Bw.Tundu Lissu siyo Intelligent!

Bw.Tundu Lissu siyo Intelligent!

Siyo kwamba Tundu Lisu hajui madhara ya matamko yake juu ya Mwl, Nyerere, amelewa sifa ya kuitwa mwanasheria maarufu, hasa hasa alivyoambiwa hivyo na Rais Kikwete.
Mtanzania halisi
Hakuna madhara kumgusa nyerere maana ameshatangulia mbele ya haki mnaogopa kwa kutoelewa tu,mwogopeni MUNGU kwa kukataa maovu maana GOD anaexist all the time kuliko kuogopa mtu aliekufa,watz vp,bado mnaabudu mizimu?
 
Mimi siku zote uwa nadhania kuwa mtu intelligent uwa anasolve tatizo kwa njia ya busara na si kuleta ubishani usio na faida na kupoteza muda....
sasa kapoteza muda gani wakati hati imeshapatikana kwa ajili ya alichosema,rais jk alishawahi kumsifia lissu kuwa yeye peke yake ni kama bunge zima?...lissu ni intelligent na INAHITAJIKA INTELLIGENT MIND KUMWELEWA LISSU
 
Bw.Tundu sio mtu intelligent kama watu wengi wanavyodhania, kwa maana mtu intelligent huwa ana uwezo wa kujua madhara ya kile anachokisema kabla hajakisema!

Mtu intelligent yoyote anapaswa kufahamu ktk Nchi kama TZ hauwezi kuanzisha Vita dhidi ya Mlm.Nyerere na ukashinda hata uwe nani, hata Raisi wa nchi leo hii akianzisha Vita dhidi ya Mlm.Nyerere hawezi kushinda mwishowe kuna mtu tu anaweza hata akajitoa mhanga kumlipua!

Ni sawa naleo hii Marekani mwanasiasa aanzishe Vita dhidi ya sijui Raisi Washington au Lincoln hawezi kushinda hata iweje hata kama huyo Mwanasiasa yuko sahihi kwa kiasi gani, vile vile kama ilivyo pia hakuna Mwanasiasa AK leo hii ambaye anaweza akaanzisha Vita dhidi ya Bw.Mandela na akashinda hata kama atakuwa sahihi kwa kiasi gani, na ndio maana utaona Wanasiasa wenye akili linapofika kwenye swala la hawa watu huwa wanakuwa waangalifu sana wawe ni Demokrats au Republikan hakuna anayethubutu kuwaongelea na kuwakashifu Lincoln hata kama walifanya makosa kiasi gani kwa maana wanafahamu kwamba hawa Watu nafasi yao imeshaandikwa kwenye Historia na huwezi kuifuta bila kukugharimu...

Bw.Tundu alipaswa aelewe kwamba hata kama Mlm.Nyerere amekosea kwa kiasi gani hakupaswa kumuongelea vile, alipaswa aelewe kwamba kuna watu wako tayari kufa kumtetea Mlm.Nyerere na hiyo ni Nchi nzima kuanzia jeshini mpaka Utingo wa daladala...
MKUU KIUKWELI WW NDO UTAKUWA SIO INTELLIGENT MAANA INTELLIGENTS WOTE TUMEMWELEWA LISSU.......HE IS THE ONLY TANZANIAN WHO DARED TO SPEAK THE TRUETH OPENLY,nyie mnazungumzia kiunafiki na kisirisiri
 
"Intelligence" ya mtu haipimwa kwa kuangalia wanaomuunga mkono. Inawezekana waliowengi wakawa na mtazamo usio sahihi kuhusu jambo fulani. Galileo alishawahi kuonekana kilaza kwa sababu ya kuibua mambo yaliyokuwa tofauti na mtazamo uliozoeleka lakini leo anakubalika kuwa alikuwa intelligent.
 
Mkuu,

Kwa HOJA zile NZITO za TUNDU LISSU ambazo wengi tulikuwa tunamsubiria mtu atakaye JITOA MUHANGA kuja kuziongelea ndani ya bunge hilo maalum la katiba ,nadhani TUNDU LISSU ni zaidi ya wajumbe wooote waliopo kwenye bunge la katiba!

Ni nani angeweza KUTHUBUTU kuongea yale aliyoyaongea kwa hawa WAHAFIDHINA walionyweshwa maji ya bendera!!?

