Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere kujengwa chini ya kiwango, naomba kuuliza haya...

Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere kujengwa chini ya kiwango, naomba kuuliza haya...

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Kama mwananchi wa nchi hii na mlipa kodi nimesoma na kusikia kupitia magazeti, luninga na mitandao kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere limejengwa chini ya kiwango. Naomba kuuliza maswali yafuatayo:-

(1) Kwanza Kampuni ya Misri iliyoshinda tenda ya ujenzi ilikuwa na uwezo, utaalaam, uwezo wa kifedha?. Kama sivyo kwa nini walimpa Mhe. Rais wa awamu ya tano OK kuwa Kampuni hii ina uwezo wa kulijenga bwawa hili. Inawezekana walimuogopa Mhe. Rais wa awamu ya tano kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa na wakamdanganya ili kazi iendelee.

(2) Je, ni Kampuni au ni Serikali iliyoteuliwa kutoa ushauri wa kitaalam?. Kama ni Kampuni binafsi inatakiwa iwajibishwe kwa kutosimamia ipasavyo taratibu zote za ujenzi kama ilivyo kwenye BOQ. lakini ni Serikali basi hii ni kosa kubwa sana kwa uamauzi uliofanywa na Serikali. Mwisho wa siku kutokana na hayo mapungufu Kampuni hiyo itakuja kuwaruka na kuitupia lawama zote Serikali.

(3) Nimesoma kuwa mpaka sasa ujenzi uko asilimia 44 tu ingawaje walitakiwa wakabidhi mradi June, 2022. Je sababu walizotoa zinaridhisha? Hapa najua watakuja na sababu ya Covi 19 na Matukio ambayo yako nje ya uwezo wao kama mvua n.k. Je Serikali imekaa nao chini na kupitia sababu zao kama ni sababu za msingi?.

(4) Kama kweli ujenzi uko chini ya kiwango ina maana dawa ni kuanza upya kwa maana kuwa yale mahandaki yanajengwa upya na kurekebisha kila kitu. Je, gharama ya marekebisho hayo nani atayabeba?. Hii ina maana kuwa muda wa kukamilisha ujenzi unaweza kwenda mpaka 2026.

(5) Je, kwanini Serikali imegeukia sasa suala la gesi na suala la Bwawa kama vile linapoapoa siyo kama zamani. Kwa hitimisho naishauri Serikali iunde Tume huru na waseme ukweli wa matatizo yote ya Bwawa hili ili taarifa ya Tume hii apelekewe Mhe. Rais ili aone la kufanya.
 
Achana na maneno ya wapiga dili wanataka TANESCO iwe tegemezi wa makampuni ya IPTL, Agreco, Symbion nk ili wakubwa waendelee kula pesa za wavuja jasho, hapo Bwawa na Mwalimu Nyerere kuna wataalam wabobezi wamesimamia, mbona hawasemi flyover za Ubungo na Tazara au Madaraja ya Tanzanite nk yamejengwa chini ya kiwango?
 
Niliposikia ile ziara ya Mama Egypt nikapata mashaka sana, lilipokuja suala la Crane ndiyo ilokaongeza shaka zaidi sasa sijui ila kuna jambo halipo sawa mahali na inaonekana kuna juhudi zinafanyika Wananchi wasikue
 
Nchi Ngumu hii
Mawazo au Pale utakapo Ishia Kuwaza Ndio mambo Yalipo Anzia
Acha tu
 
Mradi mkubwa km ule hauitaji papara sawa makosa yapo lkn all in all mwisho wa siku utakamilika tu hata km mpaka 2030
 
Achana na maneno ya wapiga dili wanataka TANESCO iwe tegemezi wa makampuni ya IPTL, Agreco, Symbion nk ili wakubwa waendelee kula pesa za wavuja jasho, hapo Bwawa na Mwalimu Nyerere kuna wataalam wabobezi wamesimamia, mbona hawasemi flyover za Ubungo na Tazara au Madaraja ya Tanzanite nk yamejengwa chini ya kiwango?
Sijui kuhusu daraja la Tanzanite, sijapita pale. Lakini miradi mingi ya JPM ipo chini ya kiwango.
1. Magufuli hotels: walichopatia pale ni jina tu.
2. Mfugale/Kijazi flyovers: ovyo kabisa
3. Bwawa la MJN: mradi uliohitaji akili kubwa ukajengwa kishkaji
4. Barabara: sub-standards za hatari nyingine hata magari hayapishashani.

