CAG Assad Mungu ampe maisha marefu sana. Aliweka wazi kuwa Bunge ni dhaifu halafu kuna watu wakaja juu na kumuondoa

CAG Assad Mungu ampe maisha marefu sana. Aliweka wazi kuwa Bunge ni dhaifu halafu kuna watu wakaja juu na kumuondoa

mr mkiki

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
5,588
Reaction score
11,668
Mh CAG Assad Mungu ampe maisha marefu sana,aliweka wazi kuwa bunge ni dhaifu halafu kuna watu wakaja juu na kumuondoa. Ule udhaifu aliousema ni huu uliotufikisha hapa leo. KATIBA imeweka wazi kazi ya bunge ni KUSIMAMIA na KUISHAURI serikali. Hii kazi ya KUSIFU tu wameitoa wapi?

Tulijiuliza mbona enzi za mwalimu watu hawakusimama kujiita wazalendo? Wakati huu mtu akisimama anajiita Mzalendo
Tofauti ni kwamba wazalendo wa Nyerere walikuwa wanaitwa na watu kwa sababu ya matendo, Wazalendo wetu wanajiita ili kuficha UFISADI.

“Matumizi mabaya ya Ofisi” “Kuisababishia Serikali hasara” haya mambo si yanaingia kama Rushwa na Uhujumu uchumi?

Kuna namna Katiba yetu inatakiwa kubadilishwa. Kiongozi akiiba hela za nchi kama hivi anatakiwa azirudishe na kufutwa uongozi kabisa maana akiendelea kuwa kuongozi ataendelea kuiba tu. Jela ndo sehemu inawafaa baada ya kufilisiwa.

Mr mkiki
View attachment 1746824
 
Bunge la wapiga meza whwa...whwa....whaaa...
Si kuna kiongozi alitwambia kuwa wasanii walijitolea Jamani sasa inakuwaje wako kwenye malipo, Kwa namna hii huu ni uhujumu uchumi watu wapelekwe mahakamani wajibu tuhuma wakikutwa na makosa wawajibike kisheria
 
Unasema kuna haja ya katiba kubadilishwa. Unadhani hili bunge la chama kimoja litakubali katiba ibadilishwe wabunge wakose ulaji? Thubutu !!
Shida mwizi wa hela za uongozi na siasa huwa hakamatwi,. inakera sana!

Hili linatuhusu sisi wananchi
 
Katiba hii haifai hata kupeleka kwa mkeo maana imezalisha dictators na wanafiki
 
Mzalendo na mtetezi wa wanyonge ameshindwa hata kubadilisha katiba , amepiga kelele bila vitendo hakuna lolote alilofanya kudeal na ufisadi
Tukawa tunapiga kelele humu miradi hii mikubwa mlioiita ya 'kimkakati' ikaguliwe kuanzia inapoanza.
 
Katiba hii haifai hata kupeleka kwa mkeo maana imezalisha dictators na wanafiki
Wakati mwingine kumtoa NYOKA mkubwa na hatari aliyeingia chumbani sio kupiga risasi kila kona. Unaweza kuchoma UDI. Chumba kinanukia vizuri na nyoka anatoka mwenyewe.

Rais hawezi kuwatoa haraka hawa watu aliomuachia mwendazake Magufuli. Wamo hadi uvunguni mwa kitanda anacholala.
 
Kikwete licha ya madudu yake mengi tunayodai lakini aliacha CAG makini saaaaana.

Akaacha walau Bunge lilioweza kusikiliza upinzani.

Akaacha vyombo vya habar vizungumze vinavyoweza kuzungumza.

Jiwe ndo alikuja kuharibu hili taifa, kiongozi wa hovyo kabisa yule.
 
Kikwete licha ya madudu yake mengi tunayodai lakini aliacha CAG makini saaaaana.

Akaacha walau Bunge lilioweza kusikiliza upinzani.

Akaacha vyombo vya habar vizungumze vinavyoweza kuzungumza.

Jiwe ndo alikuja kuharibu hili taifa, kiongozi wa hovyo kabisa yule.
Aisee
 
Mbaya zaidi kiongozi mkuu wa bunge dhaifu anasimama nakusema Magufuli alishauriwa vibaya
 
Back
Top Bottom