HEKO TUNDU LISSU!!!

MTANGANYIKA DAIMA!
 
Hivi huyu jamaa Bw.Tundu ni Mbunge wa Jimbo la Masaki? Mbona sijawahi kumsikia hata siku moja akiongelea Jimbo lake Bungeni? Kila akiongea yeye ni masuala ya Kitaifa tu. Je, Jimbo lake halina Matatizo?

Sijawahi kusikia kama wengine huwa wanaongelea matatizo ya Majimbo yao Bungeni kama Mbunge wangu Bi.Mdee huwa anaongelea mara moja moja kuhusu Jimbo letu, au Bw.Mnyika huwa namsikia akiwakilisha Ubungo, hata Bw.Lema huwa nasikia akiwakilisha Arusha Bungeni lkn huyu Jamaa (Bw.Tundu) sijawahi kumsikia akiongelea Masuala ya Jimbo lake, sasa Je, Jimbo lake ni kama Masaki (Dar)?

Mbona unaleta hoja nyingine kabla hii uliyoileta haijafika mwisho.Kweli CCM mna mambo
 
Lissu anastahili doctorate ya heshima maana ameonyesha upeo mkubwa wa kufukua na kupembua mambo kuliko midokta na miprofesa iliyokaa bungeni kutoa hoja za kitoto
 
Kumbuka mtu anayebaki kwenye historia na aliyebaki na maisha yaliyopo aiwiwe mambo mengine ya baadae basi mtu huyo ajue hawezi pata maendeleo kama wewe, kumbuka phylosophers wengi wamepita lakini bado tumeainisha mapungufu yao sasa sembuse baba wa taifa? Y yeye dont be stugnant in idiology
 
Kumbuka mtu anayebaki kwenye historia na aliyebaki na maisha yaliyopo asiwiwe na mambo mengine ya baadae basi mtu huyo ajue hawezi pata maendeleo kama wewe, kumbuka phylosophers wengi wamepita lakini bado tumeainisha mapungufu yao sasa sembuse baba wa taifa yeye? dont be stugnant in idiology
 
Bw.Tundu sio mtu intelligent kama watu wengi wanavyodhania, kwa maana mtu intelligent huwa ana uwezo wa kujua madhara ya kile anachokisema kabla hajakisema!

Mtu intelligent yoyote anapaswa kufahamu ktk Nchi kama TZ hauwezi kuanzisha Vita dhidi ya Mlm.Nyerere na ukashinda hata uwe nani, hata Raisi wa nchi leo hii akianzisha Vita dhidi ya Mlm.Nyerere hawezi kushinda mwishowe kuna mtu tu anaweza hata akajitoa mhanga kumlipua!

Ni sawa naleo hii Marekani mwanasiasa aanzishe Vita dhidi ya sijui Raisi Washington au Lincoln hawezi kushinda hata iweje hata kama huyo Mwanasiasa yuko sahihi kwa kiasi gani, vile vile kama ilivyo pia hakuna Mwanasiasa AK leo hii ambaye anaweza akaanzisha Vita dhidi ya Bw.Mandela na akashinda hata kama atakuwa sahihi kwa kiasi gani, na ndio maana utaona Wanasiasa wenye akili linapofika kwenye swala la hawa watu huwa wanakuwa waangalifu sana wawe ni Demokrats au Republikan hakuna anayethubutu kuwaongelea na kuwakashifu Lincoln hata kama walifanya makosa kiasi gani kwa maana wanafahamu kwamba hawa Watu nafasi yao imeshaandikwa kwenye Historia na huwezi kuifuta bila kukugharimu...

Bw.Tundu alipaswa aelewe kwamba hata kama Mlm.Nyerere amekosea kwa kiasi gani hakupaswa kumuongelea vile, alipaswa aelewe kwamba kuna watu wako tayari kufa kumtetea Mlm.Nyerere na hiyo ni Nchi nzima kuanzia jeshini mpaka Utingo wa daladala...

