CAG Assad alisema ni mtu mjinga pekee ndo anaweza kufanya manunuzi cash: Anajifunza nini Entebbe Airport?

ubongo wako una kamasi.Hujui chochote kuhusiana na masuala ya kiuchumi.Cash ina kazi yake na loan ina kazi yake.You can't buy such long term assets by cash ! Niishie hapo kwanza

loan ni kwa ajili ya wafanya biashara, International loan ni kwa ajili ya kuwapiga waafrika! mpaka sasa hakuna nchi yoyote ya afrika imeweza kulipa deni lake tumebaki kukopa juu ya deni, mfano kenya wamepitiliza DEPT CEILING kiasi kwamba inabidi wakope kulipa deni lingine.

- Nadhan mpaka apo naeleweka
 
Na chief Hangaya naye ndo hivyo tena tumepigwa

Serikali inauwezo wa kukopa kiasi chochote kwenye pesa ya ndan na inaweza kulipa madeni yote ya ndan ya msaa kadhaa tu, deni la uhakika ni la nje, na ndo linalovuruga watu vichwa kulipa, huezi kopa pesa ambayo unaiendesha wewe
 
Hakuna wa kuwadhibiti marais wa Africa kwa ujumla
Katiba inawafanya wafanye wanachotaka

kenya mnaowasifia wana katiba nzuri ndo wanaongoza kwa madeni ukanda huu, wameshapitiliza dept ceiling na sasa deni lao linahesabiwa in respect to the GDP
 
vizuri saana, sasa kama biashara ya ndege ni ngumu na unajua kabisa ndan ya miaka 5 bado kutakua hamna faida, ahadi ya kurejesha huo mkopo + interest ndan ya miaka 5 unatoa wap?
Hoja ni kupanga kwa kuangalia vipaumbele vya msingi.
Hakuna mlala hoi ata moja ambaye anaunga kununua ndege mpya kila mweI.Watu wana njaa watu hawana ajira watu wanasumbuliwa mafao yao watu hawapewi mikopo ya elimu ya juu.

Kununua kwa mkopo hakumsimamishi shughuli zingine za kijamii.Ata kama ni kununua kwa keshi basio sio kila mwezi..
 

Mkuu itakusaidia sana ukitafuta na kusoma mada kuhusu “airline fleet planning and procurement strategies”. Ni taaluma nzito hasa. Unaweza hata kuomba elimu toka kwa wataalamu wa eneo hilo. Usije ukafananisha ununuzi wa ndege na mradi wa ujenzi wa fixed assets. Boeing, Airbus, nk. wamewekeza sana kwa wataalamu aina hiyo wanaoshinda kushauriana na mashirika makini ya ndege (wateja wao).

Kwanza, kutegemeana na mpango na mazingira ya kibiashara, shirika la ndege lazima lipange aina na idadi ya ndege LITAKAZOMILIKI moja kwa moja (100% ownership) na zile litakazokuwa nazo kwa vipindi vifupi vifupi (100% lease).

Kwa nchi masikini kama TZ kuna mikataba ya kimataifa inayotoa unafuu wa gharama za kununua na kukodi ndege kutokana na mwenendo wa soko na biashara na mipango yake. Ethiopian wanacheza sana na hizo instruments ili kuwa na ndege nying za kisasa muda wote kwa gharama nafuu sana. Note that these chaps are poor than us.

Ungekuwa huna kero kubwa na Prof Assad, ningekushauri ukae nae kwa utulivu akufafanulie hili somo badala ya kuja kumsema visivyo hapa JF kwa maelezo rahisi hivi yasiyowiana na somo gumu.
 
kenya mnaowasifia wana katiba nzuri ndo wanaongoza kwa madeni ukanda huu, wameshapitiliza dept ceiling na sasa deni lao linahesabiwa in respect to the GDP

Sijawahi kuwasifia hao majizi hata siku moja
Nimeandika Africa kwa ujumla hakuna sheria zinazofuatwa

Corruption kila mahali
Huwezi kufanya biashara kwa amani kama nchi zilizoendelea
Nje hatuna pressure
 
Sijawahi kuwasifia hao majizi hata siku moja
Nimeandika Africa kwa ujumla hakuna sheria zinazofuatwa

Corruption kila mahali
Huwezi kufanya biashara kwa amani kama nchi zilizoendelea
Nje hatuna pressure

izo zote sjui corruption wala hazihusiani, huezi kulipa deni na pesa mbayo hauna thats the point! Deni la taifa saaahv linakaribia around $40B kama sjakosea ina maana ukiamua kulipa hili deni mzunguko wote wa pesa unaisha na deni lingine linabaki, Kwahio kulipa deni la taifa ni uongo lazima katika kipindi flan cha maisha tutadefault kwa kiasi flan
 
Mku mbona unatuchang'anya. nkilipia cash na nkakubali kusubiri ndege yangu hata kama baada ya mwaka moja au miwili,ntakuwaje nimelipa zaidi ya bei halisi? Si nimekubali kusubiri zamu yangu ifike nitengenezewe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…