Byabato, Nape waibukia soko la Kashai usiku, wazungumza na wafanyabiashara

Byabato, Nape waibukia soko la Kashai usiku, wazungumza na wafanyabiashara

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-07-16 at 08.48.13_c617d372.jpg

WhatsApp Image 2024-07-16 at 08.48.11_590ab125.jpg

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Stephen Byabato wametinga katika Soko la Kashai mjini Bukoba, usiku wa Julai na kushiriki kikao cha wafanyabiashara wa soko hilo.

Wafanyabiashara wa soko hilo walikutana jana Julai 15, 2024 usiku kwa ajili kushiriki kikao kilichokuwa kikijadili namna ya kuboresha soko hilo ambalo linatakiwa kufanyiwa maboresho lililopo mjini Bukoba mkoani Kagera.

Mawaziri hao walifika sokoni hapo mida ya saa 2 usiku na kupata fursa ya kuzungumza nao kisha wakawapongeza wafanyabiashara hao kushiriki kikao hicho ambacho nao walikuwa wakitoa maoni yao ya kuboresha soko hilo baada ya kuona michoro ya awali kisha na wao kueleza nini kifanyiwe maboresho.
WhatsApp Image 2024-07-16 at 08.48.13_cf0e1c7e.jpg
Nape amesema kushirikishwa kwa wafanyabiashara hao kutaondoa manung’uniko na lawama kwani kumekuwa na mtindo wa wafanyabiashara kutoshirikishwa kwenye baadhi ya miradi hivyo kupelekea misigano isiyokuwa na tija.

Waziri Nape ambaye alifika mkoani humo kwa ajili ya kuendelea na ziara yake mikoa ya Kanda ya Ziwa ya kukaguwa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano inayojengwa mikoa 26 ya Tanzania Bara ambapo anatembelea mikoa ya Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza na Shinyanga.
WhatsApp Image 2024-07-16 at 08.48.14_3de6534b.jpg
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Stephen Byabato wametinga katika Soko la Kashai mjini Bukoba, usiku wa Julai na kushiriki kikao cha wafanyabiashara wa soko hilo.

Wafanyabiashara wa soko hilo walikutana jana Julai 15, 2024 usiku kwa ajili kushiriki kikao kilichokuwa kikijadili namna ya kuboresha soko hilo ambalo linatakiwa kufanyiwa maboresho lililopo mjini Bukoba mkoani Kagera.

Mawaziri hao walifika sokoni hapo mida ya saa 2 usiku na kupata fursa ya kuzungumza nao kisha wakawapongeza wafanyabiashara hao kushiriki kikao hicho ambacho nao walikuwa wakitoa maoni yao ya kuboresha soko hilo baada ya kuona michoro ya awali kisha na wao kueleza nini kifanyiwe maboresho.
Nape amesema kushirikishwa kwa wafanyabiashara hao kutaondoa manung’uniko na lawama kwani kumekuwa na mtindo wa wafanyabiashara kutoshirikishwa kwenye baadhi ya miradi hivyo kupelekea misigano isiyokuwa na tija.

Waziri Nape ambaye alifika mkoani humo kwa ajili ya kuendelea na ziara yake mikoa ya Kanda ya Ziwa ya kukaguwa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano inayojengwa mikoa 26 ya Tanzania Bara ambapo anatembelea mikoa ya Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza na Shinyanga.
Minara ni ya makampuni binafsi. Inamhusu nini Nape kama siyo ufujaji wa fedha za sirikari?
 
Tufahamishane, kitu gani kiliwafanya washindwe kufanya kikao mchana, hadi wakaamua wakifanye saa 2 usiku.
 
Back
Top Bottom