mie najua Lisu ni intel. maana sifa kubwa ya intel ni ujasiri wa kusema ukweli mambo ambayo wengine wanayaogopa.ndimo akina Yesu, Yohana mbatizaji,Socrates, Jefferson, Martin Luther,Lumumba walimopita.kusema ukweli bila kupepesa macho. mimi mwalimu licha ya kutoka mkoa mmoja nakuthibitishia kuwa is the great human I have seen alive.kila likitajwa jina lake huwa machozi yananitoka kwa kumhusudu.Lakini ni vizuri kukiri na kusema udhaifu wake pia maana huko ndio kumpenda kweli.
By the way inaonekana historia ya Marekani huijui vizuri for your information anayependwa sana na kuenziwa sana ni Jefferson, Washington anashukuriwa zaidi kwa kumwendeleza Tom na kwa kuwa rais wa kwanza. jembe lao kubwa ni Tom likifuatiwa na mzee wa maamuzi magumu Lincoln

 
tundu:flypig::flypig: lisu nouma amewanyea patamu:rapture::rapture::israel::israel::rapture: hakuna kulemba mpaka kieleweke:flypig::flypig: m4c
 
Tatizo ni Kwamba Dunia haiko hivyo unavyodhani wewe, ndio maana nikakupa Mfano wa Marekani hao Maraisi waanzilishi kama akina Lincoln na Washington wengine walikuwa wanamiliki Watumwa ingawaje ni JAMBO BAYA lkn ni MWIKO kuwaongelea vibaya hao jamaa waliopita hata iweje na kila Mwanasiasa kama anajitaka basi huwa anatafuta tu mazuri waliyoyafanya na mabaya kuyaacha, vivyo hivyo kwa Mlm.Nyerere hapa kwetu nafasi yake tayari ipo na ameshakufa hivyo kumuongelea vibaya kama Mwanasiasa hata kama uko sahihi kwa Kiasi gani (kumbuka Dunia haiko fair) hakutakufikisha mbali, hauwezi kugeuza Maoni ya Watz leo hii dhidi ya Mlm.Nyerere hata ufanye nini bila kukugharimu na haijalishi utakuwa uko sawa kwa kiasi gani yeye (Bw.Lisu) alipaswa kulifahamu hilo...

Kuna mambo mengine haupaswi kuyasema hata kama unafikiri uko sahihi, ni hivyo tu na kwa bahati mbaya Dunia ndivyo ilivyo aliyekutangulia, amekutangualia na Mlm.Nyerere tayari ameshaweka Mark yake TZ na kuiondoa ni kazi kubwa...Bw.Tundu alipaswa kufahamu hilo!

mi mbona maoni yangu kuhusu nyerere yalishabadilika muda hata kabla Tundu Lissu hajasema bungeni,kimsingi upande wa pili wa Mwalimu upo wazi katika vitabu na si katka historia inayofundishwa mashuleni,fuatilia hata Nasaha za Mihangwa.
 
Mtu asiye INTELLIGENT ni yule anayeabudu binadamu na viumbe wengine kama wewe unavyomuabudu Nyerere. Nyerere was a normal human being subjected to mistakes na kama ulivyo wewe alikuwa na vitu alivyoamini kuwa ni sahihi kwa mtazamo wake hata kama ilikuwa ni kinyume chake. Kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake juu ya jambo lolote hata kama lipo kwenye biblia au msahafu. Iweje leo Nyerere au Karume wasikosolewe kwa mambo au makosa waliyofanya? Unadhani hao akina Abraham Linkohn hawana critics ndani ya Marekani? Mbona wao pamoja na Kennedy waliuawa kwa risasi na wamarekani wenzao.

Mtu aisye intelligent ni yule ambaye anaubaka uhuru wake mwenyewe kwa woga wa kutoongea ukweli kisa maslahi yake kisiasa au kiuchumi yatatetereka kama wewe unavyofikiria kwa TL. Kumbuka kuwa kizazi kinachomsujudia Nyerere ni hiki kinachoshika dola kwa sasa na wala si wale waliozaliwa mwaka 1980 ambao ndio wanaohitaji kushika dola kwa sasa.

Nyerere mwenyewe alisema UHURU wa KWELI ni ule wa jinsi kichwa chako kinavyofikiri. Kama katika umri ulionao bado akili na uhuru wako wa mawazo unatawaliwa na hisia za kuogopa athari zinazotokana na kusema kile unachoamini kuwa ni kweli basi bado unatawaliwa na ukoloni mbaya kuliko ule wa karne ya 19 na 20.