Kifupi transparency is key!
 
... aisee, ingekuwa China tungeshashuhudia firing squad pori la Chinangali B. Majitu yote yaliyoshiriki huo mchakato yanatakiwa yapigwe risasi vinginevyo kama taifa hatuchomoki!

Ukiyakuta kwenye majukwa sasa; yanapenda kweli ku-refer China kama mfano wa nchi iliyopiga hatua kimaendeleo bila kuwategemea mabeberu ila yanajifanya hayajui kwamba China ilifika hapo ilipo in a hard way!
 
Huo mradi ulipigwa vita kubwa mno kabla haujaanza. Kama upo 44% na 6 trillions zilishalala pale inasumbua akili kukubaliana na hili. Kwa ufupi tusipokuwa macho lobbyists wataturudisha tulipotoka. Vyombo viwe macho!
 
Achana na maneno ya wapiga dili wanataka TANESCO iwe tegemezi wa makampuni ya IPTL, Agreco, Symbion nk ili wakubwa waendelee kula pesa za wavuja jasho, hapo Bwawa na Mwalimu Nyerere kuna wataalam wabobezi wamesimamia, mbona hawasemi flyover za Ubungo na Tazara au Madaraja ya Tanzanite nk yamejengwa chini ya kiwango?
Niliwahi kuandika humu Kuwa Luna watu influential hawautaki Mradi wa umeme wa JNHP ni Kwan vile tu umefika mbali ndio maana wanashindwa kuustopisha ila watajitahidi kuuchelewesha.
 
... legendry wetu; shujaa pendwa la bara hili hakuna aliyethubutu kufanya hayo Mkuu wacha utani!
Acha ujuhaa!!ina maana hizo kasoro zimejitokeza ndani ya miezi hii 11?tatizo la jiwe ilikuwa ni kutumia nguvu nyingi akili kidogo!!huyo mshauri mwelekezi alikuwa wapi?
 
Ni kawaida, maana ata mwendokasi wa mbagala tuliona taarifa unajengwa chini ya kiwango so ili la bwawa sio habari ya kushangaza.

Nje ya mada

Chukulia mfano, mwendokasi wa mbagala kuunganika magomeni. Pale msimbazi na kigogo wamerudia kosa la kufanya barabara kua chini ikiwa maji huwa yanapita juu mvua ikiwa mkubwa. Ref jangwani
 
Niliposikia ile ziara ya Mama Egypt nikapata mashaka sana, lilipokuja suala la Crane ndiyo ilokaongeza shaka zaidi sasa sijui ila kuna jambo halipo sawa mahali na inaonekana kuna juhudi zinafanyika Wananchi wasikue
Ni kweli safari ya Samia Misri ndiyo iliyokuja na kuanza kwa porojo za crane na sasa mpuuzi wake Makamba anasema ati miundombinu ya umeme haikufanyiwa maintenance kwa miaka mitano yote ya Magufuli lkn ktk miaka mitano hiyo mgao na kukatika kwa umeme kulipungua kwa karibu 70% wakati mitambo ilikuwa haifanyiwi matengenezo,,, porojo tu za Samia kupitia kwa Januari hata bungeni anajibu utumbo mtupu na wabunge wajinga wanampigia makofi kumpongeza kama kawaida yao ya kujipendekeza kwa rais na mawazi anaowateua hata kama hawafai,,Samia anaupiga mwingi kuturudisha nyuma kama kujenga mashule bila matundu ya vyoo ,,, Kiufupi huo mradi wa Rufiji unakufa kimya kimya na wakumlau ni Samia
 
