Buriani Zackaria Hanspope

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Mfanyabiashara mkubwa wa tasnia ya usafirishaji nchi Zacharia Hanspope amefariki usiku huu.

Zacharia Hanspope pia alikuwa mdau mkubwa wa michezo, na mpaka mwisho wa uhai wake alikuwa ni mjumbe wa kamati ya ligi.l na mwanachama mahiri wa club ya Simba.

Salamu zangu za pole ziende kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki, wanamichezo woye, club ya Simba na Watanzania wote kwa ujumla.
Taarifa rasmi itafuata hivi punde.

 
Baba yake aliuawa na majeshi ya Idd Amin Dada akidai ni mchina, wakati huo alikuwa kamanda wa polisi Kagera, na huo ulikuwa mwanzo wa vita vya Kagera.
 
Tusisahau kua huyu mzee alikua amechanja na bado covid imeondoka nae. Utasikia ngonjera za ukichanja inapunguza maumivu ama kulazwa ama vifo, sasa huyu mzee kafariki vipi na alikua amechanjwa?

Nimeona chats zake na Msingwa msemaji wa serikali akilalamika kwamba ugonjwa unatesa sana huku wataalam wa chanjo wanakwmabia ukichwanjwa hutateseka.
 
Wewe kama ni muerevu, pitia taarifa za nchi zilizochanja vizuri kama Israel na hata Uingereza... China pia ugonjwa ulikoanzia...Utapata majibu ya ngonjera hizo...
Pitia hata taarifa za Cuba.. Itakusaidia...

Nashindwa kuelewa baadhi yetu... Kwani Malaria, pamoja na kuwepo madawa kibao, hakuna wanaokufa kwa Malaria?
 
Hivi unaelewa tofauti ya chanjo na dawa?

Uliwahi kusikia kuna chanjo ya malaria?

Umewahi kusikia mtu mwenye chanjo ya malaria amekufa kwa malaria?

Jifunze zaidi kwanza uongeze maarifa.
 
Wewe jamaa ni kiazi..
Mahojiano na Efm uliyasikia? Alithibitisha hakuwa amechanja..
Acha kujifariji nyuma ya ujinga wako,chanjo ni muhimu sana..
 
Chanjo ni hiari kelele za nini? Tena wewe ni mwongo mkubwa kwenye mahojiano na kitenge pope alisema anaumwa covid na mazungumzo yakaishia hapo. Kitenge akaendelea kusisitiza umuhimu wa chanjo. Hakuna sehemu aliyoulizwa kama ameshachanja au hajachanja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…