CAF CHAMPIONS LEAGUE: Al Ahly, Zamalek ni anguko la wababe wa Misri au soka la Afrika limekua?

CAF CHAMPIONS LEAGUE: Al Ahly, Zamalek ni anguko la wababe wa Misri au soka la Afrika limekua?

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika inaendelea kwa sasa, ni msimu wa 2021/22 lakini kuna matukio kadhaa ambayo inawezekana yakawa na maana tofauti kuhusu soka la Afrika.

Wababe wa Misri, Al Ahly licha ya kuchukua nafasi ya tatu hivi karibuni katika Klabu Bingwa Dunia walipoenda kushiriki, lakini wamejikuta wakipoteza mchezo wao tena kwenye uwanja wa nyumbani katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kitu ambacho ni nadra kutokea.

Al Ahly wamepigwa bao 1-0 na Mamelodi ya Afrika Kusini, jana Jumamosi Februari 26, 2022 katika mchezo wa Kundi A.

Kabla ya hapo Mamelodi Sundowns ilikuwa ikiambulia sare tu tena ikiwa kwao Afrika Kusini, lakini sasa hivi wameichapa Al Ahly tena wakiwa Misri.

Kumbuka kuwa Al Ahly pia katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo waliambulia matokeo ya 0-0 dhidi ya Al Hilal ya Sudan ambayo ndiyo inayoshika mkia.

Upande mwingine, wababe wengine wa Misri, Zamalek wapo kwenye hali mbaya katika michuano hiyo, wakishika nafasi ya tatu kati ya timu nne katika Kundi D.

Zamalek hawajashinda katika mechi tatu, wana sare mbili na kupoteza moja, nao pia jana waliambulia kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Wydad AC ya Morocco.

HII MDAU UNAONAJE, NI ANGUKO LA WAKUBWA WA MISRI AU NI UPEPO TU MCHAFU WATAREJEA KATIKA MSTARI AU SOKA LA NCHI NYINGINE LIMEKUA?

AB.JPG


CD.JPG
 
We jamaa hujui mpira. Halafu wewe ni mshabiki wa yanga.
 
We jamaa hujui mpira. Halafu wewe ni mshabiki wa yanga.

Mtoa mada ameuliza tu swali. Hivyo ulitakiwa ukubali, au ukatae kwa hoja! Na kama kwa mtazamo wako unaona hajui mpira, basi mfafanulie aelewe.

Sasa masuala ya ushabiki wa Yanga yana uhusiano gani na kufanya vibaya kwa hizo timu kutoka Misri?
 
Mtoa mada ameuliza tu swali. Hivyo ulitakiwa ukubali, au ukatae kwa hoja! Na kama kwa mtazamo wako unaona hajui mpira, basi mfafanulie aelewe.

Sasa masuala ya ushabiki wa Yanga yana uhusiano gani na kufanya vibaya kwa hizo timu kutoka Misri?
Mkuu hapo ndipo utaona JF imekufa kabisaaa yaani kuna watu unawatazama una hisi wanafikiria kwa kutumia sijui nini?
 
Labda zamalek ila Al Ahly bado yupo moto na vizuri sana amecheza mechi mbili mpaka sasa kwenye kundi A na ana point moja aliyochukua away dhidi ya Al hilal ya Sudan japo amepoteza nyumbani dhidi ya sundowns kwenye mechi yake ya pili.

Al Ahly ana uhakika mkubwa wakupita kwenye hilo kundi japo anaweza kupita akiwa nafasi ya pili nyuma ya sundowns lakini si ajabu kwani hata mwaka jana Ahly alimaliza nafasi kama hiyo nyuma ya Simba Sc ya Tanzania lakini walichokwenda kukifanya mbele Al Ahly wote tunakifahamu
 
Wameharubu sana hapo UEFA champions league na EUROPA haiwezi kuta kitu kama hicho kwenye hatua kama hiyo.

Mfumo wa Uefa ni tofaut na mfumo wa caf

UEFA makundi yanapangwa mwanzo kabisa wa mashindano kabla hata mechi moja haijachezwa. Timu shiriki zote zinawekwa kwenye draw ya makundi kipindi cha ufunguzi.

Caf ni tofaut sababu timu shiriki zinaaanza kucheza mtoano kwanza kwa round mbili ili zipungue.

Sasa hapo ikitokea timu za nchi moja zimefuzu kufika group stage na hazina ubora wa juu, ni rahisi kupangwa group moja sababu Groups zinapangwa kwa mfumo wa seeding. Timu zenye same level ya seeding hazipaswi kukutanishwa same group. Sasa nyinyi mkiwa wadogo wadogo rahis kupangwa same group
 
Kama ulitazama game utaelewa jamaa bado wapo bora kwa kiasi gani.

Kupoteza game imekuwa matokeo tu. Lkn kiwango kipo juu mno. Mamelod imekuwa ni bahati tu kwao.
 
Mtoa mada ameuliza tu swali. Hivyo ulitakiwa ukubali, au ukatae kwa hoja! Na kama kwa mtazamo wako unaona hajui mpira, basi mfafanulie aelewe.

Sasa masuala ya ushabiki wa Yanga yana uhusiano gani na kufanya vibaya kwa hizo timu kutoka Misri?
Mkuu hapo ndipo utaona JF imekufa kabisaaa yaani kuna watu unawatazama una hisi wanafikiria kwa kutumia sijui nini?
Nyie vilaza ni pipa na mfuniko

Mtu wa mpira huwezi sema anguko kwa kutofanya vizuri msimu mmoja, nisawa na kusema ukifungwa mechi moja hushindi kitu vile
 
Back
Top Bottom