Bwawa la Julius Nyerere mto Rufiji: The Silver Lining!

Bwawa la Julius Nyerere mto Rufiji: The Silver Lining!

Rufiji ni changamoto inayohitaji majaabu ya haraka na kushughulikia fursa zinazojitokeza.
1. Ishu ni kuwa, kila kitu kilipaswa kiwe planned before. Lakini cha ajabu sasa hivi ni eti hata DC tu anaamrisha wananchi walioishi pale miaka na miaka na mto wao wahame baada ya kuwa wameharibu na kutaka kuwafurikisha watu na maji ya bwawa walilojenga bila kufikiria athari zake.

2. Na kwa hiyo na kwa hali ilivyo sasa, ni lazima kuwe na loss kwanza, Ili labda watu tujifunze na ndipo tu - take off kwenda tunapotaka kwenda..

3. Na mimi nina mashaka na akili za viongozi wetu hawa. Kuna possibility kubwa ya kuanguka na wakabaki hapohapo wamekata tamaa na kukaatu badala ya kunyanyuka na kusonga mbele..
 
Watanzania ni wapumbavu sana mkuu!

Ngoja ccm iendelee kuwatia madole, huku umaskini ukiendelea kukita mizizi
 
Rufiji kuna mafuriko ila ikifika mwezi 7 dar haitakuwa na maji kabisa.
.
Nchi ya watu wenye akili, hilo bonde na bwawa vingezalisha ajira nyingi hasa kilimo na uvuvi na hata utaalii pia.

Kwa akili hizi za kipumbavu tulizonazo hakuna faida itapatikana kutokana na hilo bwawa
 
Kuna project inaitwa RUBADA (Rufiji Basin Development Authority) ilianzishwa 1975 na Nyerere ililenga uanzishwaji wa;
●HEP (Hydro Electric Power)
●Kilimo
●Forestry
●Industrial developmemt
●Tourism
●Navigation

Ila points zikawa zilezile
●Lack of enough capital
●Lack of qualified personnel
●Low level of sci & tech

Kilichofanyika so far ni HEP ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHHP) angalau likaitwa kwa jina lake kumuenzi Mwalimu kwa maono yake

Lengo la Nyerere lilikuwa kufanya projects kama ile ya Tennessee River Valley Authority (TVA) ya Marekani au The Three Gorges Dam Poject on Yangtze River ya China
South to North water diversion project .

Conceived in 1950 ujenzi /utekelezaji ukaanza 2002
 
Watanzania ni wapumbavu sana mkuu!

Ngoja ccm iendelee kuwatia madole, huku umaskini ukiendelea kukita mizizi
Unakosea mkuu, usiwe mtumwa wa matatizo.
DC kazi yake ni kutoa tahadhari ya hatari iliyopo ili wananchi wajue.
Watu wengi hawajui kuwa Ikwiriri ni mji amao uliasisiwa kutokana na mafuriko ya miaka ya nyuma, na ni mji ulio well planned.
Matatizo ya mafuriko ni kule mtoni(bonde la mto Rufiji).
Kutatua changa moto zilizopo kwanza ni kua ppreciate kuwa bado kuna fursa nyingi tu tunazoweza kufaidika nazo.
Maji ni uhai.
 
Watanzania huwa tunatazama mabaya tu ya kila jambo, hatutazami upande unaoweza kutunufaisha kiuchumi.
Bwawa la kufua Umeme la Mwalimu Nyerere, mto Rufuji inabidi litufumbue macho.
Its time to think big.

Kuna miradi kadhaa inaweza kuibuliwa.
1. A Major Waterway kusafirisha mazao na binadamu. Mto unaweza kutumika vixuri .

2. Kujenga kingo, Levees, kando ya sehemu zote za mafuriko

3 Bonde lote la Rufiji laweza kutumika kwa kilimo mwaka mzima.

4 Utalii wa majini, kando ya mto na hata mtoni kuna sehemu nzuri sana kwa Utalii. Nimeona hilo pale gate la Mloka kuingia Mbuga ya Selous, na kuna ziwa zuri sana sehemu za Mbunju kama 10km toka Ikwiriri.
Si watu wengi wanajua kuwa katika mdomo(delta) ya mto rufiji, meli ya kivita, SS Koenigsberg ,meli ya kivita ya wajerumani, vita Kuu ya Kwanza 1914, hata leo ipo hapo.
Meli hii ni karibia dada yake na mv Liemba ya Kigoma, na ilizamishwa hapo mto Rufiji ili isitekwe na waingereza.
Meli hii ikiibuliwa yaweza kuwa kivutio kikubwa cha utalii.