Kuna siku utashindwa kumwambia ukweli mkeo kwamba wewe umeathirika na VVU kwa kuogopa kuwa atakukimbia bila kujali madhara makubwa ya kutomwambia (Ni mfano tu).
 
Sijasema kama Sio Intelligent kabisa bali SIYO intelligent kama ambavyo wengi wenu mnadhania.
K
uhusu kuhusu Hati ya Muungano ingeweza kuletwa bila ya yeye kuongea aliyoongea dhidi ya Mlm.Nyerere hata kama ni ya ukweli kiasi gani, Mtu Intelligent alipaswa kutambua kwamba kuwa dhidi ya Mlm.Nyerere nchi hii utashindwa tu na mwishowe watu watakuupuzia na haijalishi ulikuwa uko sahihi kwa kiasi gani!

Huyo Babu (Mlm.Nyerere) alishawahi na hakuna jinsi mtu anaweza kubadilisha hilo hata ajaribu vipi, hivyo mtu intelligent anapaswa kutambua hilo...Waswahili tunasema Ujanja kuwahi, na yeye basi alisha wahi wengine lazima tukubali tu...

Msamehe bure,unajua wakati mwingine wazazi hufanya maklsa ya kuwa watoto majina ambayo yana madhara,kama hili la TUNDU.
 
quote_icon.png
By Edwin Mtei
Nilisikiliza Mheshimiwa Tundu Lissu na nasikitika kwamba sikubaliani naye jinsi alivyoeleza shutma juu na dhidi ya Mwalimu Julius Nyerere, Baba na Muasisi wa Taifa letu. Inajulikana na umma wa Watanzania, kwamba mimi binafsi, kama Waziri wa Fedha, nilitofautiana na Mwalimu, nikajiuzulu Uwaziri Decemba,1979, nikimwomba ateuwe Mtanzania mwingine atakayeshauri mambo ya Uchumi na Fedha. Lakini tuliendelea kuwasiliana kwa maelewano bila chuki, na hata aliniteuwa niwe Mwakilishi wa Tanzania na Afrika inayoongea Kiingereza katika IMF (Shirika la Fedha Duniani) chini ya miaka mitatu baadaye Novemba, 1972. Nimekuwa na mawasiliano na maelewano mazuri sana na Mwalimu hata baada ya kuasisi CHADEMA, Julai 1992 na tulipokamilisha Katiba na Sera za Chadema, nilimtembelea Nyumbani kwake Butiama nikampa azisome ajionee jinsi tulivyonuia kuwahudumia Wananchi wetu. Hata siku moja siwezi kumtusi Muasisi wa Taifa letu. Iwe ni mwiko pia kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kumtusi Baba wa Taifa.

Ningewashauri uongozi wa Chadema na hasa Vijana wa M4C (Vuguvugu la Mabadiliko) tuendelee na uhamasishaji : kwa umakini, tukiwa na huruma kwa wanyonge maskini wa kutupwa, tukijiandaa kwa umakini na kiutaalamu Sera na Mikakati ya kuwakomboa toka katika umaskini wa kutupwa kwa kutumia nguvu ya umma (Peoples Power) tukitumia mikakati sahihi: kwani Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke: Mikakati na Sera sahihi ikiwa ni kutumia misingi ya Uchumi na Miundombinu tulionayo licha ya uhalisia dhoofu tulioridhi; tukiwaenzi walioijenga na kuturidhisha kwa unyofu wao. Roho ya Julius Nyerere ilale mahala pema Peponi. Amen!

With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE.

Edwin Mtei
Founder Chairman of CHADEMA
.
 
"Problem cannot be solved by the same level of thinking which created them".Albert Einsten
 
Kwa sababu ni mwanasheria nguli na intelligent alijua alitumia mwanya huo kuwagusa vibaya ili hati itoke. Ukiwa mwanasheria mzuri katika argument zako lazima umchokoze mpinzani wako ili akupe ushaidi zaidi. Sasa hiyo hati imeombwa miaka nenda rudi haikutoka lakini jana alipowagusa pabaya imechomoka uko speed kali
Sasa wewe unayesema siyo intelligent sijui huoni ilo? au wewe ndiye mbumbumbu
serikali wameuumbua kwa kusema uongo, walitegemea ingekuwa turufu ya kugomea majadiliano ya rasmu kama alivyofanya mnyika. Leo hawana la kuongea tena...
 
Back
Top Bottom