Mnaami hizi propaganda za kijinga,?? Kampuni kubwa kama hiyo haiwezi Jenga chini ya kiwango. Vyombo vya ulinzi na usalama nchi hii visikubali taifa kuchezewa na kikundi Cha watu wachache... maslahi ya taifa hili ni mapana kuliko interests za watu wachache wasiokuwa na chembe ya uzalendo kwa taifa. Wao wanawazia pesa tu bila kujali kuna vizazi vinakuja.
 
Serikali ya Magufuli ilikuwa kichwa ngumu sana, kwani walielezwa bila chenga kuwa Mafarao hawana uzoefu wa kujenga mabwawa lakini wakashupaza shingo!
Maghufuli hawezi kukubali such stupid thing , labda kama agenda yenu mnahisi itakwama , cha msingi liacheni Bwawa ili mtafute vyanzo vyenu mnavyoona vinafaa
 
Kama mwananchi wa nchi hii na mlipa kodi nimesoma na kusikia kupitia magazeti, luninga na mitandao kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere limejengwa chini ya kiwango. Naomba kuuliza maswali yafuatayo:-

(1) Kwanza Kampuni ya Misri iliyoshinda tenda ya ujenzi ilikuwa na uwezo, utaalaam, uwezo wa kifedha?. Kama sivyo kwa nini walimpa Mhe. Rais wa awamu ya tano OK kuwa Kampuni hii ina uwezo wa kulijenga bwawa hili. Inawezekana walimuogopa Mhe. Rais wa awamu ya tano kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa na wakamdanganya ili kazi iendelee.

(2) Je, ni Kampuni au ni Serikali iliyoteuliwa kutoa ushauri wa kitaalam?. Kama ni Kampuni binafsi inatakiwa iwajibishwe kwa kutosimamia ipasavyo taratibu zote za ujenzi kama ilivyo kwenye BOQ. lakini ni Serikali basi hii ni kosa kubwa sana kwa uamauzi uliofanywa na Serikali. Mwisho wa siku kutokana na hayo mapungufu Kampuni hiyo itakuja kuwaruka na kuitupia lawama zote Serikali.

(3) Nimesoma kuwa mpaka sasa ujenzi uko asilimia 44 tu ingawaje walitakiwa wakabidhi mradi June, 2022. Je sababu walizotoa zinaridhisha? Hapa najua watakuja na sababu ya Covi 19 na Matukio ambayo yako nje ya uwezo wao kama mvua n.k. Je Serikali imekaa nao chini na kupitia sababu zao kama ni sababu za msingi?.

(4) Kama kweli ujenzi uko chini ya kiwango ina maana dawa ni kuanza upya kwa maana kuwa yale mahandaki yanajengwa upya na kurekebisha kila kitu. Je, gharama ya marekebisho hayo nani atayabeba?. Hii ina maana kuwa muda wa kukamilisha ujenzi unaweza kwenda mpaka 2026.

(5) Je, kwanini Serikali imegeukia sasa suala la gesi na suala la Bwawa kama vile linapoapoa siyo kama zamani. Kwa hitimisho naishauri Serikali iunde Tume huru na waseme ukweli wa matatizo yote ya Bwawa hili ili taarifa ya Tume hii apelekewe Mhe. Rais ili aone la kufanya.
Umetumwa au??[emoji848][emoji848].. Kwa taarifa yako kampuni ya Misri iliyopewa hii tenda imepania Sana huu mradi ili iwekw historia kimataifa.. huo uchawi wenu kujifanya mtaka mtuletee umeme wa gesi ambao ni wa gharama kuliko.. hauiwezi kufanikiwa yani
 
Back
Top Bottom