Wizara husika zaweza kutangaza fursa hizo nzuri, bahati nzuri waziri na mbunge Mchengerwa wa Rufiji inabidi suala hili alivalie njuga.
Jidu, umekuwa kama jini lilolofungiwa ndani ya chupa. Wakati unayaeleza haya, bwawa liko kwenye hatihati ya kuvunjika kwa kuta zake na ikitokea hivyo huo ndiyo mwisho wake. Tunavyoongea wakazi wa Rufiji wapo kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko yatokayo na ujenzi wa hili bwawa.

Kwa kifu bwawa lilijengwa bila kuangalia athari za kimazingira kutokana na jiografia ya eneo hilo. Hayo yote uliyoyaorodhesha yanaenda kusombwa na mafuriko badala ya kuwa neema tofuti na hizi theories zako. Kitu chochote kinachofanywa kwa kukurupuka siku zote mwisho wake ni mbaya.
 
Lazima tuwe forward thinkers, pamoja na matatizo tunayoyaona ya mafuriko Rufiji, bado hakijaharibika kitu na fursa nyingine ziko wazi.
Kama Kuna waterways inawezekana kabisa hata ufugaji wa samaki. Kama hujawahi kufika maeneo ya bonde la Mto rufiji huwezi kujua ilivyo giant. Hapa tunazungumzia kuanzia Rufiji kusini mpaka Morogoro.

Mzungu alikuja akafanya tafiti ya uranium na kuomba idhini UNESCO na akapewa kibali kumega karibu robo ya Seleous.

Rufiji basin ni bonge la potential kwa Nchi
 
Jidu, umekuwa kama jini lilolofungiwa ndani ya chupa. Wakati unayaeleza haya, bwawa liko kwenye hatihati ya kuvunjika kwa kuta zake na ikitokea hivyo huo ndiyo mwisho wake. Tunavyoongea wakazi wa Rufiji wapo kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko yatokayo na ujenzi wa hili bwawa.

Kwa kifu bwawa lilijengwa bila kuangalia athari za kimazingira kutokana na jiografia ya eneo hilo. Hayo yote uliyoyaorodhesha yanaenda kusombwa na mafuriko badala ya kuwa neema tofuti na hizi theories zako. Kitu chochote kinachofanywa kwa kukurupuka siku zote mwisho wake ni mbaya.
Nafikiri wewe hat huo mradi wa bwawa la Mwalimu Nyerere hujafika.
Mimi nemefika na kujionea ujenzi.
Swala la kupasuka halipo, narudia halipo.
Bwawa limejengwa kwa ustadi mkubwa na wahandisi waliobobea.
Wengi hawajui kuwa sehemu ile yenye presha kubwa ya maji, kwenye msingi, bwawa lina ukuta mnene, sikosei, wa karibia mita 100( kiwanja cha mpira)

Pili, Kilichojiri ni maji kujaa katika muda mfupi kutokana na mvua zisizo za kawaida mwaka huu. Bwawa limejaa mapema kuliko muda uliokadiriwa.

Tatu , kwa nyie mliozaliwa majuzi, mafuriko ya mto Rufiji, hii si mara ya kwanza na imekuwa hivyo toka miaka ya 70 panapotokea mvua kubwa.

Nitakuwa mnafiki nikisema bwawa halijachangia, limechangia tena sana.
Bwawa la Mwalimu Nyerere lina urefu wa kilemeta 100, upana wa kilometa 25, na kina pale kwenye kinu cha kufulia umeme , kina cha mita 131.
Hayo ni maji mengi, na sasa hivi yapo na yana zidi kujaa kutokana na mvua za masika huko Mbeya, Ryvuma, Dodoma, Morogoro na kwingineko.

Tuanze kuondokana na fikra za kujifungia katika matatizo. Bado kuna fursa nyingi sana zinazotokana na bwawa hili na maji yake.
 
Back
Top Bottom