuu,Mohamed Shamte ambaye mwanaye Adam Shamte amekuwa kada wa kudumu wa CCM.Harakati za uhuru wa Zanzibar zilihusisha ubaguzi wa rangi hivyo chama ZNP kilikuwa karibu zaidi na sultan lakini hata ASP kisingeweza kusajiriwa bila kumtambua sultan kama head of state.Yaliyotokea 1964 ni ghiliba za majirani hasa Tanganyika na waingereza.Zanzibar haikutakiwa tena kuwa sovereign.
 
Lengo lilikuwa nikumrushia sultan na uarabu wake kwao .
Wabaki waafrica weusi halisi
Kwani mwarabu alikuwa na serikali toka lini? Tafuta kitabu cha Padri Sivallon kinaitwa Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania bara , utajuwa nini lengo la kanisa
 
Kwani mwarabu alikuwa na serikali toka lini? Tafuta kitabu cha Padri Sivallon kinaitwa Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania bara , utajuwa nini lengo la kanisa
Lengo la kanisa ktk nini?! Usultani au utawala wa zanzibar kama mada isemavyo?!
 
Mapinduzi ya kipumbavu, na wanaoendeleza mapinduzi haya na kuyaita matukufu basi hawako sahihi, niwashauri tu wasome dini.

Allah amrehemu na amuingize katika pepo ndugu yetu jamshid

Okello na nyerere huko waliko mhhh! Adhabu kali inawasubiri kwa kile walichowafanyia waislamu
Duu! Kwahiyo upo radhi ungetawaliwa na Sultan kutoka Oman kuliko kujitawala?
 
Back
Top Bottom